UBER Yasitisha huduma nchini Nigeria na Uganda

UBER Yasitisha huduma nchini Nigeria na Uganda

Strong ladg

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
950
Reaction score
2,232
Kampuni ya Uber inayohusika na huduma za taksi mtandao,imetangaza kusimamisha shughuli zake nchini Nigeria na Uganda kuanzia tarehe 2 Septemba 2026.

Wataalam wa biashara na uchumi tunaomba mtusaidie, je nini kinaweza kuwa chanzo cha Uber kusitisha huduma zake katika nchi hizo ikiwa ni baada ya kusitisha huduma zao katika nyingine mfano Tanzania ?.Je ni ushindani kutoka kwa kampuni nyingine,hali ya uchumi au mazingira ya kufanyia biashara??
 
Kama ilivyotokea Tanzania kipindi cha nyuma, Uber wamekuwa wakipata wakati mgumu sana na mamlaka za udhibiti. Mfano mzuri ni lile sakata la juzi la mamlaka za viwanja vya ndege Nigeria (FAAN) kupiga marufuku huduma zao hapo uwanjani.

Ingawa Uber wanasema haihusiani moja kwa moja, ila hizi vurugu za kisheria huwa zinawachosha sana wawekezaji.
 
Mfano, nyakati hizi abiria wengi wa bodaboda wanapanda mshikaki, unafikiri hawa Uber watapata wapi hela?
 
Back
Top Bottom