Ubabe wa Clouds FM uangaliwe

Ubabe wa Clouds FM uangaliwe

Sasa hapo wa kulaumiwa nani? Clouds au Watangazaji wenyewe

Hata mimi nimejiuliza, utafikiri wanapigwa bakora waende Clouds... huyu mmmmh ana lake na ni kauchochezi ambako hakana miguu wala kichwa.
 
Kwa avatar yako duh unaonyesha upo kwenye mambo ya muziki, si uende uongee nao na wewe upate maarifa au!? Inaonyesha umekaa ukaona uje uwaharibie humu kumbe ndio umesaidia kuwapa promo haswaaa ya kuwa keanini hao wote eapende kujiunga na Clouds na wala hawakubebwa au kutekwa kwenda kuwafanyia kazi

Lengo lako limepiga chini, uko ulipo jiongezeni tu muendelee kushindana huku mkituburudisha sisi wananchi.
 
Habari wakuu,

kiukweli nimekua mdau wa media kwa muda sana na kujua mazuri na mabaya ya baadhi ya media.

Leo acha niongelee hii redio clouds fm juu ya mambo wanayoyafanya ambayo ni kama vitendo vya kikatili.

Mwanzoni wasanii wengi walikua wanailalamikia redio hiyo kuwa ndio wanaowadhurumu kazi zao na mapato yao kwa kuwapa masharti magumu ambayo mwisho wa siku yanawakandamiza wasanii na hatimaye kujikuta kuishia masikini na kutonufaika na kazi zao za kisanii.

Kikubwa zaidi ni hiki cha kuingilia tasnia ya utangazaji, ambapo mwanzoni wakati huo kuna mtangazaji anafahamika kwa jina la paul james "p.j" ambaye ni moja kati ya watangazaji mahili na wenye weledi katika tasnia ya habari, lakini wakati fulani alihama redio hiyo na kuhamia e f.m redio ambapo aliambatana na mtangazaji mwenzake "gerald hando" ambapo walifanya kazi nzuri sana na kufanya kipindi walichotangaza kuwa moja kati ya vipindi pendwa vya asubuhi.

Lakini hawa clouds fm wakafanya ya kufanya wakamrudisha clouds fm p.j lakini hakupewa hadhi kama ile aliyokuwa nayo awali kabla hajahama na hii kumfanya mtangazaji huyo kushuka thamani kwa sasa.

Vilevile e f.m ilikua na mtangazaji wake mahili sana hasa katika kipindi cha genge ambacho alivuma sana na aina ya mziki wa singeri ambapo mtangazaji huyo alijulikana kwa jina la kicheko, kama haitoshi clouds fm wakafanya ya kufanya na hatimaye kumnyakua kicheko na uhamisho wake ulivunja record ambayo haijawahi kutokea kwani alisindikizwa na bodaboda takribani 150, pamoja na kuwa na thamani kubwa alipokua e f.m lakini alipotua clouds fm hakupewa thamani ile ambayo alistahili kwni akawa anapewa segment ndogo sana na kuna wakati huwa hasikiki kabisa..

Sasa hii imejidhihirisha kuwa hawa clouds fm wapo kwaajili ya kuua vipaji na sio kuendeleza....
Sasa tatizo ni nn ? Kwani wamelazimishwa kuendelea kufanya kazi ? Ujui kuwa ni soko huria ? Maelezo mengi lakini hamna kitu
 
Watu wengine bhana wanafurahisha
Wanasikitisha
Wanahuzunisha na kushangaza pia,
Hivi mkuu kiuhalisia kutokana na Thread yako ubaya wa Clouds uko wapi? Hao watangazaji walishikiwa viboko na bastola hili waje wasain kufanya kazi clouds? Unawazidi akili hao wahusika wenyewe walioamua kufanyapo kazi? Halafu badala ya kuwa na hoja nzuri unashabikia na kuhamasisha Watu wasikilize EAradio na Efm what for? Komaa na radio zako unazozipenda na sisi tunaoielewa clouds tutaendelea nayo, nani hajui mchango wa clouds katika kuinua na kuwafaidisha wasanii na kupata ajira mbali mbali kwa vijana? Japo wana mapungufu yao make clouds inaendeshwa na binadamu isitoshe wanadamu hatujakamilika, ebu wanapofanya mazuri wape credit zao na wanapokosea waambie pia, sisi ngoja tuendelee kupasua mawingu.
TUNAKUFUNGULIA DUNIA KUWA UNACHOTAKA
KAMATA FURSA TWENDE ZETU
HII NDO THE PEOPLE'S STATION.
 
Mtoa mada subil nikwambie hakuna mtangazaji Tz atakayekataa kwenda clouds!. Pamoj na mapungufu yao ila ndo media inayoongoza kuwalipa vizuri wafanyakazi wao na inawapa nafasi bila kuwabanabana wafanyakazi wao hasa kwenye shughuli zao binafsi mfano mirad ayo anauwezo wakuitangaza brog yake kupitia kipindi chake na hakuna tatizo lakini kitu hichohicho huwezi kukifanya kwenye radio nyingine Tanzania hii..
 
yah ni kweli..ila ndo naona umuhimu wa mikataba..kama wangekua namikataba wasingezungushwa zungushwa
Unajua watangazaji na madjs wanapenda kwenda clouds kwakuwa inawapa fursa za kufanya mambo mengine huku wakiwapa support.
Yani mtangazaji au dj anakuwa na uwezo wa kuja na idea yake na akaifanyia kazi.
Mfano soudy brown na mwenzake idea yao ya ubuyu, umekuwa mashuhuri kwasababu wanautangaza bure kupitia clouds na watakuwa wanapiga ela kweli kweli maana wana mawakala almost kila mkoa.
Bado tour wanazofanya hawabanwi kitu kinacho wafanya hata wengine watamani kujiunga clouds.
Yani watangazaji wa kila kipindi utakuta wanajitahidi waandae kitu ambacho kitawawezesha wapige tour na kuandaa show za nje waingize mkwanja.
Mwisho wa siku kila mtu anaangalia maslahi yake dogo janja anakwambia kwa sasa anapambana kutetea maisha sio hip hop hivyo hivyo kwa kila mtu anapambana apate maslahi sio jina tu.
 
yani wakiona mtu kang'aa tu lazma wamchukue inshort wanataka wawe juu daily
Sasa kwani hilo ni kosa? Ni sawa na mpira tu mwenye kisu kikari anabeba wachezaji wazuri.
Mbona efm waliwachukua akina hando japo waliweza mrudisha mmoja lakini hakuna aliyesema lilikuwa kosa.
Na ukifuatilia utakuta watangazaji wengi na.madjs waliotoka redio nyingine wao ndiyo walikuwa wa kwanza kumuomba ruge kuja clouds.
 
Back
Top Bottom