Tusipotoshe umma, Tanzania ni Nchi inayofuata mfumo wa vyama vingi, sio lazima Wapinzani kuchaguliwa kuwa Wabunge

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Ibara ya 3(1) ya katiba ya JMT inasema wazi kabisa kuwa Tanzania ni nchi isiyo na Dini,bali ni Nchi ya kidemokrasia ambayo inafuata misingi ya vyama vingi.

Tarehe 28 mwezi jana Watanzania walipiga kura,na walifanya maamuzi ya nani awe Mbunge, Diwani au Rais. Na matokeo yametoka na CCM imeibuka kidedea.

Vyama vya upinzani vimeanguka na ni anguko ambalo kila mtu alilitarajia tokea JPM alipoingia madarakani. Hii ni kwa sababu walichokuwa wanakihubiri wapinzani kwa miaka ishirini (ufisadi), kilipatiwa ufumbuzi. Na ufumbuzi wenyewe ni kudhibiti rushwa,ubadhirifu na kuleta uadilifu kwa watumishi wa Umma.

Kwa hiyo wananchi kuchagua wabunge wengi wa CCM na Wapinzani kuambulia wabunge nane sio hoja kuwa sasa tumerudi kwenye mfumo wa chama kimoja. Maana sio lazima tuwachague kama tunaona hamtufai. Mch Mtikila (RIP) hakuwahi kuwa mbunge lakini alikuwa mwanasiasa makini na mwenye hoja zenye mashiko. Hivyo kuingia bungeni sio sifa ya kuwa mpinzani makini.

Namalizia kusema watanzania wamechagua CCM sababu ya mambo makubwa iliyofanya miaka yote iliyopita na pia kwa kusikiliza kwa umakini ahadi zilizopo kwenye ilani ya CCM ya 2020-2025 ambayo wao wanauhakika kuwa itatekelezwa sababu ufisadi umebinywa na fedha za kutekeleza miradi zipo na kiongozi mkuu wa sasa ni msimamizi na mtekelezaji mahiri. Tumuombee kwa Mungu tarehe tano aapishwe ili kazi ziendelee kusonga mbele.
 
"Mkichagua upinzani sitawaletea maendeleo"!

"Nikulipe mshahara halafu utangaze mpinzani kashinda"!

Kauli hizo hazijawahi kutolewa na kiongozi yeyote anayeheshimu misingi ya kidemokrasia!

Wananchi wanapaswa kuwa huru kuchagua! Na sio kutishwa kama ilivyotokea!

Mfumo wa Tanzania bado hautoi fursa kwa demokrasia kuchukua mkondo wake!

Sasa angalia ni kamata kamata ya wapinzani ndiko kunakoendelea!
 
Wapinzani hawalalamikii idadi ya wabunge,wanalalamikakia zoei la uchaguzi.
Mimi sio mpinzani lakini kama kuna namna wanaona haikuwa sawa, wasikilizwe.
Kuanzisha mada kama hizi unatakiwa ueleze upande wako wa kisiasa ili ueleweke vizuri..
 
Nani kasema kuwa uchaguzi huu una kasoro kwa sababu ya chadema kukosa ubunge?Hii kauli yako ina source/reference?Nipe source ya hii kauli yako,au umejitungia tu kujifurahisha wewe mwenyewe pamoja na nafsi yako?
Unadhani watanzania ni watoto?
 
Nimekuuliza maswali kadhaa hapo juu hujajibu hata moja.Mimi siyo mpenzi wa porojo,kama wewe ni muumini wa porojo kaa mbali kabisa na mimi.Narudia tena kukuuliza,nani kasema kuwa uchaguzi huu una kasoro kwa sababu ya chadema kukosa ubunge?Au umejitungia tu kauli hii ili kujifurahisha wewe pamoja na nafsi yako?Una reference ya kiongozi yoyote wa chadema ambae ametoa kauli ya kikhanithi kama hii?Hii dhana ya kikhanithi umeitoa wapi?
Huna akili we fala, kama hawalalamiki kwa unafiki wangeitisha haya maandamano? Pumbavu mjinga unaejifanya una akili.
 
"Mkichagua upinzani sitawaletea maendeleo"!

"Nikulipe mshahara halafu utangaze mpinzani kashinda"!

Kauli hizo hazijawahi kutolewa na kiongozi yeyote anayeheshimu misingi ya kidemokrasia!

Wananchi wanapaswa kuwa huru kuchagua! Na sio kutishwa kama ilivyotokea!

Mfumo wa Tanzania bado hautoi fursa kwa demokrasia kuchukua mkondo wake!

Sasa angalia ni kamata kamata ya wapinzani ndiko kunakoendelea!
Monkey
 
Back
Top Bottom