Tusipende kupiga watoto wetu

Tusipende kupiga watoto wetu

Huwezi kumfanyia ubaya mwanao kisa mwanaume tu mnayeweza kuachana hata kesho;mnakosea!
Huwezi kuelewa mkuu, hakuna mama anapenda iwe hivyo, ila inatokea tu, watoto wanageuka ndo wanyonge wake kwa kuwa anawamudu

Na mara nyingi unakuta wanawake wa hivi wakishawaadhibu watoto, wanaanza kujishangaa na kujutia walichokifanya


Japo pia kuna wanaume nao wanapiga mno watoto wakidhani ndio ubaba
 
Huwezi kuelewa mkuu, hakuna mama anapenda iwe hivyo, ila inatokea tu, watoto wanageuka ndo wanyonge wake kwa kuwa anawamudu

Na mara nyingi unakuta wanawake wa hivi wakishawaadhibu watoto, wanaanza kujishangaa na kujutia walichokifanya


Japo pia kuna wanaume nao wanapiga mno watoto wakidhani ndio ubaba
Hiyo situation naielewa dadaa... Kuna wakati mwanaume anakukwaza hadi unakuwa full kwa hasira halafu hicho kipindi sasa katoto kakizingua hata kidogo kataona moto.Kuna mama hawakuelewana na mumewe hadi hasira zikapanda.Mumewe alivyoondoka katoto kakamwita tu sijui kalihitaji nn.Mama sasa akakafokea 'nyoko wewe si ufanye hivi na vile...'. Ila baadaye alivyotulia akambeba na kumbeba mtoto.Sasa hao sawa wanaojutia ila kuna wengine ni kupiga sana kila siku.Hao ndo wabaya.
 
Ungekuwa mwanamke ungewaza kama mwanamke
Ila unashindwa kujua namna ya mwanaume kufikiri na kuchukulia mambo ni tofauti kabisa na mwanamke.
Nshaelezea post no.83. Icheki kama hutojali.
 
Sioni umuhimu wa kiboko kwasababu hata mimi siijui rangi,harufu au taste ya viboko kutoka kwa baba na mama


Ni akili za kitumwa tu zinasumbua mtoto inatakiwa umuelekeze na si lazima kwa kiboko hata maneno
 
Mtoto ni zawadi.Ndiyo alama yako utakayoacha hapa duniani. Hizo mali utakazoacha zitagombaniwa zitaisha.Ila jina lako atabaki nalo wewe na atalitumia kwa mjukuu wako kama jina lake la tatu. Tusitelekeze wala kuwapiga piga watoto.

Huwa najisikia vibaya pale mzazi au yoyote yule anamposhushia kipigo mtoto tena kilichozidi umri wake.Huku kitaa kuna mama huwa anampiga sana mwanae.Mwanae yupo la pili ni wa kike.Yule mtoto anafanya kazi nyingi jamani.Siku dogo alichelewa kurudi akarudi saa 9 badala ya saa 7 basi kaingia ndani tu hivi ndani kamsalimia mama kakutana na kipigo.Hapo hata hajauliza shida nn ya kuchelewa.

Kumbe dogo alikutana na wahuni wa shule huko yale madarasa ya juu wakampora baadhi ya vitu basi dogo akaenda kushitaki kwa ticha sasa hiyo process hadi ya kupata vitu vyake ndo muda ukapotea hapo.Sisi tumetulia hatuna habari tukashtushwa na kelele hiyo nyumba.Kelele yenyewe si ya kawaida! Ikabidi twende yawezekana shida ni kubwa.

Kumbe bhana sijui alikosa cha kumpigia humo ndani basi akatumia mwamvuli ile ncha iliyochongoka! Kampiga usoni! Mungu mkubwa alimiss jicho! La sivyo alikuwa analiondoa! Ilo usoni alimpompiga palianza kubreed! Sasa mtu wa hivi usipomuita mzazi ukamuita shetani utakuwa na kosa?

Jioni mzee wa nyumba aliporudi ikabidi amuulize kulikoni mwanae! Mtoto akajieleza vizuri huku baba anasikiliza kwa makini! Kilichofuata yule mama alitwangwa,alipigwa,alinyooshwa sana.Mimi huwa sipendi kuona au kusikia mwanamke anapigwa na mwanaume ila hiyo siku nilifurahi sana! Alipata dawa yake.Mtoto kama vile sio wake wa kuzaa.

Wengine hadi vitoto vidogo wakiwa wanaviogesha basi wanavichapa humo humo kwenye beseni.Vinalia hadi vinahuzunisha.Sio vizuri hivyo.
Wakati wa kutaka mwanao akuelewe kwa vipigo ushaisha huko! Mengine tuwaachie mababu zetu waliopenda waogopeke ili wakiingia nyumbani kutoka shamba basi watoto wajifiche.Huu muda ni wa kutengeneza urafiki na watoto wetu ili wawe huru kueleza changamoto zao kisha tuzitatue.

Watoto wa zamani waliwapenda bibi na babu zao sababu waliwasikiliza tofauti na wazazi waliopenda kutumia silaha ya mkono.
Mimi sitapiga mwanangu yoyote kabisakabisa.
Umeongea mwa uchungu sana hadi nime ifeel. Hongera sana kwa ushauri mzuri kila mzazi auchukue. Asante sana
 
Umenikumbusha, jana nilikuwa sehemu sasa kuna mtoto anamwambia mama yake nasikia njaa huku analia, yule mama alichukua fimbo akaanza kuchapa jamani, yule niliyekuwa nae akakosa uvumilivu alimsema sana yule mama.... Unakuta mzazi ana stress zake binafsi anamalizia kwa mtoto
Hii ipo sana siku hizi. Watoto wanalipa madhaifu ya baba zao yanayopelekea mam kuwa na stress. Mtoto akilia kidogo tu, fimbo! Akiuliza hiki atajibiwa kwa ukali
 
Dogo anashida na mama ake huko jikoni..... Akikosea hachapwi anasonywa ....Sasa hivi kamekuwa kasonyi kweli ....Ukikaelekeza kuwa ni vibaya kanaacha ...ila kesho akishinda na mama Yake Anarudia Tena......ngoja ntamkata mama ake mdomo shwaini(swine)......kina mama mnachangia snaa watoi kuwa Na tabia za ajabu
 
Back
Top Bottom