Liverpool VPN
JF-Expert Member
- Aug 29, 2020
- 5,839
- 13,094
Introduction
Haya matokeo ya Mpira yameniuma balaa. Liverpool kapigwa. Yanga holaaaaa. Tuachane na hilo, turudi kwenye mada.
Scenario
Ngoja niongee kwa mifano halisi ili uweze kunielewa. Mimi kwa mwaka huu tu nimepata kazi nyingi sanaa za field ila jana niliangalia account nakuta kuna 500k na elfu nane tu. Sijui hela zimeenda wapi. Dah Ujana nomaaaa.
1. Safari ya Dom
Mwezi wa pili mwishoni nilipata safari ya kwenda kwenye kikao kimoja hivi cha shirika la wazungu. Shirika hilo kwa kushirikiana na Wizara inayonihusu (idara yangu) walituita Dom. Tulikaa siku 5 (Juma3 mpaka ijumaa).
Ila Dom niliondoka jumapili nikiwa sijui na hela ya chai tu. Sasa najiuliza nani kamaliza hela zangu.
Ni ile guest niliyolala pale makole, ni ile bar ya Shangwe, Rainbow pale au Bambalaga? HATA SIJUI!
2. Kazini
Narudi kazini nikakuta zoezi la kwenda kukusanya mapato mtaani. Namsikia kiongozi fulani "Lazima uende wewe ni kijana mmoja wapo tegemeo la timu ya mapato". Tukapewa posho yetu fullll, sasa kwa level ya mshahara wangu (miaka 13 kazini) nikapewa posho nzuri tu (usisahau hapo nimetoka Dom Juzi yake).
Kazi ikaanza juma5 jioni. Kufika jumapili tunaambiwa turudishe gari ofisini maana kuna ugeni mkubwaa unakuja na hilo gari ni muhimu kwenye huo msafara. Tukarudi, sasa sijui hela hata ziliishia wapi ile posho?
3. Mkoani kikao
Juma 5 ya wiki nyengine naambiwa mkoani kuna kikao hivyo natakiwa kuwepo kutoka halmashauri yangu.
Basi bwana alhamisi nikatimba na Inumaa kikao kikaisha na nikalipwa. Ila bana, kutoka mkoani mpaka home ni masaa 2 tu, Ila huwezi amini gheto nilirudi jumapili usiku. Jumamosi na Jumapili sijui nilikuwa nafanya nini kule mjini.
4. Mbeya
Tokea juma5 iliyopita nipo Mbeya. Na hii kazi iliyonileta ni ya siku 23. Hivyo nipo Sanaa Mbeya. Kuna Wizara china ya Taasisi yake imetuita. Sasa bana, jana nimekaa John liquor palee (mbele ya Ilembo jirani na Mbeya pazuri), nilifika na na Msimbazi tu, nikacheki game ya Liverpool #YNWA. Nikaona "ngoja nichukue boda niwahi Kabwe nika-draw kwenye ATM halafu nikaangalizie Mpira wa Team yangu (YANGA) Mbeya pazuri"
Sasa kufika ATM, kuna sauti ikaniambia "hebu angalia kwanza salio" Mamaaaaaaa ile kucheki naona nina 500k tuu na kaelfu nane. Nikarudi, Mbeya pazuri na mawazo yangu "Posho yoteee niliyolipwa miezi hii miwili IKO WAPII? Mbeya pazuri penyewe palikua pachunguu maana Mzize kakosa Sanaa magoli.
Problem
Kuna jini limekula hela yangu au pesa za per-diem sio za kujengea au ndio...
Big Problem
Hapo usisahau hizo hapo juu ni posho za safari tu. Bado kuna posho za:
1. Vikao
Kama vi 5 au 6 hivi nilihudhuria na kusaini hii miezi miwili.
2. Extra duty
Mimi bwana ikifika tu saa 15:31 nataka unilipe, huwezi basi acha niende home. Mwisho wa kazi ni 15:30.
3. Kuna zile unakuta, hujui kitu Mara mwana aliandika jina lako kwenye activity fulani hivi kisa anakuelewa au ulimshauri vizuri kazi yake ikaenda, unalamba posho.
4. Kuna zile "Asante afisa, kutoka kwa mteja"
Conclusion
Hivi nani anakula hela za vijana?
Anyway maisha ndio hayahaya, STAREHE MUHIMU na KUJIPA RAHA LAZIMA. Maisha yenyewe Mafupi.
#Yanga Bingwa
#YNWA
Haya matokeo ya Mpira yameniuma balaa. Liverpool kapigwa. Yanga holaaaaa. Tuachane na hilo, turudi kwenye mada.
Scenario
Ngoja niongee kwa mifano halisi ili uweze kunielewa. Mimi kwa mwaka huu tu nimepata kazi nyingi sanaa za field ila jana niliangalia account nakuta kuna 500k na elfu nane tu. Sijui hela zimeenda wapi. Dah Ujana nomaaaa.
1. Safari ya Dom
Mwezi wa pili mwishoni nilipata safari ya kwenda kwenye kikao kimoja hivi cha shirika la wazungu. Shirika hilo kwa kushirikiana na Wizara inayonihusu (idara yangu) walituita Dom. Tulikaa siku 5 (Juma3 mpaka ijumaa).
Ila Dom niliondoka jumapili nikiwa sijui na hela ya chai tu. Sasa najiuliza nani kamaliza hela zangu.
Ni ile guest niliyolala pale makole, ni ile bar ya Shangwe, Rainbow pale au Bambalaga? HATA SIJUI!
2. Kazini
Narudi kazini nikakuta zoezi la kwenda kukusanya mapato mtaani. Namsikia kiongozi fulani "Lazima uende wewe ni kijana mmoja wapo tegemeo la timu ya mapato". Tukapewa posho yetu fullll, sasa kwa level ya mshahara wangu (miaka 13 kazini) nikapewa posho nzuri tu (usisahau hapo nimetoka Dom Juzi yake).
Kazi ikaanza juma5 jioni. Kufika jumapili tunaambiwa turudishe gari ofisini maana kuna ugeni mkubwaa unakuja na hilo gari ni muhimu kwenye huo msafara. Tukarudi, sasa sijui hela hata ziliishia wapi ile posho?
3. Mkoani kikao
Juma 5 ya wiki nyengine naambiwa mkoani kuna kikao hivyo natakiwa kuwepo kutoka halmashauri yangu.
Basi bwana alhamisi nikatimba na Inumaa kikao kikaisha na nikalipwa. Ila bana, kutoka mkoani mpaka home ni masaa 2 tu, Ila huwezi amini gheto nilirudi jumapili usiku. Jumamosi na Jumapili sijui nilikuwa nafanya nini kule mjini.
4. Mbeya
Tokea juma5 iliyopita nipo Mbeya. Na hii kazi iliyonileta ni ya siku 23. Hivyo nipo Sanaa Mbeya. Kuna Wizara china ya Taasisi yake imetuita. Sasa bana, jana nimekaa John liquor palee (mbele ya Ilembo jirani na Mbeya pazuri), nilifika na na Msimbazi tu, nikacheki game ya Liverpool #YNWA. Nikaona "ngoja nichukue boda niwahi Kabwe nika-draw kwenye ATM halafu nikaangalizie Mpira wa Team yangu (YANGA) Mbeya pazuri"
Sasa kufika ATM, kuna sauti ikaniambia "hebu angalia kwanza salio" Mamaaaaaaa ile kucheki naona nina 500k tuu na kaelfu nane. Nikarudi, Mbeya pazuri na mawazo yangu "Posho yoteee niliyolipwa miezi hii miwili IKO WAPII? Mbeya pazuri penyewe palikua pachunguu maana Mzize kakosa Sanaa magoli.
Problem
Kuna jini limekula hela yangu au pesa za per-diem sio za kujengea au ndio...
Big Problem
Hapo usisahau hizo hapo juu ni posho za safari tu. Bado kuna posho za:
1. Vikao
Kama vi 5 au 6 hivi nilihudhuria na kusaini hii miezi miwili.
2. Extra duty
Mimi bwana ikifika tu saa 15:31 nataka unilipe, huwezi basi acha niende home. Mwisho wa kazi ni 15:30.
3. Kuna zile unakuta, hujui kitu Mara mwana aliandika jina lako kwenye activity fulani hivi kisa anakuelewa au ulimshauri vizuri kazi yake ikaenda, unalamba posho.
4. Kuna zile "Asante afisa, kutoka kwa mteja"
Conclusion
Hivi nani anakula hela za vijana?
Anyway maisha ndio hayahaya, STAREHE MUHIMU na KUJIPA RAHA LAZIMA. Maisha yenyewe Mafupi.
#Yanga Bingwa
#YNWA