Tuwaache abiria wa daladala washuke kabla ya sisi kupanda

OleWako

Member
Sep 7, 2021
6
9
25551935_2219834718030934_4359429907611631078_n.jpg

Ukipanda daladala unaweza kugundua jambo lilelile kila siku: kila daladala inapofika kituo chenye watu wengi mlango umeshazibwa na watu ambao hawawezi kusubiri kupambana kwa vile viti vichache. Mara nyingi watu wanapandaga hata kabla ya watu wote kushuka.

Aidha makondakta wanachangia kuongeza kero wakirudisha change mbele ya mlango kusababisha watu wanaosubiri change kuziba mlango. Hivi vitendo ni kero kwa watu wanaoshuka lakini pia inawachelewesha watu wote wanaotumia daladala pamoja na kuwa hasara kwa wazee, wagonjwa, wajauzito, nk. ambao hawana nguvu ya kupambana kupanda daladala.

Suluhisho ni rahisi: tuache ubinafsi na tuongeze utulivu.

Tuwape watu nafasi ya kutosha kushuka na kutoka halafu tukipanda tuheshimu wenzetu. Mwisho wa siku ni faida ya sisi wote; wanaoshuka wanaweza kushuka chap na bila kero na wanaopanda wanaweza kuwahi kupanda kuliko wakipanda kwenye ile fujo inayotokea mlango ukizibwa.
 
Hii ni issue ya ''Ustaarabu'' ni tabia tu,nchi kama Japan huwezi kukuta watu wanagombania kuingia kwenye Public transport kabla ya wanaoshuka hawajashuka,

Ni ngumu kuibadili hii tabia kwa kuandika tu Uzi hapa JF,
Haya mambo yaanze kufundishwa kwa watoto toka wakianza Chekechea.
 
we itakuwa ni kimbaumbau ndio maana unalalamika!,maana nyie ndio huwa mnaangukaga milangoni!,jitahidi ule na ufanye mazoezi hili dodoso lako hapo hatutalielewa!..😂
Kwahiyo mkuu unaona ni sahihi kwa watu 4 kugombania kuingia kwenye mlango kwa pamoja, mlango ambao una uwezo wa kuruhusu mtu mmoja tu kuingia at a time?

Vipi kuhusu wazee, Wagonjwa, watoto, wajawazito?
 
Hapo ndio Kuna kuibiana,kuambukizana mavifua makuu nk..
Mi mara nyingi huwa nawaacha wagombaniane wajaze siti!
Kama vipi nitasimama manake sipungukiwi kitu!
Au ntajiongeza tu nichukue usafiri mwingine kama Kuna ulazima
 
Kwahiyo mkuu unaona ni sahihi kwa watu 4 kugombania kuingia kwenye mlango kwa pamoja,mlango ambao una uwezo wa kuruhusu mtu mmoja tu kuingia at a time?

Vipi kuhusu wazee,Wagonjwa,watoto,wajawazito?
sio sahihi ndio lakini unafikiri hiyo mimtu itakuelewa kwa wewe kuja kuandika humu..? hili tatizo linaanzia mbali maadili toka kwenye familia huko,uchumi nao unachangia jamii yetu ni maskini kifikra mpk uchumi na hayo ndio matokeo.. unafikiri tungekuwa sote tunanidhamu ungeliona hilo..?

sasa hakuna nidhamu nikukanyagana tu! hakuna ambae hajui utaratibu mzuri ni upi we angalia hata mazingira yetu tunavyoyachafua utagundua inatakiwa tuanze kutibu nini ili tusione nini!..
mkuu ukikaa mlangoni halafu mimi ndo napanda sikupishi nipishe wewe! kama unataka raha nunua gari yako tushavurugwa sie....😂
 
sio sahihi ndio lakini unafikiri hiyo mimtu itakuelewa kwa wewe kuja kuandika humu..? hili tatizo linaanzia mbali maadili toka kwenye familia huko,uchumi nao unachangia jamii yetu ni maskini kifikra mpk uchumi na hayo ndio matokeo.. unafikiri tungekuwa sote tunanidhamu ungeliona hilo..?

sasa hakuna nidhamu nikukanyagana tu! hakuna ambae hajui utaratibu mzuri ni upi we angalia hata mazingira yetu tunavyoyachafua utagundua inatakiwa tuanze kutibu nini ili tusione nini!..
mkuu ukikaa mlangoni halafu mimi ndo napanda sikupishi nipishe wewe! kama unataka raha nunua gari yako tushavurugwa sie....😂
Mabadiliko hayaji mara moja, huanza taratibu na kusambaa,
Ukianza wew na mm kubadilika, na familia zetu, tutawaambukiza na wengine ustaarabu, ndani ya mwaka utakuta utamaduni ni mpya
 
Hii ni issue ya ''Ustaarabu'' ni tabia tu,nchi kama Japa huwezi kukuta watu wanagombania kuingia kwenye Public transport kabla ya wanaoshuka hawajashuka,

Ni ngumu kuibadili hii tabia kwa kuandika tu Uzi hapa JF,
Haya mambo yaanze kufundishwa kwa watoto toka wakianza Chekechea.
Nakubali, kuandika uzi huku hakubadili chochote moja kwa moja. Kubadilisha tabia ya watu ni mchakato mrefu..
Nilikasirika tu baada ya kupanda dala leo asubuhi nikibishana na mtu aliyeziba mlango. Ndo maana sina matarajio ya uzi huu kubadilisha jamii, ni ku vent tu na kuanzisha mjadala kupata maoni ya wadau
 
Ni kutokuwa wastaarabu tu
Mnahitaji kuwa na subra, sijui kwanini wengi wa watu ustaarabu zero
Kwani mkipanga foleni mnapungukiwa nini
Ukiachana na ustaarabu,kingine ni ubinafsi,
Na sio tu kwenye Daladala,mfano hata kuingia mpirani unakuta kila mtu anataka yeye ndio aingie kwanza kabla ya mwenzake!

Hata kwenye Mabasi ambayo kila mtu ana tiketi yake na namba ya kiti,usishangae kuona watu wakigombania kuingia,na hii tabia imekua hata kwenye kushuka,watu hugambania hata wakati wa kushuka,kila mtu anataka ashuke kabla ya mwenzake!
 
Mabadiliko hayaji mara moja, huanza taratibu na kusambaa,
Ukianza wew na mm kubadilika, na familia zetu, tutawaambukiza na wengine ustaarabu, ndani ya mwaka utakuta utamaduni ni mpya
Sahihi kabisa mkuu,mabadiliko huanza na ''Wewe''' na sio kusubiri wengine waanze,

Be the change you wish to see in the World.
 
Unatoka Mbezi unaenda Mbagara. Mzee hilo foleni la hapo kati usimame?

Umepigwa jua non stop, jasho limekutiririka vilivyo halafu ije daladala ulete ustaarabu mwisho wa siku usimame!!
Afe kipa afe beki hasimami mtu.
 
Ukiachana na ustaarabu,kingine ni ubinafsi,
Na sio tu kwenye Daladala,mfano hata kuingia mpirani unakuta kila mtu anataka yeye ndio aingie kwanza kabla ya mwenzake!

Hata kwenye Mabasi ambayo kila mtu ana tiketi yake na namba ya kiti,usishangae kuona watu wakigombania kuingia,na hii tabia imekua hata kwenye kushuka,watu hugambania hata wakati wa kushuka,kila mtu anataka ashuke kabla ya mwenzake!
Maajabu ya nchi masikini mkuu ni ujinga tu hata ferry huwa naona wakishuka wanavyokimbia kama wehu utafikiri kuna vita. Ni ulimbukeni halafu wanajiita watoto wa mjini
 
ila mbagala kwa kweli napavulia kofia....tangu ofisi iwe mbagala asubuhi naenda pale rangi 3 kushuka ni kipengele......watu hawana muda wa kupoteza kukusubiri ushuke utajua mwenyewe ushuke vipi...........
kiufupi mwendokasi inaleta unafuu kidogo unakua na option ya pili kuhofia kuchelewa kazini ama kupambanaiwa......
 
View attachment 2989788
Ukipanda daladala unaweza kugundua jambo lilelile kila siku: kila daladala inapofika kituo chenye watu wengi mlango umeshazibwa na watu ambao hawawezi kusubiri kupambana kwa vile viti vichache. Mara nyingi watu wanapandaga hata kabla ya watu wote kushuka. Aidha makondakta wanachangia kuongeza kero wakirudisha change mbele ya mlango kusababisha watu wanaosubiri change kuziba mlango. Hivi vitendo ni kero kwa watu wanaoshuka lakini pia inawachelewesha watu wote wanaotumia daladala pamoja na kuwa hasara kwa wazee, wagonjwa, wajauzito, nk. ambao hawana nguvu ya kupambana kupanda daladala.

Suluhisho ni rahisi: tuache ubinafsi na tuongeze utulivo.
Tuwape watu nafasi ya kutosha kushuka na kutoka halafu tukipanda tuheshimu wenzetu. Mwisho wa siku ni faida ya sisi wote; wanaoshuka wanaweza kushuka chap na bila kero na wanaopanda wanaweza kuwahi kupanda kuliko wakipanda kwenye ile fujo inayotokea mlango ukizibwa.
Haya maoni konda atayaona kweli??

Au yatazingatiwa!?

Suruhisho ni kuongeza idadi ya basi
 
Back
Top Bottom