Tuwakumbuke waandishi wetu wa Riwaya

Song of Lawino
Trial of Brother Jero
Things Fall Apart
Three Suitors One Husband
Is it Possible?
Masimulizi ya Alfu Lela Ulela
Kuli

na hivi mnavikumbuka?
Safari ya Bulicheka
Someni Bila Shida
 
Song of Lawino
Trial of Brother Jero
Things Fall Apart
Three Suitors One Husband
Is it Possible?
Masimulizi ya Alfu Lela Ulela
Kuli

na hivi mnavikumbuka?
Safari ya Bulicheka
Someni Bila Shida

Mine boy,
Hekaya za abunuwasi
 
Nilikwenda pale TPH hawana hata nakala ya vitabu vyao vya zamani na wala hawajui vinapatikana wapi, Library nako hakuna kitu, sijui wasomaji walipungua au vitabu viliisha kwenye ma-shelf na hawakurudishia.

TPH pale Samora Av. wabebakia kama duka linalouza vitabu vya watu wengine, sina hakika kama viongozi wa ile taasisi waliopo sasa hivi ana vision juu ya future ya TPH.
Mimi niliwahi kuagiza vitabu vya Alfu Leila U Leila na vile vya Bwana Msa, kutoka kampuni za uchapishaji Nairobi Kenya.

Labda mnaweza kujaribu uko.
 
Kuna waandishi mmewasahau kama

1 Faraji Hussein Hassan Katalambula- Buriani, Simu ya kifo

2. John M.S Simbambwene- Je kweli unanipenda?, Kivumbi uwanjani, Asha, n,k

3. Hemedi Kimwanga- Lazima Afe, Mnuko wa damu, Kazikwa yu hai, nani kaua,

4. Kajubi D. Mukajanga-Mpenzi, tuanze lini. n.k

5. Elvis Musiba-Kufa na kupona, Kikosi cha kisasi, hofu, njama
Mkuu katika watunzi ambao walikuwa sipendi kusoma vitabu vyao basi huo niliye mkoza hapo juu, alikuwa mmoja wapo... Sababu alikuwa ananakilii neno kwa neno kutoka kwenye vitabu vingine vya kiingereza.
 
Mkuu katika watunzi ambao walikuwa sipendi kusoma vitabu vyao basi huo niliye mkoza hapo juu, alikuwa mmoja wapo... Sababu alikuwa ananakilii neno kwa neno kutoka kwenye vitabu vingine vya kiingereza.

Ni kweli, vile vya baadaye alipoanza kuandika mambo ya upelelezi na ujambazi alikuwa ananakili. Lakini vya mapenzi alivyotoa mwanzo vilikuwa vizuri tu hasa kama hicho cha kivumbi uwanjani na je kweli unanipenda.

Kulikuwa na mwandishi pia aliitwa Nico ye mbajo, ulimsoma huyo?
 
Mimi niliwahi kuagiza vitabu vya Alfu Leila U Leila na vile vya Bwana Msa, kutoka kampuni za uchapishaji Nairobi Kenya.

Labda mnaweza kujaribu uko.

Vipo Dar, mtaa wa samora. Hata bulicheka na abunuwasi
 
1. Salam toka kuzimu
2. na ile hadithi ya baba naye anataka kuna mtu anaikumbuka
:smile-big:
 
duh.. kweli ndio mtu unajiona mzee hivi hivi!

Siku hazigandi,

Vitabu vyote hivyo vinavyotajwa hapo ninavyo huko nyumbani ila sijui kama bado viko salama. Ni pamoja na vitabu vya James Hadley Chase, Nick Carter, Denise Robins, Agatha Christie ma vinginevyo vingi vya riwaya za kiswahili na kiingereza. Ngoja niwakumbushe riwaya hii:


Bulicheka alikwa mwalimu wa shule ya Kilakala. Siku moja akamwambia mke wake Lizabeta, tufunge safari tuweze kuiona dunia. Lizabeta akajibu, ukitaka kufunga safari uone dunia nzima, nenda peke yako, mimi siendi. ......

Zaidi ya david Mailu, hapo afrika ya mashariki kulikuwa na mwandishi mwingine kutoka uganda ambaye naye alikuwa akiandika vitabu erotic sana. Character wake mmoja alikuwa akiitwa Matama; kwa bahati mbaya sasa hivi sikumbuki jina la mwandishi huyo tena.
 
Siku hazigandi,

Vitabu vyote hivyo vinavyotajwa hapo ninavyo huko nyumbani ila sijui kama bado viko salama. Ni pamoja na vitabu vya James Hadley Chase, Nick Carter, Denise Robins, Agatha Christie ma vinginevyo vingi vya riwaya za kiswahili na kiingereza......

....Zaidi ya david Mailu, hapo afrika ya mashariki kulikuwa na mwandishi mwingine kutoka uganda ambaye naye alikuwa akiandika vitabu erotic sana. Character wake mmoja alikuwa akiitwa Matama; kwa bahati mbaya sasa hivi sikumbuki jina la mwandishi huyo tena.

Niliwahi kusoma kimoja cha huyo mganda, unfortunately nimesahau jina la mwandishi. Kilikuwa kizuri.

baadhi ya vitabu vya Nick Carter ndio vilikuwa vinatoa stori za willy gamba kwenye vitabu vya Musiba.

Kulikuwa na kitabu cha Denise Robins kinaitwa "two loves", ilikuwa ni story sana nzuri ya mapenzi-ambapo bondia pamoja promoter wake walimuoa mrembo mmoja bila wao kukijijua kwa siku kadhaa..., ila sikubahatika kuviona vitabu vyake vingine.

Je yule mtaalam, Harold Robbins ulivisoma vitabu vyake?

Vitabu vya Agatha Christie James Hardley chase sasa hivi vipo madukani ila vijana wa sasa hawavisomi, wanasoma stori za shigongo, poor them!
 
Sultani akakubali.
Akamchinja mbuzi,
naye mbuzi akanywa maji,
nayo yakazima moto,
moto ukaichoma fimbo,
nayo ikampiga mbwa
mbwa akamuuma kalume-kenge
naya kalume-kenge akaenda shule
 
1. Mazungumzo ya Alfu-lela-ulela, au Siku elfu na moja.

Kimefasiriwa kwa Kiswahili na Edwin W. Brenn na kuhaririwa na F. Johnson

2. Lila na Fila - Kiimbila
3. Ubeberu Utashindwa - Kiimbila
 
Riwaya ya KULI Shafi Adam Shafi


shida mtunzi ndyanao balisidya

Duh! mkuu umenikumbusha form four pale kibasila, 1997!!
Kwenye hicho kitabu kuna sehemu muhusika mkuu anaeitwa chonya alikuwa akitoa msaada kwa mtoto aliyegonwa na gari. Chonya alisema, "I am taking this boy to the hospito, if police men come tell him me chonya of chilonywa", kwa lafudhi ya kigogo. Katika mtihani mmoja wa kiswahili kulikuwa na swali lililotaka wanafunzi wamchore chonya, kwa maana ya kutoa wasifu wa chonya. Basi kuna mwanafunzi mmoja aliamua kumchora kwa kutumia pencel, hakuelewa swali!
Tuliosoma vitabu vya zamani tulifaidi sana, sijui wakati huu mambo yakoje!



......... Mbona vya Eric mie vinanishinda !? :smile-big:

Unakusudia eric shigongo???!!! Lakini shigongo ni mwandishi wa juzi juzi tu!!! Mi nadhani mtoa mada alikusudia tuwakumbuke waandishi wa zamani!!

Hivi hawa watoto wa siku hizi wanasoma vitabu gani?

Watoto wa siku hizi wanahifadhi nyimbo katika vichwa vyao, muda mwingi headphone masikioni mwao, wanajaza ujinga.

duh.. kweli ndio mtu unajiona mzee hivi hivi!

Mzee ukiona hivyo ujue ndo utu uzima unakufuata, mda si mrefu utaitwa babu na kutembelea mkongojo.
 
Wadau, siku hizi moyo wa kusoma vitabu vya aina zote-vya Taaluma na Riwaya umepungua sana na imepelekea Watunzi wa Riwaya kutoandika tena vitabu. Leo nawakumbuka baadhi ya Waandishi/ Watunzi wa Riwaya wa Tanzania.

Hamie Rajab
1. Miujiza ya Mlima Kolelo
2. Dunia Hadaa

S.M.Bawji
1. Usiku wa Blaa
2. Kisiwa cha Mayuku

Duh! mkuu umenikumbusha mbali kidogo!!! Nilisoma kitabu cha usiku wa balaa, nakumbuka nikiwa standard 4 mwaka 1990, kabla ya akina mzee ole kuingizwa katika gazeti la sani. Usiku wa balaa ilikuwa ni hadithi ya kutisha sana, nakumbuka jinsi nilikuwa nikipatwa na hofu na moyo kunienda mbio wakati wa usiku nilipokuwa nikisoma kitabu hicho.

Kwa upande wa vitabu vya kipelelezi, mie nilikuwa navipenda vitabu vya mpelelezi joram kiango. kwa kweli zamani tulifaidi sana na tulikuwa tunapenda kusoma.
 
Penina alikuwa mmoja wa waandishi wa kweli miaka ile ya sabini na mwanzo wa themanini. Pia aliandika vitabu vifuatavyo (ingawa aliegemea zaidi katika michezo ya kuigiza):

1. Hatia
2. Tambueni haki zetu
3. Pambo
4. Lina Ubani
5. Wizara ya Mitumba
6. Nguzo Mama

Waandishi wengine kipindi hicho ninaowakumbuka:
Ngalimecha Ngahyoma
1. Kijiji Chetu

Gabriel Ruhumbika
1. Parapanda
2. Uwike usiwike kutakucha

Seith Chachage
1. Sudi ya Yohana
2. Almasi za Bandia
3. Kivuli



CHACHAGE
Makuadi wa Soko Huria

Gabriel Ruhumbika
1. Janga Sugu la Wazawa
2. Miradi Bubu ya Wazalendo.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom