Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,664
- 218,152
Wakuu natanguliza salamu, baada ya salamu hizi naingia moja kwa moja kwenye mada.
Tulishasema humu mara kadhaa na labda turudie tena kwa wale ambao hawakuelewa , CCM BILA POLISI NI WEPESI KULIKO PAMBA, na hili sasa limedhihirika kwa awamu zote za serikali ya chama hicho.
Twaha Mwaipaya ni kiongozi wa Bavicha anayepitia misukosuko mingi mno , huyu kijana alishakamatwa mara kadhaa na kurundikwa kwenye selo mbalimbali , mara zote Polisi wameshindwa kuthibitisha makosa yake , huwa anaachiwa tu katika mazingira tata, mara ya mwisho alitolewa gerezani usiku na mwenzake Nusrat Hanje , ambaye baadaye alipewa Ubunge na Job Ndugai.
Bado haijafahamika sababu hasa ya Serikali zote za CCM kumuogopa kijana huyu, kiasi cha kuwatumia Polisi kumkamata kila uchao.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliwahi kuwakanya wanaccm wenzake kuhusu madhara ya kuitegemea Polisi .
Tulishasema humu mara kadhaa na labda turudie tena kwa wale ambao hawakuelewa , CCM BILA POLISI NI WEPESI KULIKO PAMBA, na hili sasa limedhihirika kwa awamu zote za serikali ya chama hicho.
Twaha Mwaipaya ni kiongozi wa Bavicha anayepitia misukosuko mingi mno , huyu kijana alishakamatwa mara kadhaa na kurundikwa kwenye selo mbalimbali , mara zote Polisi wameshindwa kuthibitisha makosa yake , huwa anaachiwa tu katika mazingira tata, mara ya mwisho alitolewa gerezani usiku na mwenzake Nusrat Hanje , ambaye baadaye alipewa Ubunge na Job Ndugai.
Bado haijafahamika sababu hasa ya Serikali zote za CCM kumuogopa kijana huyu, kiasi cha kuwatumia Polisi kumkamata kila uchao.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliwahi kuwakanya wanaccm wenzake kuhusu madhara ya kuitegemea Polisi .