Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,789
- 218,431
Mwanasiasa Kijana , Mfungwa wa Kisiasa na Mateka wa awamu ya 6, Katibu mwenezi wa Bavicha, Twaha Mwaipaya, akizungumza kwenye Maadhimisho ya miaka miaka 3 tangu kufariki kwa Gwiji la siasa za Zanzibar, Maalim Seif, ameilaumu BAKWATA kwa kuwekwa mfukoni na serikali kiasi cha kushindwa kuikosoa serikali hata kwenye makosa ya wazi kabisa.
Twaha ambaye kwa dini ni Muislam, amemsifu shehe Issa Ponda kwa ujasiri wa kukosoa bila woga huku akiwasifu TEC Kwa waraka za mara kwa mara bila uoga pale serikali inapoboronga.
=====
Swali langu: Je, ni kweli Bakwata ilianzishwa na Mwl Nyerere kwa kushirikiana na Paulo Bomani?