Tusipopata UKWELI huu Wengi tutaihama CHADEMA

Tusipopata UKWELI huu Wengi tutaihama CHADEMA

Ole wenu mnaohoji mapato na matumizi ndani ya chadema
Umenikumbusha enzi za mwalimu.Mambo ya kuhoji ----- hayakuwepo,na wengine wakasema mwalimu ni dikteta.
lakini mashule yote yalikuwa na madawati,walimu walilipwa mishahara yao vizuri n.k
Cha kushangaza hata baada ya kifo chake watu wanapenda sana kusikiliza hotuba zake pamoja na kwamba alikufa mwaka 1998
lakini hotuba zake zinaheshimika kuliko za viongozi walio hai.
Hivyo nawapongeza viongozi wa CDM na ninawaomba msitoe nafasi kwa wanaofanya kazi ya kuhoji lakini hawana mawazo ya kujenga
Tupelekeni mwendo wa mwalimu J.K. Mpaka TZ ikombolewe.Tukiisha kombolewa tutawaelewa tu
Kazi yenu ni njema tunaiona bungeni na kila mnaposimama kufanya jambo linafanikiwa.
 
1. Unataka uambiwe mipango ya chama kujenga ofisi wewe ni nani? kila kitu kina taratibu zake na sehemu muhimu ya kujadili masuala ya CHADEMA ni kwenye vikao vyake

2. Ukomo wa uongozi tafuta katiba uisome utaelewa nini kilichoandikwa unapotaka uambiwe huo ni uzuzu kwani kama mwanachama lazima utakuwa na katiba na utakuwa umeisoma na kuielewa.

3. Mapato na matumizi taarifa zake zinatolewa katika vikao vya chama na zipo katika ofisi za makao makuu ya chama nenda ukaombe upewe lakini kwa sababu unaandika huku ukiwa umejificha ID hauwezi kufanya hivyo kwa sababu ya unafiki

4. Zitto sio kama hapewi nafasi isipokuwa ni yeye asiyewajibika katika nafasi yake kwa sababu ya kujitenga kwake na kujiingiza katika kuunda vikundi vya uasi ndani ya chama.

Hicho ndio Chama Cha Demokrasia na Maendeleo bana! Ha ha ha! Eti hakuna haja ya ukomo wa uongozi! Dah! Kweli hi ni demokrasia ya wanaukoo wa chadema!
 
Hujawahi kuwa CDM wewe.Ulivyoandika inaaonyesha unamajibu ya yote ulioyouliza.Acha utoto
 
kwanini usiihame serikali yako iliyoshindwa kujenga nyumba kwaajiri ya viongozi wake badala yake imewapangishia na ina mapesa lukuki yawalipa kodi
 
Usisubiri majibu, anza mbele na matangazo. huna tofauti na juliana shonza na mtela mwampamba, nimekudharau sana. chapa mwendo lakini tutaikomboa nchi ili ufaidi maziwa na asali vipatikanavyo kwayo.

utaikomboa nchi kwa utaratibu gan weweeeee? kwa utaratibu huo ambao watu wakilalamikia matumizi mabovu_MSHUMBUSi anasema acha watanue coz wame_invest sana? acha uzembe huo weweeee
 
Salam wanaJF,

Katika nagzi za uatwala bora na uwajibikaji ni pamoja na ushirikishwaji, uwazi na kujali haki kwa wote. Sie wafuasi sugu wa CDM tunaomba tupewe ukweli kwa yanayojiri kwenye vyombo vya habari na pia uchaguzi ujao. Tunahitaji kujua haya:

1. Mipango ya chama kuwa na ofisi yake bila kukodisha kwani kinapokea ruzuku toka serikalini na hakuna sababu ya kukodisha majengo kwani uwezo wa kuwa na ofisi mikoani upo
2. Ukomo wa uongozi kwa mujibu wa katiba ya chama
3.Mapato na matumizi ya chama
4.Mafanikio ya wabunge wa cham kwa umma japo tunafahamu fika kuwa CCM ndio inayotekeleza sera zake kwani ndyo chama kinachounda serikali.
5. Je kwa nini Zitto Zuberi Kabwe hapewi nafasi kama Naibu Katibu Mkuu wa Chama.


Nawasilisha.

Hapo kwenye 5 umemaliza kabisa.Hilo ni jibu tosha la kuonyesha kuwa wewe ni mtu wa namna gani na lengo lako ni lipi.
 
Mimi binafsi nisipofahamu yafuatayo nitabaki mwananchi asiye na chama chochote, kwanza kwa nini chadema tuendelee kupanga jengo la makao makuu? Kwa nini tusijenge wenyewe? Je lini chuo cha uongozi cha chama kitajengwa? Je gazeti la chama litaanzishwa lini? Badala ya kuendelea kutumia gazeti la mh. Mbowe? Je kwa nini m4c zimesimama? Nisipopata majibu haya ya kuridhisha nitakuwa mwananchi huru without to support magamba or magwanda! Tanganyika kwanza!

nilijiunga CDM mwaka 2001 siku na muda mmoja na ZZK, nilikipenda sana sana Chama_lakin kadri muda ulivyokuwa ukienda hali ya sintofaham ilizidi kunizonga na mwaka 2011 niliwahi kuja na hoja ambayo mpaka Mello na Moderator wakanifanya kama muhaini na NIKAINGOZWA KIFUNGONI_nashukuru sana mambo haya sasa yanajidhihirisha machoni kwa wengi na sasa kwamba chama kinaendeshwa kwa akili na matakwa ya wachache na KATIBA haifuatwi na wakosefu ni wale wanaosema Ukweli sasa mambo haya yanadhihirika machoni mwa wengi_nikiwa kidato cha IV Mwigamba alikuwa kidato cha III, naamini tulisomeshwa na waalim sahihi kwasababu ya kushahabiana kifikra. vijana siku hizi wamekuwa waoga wa maisha kiasi kwamba wameamua kuburuzwa kwa mahitaji ya wachache kwsbb ya kuendekeza mabakuli kwa viongozi
 
Salam wanaJF,

Katika nagzi za uatwala bora na uwajibikaji ni pamoja na ushirikishwaji, uwazi na kujali haki kwa wote. Sie wafuasi sugu wa CDM tunaomba tupewe ukweli kwa yanayojiri kwenye vyombo vya habari na pia uchaguzi ujao. Tunahitaji kujua haya:

1. Mipango ya chama kuwa na ofisi yake bila kukodisha kwani kinapokea ruzuku toka serikalini na hakuna sababu ya kukodisha majengo kwani uwezo wa kuwa na ofisi mikoani upo
2. Ukomo wa uongozi kwa mujibu wa katiba ya chama
3.Mapato na matumizi ya chama
4.Mafanikio ya wabunge wa cham kwa umma japo tunafahamu fika kuwa CCM ndio inayotekeleza sera zake kwani ndyo chama kinachounda serikali.
5. Je kwa nini Zitto Zuberi Kabwe hapewi nafasi kama Naibu Katibu Mkuu wa Chama.


Nawasilisha.

Nilidhani wewe ni miongoni mwa wapamanaji kumbe gamba! dah! nikupe ushauri ni vizuri ubaki uliko kwa kuwa huna pa kuhamia. Umeshindwa kuwahoji wenzako mikataba ya madini ambayo hata mwenyekiti wako wa Chama alikiri wazi kuwa tumeliwa? Umeshindwa kuwauliza wenzako mikataba ya nyumba za chama chako ya miaka 265 ina manufaa gani kwa CCM? umeshindwa kuhoji bilioni zaidi ya 50 za kodi za watanzani mnazitumiaje? Achilia mbali rushwa na ujagili hayo yote hayakusumbui. Ama kweli toa kwanza boriti kwenye jicho lako ndipo uweze kuona kibanzi katika jicho la mwenzako.
 
Nani kakuruhusu kuhoji?
Wewe ni msaliti na umevuliwa unanachama wako kuanzia leo

1385336_352047558265584_1105770853_n.jpg

Lumumba buku7fc
 
hapa kweli wamewashika ina maana unataka kusema uchaguzi hautafanyika kwa kuogopa mamluki? kama ndo hivyo tutegemee Mbowe na Slaa watakaa madarakani milele Maana sina uhakika kama mamluki wanaweza wakaisha kwenye chama leo ukimwondoa mamluki mmoja kesho wanazaliwa wawili

well said mkuu!

ivi wana chadema kweli hata hoja za msingi hamuoni kazi yenu ni kujipanga kubishana tuu daah! ni wakat sasa u need to think out of the box.....! hampambanui mambo nyie mko mmejiandaa kubisha tuu poor you.
 
Mods, hu Ukabila na Udini kama tukiachia na tusipoupiga vita tokea hatua za awali, utatugharimu sana kuundoa baadae. Watu kama huyu si wa kuachwa hivi hivi pasi kupata la kjifunza. Mwezi mmoja wa ban unamtosha sana na itakuwa fundisho na kwa wengne wanaotaka kutupleka huko ujingani. Asante.

Wewe ndio mjinga sana. Yaani kuhoji mambo ya msingi kuhusu chadomo ndio wamfungie?. Mbona nyie watu wa chadema mna akili nyepesi hivyo. Fikra zenu ni finyu sana. Huwezi kuahirisha akili zako kufikiri ili akufikirie mwingine. Madhara yake ni makubwa. Tazama Germany walipoacha kufikiri na kuruhusu mawazo ya Hitler yawe ndio sera ya Germany. What happened?. Acheni upuuzi matusi hayataisaidia Chadema. Kwa taarifa yenu tu, Taswira ya Chadema miongoni mwa watz wengi imeshaingia doa. Pale mnapofanya usanii kwenye mambo ya msingi watz wameshawabaini. Ikulu mtaisikia na kuiona tu kwenye TVs tu. Tukana, vimba, nuna lakini ukweli ndio huo.
 
Salam wanaJF,

Katika nagzi za uatwala bora na uwajibikaji ni pamoja na ushirikishwaji, uwazi na kujali haki kwa wote. Sie wafuasi sugu wa CDM tunaomba tupewe ukweli kwa yanayojiri kwenye vyombo vya habari na pia uchaguzi ujao. Tunahitaji kujua haya:

1. Mipango ya chama kuwa na ofisi yake bila kukodisha kwani kinapokea ruzuku toka serikalini na hakuna sababu ya kukodisha majengo kwani uwezo wa kuwa na ofisi mikoani upo
2. Ukomo wa uongozi kwa mujibu wa katiba ya chama
3.Mapato na matumizi ya chama
4.Mafanikio ya wabunge wa cham kwa umma japo tunafahamu fika kuwa CCM ndio inayotekeleza sera zake kwani ndyo chama kinachounda serikali.
5. Je kwa nini Zitto Zuberi Kabwe hapewi nafasi kama Naibu Katibu Mkuu wa Chama.


Nawasilisha.

Habari ndugu,

upmejitambulisha kama 'wanachama sugu' na mimi nakujibu baadhi kama mmoja kati ya wanachama

Naamini ukiwa mmoja kati ya 'wanachama sugu' utakuwa unafahamu mengi zaidi kama ulijishughulisha kutaka kuyajua,

Umesema Chadema vyema juu ya chama kuwa na ofisi yake hasa ya makao makuu na kuwa na majengo ya ofisi mikoani, sababu chadema inapokea ruzuku kubwa!

Chadema ni chama cha wanachama, ambacho hata bila ya ruzuku kitawategemea wanachama wake, na nyinyi wanachama sugu ndio tunawategemea kwenye kuhamasisha ili tuweze kupata maeneo ya kujengea ofisi

ilipozinduliwa M4C, na nyiny 'wanachama sugu' kupitia matawi yenu mlipaswa kuwaendea wananchi kwenye maeneo yenu na kufanya harambee kwa ajili ya kukusanya pesa kwa ajili ya kununua eneo, matofali nk kwa ajili ya ujenzi wa ofisi

Nakupa mfano:- nenda kimara rombo, ulizia msingi wa Chadema wa Tarime, utaelezwa juhudi zao mpaka kujenga ofisi ya msingi sio Tawi (msingi)

Huu ni mfano wa uwajibikaji wa wanachama kwa chama chao

Kuhusu ukomo wa uongozi, kwa kuwa wewe na wenzako ni wanachama sugu, ina maana mmesoma katiba, kama mmesoma imejieleza vyema, ila jisikie huru kwenda ofisi ya katibu mkuu atakupa maelezo

Na kuhusu mapato na matumizi, kwa mujibu wa sheria ni msajili ndiye mwenye kutangaza kwenye gazeti la serikali, mapato na matumizi ya kila chama, ila hajawahi kutangaza ya chama chochote, sasa hata kama mnataka kuhama chadema, hameni ila nendeni UMD, SAU nk vyama ambavyo havijawahi kupata ruzuku, hivyo labda ni visafi, au undeni chama chenu, ni jambo la ki katiba mnaruhusiwa,.

Jambo jingine, umezungumzia juu ya mafanikio ya wabunge wa chama, nadhani labda wewe sio mfuatiliaji wa Bunge, wabunge wa chama kwa habari ya uwakilishi wao bungeni unaonekana wazi, labda huko majimboni ambapo napo hakuna malalamiko kutoka kwa wananchi wao, wengi wao wanafikia malengo

Na lingine juu ya Zitto, Zitto nafasi yake ya unaibu ni nafasi inayojitegemea na yenye majukumu yake kipekee, Zitto sio katibu mhutasi wa Slaa yeye ni sawa na kusema Katibu wa Chadema Tanganyika, ama Tanzania Bara na Slaa ni Katibu wa Chadema Tanzania, Zitto na Slaa kila mmoja ana majukumu yake sawa sawa na katiba inavyosema, na ofisi zao hazina migongano.

Usiku Mwema

M/Chama ChademaTz
Joash Mussa
 
HAKUNA ANAYEWEZA KUDANGANYIKA NA THREAD ZA INFLICTOR,DHAIFU WATAONDOKA,SISI WANACHAMA SAFI CDM TUNASUBIRI MATAMKO KUTOKA KWA VIONGOZI KWANI HAYA YALIYOTOKEA TUNAAMINI CHAMA KINAYATAFAKARI KWANZA ILI KUJIPANGA KUJA NA MAJAWABU YATAKAYOJITOSHELEZA, CDM SIO CHAMA CHA WAKURUPUKAJI KWANI HAKIBAHATISHI,NA NINA AMINI HAPANA MUDA MREFU TUTAPATA MAJIBU SAHIHi, "KUMBUKA" MAADUI WA CHAMA CHETU HAWALALI KUJITAHIDI KUHAKIKISHA KINADONDOKA AIDHA KINASAMBARATIKA KTK MEDANI ZA SIASA, NI MUDA MUHAFAKA WA KUONGEZA MSHIKAMANO MIONGONI MWETU, MUNGU IBARIKI CDM
 
Wewe ndio mjinga sana. Yaani kuhoji mambo ya msingi kuhusu chadomo ndio wamfungie?. Mbona nyie watu wa chadema mna akili nyepesi hivyo. Fikra zenu ni finyu sana. Huwezi kuahirisha akili zako kufikiri ili akufikirie mwingine. Madhara yake ni makubwa. Tazama Germany walipoacha kufikiri na kuruhusu mawazo ya Hitler yawe ndio sera ya Germany. What happened?. Acheni upuuzi matusi hayataisaidia Chadema. Kwa taarifa yenu tu, Taswira ya Chadema miongoni mwa watz wengi imeshaingia doa. Pale mnapofanya usanii kwenye mambo ya msingi watz wameshawabaini. Ikulu mtaisikia na kuiona tu kwenye TVs tu. Tukana, vimba, nuna lakini ukweli ndio huo.
Mbona na wewe unaongea umevimba mdau? kama ushauri unampa mtu umetuna hvo kweli ataufuata? kweli mumechanganyikiwa nyie maccm. chadema iko sawasawa sana. ccm mmelinyima taifa utamaduni wa kuwajibika na kuwajibisha. CHADEMA NI MWL WENU HATA KAMA HAMTAKI.
 
Mimi nadhani taifa limepoteza yote mawili. 1. utamaduni wa kuhoji< kuhoj jambo sahh, mahali sahh na kwa chanzo sahh> 2. kuwajibika ama kuwajibishwa na mamlakahucka. JAMBO LILILOTOKEA, Alotaka kujua mambo hayo akloya.andika hakusema kwa chanzo sahh cha majibu, japo amewajibishwa kwa utaratibu mzuri, awe mpole, hakuna jambo liclo na mwisho.
 
Mimi nadhani taifa limepoteza yote mawili. 1. utamaduni wa kuhoji< kuhoj jambo sahh, mahali sahh na kwa chanzo sahh> 2. kuwajibika ama kuwajibishwa na mamlakahucka. JAMBO LILILOTOKEA, Alotaka kujua mambo hayo aloya.andika hakusema kwa chanzo sahh cha majibu, japoamewajibishwa kwa utaratibu mzuri, awe mpole, hakuna jambo liclo na mwisho.
 
Mamluki wengi ambao wapo kimaslahi zaidi hawana nafasi katika siasa za upinzani na wapishe njia,maana hakuna muda wakupoteza kupambana na wajinga wanaorudusha nyuma jitihada za upinzani kwa hoja muflis zisizo na mashiko kwa kipindi hiki ambacho watu wanahitaji mageuzi.
Chadema ina weza kuwa na watu wengi wa aina hii wanaotumiwa kukivuruga chama ili kuwapoteza malengo.
Ushauri wangu wafukuzwe wote na wahame na wafuasi wao ili kukiacha chama na wanamageuzi wachache ambao wataikomboa nchi hii badala ya hao wachache wanaonunuliwa kirahisi ili kukivuruga chama.
 
tusipopewa? ww na nani jisemee mwenyewe na wala hautokuwa wa kwanza kuhama au na ww una jina feki kama mwenzio?

usiende paspo kufikiri cdm ni chama ambacho kimekuwa mstari wa mbele kupambana na ufisadi na kupigania demokrasia nchini, hivyo basi kutokana na wanachama wa cdm kuanza kuwa na mashaka kuwa kuna uwezekano uongozi wa juu wa cdm kujihusisha na ufisadi wa fedha za chama na pia kuwajengea hof wanachama hadi anayehoji mapato ya chama anaonekana msaliti, kuna umuhimu uongozi utoa majibu ya hoja zinazotolewa na wadau mbalimbali hasa kuhusu mapato na matumizi ya chama na ukomo wa uongozi
 
Back
Top Bottom