Ubabe wa Clouds FM uangaliwe

Ubabe wa Clouds FM uangaliwe

Kwani we una bifu na clouds fm.? hapo sijaona ubabe uliotumika au nimeelewa vibaya mkuu
 
Na Gardena G Habash nae kapotea baada ya kurudi Clouds
 
unamaanisha huyo P.J ni mtoto mdogo hajielewi mpaka anyanyaswe alafu abaki kimya tu namna hii??
 
Acha kudanganya watu we jamaa, nitakubaliana na wewe kwa upande mmoja tu wa wasanii, ni kweli inawanyonga vibaya, ila kwa watangazaji clouds inawalipa vizuri mno usipotoshe
 
Mkuu huyo Jamaa ni ' Mwanangu ' sana tena tokea Mwananyamala enzi hizo na nimeandika hayo kwa ' masikitiko ' makubwa mno huwezi amini Mtu wangu. Na hatari zaidi ' akishalanduka ' tu basi ghafla hapo hapo anageuka ' ngumi jiwe / mgomvi ' sema uzuri wake hata ' Ugomvi ' nao anaujua vile vile kutokana na kwamba ni Mtoto wa Kisela sana halafu alishafanya ' matukio ' makubwa na ya kutisha sana pande za Mwananyamala na najua wapo humu Watu wa Mwananyamala wanaomjua ' Kindakindaki ' pia.

Narudia tena kusema na kusisitiza kuwa japo ana hayo ' mapungufu ' yake yote ila ' Jamaa ' ana ' Vipaji ' vingi sana na ni ' Mbunifu ' mno kiasi kwamba kama akipata Mshauri / Kiongozi / Msimamizi mzuri sisi Wasikilizaji wa Redio tutafaidika nae sana. Ushawishi wake mbele ya Jamii hasa ya Vijana ni kubwa mno. Personally namkubali kinomanoma!

Ha ha Haaa mkuu kweli unamjua.. Huyu ni msela mavi haswaa.. Anatusumbua Sana huku mwananyamala..
 
ila kwa kicheko roho inaniuma sana sababu alishakua na utambulisho wake wa singeri sasa kule amefunikwa kabisa..
kicheko alinifanya nikapenda kipindi cha genge.kuna kipindi alikuwa anaweka nyimbo cha kiingereza anajifanya kutafsiri ahaha fix tupu ilikuwa kicheko balaa
 
Kwani wamehama kwa kulazimishwa?
Hakuna aliyeshikiwa silaha siwaondoke?
 
Ndio kosa wafanyalo hao watu hawataki jijengea jina wao wanataka hela tu
 
Tatizo la clouds wanapenda kuchukua watangazaji mahiri ila wawe kwao,lakini wakishawachukua wanakuwa hawana muda wa hewani wa kuwapa,kwahyo hapo lazima uwe unaua kipaji.
 
Ubabe uko wapi apo sasa alfu kumbuka msemo wa mm hapa mhenga kma huna pesa huna haki
 
Wahenga walisema;

"Kama hauwezi kupambana nao ungana nao"
 
Back
Top Bottom