lenpel
JF-Expert Member
- Dec 7, 2012
- 253
- 165
Tv imaan yapata kibali rasmi. Tv hii inaendeshwa na islamic foundation.
Licha ya islamic foundation kumiliki tv. Pia ina redio na shule za sekondari.lakini inamiliki zahanti nyingi hapa nchini zinazosaidia waislam na wasiokuwa waislam
pia ni taasisi iliokaribu sana na chuo kikuu cha waislam morogoro ambapo mwenyekiti wa islamic foundation ndie mshauri mkuu wa fedha chuoni.
Ni jambo jema kuwa na chombo cha habari kitakacho chochea watu kumrudia Muumba wao ilimradi tu kifuate sheria za nchi ikiwa pamoja na haki za binadamu!
Maoni yangu kama wahusika wapo huku tunaomba muweke vipindi elimishi kwa jamii katika kila nyanja na sio dini tu!
Na cha muhimu msichukulie hii kama njia ya kueneza yale ambayo yatahatarisha umoja wa nchi na kuvuruga amani na maendeleo bali muwe kichochep cha hayo kwa ustadi na uweledi mkubwa!!!
Nawatakia kila la kheri!!!