Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
<br />
<br />
toa ujinga wako hapa
Scope,
Huo si ubunifu hata kidogo!!! Ni udhalilishaji wa wanyama.Wanyama kazi wote si kwa ajili ya kubeba watu ni kwa ajili ya kubeba mizigo,kulima na wengine kwa usalama wa nyumba zetu. kubeba watu ni kukiuka haki za wanyama.Kwani hilo ni gari la abiria? Ndio maana hata serikali yetu inakataza malori kubeba abiria.
 
Mkuu naomba unikosoe kwa hoja lakini usiuhusishe ulemavu wangu..Jenga hoja lakini si vema kushambulia mumble ya watu,hakuna mtu aliyemuomba MUNGU kuwa jinsi alivyo,awe mbaya,mzuri,mwenye ulemavu au kutokuwa na ulemavu..

Hakuna uhusiano wa ulemavu na kuwa muaminifu au kutokuwa mwaminifu...Haya mengine ni tabia na ulemavu ni hali.

Usicheze na MUNGU,Mshukuru MUNGU kama huna ulemavu wa aina yeyote ile.

MUNGU akubariki sana na nakuombea MUNGU asikupe ulemavu ama wewe au yeyote yule katika familia yako..

Pole Regia. Huyo Mzee wa Posho hakustahili kuandika alichoandika. Watu wengine akili zao ni finyu sana kiasi kwamba unashindwa hata kumwelewesha jambo!
 
Heshima yenu wakubwa,

Asubuhi hii nimesoma habari ya Nape Nnauye kupigwa biti na katibu mkuu wake Wilson Mkama ktk gazeti la Mwanahalisi kwa sababu ya kwenda Igunga kuhani msiba wa Kijana aliyegongwa gari ktk msafara wa CCM na kufa papo hapo huko Igunga.

Taarifa zinasema kitendo chake hicho kimeuwaudhi sana Rais JK na W. Mkama kwa madai kwamba kitendo hicho kinaweza kumuudhi Rostam na kusababisha uchaguzi Igunga kuharibika.

Taarifa zinaendelea kusema kuwa, sokomoko hili lilitua mpaka kwa katibu mkuu Wilson Mkama aliyemwuliza Nnape, Nanukuu gazeti,

Nnape kwanini ulienda Igunga? Ulikatazwa na kamati kuu usiende, sasa, kwanini umeenda Igunga? \

Nnape alijibu, Nilikwenda kuhani msiba
.

Mkama; Nani amekutuma? Mkama alifoka?
Nape hakuwa na jibu.

Gazeti lilimtafuta Nnape kwa simu na kumuuliza kuhusu sokomoko hilo naye akajibu,


Alfred
(mwandishi), mimi sina la kujibu kuhusu hilo. Akauliza, Jamani mimi ni kijana mwenzenu, nimewakosea nini?

Mkama alipopigiwa simu kuhusu habari hiyo, kwanza alicheka ha ha ha ha. Kisha akasema,
fahamu sisi hatufanyi kazi za kiutendaji kupitia magazetini. Isitoshe, si vema kuzungumzia mambo mazito kama haya magazetini. Nakwenda Zanzibar, nitarudi kesho kutwa( Jumatano) njoo ofisini tuzungumze. Alipoambiwa kuwa gazeti liko mbioni kuchapishwa, alijibu sawa, lakini kwanini usije ofisini?

In my view, M
kama hakukanusha kumpiga biti Nnaye, ina maanisha alifanya hivyo( This is my opinion).
Gazeti pia lilikumbusha kuwa Nnape amewahi kujigamba ktk mtandao wa kijamii ( Jamii forums) kuwa mliosema sitaenda Igunga, mbona nimetinga
Igunga?


My take,


Nnape anajua alitendalo ndani ya CCM? Anaujua kweli msimamo wa JK?

Je, huku siko kushindwa kwa wazi kwa JK kwa hoja yake ya kuvuana magamba?

Mkuu kwahilo me wala sishangai
CCM huwa wanamakubwa hilo ni dogo wala msishangae hapo ilipo ina majibishano sana na majungu kwa fitna nyingi tuu
 
binafsi sikuhitaji CHADEMA maana we ni nani mpaka uweke masharti haya ,utatusaidia nini kama mpaka sasa ujaona mazuri yetu.
 
Mkuu naomba unikosoe kwa hoja lakini usiuhusishe ulemavu wangu..Jenga hoja lakini si vema kushambulia mumble ya watu,hakuna mtu aliyemuomba MUNGU kuwa jinsi alivyo,awe mbaya,mzuri,mwenye ulemavu au kutokuwa na ulemavu..

Hakuna uhusiano wa ulemavu na kuwa muaminifu au kutokuwa mwaminifu...Haya mengine ni tabia na ulemavu ni hali.

Usicheze na MUNGU,Mshukuru MUNGU kama huna ulemavu wa aina yeyote ile.

MUNGU akubariki sana na nakuombea MUNGU asikupe ulemavu ama wewe au yeyote yule katika familia yako..
Maneno ya hekima sana haya mdogo wangu Regia, Msamehe bure huyo maamuma wa akili. Mie nakupongeza sana kwa ujasiri ulionao na MUNGU atakuongezea na kukupandisha juu katika siasa za nchi hii na hata nje hapo baadae.
Usife moyo.
 
Juzi Wamemuonyesha akiwa ana hutubia watu wachache mno katika mkutano wa kampeni kata ya simbo wilayani igunga pembeni akiwepo punda kihongwe akila majani, Jana wamemuonyesha lakini ITV wakachakachua picha wakaweka umati wa cuf badala wa cdm, Leo tena wamemuonyesha akiwa juu ya fuso la cdm akihutubia na watu wachache sana wakimsikiliza wengine wakiwa wamesimama mbali sana karibu mita 50, Nashindwa kuelewa Dk Slaa huyu aliyepo Igunga ndiye yule tuliye mzoea akihutubia umati wa maelfu ya watu? au kujitokeza watu wacheche ktk mikutano yake ndio umaarufu wake umepungua? wanajf tulijadili hili na majibu tumpekee DK. slaa.
 
mkuu wanapata order kutoka kwa boss wao Mengi,,yule mzee ni mnafiki kinoma,,mwenyekiti wa ccm kilimanjaro anaitwa mama nsilo na ni rafiki mkubwa wa huyo mmiliki wa itv
 
Je,alihutubia watu wachache?...kama ndiyo sasa unalalamika nini?....na huyo punda alikuwepo?...au unadhani alibandikwa?
 
akihutubia wakazi hao wa igurubi waliojitokeza kwa wingi kuja kumsikiliza mtaalam huyo wa uchumi duniani Prof Lipumba amesihi sana wakazi hao kutoichezea nafasi hiyo ya kupiga kura kwani ndio itakayo toa mwanga kwa uchaguzc ujao wa 2015, pia ameomba kutomchagua mgombea wa ccm Dalali kafumu kwani kufanya nl kumpa udalali wa kuuza madini yenu, huyu ndiye aliyeingiza nchi ktk mikataba mibovu msimchague aliasa Prof Lipumba.
 
mkuu wanapata order kutoka kwa boss wao Mengi,,yule mzee ni mnafiki kinoma,,mwenyekiti wa ccm kilimanjaro anaitwa mama nsilo na ni rafiki mkubwa wa huyo mmiliki wa itv

Licha ya kuwa marafiki pia ni majirani kule machame, pia mumewe na Mama vick marehemu Asanterabi Nsilo Swai alikuwa mfadhili mkubwa wa Mengi kipindi cha nyuma hapo....


Ila hayo yote hayafanyi ITV kuchakachua picha... Bali haya ni majungu ya mleta bada tu hamna ukweli wowote wa uchakachuaji wa picha, na Dr.Slaa amekuwa akijaza sana kwenye mikutano wanayofanya kwenye kata za jimbo la Igunga.
 
ka ni kweli watu wachache wacha waoneshe hvo hvo coz ndivo ilivokua ka wengi wataonesha ni wengi FULL STOP
 
ondoa shaka mkuu, kwani wapiga kura ndio last say hata kama ITV watamwosha akiwa na watu wawili, na zote hizo nik fitina za kisiasa
 
Waambie wana Igunga, bila kutokomeza ufisadi ndoto ya maendeleo itakuwa ni ndoto ya kudumu kwao na kwa Watanzania wote.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom