Uandaaji wa filamu ya Royal Tour tumepigwa lakini uzinduzi wake tunapigwa zaidi!

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,797
12,239
Sijui viongozi wetu wanawaza nini lakini kwa kifupi ama wamepotoka au wanapotoshwa. Filamu ya aina ya Royal Tour si ya kwanza kuandaliwa duniani, ndugu zetu wa Rwanda walikwisha iandaa na imekwisha tazamwa sana. Sasa sijui kama viongozi wetu walikwisha fanya research ndogo tu kuona imeinufaishaje Rwanda. Manufaa ambayo kama Rwanda imepata basi yasingeweza kuwa siri ya ndani ya Rwanda bali pia spill over tungezipata hapa Tanzania au nchi nyingine za jirani.

Kitu cha kuzingatia ni kuwa wazo la kuandaa filamu hizi si la kwetu bali la hao wenye kumiliki uchumi lakini gharama ni za kwetu. Siyo siri katika kujenga uchumi wa nchi hakuna rafiki bali mwenye nguvu ndiye hushinda na kufaidi. Akili mu kichwa! Walio andaa wamefanikisha malengo yao bila jasho na kwa gharama nafuu.

Uzinduzi wa Royal Tour umekuwa balaa zaidi kwa hazina ya nchi! Rais wa nchi akiwa na wapambe wapatao 50 wamekaa zaidi ya wiki mbili nchini Marekani kufanya uzinduzi wa filamu hii kwa gharama za Watanzania walipa kodi. Wamarekani wamenufaika kwa kutembelewa na watalii kutoka Tanzania. Big brain amenufaika!

Kama hiyo haitoshi sasa uzinduzi utafanyika tena Tanzania kwa kodi zetu. Uzinduzi utafanyika Arusha, Zanzibar na Dar es Salaam. Tena washiriki watakuwa wengi zaidi! Haya ni matumizi mabaya ya fedha za umma! Tumepigwa!

Tujisahihishe!
 
Umeniwahi, nilikua naanda mada niliyotaka kusema bado uwazi ni tatizo chini ya serikali hii ya CCM.
Wameenda kundi kubwa la watu, wamekaa wiki mbili na hakuna anayejua wametumia gharama kiasi gani
Tatizo kubwa lilipo sasa Ni kuwa pesa inatumika kununua waandishi kuandika mazuri. Wakati uliopita nguvu ilitumika kuwafanya waandishi waandike mazuri
Pesa vs nguvu, Ila lengo ni moja
 
Sijui viongozi wetu wanawaza nini lakini kwa kifupi ama wamepotoka au wanapotoshwa. Filamu ya aina ya Royal Tour si ya kwanza kuandaliwa duniani, ndugu zetu wa Rwanda walikwisha iandaa na imekwisha tazamwa sana. Sasa sijui kama viongozi wetu walikwisha fanya research ndogo tu kuona imeinufaishaje Rwanda. Manufaa ambayo kama Rwanda imepata basi yasingeweza kuwa siri ya ndani ya Rwanda bali pia spill over tungezipata hapa Tanzania au nchi nyingine za jirani.

Kitu cha kuzingatia ni kuwa wazo la kuandaa filamu hizi si la kwetu bali la hao wenye kumiliki uchumi lakini gharama ni za kwetu. Siyo siri katika kujenga uchumi wa nchi hakuna rafiki bali mwenye nguvu ndiye hushinda na kufaidi. Akili mu kichwa! Walio andaa wamefanikisha malengo yao bila jasho na kwa gharama nafuu.

Uzinduzi wa Royal Tour umekuwa balaa zaidi kwa hazina ya nchi! Rais wa nchi akiwa na wapambe wapatao 50 wamekaa zaidi ya wiki mbili nchini Marekani kufanya uzinduzi wa filamu hii kwa gharama za Watanzania walipa kodi. Wamarekani wamenufaika kwa kutembelewa na watalii kutoka Tanzania. Big brain amenufaika!

Kama hiyo haitoshi sasa uzinduzi utafanyika tena Tanzania kwa kodi zetu. Uzinduzi utafanyika Arusha, Zanzibar na Dar es Salaam. Tena washiriki watakuwa wengi zaidi! Haya ni matumizi mabaya ya fedha za umma! Tumepigwa!

Tujisahihishe!
Umejaa wivu tu
 
Sijui viongozi wetu wanawaza nini lakini kwa kifupi ama wamepotoka au wanapotoshwa. Filamu ya aina ya Royal Tour si ya kwanza kuandaliwa duniani, ndugu zetu wa Rwanda walikwisha iandaa na imekwisha tazamwa sana. Sasa sijui kama viongozi wetu walikwisha fanya research ndogo tu kuona imeinufaishaje Rwanda. Manufaa ambayo kama Rwanda imepata basi yasingeweza kuwa siri ya ndani ya Rwanda bali pia spill over tungezipata hapa Tanzania au nchi nyingine za jirani.

Kitu cha kuzingatia ni kuwa wazo la kuandaa filamu hizi si la kwetu bali la hao wenye kumiliki uchumi lakini gharama ni za kwetu. Siyo siri katika kujenga uchumi wa nchi hakuna rafiki bali mwenye nguvu ndiye hushinda na kufaidi. Akili mu kichwa! Walio andaa wamefanikisha malengo yao bila jasho na kwa gharama nafuu.

Uzinduzi wa Royal Tour umekuwa balaa zaidi kwa hazina ya nchi! Rais wa nchi akiwa na wapambe wapatao 50 wamekaa zaidi ya wiki mbili nchini Marekani kufanya uzinduzi wa filamu hii kwa gharama za Watanzania walipa kodi. Wamarekani wamenufaika kwa kutembelewa na watalii kutoka Tanzania. Big brain amenufaika!

Kama hiyo haitoshi sasa uzinduzi utafanyika tena Tanzania kwa kodi zetu. Uzinduzi utafanyika Arusha, Zanzibar na Dar es Salaam. Tena washiriki watakuwa wengi zaidi! Haya ni matumizi mabaya ya fedha za umma! Tumepigwa!

Tujisahihishe!
Kwanza hongera sana umejitahidi kutoa ufafanuzi wako kwenye filamu ya Royal Tour, lakini niseme tu andika lako limejaa hisia sana (subjective) kuliko kuunda hoja zenye mashiko (objective) ili kubainisha uzito na ukweli wa hoja zako.

Kwanza kabisa: Hadi uamuzi wa kurusha Royal Tour kufikiwa kufanyika Amazon, watu wanatazama data, Amazon mwaka 2021 ilikuwa na Subcribers 200 milioni duniani zote, ambapo siku nne zilizopita Netflix wana watumiaji 221 milion, unaweza kuona kuona tofauti ni ndogo tu.

Hata hivyo, watu wanahama kutoka kwenye traditional media kama Televisheni kuhamia kwenye matumizi ya internet, hivyo kuiweka Amazoni ni rahisi zaidi watu kutazama kupitia simu janja kuliko National Georaphic and Animal Planet kama unavyosema.

Pili: Rais Samia ni maarufu zaidi unavyodhani, hata hivyo, Royal Tour kuja Tanzania ni kwa sababu ya Rais Samia Suluhu. Unadhani kama angekuwa Magufuli Peter Greeneberg angekuja?

Umaarufu wa Rais Samia Suluhu kwanza umeletwa na umaarufu wa Tanzania wakati wa Hayati Magufuli, dunia ilifuatilia hasa siasa za Tanzania na hata Magufuli alipofariki Tanzania ikawa maarufu zaidi na hata Rais aliyefuata akawa maarufu maradufu kwani ni mara ya kwanza, kwa Tanzania kuwa na Rais wa kwanza mwanamke.

Rais Samia Suluhu amekuwa maarufu baada ya kuhutubia Baraza la Umoja wa Mataifa 2021. Rais Samia pia ameingia katika rekodi ya wanawake 100 wenye ushawishi Duniani 2021 katika Jariba la Forbes.

Rais Samia hakuwa na ulazima wa kushika kila taarifa, lengo la filamu ni kuonesha zaidi mandhari na uzuri wa nchi. Rais ni tour guide kwenye ile movie, na kumtumia Rais kuwa tour guide ni kichochoe tu watu wengi duniani wafuatilie, ila sio kutegemea Rais awe packed na kila taarifa ya Mbuga na mnyama, ingeboa. Ndio maana, filamu ilikuwa na shots kali mwanzo mwisho, na most of time, Peter aliingiza sauti mwenyewe.

Peter Greenberg hajaanza na Rwanda kama unavyosema, soma hapa; "He also produces and hosts a television series called The Royal Tour which airs on PBS. The series features various heads of state giving Greenberg and viewers a personal tour of their country. It has featured a number of world leaders including New Zealand's Helen Clark, Israel's Benjamin Netanyahu, Abdullah II of Jordan, Peru's Alejandro Toledo, Mexico's Felipe Calderón, Rwanda's Paul Kagame, Poland's Mateusz Morawiecki and Tanzania's Samia Suluhu Hassan. Greenberg was previously the Travel Channel's chief correspondent."

Filamu ya Royal Tour tayari kabla ya kutoka, ilishavuta watalii wengi, zaidi ya 600 kutoka Israeli, zaidi ya 200 kutoka France na nchi nyingine za Ulaya.
 
Sijui viongozi wetu wanawaza nini lakini kwa kifupi ama wamepotoka au wanapotoshwa. Filamu ya aina ya Royal Tour si ya kwanza kuandaliwa duniani, ndugu zetu wa Rwanda walikwisha iandaa na imekwisha tazamwa sana. Sasa sijui kama viongozi wetu walikwisha fanya research ndogo tu kuona imeinufaishaje Rwanda. Manufaa ambayo kama Rwanda imepata basi yasingeweza kuwa siri ya ndani ya Rwanda bali pia spill over tungezipata hapa Tanzania au nchi nyingine za jirani.

Kitu cha kuzingatia ni kuwa wazo la kuandaa filamu hizi si la kwetu bali la hao wenye kumiliki uchumi lakini gharama ni za kwetu. Siyo siri katika kujenga uchumi wa nchi hakuna rafiki bali mwenye nguvu ndiye hushinda na kufaidi. Akili mu kichwa! Walio andaa wamefanikisha malengo yao bila jasho na kwa gharama nafuu.

Uzinduzi wa Royal Tour umekuwa balaa zaidi kwa hazina ya nchi! Rais wa nchi akiwa na wapambe wapatao 50 wamekaa zaidi ya wiki mbili nchini Marekani kufanya uzinduzi wa filamu hii kwa gharama za Watanzania walipa kodi. Wamarekani wamenufaika kwa kutembelewa na watalii kutoka Tanzania. Big brain amenufaika!

Kama hiyo haitoshi sasa uzinduzi utafanyika tena Tanzania kwa kodi zetu. Uzinduzi utafanyika Arusha, Zanzibar na Dar es Salaam. Tena washiriki watakuwa wengi zaidi! Haya ni matumizi mabaya ya fedha za umma! Tumepigwa!

Tujisahihishe!
Tupe uthibitisho wa kuwa tumepigwa?
Unajua faida ya hiyo filamu? Umefanya analysis?
 
Kwanza hongera sana umejitahidi kutoa ufafanuzi wako kwenye filamu ya Royal Tour, lakini niseme tu andika lako limejaa hisia sana (subjective) kuliko kuunda hoja zenye mashiko (objective) ili kubainisha uzito na ukweli wa hoja zako.

Kwanza kabisa: Hadi uamuzi wa kurusha Royal Tour kufikiwa kufanyika Amazon, watu wanatazama data, Amazon mwaka 2021 ilikuwa na Subcribers 200 milioni duniani zote, ambapo siku nne zilizopita Netflix wana watumiaji 221 milion, unaweza kuona kuona tofauti ni ndogo tu.

Hata hivyo, watu wanahama kutoka kwenye traditional media kama Televisheni kuhamia kwenye matumizi ya internet, hivyo kuiweka Amazoni ni rahisi zaidi watu kutazama kupitia simu janja kuliko National Georaphic and Animal Planet kama unavyosema.

Pili: Rais Samia ni maarufu zaidi unavyodhani, hata hivyo, Royal Tour kuja Tanzania ni kwa sababu ya Rais Samia Suluhu. Unadhani kama angekuwa Magufuli Peter Greeneberg angekuja?

Umaarufu wa Rais Samia Suluhu kwanza umeletwa na umaarufu wa Tanzania wakati wa Hayati Magufuli, dunia ilifuatilia hasa siasa za Tanzania na hata Magufuli alipofariki Tanzania ikawa maarufu zaidi na hata Rais aliyefuata akawa maarufu maradufu kwani ni mara ya kwanza, kwa Tanzania kuwa na Rais wa kwanza mwanamke.

Rais Samia Suluhu amekuwa maarufu baada ya kuhutubia Baraza la Umoja wa Mataifa 2021. Rais Samia pia ameingia katika rekodi ya wanawake 100 wenye ushawishi Duniani 2021 katika Jariba la Forbes.

Rais Samia hakuwa na ulazima wa kushika kila taarifa, lengo la filamu ni kuonesha zaidi mandhari na uzuri wa nchi. Rais ni tour guide kwenye ile movie, na kumtumia Rais kuwa tour guide ni kichochoe tu watu wengi duniani wafuatilie, ila sio kutegemea Rais awe packed na kila taarifa ya Mbuga na mnyama, ingeboa. Ndio maana, filamu ilikuwa na shots kali mwanzo mwisho, na most of time, Peter aliingiza sauti mwenyewe.

Peter Greenberg hajaanza na Rwanda kama unavyosema, soma hapa; "He also produces and hosts a television series called The Royal Tour which airs on PBS. The series features various heads of state giving Greenberg and viewers a personal tour of their country. It has featured a number of world leaders including New Zealand's Helen Clark, Israel's Benjamin Netanyahu, Abdullah II of Jordan, Peru's Alejandro Toledo, Mexico's Felipe Calderón, Rwanda's Paul Kagame, Poland's Mateusz Morawiecki and Tanzania's Samia Suluhu Hassan. Greenberg was previously the Travel Channel's chief correspondent."

Filamu ya Royal Tour tayari kabla ya kutoka, ilishavuta watalii wengi, zaidi ya 600 kutoka Israeli, zaidi ya 200 kutoka France na nchi nyingine za Ulaya.
Umemaliza kila kitu
 
  • Thanks
Reactions: BRN
Kwanza hongera sana umejitahidi kutoa ufafanuzi wako kwenye filamu ya Royal Tour, lakini niseme tu andika lako limejaa hisia sana (subjective) kuliko kuunda hoja zenye mashiko (objective) ili kubainisha uzito na ukweli wa hoja zako.

Kwanza kabisa: Hadi uamuzi wa kurusha Royal Tour kufikiwa kufanyika Amazon, watu wanatazama data, Amazon mwaka 2021 ilikuwa na Subcribers 200 milioni duniani zote, ambapo siku nne zilizopita Netflix wana watumiaji 221 milion, unaweza kuona kuona tofauti ni ndogo tu.

Hata hivyo, watu wanahama kutoka kwenye traditional media kama Televisheni kuhamia kwenye matumizi ya internet, hivyo kuiweka Amazoni ni rahisi zaidi watu kutazama kupitia simu janja kuliko National Georaphic and Animal Planet kama unavyosema.

Pili: Rais Samia ni maarufu zaidi unavyodhani, hata hivyo, Royal Tour kuja Tanzania ni kwa sababu ya Rais Samia Suluhu. Unadhani kama angekuwa Magufuli Peter Greeneberg angekuja?

Umaarufu wa Rais Samia Suluhu kwanza umeletwa na umaarufu wa Tanzania wakati wa Hayati Magufuli, dunia ilifuatilia hasa siasa za Tanzania na hata Magufuli alipofariki Tanzania ikawa maarufu zaidi na hata Rais aliyefuata akawa maarufu maradufu kwani ni mara ya kwanza, kwa Tanzania kuwa na Rais wa kwanza mwanamke.

Rais Samia Suluhu amekuwa maarufu baada ya kuhutubia Baraza la Umoja wa Mataifa 2021. Rais Samia pia ameingia katika rekodi ya wanawake 100 wenye ushawishi Duniani 2021 katika Jariba la Forbes.

Rais Samia hakuwa na ulazima wa kushika kila taarifa, lengo la filamu ni kuonesha zaidi mandhari na uzuri wa nchi. Rais ni tour guide kwenye ile movie, na kumtumia Rais kuwa tour guide ni kichochoe tu watu wengi duniani wafuatilie, ila sio kutegemea Rais awe packed na kila taarifa ya Mbuga na mnyama, ingeboa. Ndio maana, filamu ilikuwa na shots kali mwanzo mwisho, na most of time, Peter aliingiza sauti mwenyewe.

Peter Greenberg hajaanza na Rwanda kama unavyosema, soma hapa; "He also produces and hosts a television series called The Royal Tour which airs on PBS. The series features various heads of state giving Greenberg and viewers a personal tour of their country. It has featured a number of world leaders including New Zealand's Helen Clark, Israel's Benjamin Netanyahu, Abdullah II of Jordan, Peru's Alejandro Toledo, Mexico's Felipe Calderón, Rwanda's Paul Kagame, Poland's Mateusz Morawiecki and Tanzania's Samia Suluhu Hassan. Greenberg was previously the Travel Channel's chief correspondent."

Filamu ya Royal Tour tayari kabla ya kutoka, ilishavuta watalii wengi, zaidi ya 600 kutoka Israeli, zaidi ya 200 kutoka France na nchi nyingine za Ulaya.
Nashukuru kwa maelezo yako marefu lakini kuweka rekodi sawa watalii kutoka Israel na France siyo matunda ya Royal Tour kwa sababu wamekuja hata kabla ya uzinduzi na pia wengi walishakuja kabla!
 
Sijui viongozi wetu wanawaza nini lakini kwa kifupi ama wamepotoka au wanapotoshwa. Filamu ya aina ya Royal Tour si ya kwanza kuandaliwa duniani, ndugu zetu wa Rwanda walikwisha iandaa na imekwisha tazamwa sana. Sasa sijui kama viongozi wetu walikwisha fanya research ndogo tu kuona imeinufaishaje Rwanda. Manufaa ambayo kama Rwanda imepata basi yasingeweza kuwa siri ya ndani ya Rwanda bali pia spill over tungezipata hapa Tanzania au nchi nyingine za jirani.

Kitu cha kuzingatia ni kuwa wazo la kuandaa filamu hizi si la kwetu bali la hao wenye kumiliki uchumi lakini gharama ni za kwetu. Siyo siri katika kujenga uchumi wa nchi hakuna rafiki bali mwenye nguvu ndiye hushinda na kufaidi. Akili mu kichwa! Walio andaa wamefanikisha malengo yao bila jasho na kwa gharama nafuu.

Uzinduzi wa Royal Tour umekuwa balaa zaidi kwa hazina ya nchi! Rais wa nchi akiwa na wapambe wapatao 50 wamekaa zaidi ya wiki mbili nchini Marekani kufanya uzinduzi wa filamu hii kwa gharama za Watanzania walipa kodi. Wamarekani wamenufaika kwa kutembelewa na watalii kutoka Tanzania. Big brain amenufaika!

Kama hiyo haitoshi sasa uzinduzi utafanyika tena Tanzania kwa kodi zetu. Uzinduzi utafanyika Arusha, Zanzibar na Dar es Salaam. Tena washiriki watakuwa wengi zaidi! Haya ni matumizi mabaya ya fedha za umma! Tumepigwa!

Tujisahihishe!
Tuwe na subira ya kuona matokeo ya filamu hii katika sekta ya utalii, muda ni hakimu mzuri.
 
Kwanza hongera sana umejitahidi kutoa ufafanuzi wako kwenye filamu ya Royal Tour, lakini niseme tu andika lako limejaa hisia sana (subjective) kuliko kuunda hoja zenye mashiko (objective) ili kubainisha uzito na ukweli wa hoja zako.

Kwanza kabisa: Hadi uamuzi wa kurusha Royal Tour kufikiwa kufanyika Amazon, watu wanatazama data, Amazon mwaka 2021 ilikuwa na Subcribers 200 milioni duniani zote, ambapo siku nne zilizopita Netflix wana watumiaji 221 milion, unaweza kuona kuona tofauti ni ndogo tu.

Hata hivyo, watu wanahama kutoka kwenye traditional media kama Televisheni kuhamia kwenye matumizi ya internet, hivyo kuiweka Amazoni ni rahisi zaidi watu kutazama kupitia simu janja kuliko National Georaphic and Animal Planet kama unavyosema.

Pili: Rais Samia ni maarufu zaidi unavyodhani, hata hivyo, Royal Tour kuja Tanzania ni kwa sababu ya Rais Samia Suluhu. Unadhani kama angekuwa Magufuli Peter Greeneberg angekuja?

Umaarufu wa Rais Samia Suluhu kwanza umeletwa na umaarufu wa Tanzania wakati wa Hayati Magufuli, dunia ilifuatilia hasa siasa za Tanzania na hata Magufuli alipofariki Tanzania ikawa maarufu zaidi na hata Rais aliyefuata akawa maarufu maradufu kwani ni mara ya kwanza, kwa Tanzania kuwa na Rais wa kwanza mwanamke.

Rais Samia Suluhu amekuwa maarufu baada ya kuhutubia Baraza la Umoja wa Mataifa 2021. Rais Samia pia ameingia katika rekodi ya wanawake 100 wenye ushawishi Duniani 2021 katika Jariba la Forbes.

Rais Samia hakuwa na ulazima wa kushika kila taarifa, lengo la filamu ni kuonesha zaidi mandhari na uzuri wa nchi. Rais ni tour guide kwenye ile movie, na kumtumia Rais kuwa tour guide ni kichochoe tu watu wengi duniani wafuatilie, ila sio kutegemea Rais awe packed na kila taarifa ya Mbuga na mnyama, ingeboa. Ndio maana, filamu ilikuwa na shots kali mwanzo mwisho, na most of time, Peter aliingiza sauti mwenyewe.

Peter Greenberg hajaanza na Rwanda kama unavyosema, soma hapa; "He also produces and hosts a television series called The Royal Tour which airs on PBS. The series features various heads of state giving Greenberg and viewers a personal tour of their country. It has featured a number of world leaders including New Zealand's Helen Clark, Israel's Benjamin Netanyahu, Abdullah II of Jordan, Peru's Alejandro Toledo, Mexico's Felipe Calderón, Rwanda's Paul Kagame, Poland's Mateusz Morawiecki and Tanzania's Samia Suluhu Hassan. Greenberg was previously the Travel Channel's chief correspondent."

Filamu ya Royal Tour tayari kabla ya kutoka, ilishavuta watalii wengi, zaidi ya 600 kutoka Israeli, zaidi ya 200 kutoka France na nchi nyingine za Ulaya.
Umeandika vitu vya kubumba, tena kubumba haswa. Eti Samia Suluhu ni mtu maarufu sana duniani? Kivipi? Kwa lipi?
Mimi ni miongoni mwa watu waliompinga Magufuli kwa 100% na mpaka leo hii simkubali, lakini katika suala la umaarufu, Magufuli alikuwa maarufu huenda mara tano zaidi ya Samia Suluhu, iwe hapa Tanzania au duniani. Kwa nini? Sababu kuu ni hizi.

1. Magufuli alipenda na kulazimisha aonekane maarufu kuliko mtu yoyote, kwa gharama zote. Magufuli alitamani kuua umaarufu wa wanasiasa wote ili umaarufu wote ubakie kwake. Ndio rais aliyetaka picha yake kwa lazima itundikwe kwenye ofisi zote za umma na binafsi nchi nzima kwa lazima. Popote alipokuwepo alitaka redio na Tv zote zirushe tukio lake kwa lazima tena live.

2. Misimamo migumu, ya ajabu, isiyoyumba yumba. Duniani ilimfahamu Magufuli kwa misimamo yake ya ajabu. Kuanzia misimamo ya kuwapinga vikali mabeberu, kuwaangamiza wapinzani wake, Korona.

3. Visa, vituko na mikasa. Magufuli alikuwa ni mzee wa drama mwanzo mwisho. Magufuli aliona fahari kujiita Kichaa na kujifananisha na mungu. Magufuli aliamini anajua kila kitu na anaweza kufanya kila kitu na kikafanikiwa. Mtu wa namna hii akicheza movie ni lazima ingehit tu duniani.

Note:
Waandaji wa Royal tour hawakuwa wanamtafuta mtu maarufu ili kutengeneza movie yao bali walikuwa wanatafuta mkuu wa nchi husika (rais) ili kucheza movie yao kwa sababu ya aina ya maudhui( mchango wa wanasiasa katika kukuza utalii) na malengo (kutangaza utalii) ya movie yao. Hata kama Samia Suluhu angekuwa maarufu sana kisiasa duniani bado asingetosha kucheza movie yoyote maarufu huko marekani kwa kuwa hana kipaji chochote cha kucheza movie. Mwisho kabisa unapaswa kufahamu kuwa project ya Royal tour ilianza kabla hata Samia hajawa rais wa Tanzania, na rais yoyote wa Tanzania ambaye angekuwa madarakani ingemhusu ikiwa angeridhia kushiriki.
 
Nashukuru kwa maelezo yako marefu lakini kuweka rekodi sawa watalii kutoka Israel na France siyo matunda ya Royal Tour kwa sababu wamekuja hata kabla ya uzinduzi na pia wengi walishakuja kabla!
Uko ileje kweli au jina lako 2, shida ya watz ndo hiyo unawekeza leo halafu unataka faida mwaka huo huo, wengine tuna miaka 5 na bado tunaamini faida itakuja2. Kwa hiyo ulitaka waende huko kwa kodi ya nani? Nyumbani kwako kukiwa na njaa unajifungia au unatoka kuokoa jahazi. Poor iq
 
Back
Top Bottom