Ubaya wa Muswada wa katiba kama ulivyo?

Topical mimi naunga mkono msingi wa hoja yako kwa asilimia miamoja! Kimsingi watu wamebebwa na mkumbo tu kwamba mswada ni mbaya lakini ukiwataka wabainishe ubaya wake ndo kama hivi wanalete maswali ni misemo ya wahenga! Niliwahi kusema hapa kuwa hawa wanaharakati wanatupotosha watu wakabisha kwa ushabiki, kisa wameshalishwa sumu! Watanzania tuwe makini tusiweke rehani uwezo wetu wa kudadavua mambo yanayotuhusu!
 
Topical mimi naunga mkono msingi wa hoja yako kwa asilimia miamoja! Kimsingi watu wamebebwa na mkumbo tu kwamba mswada ni mbaya lakini ukiwataka wabainishe ubaya wake ndo kama hivi wanalete maswali ni misemo ya wahenga! Niliwahi kusema hapa kuwa hawa wanaharakati wanatupotosha watu wakabisha kwa ushabiki, kisa wameshalishwa sumu! Watanzania tuwe makini tusiweke rehani uwezo wetu wa kudadavua mambo yanayotuhusu!

Umeona aise, ngoja tusubiri watueleza ubaya wa muswada kama ulivyo..

Halafu anaweza kupelekwa barabarani bure kazi kweli kweli..
 
Matatizo ya muswada huu kama ulivyo, samahani kaka nakujibu kwa kutumia akili zako.....

a)Unampa madaraka makubwa rais ambayo tunayapinga muda wote, hata kama kukiwa na bunge la katiba bado utampa rais mamlaka ya mwisho ya kuamua nini kifanyike katika katiba yetu......ambapo hatutaki yeye awe na mamlaka nayo kama mtu binsfsi. (means tunataka taasisi inayojitegemea)
Kumpa mtu mmoja madatraka makubwa hapa mwanzo ni kuharibu mfumo wa kutupatia katiba na katiba yenyewe kabisa.

b)Haimaanishi kwamaba hata kama muswada ni mzuri basi hauna haki ya kwenda kwa wananchi, bado watanzania walikuwa na haki ya kuujadili hata kama ni mzuri kiasi gani.

c)Mswada haujachumbua vyema nafasi ya Tanganyika kama ulivyojidadavu kuhusu Zanzibar. Zanzibar wameweza kujadili mambo yao na wakaafikiana vivyo hivyo na sisi watanganyika pia......muswada ulipaswa kuchambua nafasi ya Zanzibar na Tanganyika kwa usawa. Si kwa vile wewe ni mkubwa basi ukipigwa na mdogo usisema....atleast unamkanya.

d)Haujaainisha vyema jinsi makundi mambilibmali ya kijamiii yatakavyo husika, kwamfana Tz si Dodoma,DSM na Zanzibar.

kama bado hujaelewa dhen ntafute kwa muda wako.......napatikana Kigogo Luhanaga mkuu.
 
Matatizo ya muswada huu kama ulivyo, samahani kaka nakujibu kwa kutumia akili zako.....

a)Unampa madaraka makubwa rais ambayo tunayapinga muda wote, hata kama kukiwa na bunge la katiba bado utampa rais mamlaka ya mwisho ya kuamua nini kifanyike katika katiba yetu......ambapo hatutaki yeye awe na mamlaka nayo kama mtu binsfsi. (means tunataka taasisi inayojitegemea)
Kumpa mtu mmoja madatraka makubwa hapa mwanzo ni kuharibu mfumo wa kutupatia katiba na katiba yenyewe kabisa.

b)Haimaanishi kwamaba hata kama muswada ni mzuri basi hauna haki ya kwenda kwa wananchi, bado watanzania walikuwa na haki ya kuujadili hata kama ni mzuri kiasi gani.

c)Mswada haujachumbua vyema nafasi ya Tanganyika kama ulivyojidadavu kuhusu Zanzibar. Zanzibar wameweza kujadili mambo yao na wakaafikiana vivyo hivyo na sisi watanganyika pia......muswada ulipaswa kuchambua nafasi ya Zanzibar na Tanganyika kwa usawa. Si kwa vile wewe ni mkubwa basi ukipigwa na mdogo usisema....atleast unamkanya.

d)Haujaainisha vyema jinsi makundi mambilibmali ya kijamiii yatakavyo husika, kwamfana Tz si Dodoma,DSM na Zanzibar.

kama bado hujaelewa dhen ntafute kwa muda wako.......napatikana Kigogo Luhanaga mkuu.

a. kama hutaki rais awe na madaraka hayo taasisi hiyo unayosema ni ipi? na itatengenezwa vipi? na itapata mandate kutoka wapi?

b. kujadiliwa na wananchi wote isingewezekana ndio maana tunawawakilishi wa wananchi (bunge)

c. nafasi ya tanganyika, niambie tanganyika inakosa nini muswada ulivyo?? taja mambo mawili tutakayakosa?

d. Hiyo siyo kweli kila taasisi ina haki ya kwenda kwenye tume nakupeleka mapendekezo yake?? (acha uwongo)

Nafikiri una akili sana embu nijibu kidogo hizo concern zangu.
 
Tropical, Mkuu unajua unauliza maswali kama hujui ama unauliza kwa udadisi?.. Hivi nikuulize wewe lini mtumwa asimtumikie bwana wake.... Iliona wapi..Kwa nini sisi wananchi tusitoe jukumu hilo la rais kuunda tume ama bunge ama wote ama taasisi ya katiba ama lolote lile libadilishwe ikiwa yeye rais anafahamu kwamba sisi ndio waajiri wake. Na rais ajaye atalinda kile tulichomkabidhi..

Na labda nikuulize wewe nambie Kiongozi yeyote aliyechaguliwa na rais ambaye sii mwanaCCM, toka NEC, UWT na kwingineko.. Na sababu gani zimetokana na uchaguzi huo?

Pili, nambie tume yeyote ya rais ambayo imeweza kuwakilisha taarifa safi na ikitendewa haki kama ilivyowakilishwa..Hakuna hata hiyo ya Richmond imefukiwa kukidhi maslahi yao waajiri, leo bado unataka wananchi tuwe na imani na muswada ambao tunajua fika kwamba haukidhi mahitaji yetu.

Tatu, Kwa nini ktk ibara ya tatu rais kaweka masharti ktk baadhi ya sehemu ziheshimiwe zisiguswe, yeye nani inapofikia swala la katiba mpya kama sii kutuonyesha kwamba katiba itaundwa kwa mapenzi yake (chama) na sii ya Kitaifa..

Nne, Kwa nini yeye ndiye amchague katibu na sii tume yenyewe kuchagua viongozi na makatibu wake ambao watakuwa huru.. na watawasilisha taarifa ya tume baada ya kumaliza na sio mtu alokuwa karibu naye...

Tano, katika katiba ya taifa kundi la baraza la Mapinduzi haliwezi kuwa exceptional wakati kuna vyama vingi na tumeungana. Haya maswala ya Uuwiano ktk tume hayajengi usawa wa mawazo bali kuridhisha watu. Mfumo ule ule wa kiutawala wa kuleta uuwiano wa waislaam, wakristu, Uzanzibar na Ubara ndio tunataka kuuvunja. Tunataka kuwepo serikali tatu na kaa atachagua tume atahakikisha swala hili haliguswi kama alivyoeleza..Yeye bado anafikiria mawazo ya mgawanyiko kutokana na shinikizo pengine la Baraza la Mapinduzi akini nchi hizi zimeungana na zina vyama vingi.. Baraza la Mapinduzi linaweza kujenga na wazee wa Zanzibar bila kujali wanatoka chama gani..

Kifupi tunataka TUME HURU - Je, tutaipata vipi ndio liwe swali na sii vinginevyo! Soma tena muswada halafu nambie kama hiyo itakuwa tume huru.
 
Mimi jambo moja linalonikera kabisaaaa,
ni kule kutokutafuta maoni kwa wananchi, kutokuwa wazi na taarifa ya maoni machache na yalikotoka. Huo usiri mie ndio unanikatisha tamaa.
Inakuwaje kuwa hapa mwanzoni kabisa, hatupewi taarifa, kwani si haki yetu??
Ni wazi kuwa ukosefu wa imani uliotokana na madhaifu ya uongozi uliopo madarakani unajulikana na kila mtu.
Ni dharau? au they do not feel the weight of responsibility to report everything to us the people?
walimpa nani hio taarifa?
Nilisikia wakisema '... watu na makundi mbalimbali walihojiwa na baadhi ya maoni yao yamejumuishwa...'
Mimi naona hii statement ni kama tunataka kurudi nyuma,
ni uhakika hatutaenda mbele kama kuna watu wenye mentality kama yangu,
Sie wananchi tunataka kuona nguvu yetu juu yao.
Iko wapi?
Kwa matazamo wangu hio ndio tunaipigania.
Mimi binafsi nataka kujua kama hao watu wachache waliohojiwa ni watu ambao naweza sema wanawakilisha kundi langu, ili nipate amani.

Tukija upande wa hotuba tukuka ya Lissu (japo nakubaliana mmoja aliesema body language iliidilute) je ina maana aliosema sio pointi?
Kweli Tanganyika inawezekana kweli tusiwe na HAKI ya kuwa na mambo yetu wenyewe? Hapo mie sielewi kabisa, nadhani kuna jambo wenzangu mnaoona sawa mnabidi kunielewesha, ni kwanini muungano wetu unatuonea?
Ni kwanini mtu mmoja RAIS tayari ameshapanga sehemu za katiba za kujadili na za kutokujadili? bila kutuconvince?
je ana kiapo kingine licha ya lile tunachokijua??
 
VICHEKESHO VINGINE HUHITAJI KWA GENIUS KUONA HUU UTUMBO.!!!!

1. Rais (kwa kushauriana na mwezake wa Znz) ndiye atakaye pendekeza tume ya kukusanya maoni.
2. Rais ndiye atakaye tengeneza hadidu za rejea za tume. (Hairuhusiwi kujadili nje ya hizi hadidu za rejea
na kwa vile tushamsikia akisema mambo kama Muungano, Madaraka ya rais yashawekewa mipaka)
3. Tume ikimaliza kukusanya maoni inarudisha kwa rais ambaye atafanya marekebisho kwa kadri ATAKAVYO ONA INAFAA.
4. Tume ya uchaguzi ndo itasimamia mchakato wa kukusanya maoni. Mwenyekiti ni mteule wa rais
5. Bunge la katiba lina wabunge zaidi ya 2/3 wa CCM ambao kama inavyofahamika wanatumikia chama hence mwenyekiti wake ambaye ni rais.

e.t.c
List unaweza itengeneza ni ndeeeefu sana. HUU NI MZAHA!!!

Mpaka hapo sijui hiyo ni KATIBA ya wananchi au ya RAIS!!!!
 
Huo muswada wenyewe uko wapi? Watu wanajadili hewa tu.
Tunachoelewa sisi ni kwamba muswada uliopo ni ule ule ulokuja mara ya kwanza kwa kiingereza sasa umerudishwa kwa kutafsiriwa tu kuja lugha ya kiswahili kwa sababu hilo lilikuwa moja ya maswala mengi yaliyokataliwa.. Sasa kinachotushanga kulikuwa na vikao kibao ambavyo vimefanyika na vinaendelea kufanyika ktk kuujadili muswada huo na kuuboresha lakini mengi yaliyojadiliwa leo hayana maana tena..
Kwa mfano taarifa ya kikao kama hiki iko wapi Bofya
 
Huo muswada wenyewe uko wapi? Watu wanajadili hewa tu.

Nakushauri uendelee kuutafuta,then uusome, mie sijausoma ila nimeusikia in kwa kifupi wakati wa bunge, tunapoteza wakati na fedha.
Kwa uhakika balaa litaanza pale katiba itakapopita kwa njia hii.
 
Nakushauri uendelee kuutafuta,then uusome, mie sijausoma ila nimeusikia in kwa kifupi
Ndio maana nikasema mko hapa mnajadili hewa tu. Hujausoma? Sasa utajadilije kitu hujakisoma? Na utanambiaje mimi nikausome wakati we mwenyewe hujui unajadili kitu gani kwenye muswada? Wabongo sijui tukoje.

 
Tropical, Mkuu unajua unauliza maswali kama hujui ama unauliza kwa udadisi?.. Hivi nikuulize wewe lini mtumwa asimtumikie bwana wake.... Iliona wapi..Kwa nini sisi wananchi tusitoe jukumu hilo la rais kuunda tume ama bunge ama wote ama taasisi ya katiba ama lolote lile libadilishwe ikiwa yeye rais anafahamu kwamba sisi ndio waajiri wake. Na rais ajaye atalinda kile tulichomkabidhi..

Na labda nikuulize wewe nambie Kiongozi yeyote aliyechaguliwa na rais ambaye sii mwanaCCM, toka NEC, UWT na kwingineko.. Na sababu gani zimetokana na uchaguzi huo?

Pili, nambie tume yeyote ya rais ambayo imeweza kuwakilisha taarifa safi na ikitendewa haki kama ilivyowakilishwa..Hakuna hata hiyo ya Richmond imefukiwa kukidhi maslahi yao waajiri, leo bado unataka wananchi tuwe na imani na muswada ambao tunajua fika kwamba haukidhi mahitaji yetu.

Tatu, Kwa nini ktk ibara ya tatu rais kaweka masharti ktk baadhi ya sehemu ziheshimiwe zisiguswe, yeye nani inapofikia swala la katiba mpya kama sii kutuonyesha kwamba katiba itaundwa kwa mapenzi yake (chama) na sii ya Kitaifa..

Nne, Kwa nini yeye ndiye amchague katibu na sii tume yenyewe kuchagua viongozi na makatibu wake ambao watakuwa huru.. na watawasilisha taarifa ya tume baada ya kumaliza na sio mtu alokuwa karibu naye...

Tano, katika katiba ya taifa kundi la baraza la Mapinduzi haliwezi kuwa exceptional wakati kuna vyama vingi na tumeungana. Haya maswala ya Uuwiano ktk tume hayajengi usawa wa mawazo bali kuridhisha watu. Mfumo ule ule wa kiutawala wa kuleta uuwiano wa waislaam, wakristu, Uzanzibar na Ubara ndio tunataka kuuvunja. Tunataka kuwepo serikali tatu na kaa atachagua tume atahakikisha swala hili haliguswi kama alivyoeleza..Yeye bado anafikiria mawazo ya mgawanyiko kutokana na shinikizo pengine la Baraza la Mapinduzi akini nchi hizi zimeungana na zina vyama vingi.. Baraza la Mapinduzi linaweza kujenga na wazee wa Zanzibar bila kujali wanatoka chama gani..

Kifupi tunataka TUME HURU - Je, tutaipata vipi ndio liwe swali na sii vinginevyo! Soma tena muswada halafu nambie kama hiyo itakuwa tume huru.

Mkuu shukran kwakuwa ni wewe pekee ndiye uliyeweza kunielewesha..

Moja: wananchi watapataje wajumbe wa tume (utaratibu gani) ambao utakidhi mahitaji ya kila mtanzania asilalamike? utaratibu gani utumike? besides urais ambayo itaepuka biaseness i.e. mtumwa na mtwana unayoisema??

Mbili: Hoja yako ya pili inatokana na historia ya tume kutofanya vizuri inaweza kutosha kuwa sababu maana itaonekana kama unazugumzia wakati ujao..itatokea?? kwanini tusimpe rais benefit of dought

tatu: Hilo la masharti ni kero kubwa sana, kuweka mipaka ya mijadala ni tatizo la msingi ambalo linahitaji kelele za kutosha tuko pamoja..

nne: Hilo la uteuzi linaendena na hoja ya kwanza system gani unafikiri ni bora kwa mazingara yetu, nionavyo mimi ukikubali kupeleka bungeni ni tabu tupu, ukifanya kutangaza ili watu waombe process nzima itakuwa corrupt na system nzima wanaweza kuwonga hata nape au tambwe akawa katibu ...

tano: hiyo tano sijakuelewa kwa zanziba kwenye, muungano lazima iwe na iko say kama nchi..bila kujali ukubwa wake.. (acha uwongo) sheria kama ilivyo inakataza watu kuvunja muungano lakini inaruhusu kuongelea muungano ikiwemo muundo wa serikali tatu ambao CUF na Chadema wako na proposal hiyo nafikiri ultimately tutakuwa na serikali tatu..

Mkuu TUME HURU ni very subjective term tusema at least fair representation...
 
VICHEKESHO VINGINE HUHITAJI KWA GENIUS KUONA HUU UTUMBO.!!!!

1. Rais (kwa kushauriana na mwezake wa Znz) ndiye atakaye pendekeza tume ya kukusanya maoni.
2. Rais ndiye atakaye tengeneza hadidu za rejea za tume. (Hairuhusiwi kujadili nje ya hizi hadidu za rejea
na kwa vile tushamsikia akisema mambo kama Muungano, Madaraka ya rais yashawekewa mipaka)
3. Tume ikimaliza kukusanya maoni inarudisha kwa rais ambaye atafanya marekebisho kwa kadri ATAKAVYO ONA INAFAA.
4. Tume ya uchaguzi ndo itasimamia mchakato wa kukusanya maoni. Mwenyekiti ni mteule wa rais
5. Bunge la katiba lina wabunge zaidi ya 2/3 wa CCM ambao kama inavyofahamika wanatumikia chama hence mwenyekiti wake ambaye ni rais.

e.t.c
List unaweza itengeneza ni ndeeeefu sana. HUU NI MZAHA!!!

Mpaka hapo sijui hiyo ni KATIBA ya wananchi au ya RAIS!!!!

Kwanza umesahau kuwa rais ni taasisi siyo mtu??

Pili hujatoa unafikiri alternatives ni ipi? maana kila alternatives ina weaknesses zake..
 
ndio maana nikasema mko hapa mnajadili hewa tu. Hujausoma? Sasa utajadilije kitu hujakisoma? Na utanambiaje mimi nikausome wakati we mwenyewe hujui unajadili kitu gani kwenye muswada? Wabongo sijui tukoje.

pls quote sentensi nzimaaaaaaaa
mie siko kwenye huo umbea na kutwist maneno ya watu,

tafadhali kabisa

tafadhali kaka/dada
kama wewe ni msomi unajua namna ya kusoma na kuelewa vitu kama mswada umejadiliwa bungeni kipengele kwa kipengele, siruhusiwi kuwa na moani kuhusu hilo? Wewe umeuona mzuri, na umeridhika, inakuwaje mimi siruhusiwi kutokuridhika?
na kama umesoma post yangu ya nyum autajua concerns zangu kuhusu mswada, zinaweza usikubaliane nazo, basi tujadiliane hayo, najua kuna mambo mengi ya kisheria siwezi kuyachambua, ila kwa ufahamu wangu ndio nilieleza hapo nyuma, please pitia
 
naomba nieleweshe wewe uliyona kasoro zake say a, b, c, d...na pengine ulitaka iwekwe nini badili yake?

Wewe kama kichwa kibovu kitaendelea kuwa kibovu tu! Mchakato mzima unaonesha kuwa Katiba itakayoundwa ni "Katiba ya Rais" na si ya wananchi!
1. Wajumbe wa Tume ya Kukusanya maoni ni wateuliwa wa Rais,
2. Hadidu za rejea wanapewa na Rais,
3. Maoni yakishakusanywa anapelekewa Rais ambaye kwa mujibu wa Katiba iliyopo "halazimiki" kufuata ushauri wa mtu yeyote,
4. Tume isiyo huru ya Taifa ya uchaguzi ambaye Mwenyekiti wake ndiye mteule wa Rais, itasimamia zoezi zima la kura za maoni,
5. Baadhi ya masuala kutojadiliwa ni matakwa ya wananchi au matakwa ya Rais?
Kwa ujumla JK anataka kututungia Katiba na sio kuturuhusu wananchi kutunga Katiba iliyo na ridhaa ya kweli ya wananchi! Ndio maana wananchi wanapotaka kuandamana kupinga Muswada wanaambulia moshi wa mabomu ya machozi! Sasa kama huko si kulazimishana ni nini?
 
3. Nimesema tukiacha malumbano ya kusomwa mara ya kwanza na ya pili maana nataka nifahamu tatizo la muswada kama ulivyo una shida gani kwa wananchi kupata katiba nzuri??

Kwa vile kanuni inataka mswada usomwe mara ya kwanza na mara ya pili, kwa nini serikali ivunje kanuni hiyo? Je raia nao tukivunja shera za nchi kwa makusudi kama serikali inavyofanya itakuwaje?
 
Kwa vile kanuni inataka mswada usomwe mara ya kwanza na mara ya pili, kwa nini serikali ivunje kanuni hiyo? Je raia nao tukivunja shera za nchi kwa makusudi kama serikali inavyofanya itakuwaje?

Ebana ile kesi yako dhidi ya Msekwa imefikia wapi?
 
topical hawawezi kukuonesha wala kukupa mfano wote wanafata mkumbo,bila kujua chochote.Kisa kasema kiongozi wooooote wanafata bila kuhoji
 
Tunachoelewa sisi ni kwamba muswada uliopo ni ule ule ulokuja mara ya kwanza kwa
Tunachoelewa sisi? Wewe na nani, jiongelee mwenyewe. Tunaenda na facts, sio "tunachoelewa sisi." Watu hawafungui muswada badala yake wanajadili makisio ya kubahatisha bahatisha tu.

...mie siko kwenye huo umbea na kutwist maneno ya watu... tafadhali kabisa tafadhali kaka/dada... kama wewe ni msomi unajua namna ya kusoma na kuelewa
Utanipaje lecture ya kujua kusoma na kuelewa wakati wewe mwenyewe umekiri muswada hujausoma? Kituko kikubwa sana. Na huwezi kusema nina "twist maneno ya watu," kuna rekodi ya kila maneno ya mtu hapa, uta twist vipi?

Unapinga kilichomo kwenye muswada, kuna nini kwenye muswada, hujui! Ndio kujadili hewa huko! Hebu eleza unapinga sehemu gani ya muswada na inasema nini, kama unajua unachokipinga.


Nakushauri uendelee kuutafuta,then uusome, mie sijausoma ila nimeusikia in kwa kifupi
 
Back
Top Bottom