sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,034
Muhimu: Kiingereza ni lugha sio kipimo cha akili au mafanikio, Faida ya kumpeleka mapema mtoto shule ya kiingereza ni sawa na kukijua kiswahili mapema kwenye kijiji wanachoongea kisukuma
Nikiwa shuhuda mwenyewe, binafsi nimesoma shule ya english medium nami nimekuwa mkubwa najinyima kuwapeleka watoto shule hizi.
Inahitaji uwe na pesa nyingi kusomesha shule za kiingereza ? Inategemeana na mkoa, Sehemu kama Mbeya kwa ada ya shilingi laki 2 na nusu zipo shule za msingi 4 za serikali za kiingereza, zipo private za laki 6 hadi milioni na kitu (day),
Kwa uzoefu wangu shule nzuri za English inabidi walimu wawe wakenya, waganda ama wazambia, shule nyingi zenye walimu wa kitanzania zina changamoto maana hata wao lugha ya kiingereza inawapa shida,
FAIDA YA KUSOMA SHULE ZA KIINGEREZA
Tangu nikiwa na miaka 7 nilikuwa nakielewa, kanisani tukienda kukiwa na mchungaji mgeni anahubiri kwa kiingereza niliweza kuanza kutafsiri na watu wanashangaa tunaendana na mkalimani aliekuwa anakunja pesa kwa kukijua kiingereza, Muvi hizi za kiingereza nilikuwa natafsiria wengine kama hazikutafsiriwa na DJ Afro.
Mambo ya kidunia sidanganywi kirahisi kwenye media, Mfano huu waraka wa Papa Francis niliweza kuuelewa mwenyewe bila kutegemea utafsiriwe, mwanzoni watanzania wengi waliaminishwa kirahisi ni upotoshaji ila nchi kama Nigeria, Kenya, Zambia zinazoelewa kiingereza ziliuelewa na kuupinga, na sasa hata maaskofu wa Tanzania wameuelewa wanaupinga, Hata Trump watanzania wengi walikuwa wanamchukia kwa habari za kutafsiriwa zenye uzushi ila ndio wamekuja kustuka sikuhizi kwamba Trump alipigwa vita sababu alikandamiza vitu kama ushoga wamaerekani hawakupenda, mimi najua haya tangu 2015.
Shule ya msingi kujifunza kwa kiingereza ni advantage, mkifika sekondari hakuna maswali ya kiswahili kwenye hesabu, sayansi, n.k. ni kiingereza tu ambacho hakina ugeni wowote tofauti na wale waliosoma za kiswahili.
Notes nilikuwa nazielewa kwa kiingereza inakuwa rahisi kwangu kuliko mtu ambae kaanza kukielewa kiingereza sekondari anasoma kwa kukariri atatumia system hii pengine mpaka chuo,
hii lugha ya kiswahili ilipaswa iwe ya kuongea tu sio kwenye suala la academics nje ya somo lake maalum.
UPOTOSHAJI HAUJAANZA LEO, SHULE PRIVATE ZINASAGIWA KUNGUNI
Kuna upotoshaji tangu zamani enzi nasoma kwamba shule hizi zinaharibu watoto kimaadili, siku hizi watu wamefikia mpaka hatua kusema zinafundisha ushoga na usagaji, Mimi sikubaliani kabisa na huu uzushi bali naziona ni kauli za kumasikini, Nilikuwa na marafiki kibao wa shule za serikali na nikiri kwamba niliweza kuona kwa macho yangu walioanza kuvuta bangi na kunywa viroba vya power vile vya Malawi wakiwa darasa la sita, sababu niliyokuja kugundua ni kwamba shule za serikali zina asilimia kubwa ya wazazi wasiofatilia mienendo ya watoto wao.
Na kuhusu mambo ya ushoga hasa kwa shule za baarding haya mambo yalianzia shule za serilali kwasababu shule private hazikuwepo zamani, Shule za boys kibao zinazosifika kwa mambo haya nisingependa kuzitaja nyingi ni za serikali, chanzo kikuu huwa ni kwamba shule hizi huwa na yale maisha ubabe wa wazi wazi na yabia hizi watu huzichukua katika makuzi yao huko uswazi kuleta shuleni, na ndio hapa sasa wababe wakipata wanyonge huwaingilia, Ukienda shule za private ni ngumu sana kukuta haya mambo ya ubabe, shule niliyosoma hadi usikie mtu kaonewa ilikuwa ni nadra sana, kulikuwa na ngumi tukipisha kauli lakini hakukuwa na mambo ya kuoneana.
Nikiwa shuhuda mwenyewe, binafsi nimesoma shule ya english medium nami nimekuwa mkubwa najinyima kuwapeleka watoto shule hizi.
Inahitaji uwe na pesa nyingi kusomesha shule za kiingereza ? Inategemeana na mkoa, Sehemu kama Mbeya kwa ada ya shilingi laki 2 na nusu zipo shule za msingi 4 za serikali za kiingereza, zipo private za laki 6 hadi milioni na kitu (day),
Kwa uzoefu wangu shule nzuri za English inabidi walimu wawe wakenya, waganda ama wazambia, shule nyingi zenye walimu wa kitanzania zina changamoto maana hata wao lugha ya kiingereza inawapa shida,
FAIDA YA KUSOMA SHULE ZA KIINGEREZA
Tangu nikiwa na miaka 7 nilikuwa nakielewa, kanisani tukienda kukiwa na mchungaji mgeni anahubiri kwa kiingereza niliweza kuanza kutafsiri na watu wanashangaa tunaendana na mkalimani aliekuwa anakunja pesa kwa kukijua kiingereza, Muvi hizi za kiingereza nilikuwa natafsiria wengine kama hazikutafsiriwa na DJ Afro.
Mambo ya kidunia sidanganywi kirahisi kwenye media, Mfano huu waraka wa Papa Francis niliweza kuuelewa mwenyewe bila kutegemea utafsiriwe, mwanzoni watanzania wengi waliaminishwa kirahisi ni upotoshaji ila nchi kama Nigeria, Kenya, Zambia zinazoelewa kiingereza ziliuelewa na kuupinga, na sasa hata maaskofu wa Tanzania wameuelewa wanaupinga, Hata Trump watanzania wengi walikuwa wanamchukia kwa habari za kutafsiriwa zenye uzushi ila ndio wamekuja kustuka sikuhizi kwamba Trump alipigwa vita sababu alikandamiza vitu kama ushoga wamaerekani hawakupenda, mimi najua haya tangu 2015.
Shule ya msingi kujifunza kwa kiingereza ni advantage, mkifika sekondari hakuna maswali ya kiswahili kwenye hesabu, sayansi, n.k. ni kiingereza tu ambacho hakina ugeni wowote tofauti na wale waliosoma za kiswahili.
Notes nilikuwa nazielewa kwa kiingereza inakuwa rahisi kwangu kuliko mtu ambae kaanza kukielewa kiingereza sekondari anasoma kwa kukariri atatumia system hii pengine mpaka chuo,
hii lugha ya kiswahili ilipaswa iwe ya kuongea tu sio kwenye suala la academics nje ya somo lake maalum.
UPOTOSHAJI HAUJAANZA LEO, SHULE PRIVATE ZINASAGIWA KUNGUNI
Kuna upotoshaji tangu zamani enzi nasoma kwamba shule hizi zinaharibu watoto kimaadili, siku hizi watu wamefikia mpaka hatua kusema zinafundisha ushoga na usagaji, Mimi sikubaliani kabisa na huu uzushi bali naziona ni kauli za kumasikini, Nilikuwa na marafiki kibao wa shule za serikali na nikiri kwamba niliweza kuona kwa macho yangu walioanza kuvuta bangi na kunywa viroba vya power vile vya Malawi wakiwa darasa la sita, sababu niliyokuja kugundua ni kwamba shule za serikali zina asilimia kubwa ya wazazi wasiofatilia mienendo ya watoto wao.
Na kuhusu mambo ya ushoga hasa kwa shule za baarding haya mambo yalianzia shule za serilali kwasababu shule private hazikuwepo zamani, Shule za boys kibao zinazosifika kwa mambo haya nisingependa kuzitaja nyingi ni za serikali, chanzo kikuu huwa ni kwamba shule hizi huwa na yale maisha ubabe wa wazi wazi na yabia hizi watu huzichukua katika makuzi yao huko uswazi kuleta shuleni, na ndio hapa sasa wababe wakipata wanyonge huwaingilia, Ukienda shule za private ni ngumu sana kukuta haya mambo ya ubabe, shule niliyosoma hadi usikie mtu kaonewa ilikuwa ni nadra sana, kulikuwa na ngumi tukipisha kauli lakini hakukuwa na mambo ya kuoneana.