Tundu Lissu na Kiinimacho cha Muungano

chambua ukweli zaidi juu ya mapinduzi wewe unasema baada ya kujitoa katika utawala wa kisultani lakini huku znz wanasema akupinduliwa mwarabu alipinduliwa mzanzibar tafuta ukweli zaidi juu ya mapinduzi .....na hayo mengine me naona upo sawa tu lakini huku wabongo tunachukiwa sana
 
Nyoka na nguchiro wamo chunguni na maji yameanza kupata vuguvugu. Subirini, kama hamkuweka tofari tatu juu ya mfuniko wa chungu mtajujuu. Mimi sasa natoka nje ya hiyo nyumba yenu. nasikie nyie mnaimba liwalo na liwe. Haya wajameni.
 
Kama ni hivyo, kwa nini orodha ya mambo ya muungano imekuwa ikiongezeka?

Pia kwa nini dola moja ina serikali mbili? Au ni uhusiano upi uliopo baina ya serikali ya muungano na serikali ya Zanzibar?

Pia kwa nini mamlaka ya serikali ya Tanganyika kwa mambo ambayo si ya muungano yamekasimiwa kwa serikali ya Muungano? Je hii sio sawa na kuitia serikali ya Tanganyika mafichoni, isionekane wakati taasisi zake kwa mambo yasiyo ya muungano zipo na zinaonekana? kwa mfano, mahakama ya rufaa tu ndio jambo la muungano lakini mahakama nyengine zote ni mahakama za Tanganyika. Wizara ya Afya. Wizara ya kilimo, utalii, miundo mbinu, michezo nk.

Hapa nitofautiane nawe kidogo. EU (na sio EEC) unasema ni jumuia. Foreign policy sasa linaamuliwa katika jumuia hii na hivyo nchi wanachama wa EU hazijasita kuwa dola ingawaje wamesalimisha baadhi ya powers zao Brussels, makao makuu ya EU. Pia wamo katika mchakato wa kuwa na Katiba ya EU ambayo inakataliwa kupitia kura katika nchi wanachama.

Kilichofanyika katika mkataba wa Muungano ni kukabidhi baadhi ya mamlaka kwa taasisi ya pamoja na kubakisha baadhi ya mamlaka katika serikali za pande husika.

Kama tutakubaliana na maelezo yako basi hakukuwa na sababu ya kuongeza mambo ya muungano baada ya yale 11.Kuongeza mambo ya muungano maana yake ni kuchukua mamlaka zaidi kutoka katika serikali zilizounda muungano na kuweka mamlaka hayo kwa dola ,ambayo wewe unasema ni moja na ambayo tayari iko kamili kwa vile mamlaka ya dola zile mbili yalifikia ukomo. Kama zile dola mbili hazikuwa tena na mamlaka ya kidola kwa nini serikali ya muungano ikwapue mamlaka yaliyobaki kutoka kwa serikali mbili hizo?
Kwa nini inafanya hivyo? Na kwa manufaa gani?



Joka Kuu
Dola ya Tanganyika haikukabidhi(surrender) mamlaka yake yote kwa serikali ya muungano, ndio maana msemo wa kukasimu(delegate) mamlaka yake unatumika. Pia Zanzibar haitoa mamlaka yake yote kwa Muungano, ilibakisha baadhi.
Na kama kiini macho cha kukasimisha madaraka ya Tanganyika kwa serikali ya muungano hakikufanyika ni wazi zingekuwepo serikali tatu. Serikali ya Tanganyika(mambo yasiyo ya muungano) Serikali ya muungano(mambo ya muungano) na serikali ya Zanzibar( mambo yasiyo ya muungano).

Nchi mbili zinapoungana na kuwa Nchi moja mifumo ya kawaida ya miundo ya Katiba ni miwili: Muungano wa Serikali Moja, au Shirikisho la serikali Tatu. Kwa mfumo wa kwanza kila nchi itafuta serikali yake na nchi mpya inayolizaliwa itakuwa ni nchi moja yenye Serikali moja. Katika mfumo wa pili kila nchi itajivua madaraka ambayo yatashikwa na serikali ya shirikisho na itakuwa na serikali ambayo itakuwa na mamlaka juu ya mambo yaliyobaki.

Kwa hiyo mimi nilipinga mfumo wa Serikali Moja. Shirikisho la Serikali Tatu lingekuwa ni gharama kubwa mno kwa Tanganyika. Zanzibar ingeendesha Serikali yake na kuchangia gharama za kuendesha Serikali ya Shirikisho; uk 10-11 link Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere)




Hilo nalo lilifanyika kinyemela kama ilivyofanyika kubadilisha jina la nchi kutoka Jamhuri ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuwa Tanzania. Na baada ya ukimya wa miaka 48 sasa Zanzibar wanataka kiti chao UN.

Ukiini macho huu hautaki darubini, Joka Kuu. Kila sehemu ambayo ilisomeka Tanganyika,ilibadilishwa kuwa Tanzania. Kuanzia kutoka katiba ya Tanganyika kupata ya Muungano na mengine yote.

Unafikiri kulikuwa na umuhimu wa kubadili jina la asili/awali la Jamhuri ya muungano na hivyo kulipoteza jina Tanganyika?



Ni kutokana na kulazimishwa na pia usisahau ushawishi wa nchi za US na UK katika kuundwa kwa muungano wa Nyerere na Karume.

Kama unataka kujua kuwa nchi za mataifa hazikuisahau Zanzibar fuatilia vipi wameibana serikali ya muungano na vipi wameshiriki katika kuleta miafaka baada ya migogoro iliyotokana na CCM kung'ang'ania madaraka huko Zanzibar kila baada ya uchaguzi mkuu.


Hukumu ile imeishusha hadhi mahakama ambayo uwepo wake pia umetokana na uchakachuaji kama alivyoelezea Mchambuzi.( au Lissu?). Ukiitafsiri hukumu ile ni kuwa Mahakama ilisema kuwa Zanzibar ni mkoa , wilaya au serikali ya Zanzibar ina hadhi ya serikali ya mtaa/wilaya/mkoa. Kama mahakimu hawakuwa waoga wangesema hadharani hadhi ya serikali ya Zanzibar si zaidi ya serikali ya mtaa au vipi?. Unafiki ndio unaongeza utata wa muungano huu.


Joka kuu
EU sasa imeshapita hatua ambazo iko Jumuiya ya Afrika Mashariki. Wameshafikia hatua ya kutaka kuwa na katiba ya EU.
Nafikiri kosa ambalo sisi tunafanya ni kusema Tanzania ni nchi moja, dola moja(kuelekea serikali moja?). Tanzania si nchi moja bali ni muungano wa nchi mbili, tena kwa mambo 11 tu.



Aliyekiuka mkataba wa muungano ndie ambaye anapaswa kubeba lawama ya ukiini macho/mazingaombwe haya. (Mwalimu na CCM).Mchambuzi ameataja kwa uwazi huku kukiwa na vitisho anapata kutokana na kuweka unafiki pembeni.
Tanganyika itarudi tukitaka irudi lakini kwa umma wetu wa wadanganyika ulivyo inaonekana tunapenda kuziba macho ili kiza kitawale wakati jua la kiangazi la saa 6 mchana linawaka.
Wadanganyika kwa pamoja na kwa amani tunaweza kuirudisha Tanganyika na kumaliza mazingaombwe ya muungano. Wazanzibari wameshatuonesha njia. Tudai Tanganyika yetu.

Nonda,

..Let me make it simple here.

..ukipitia the current list ya dola zinazotambulika duniani kule UN hutakuta majina ya Tanganyika na Zanzibar. Utakuta jina TANZANIA. kwa maana hiyo basi TANZANI ndiyo dola iliyochukua nafasi ya dola za Tanganyika na Zanzibar baada ya utiaji saini wa yale mambo 11 original ya muungano.

..There is only ONE government of the UNITED REPUBLIC OF TANZANIA. Kuwepo kwa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar hakumaanishi kwamba kuna serikali mbili za jamhuri ya muungano, au kuna amiri jeshi wakuu wawili. Jamhuri na dola ni moja tu, nayo ni Tanzania.


..Kuhusu hukumu ya mahakama ya Rufaa, shauri lililokuwepo mbele yake ni kama Zanzibar ni dola, na kama unaweza kutenda kosa la uhaini dhidi ya Zanzibar au serikali ya mapinduzi ya Zanzibar. Mahakama ya Rufaa ilikubaliana na hoja za chama cha CUF kwamba Zanzibar siyo dola, na pia huwezi kutenda kosa la uhaini dhidi ya Zanzibar.

..Mahakama haikuweza kutamka kwamba Zanzibar ni mkoa au wilaya kwasababu hilo halikuwa shauri lililokuwa mbele ya mahakama hiyo.


..Mwisho, hata ukisikiliza madai na kauli zinazotolewa na Maalim Seif na Ismail Jussa, wote kwa nyakati mbalimbali wamesema wanataka Zanzibar iwe "huru" tena na kuwa dola inayotambulika kimataifa.
 
Last edited by a moderator:
Huu moto hautatulia mpaka baadhi ya risasi kama zile zilizompata Shehe Anti-Kenya Mombasa last month, kosa ni pale walipolegezewa na Pinda kuwa Zanzibar ni nchi, sasa wanataka kukubaliwa kuwa ni Jamhuri, kisha watakataa Muungano wa mkataba, kisha waitaidai pwani ya Tanzania bara, kwa hiyo huyu ibilisi hatotuacha daima, ikiwezekana serikali moja haraka basi ndio njia peke nafuu, japo vifujo vya hapa na pale.
 
HOJA KWAMBA SERIKALI YA TANGANYIKA ITAKUWA MZIGO KWA WALIPA KODI NI HOJA POTOFU KUTOKA KWA WANASIASA.

CC: ndamo Emmanuel, Kobello,

Kwa muda mrefu sasa hoja kwamba Uanzishwaji wa Serikali ya Tanganyika itakuwa ni mzigo wa walipa kodi imekuwa ikitumika sana na Wanasiasa kama njia ya kuzima vuguvugu la watanganyika kudai serikali yao; Hoja hii ni potofu kwani mfumo wa sasa wa serikali mbili ni gharama zaidi kwa walipa kodi; Kwa upande mmoja, Serikali ya Tanganyika haipo, lakini ipo kwa uvunguni, huku masuala yake yote (ambayo sio ya muungano), yanashughulikiwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano, ambayo in principle, inatakiwa kusimamia Masuala ya Muungano peke yake, per Articles of the Union, 1964; Mbaya zaidi, hata masuala haya ya muungano yameongezeka kutoka kumi na moja na kukimbilia maradufu ya idadi hii; This is both – a burden to tax payers and also contravenes the Articles of the Union, 1964.
Ningependa kuanza kwa kuweka mambo yafuatayo sawa; If you believe in DECENTRALIZATION, then you must believe in FEDERAL structure of government; AND, if you believe in CENTRALIZATION, then you must believe in UNITARY Structure of Government;

Mpaka hapa nina uhakika wapo watu nilio wachanganya kidogo; Lakini hiki ndio kiini macho chetu, pole pole tutaelewana. Nina uhakika kwamba wapo watu wasiokubaliana na mimi: Wapo wenye kuamini katika Decentralization, huku pia wakiamini katika Unitary form of government; vile vile wapo wanaoamini Centralization, huku pia wakiamini Federal form of government; Vinginevyo kanuni niliyotamka i.e. If you believe in DECENTRALIZATION, then you must believe in FEDERAL structure of government; AND, if you believe in CENTRALIZATION, then you must believe in UNITARY Structure of Government, is as simple as it can get;

Ndamo Emmanuel amekuja na formula kwamba 1 + 1= 2; Niliona formula yake hii pia kule kwenye mjadala wa barubaru, na kimsingi, anaitumia kupinga dhana ya kuzaliwa kwa Tanganyika ndani ya muungano; Suala kwamba 1 + 1 = 2, halina ubishi kwani sote tumejifunza arithmetic tukiwa na umri mdogo sana; Lakini as you grow up, unajifunza kwamba katika arithmetic, there is also synergy; Pengine nifafanue maana ya neno synergy:

Synergy means – the working together of two things to produce an effect that is greater than the SUM OF THEIR INDIVIDUAL EFFECTS; In other words, you’ve two or more things together to produce a result that is not obtainable independently; In this context, 1+1 MUST NOT BE 2, but GREATER THAN TWO; Kwahiyo arithmetic wise, upo sahihi kwamba 1+1 = 2 kwani unachoangalia wewe hapa ni QUANTITY, sio QUALITY, na Mzigo in terms of QUANTITY kwa kawaida ni MZITO MNO; Lakini mzigo in terms of QUALITY, always huwa UNABEBEKA KIRAHISI SANA; Lakini hapa sina maana kwamba nakubali Tanganyika ni Mzigo, bado napinga hilo, na nitafafanua; Vinginevyo, katika mazingira ya hoja hii, mzigo maana yake ni kujiongezea majukumu, but if it if pays, WHY NOT? Isitoshe, sisi kukwepa Tanganyika, ni kukwepa MAJUKUMU; Ewe Mtoto Tanzania, Kwanini Unamkana Mzazi wako Tanganyika? Jukumu La Kumwangalia na Kumuenzi Liwe La Nani?

Zifuatazo ni Hoja Zangu Za Msingi Kupinga Hoja Kwamba Tanganyika Itakuwa ni Mzigo kwa Walipa Kodi;

Kwanza, chini ya mfumo wa shirikisho, ambao kimsingi ndio uliokubaliwa katika Mkataba wa Muungano, 1964, ni rahisi for supervision of the state(s) by the people na pia inaboresha maamuzi yawe ya haraka na yenye tija; Tofauti na hili, chini ya mfumo wa sasa, kuna mkanganyiko mkubwa sana katika maamuzi, kwani maamuzi muhimu huchukua muda mrefu, kupitia VIKAO VIKAO VIKAO, vinavyogharimu sana walipa kodi; Serikali shirikishi ya Tanganyika ikirudi sambamba na serikali ya Zanzibar, kutakuwa na gharama ndogo zaidi za kusimamia watumishi wa umma, kwani watumishi watakuwa ni wachache zaidi, miradi itakuwa ni michache zaidi, na hii itapunguza mzigo kwa walipa kodi; ili kuelewa hili kwa undani, zingatia mfumo wa sasa ambapo masuala ya muungano na masuala ya Tanganyika, yote yanagharimiwa na serikali ya Jamhuri wa Tanzania; huu ni mzigo mkubwa sana, lakini pia ni kinyume na Mkataba wa Muungano, 1964;

Pili, kwa sababu serikali/nchi shirikishi hazitakuwa na mamlaka ya kuchapisha fedha ovyo kama ilivyo sasa chini ya serikali ya JMT, au kuchota chota hela kwa visingizio vya ovyo kama ilivyotokea wakati wa EPA, au kuchukua mikopo ndani na nje kiholela holela, mfumo wa shirikisho utapunguza sana this abuse of resources;

Tatu, mfumo wa shirikisho unazipa nchi washiriki motisha na uwanja mpana zaidi wa ushindani – kiutendaji, kiufanisi, balancing the budget n.k, kwani serikali itakayokosea katika haya itaonekama wazi; hii itapunguza sana ‘WASTES’ na inasaidia uwepo wa mchanganyiko mzuri baina ya mapato kutokana na KODI na HUDUMA za kijamii zinazotolewa; Kwa mfano, nchi ya New Zealand inafuata Unitary Form of Government kama Tanzania, lakini gharama za uendeshaji wa nchi hiyo, ni kubwa kuliko taifa kubwa zaidi na jirani yake la Australia, ambalo linafuata Federal form of Government; Kutokana na hili, New Zealand wanajaribu kubadilika;

Nne, kwa vile Federation means Decentralization, hii insaidia sana supervision ya umma juu ya serikali; Chini ya shirikisho, serikali husika ubanwa ili kufanya MAAMUZI BORA, tofauti na chini ya Unitary Government ambapo serikali hupata mianya ya kufanya BORA MAAMUZI; Sina haja ya kufafanua hili kwa undani kwani sote tunaona kule Kungeni jinsi Makofi ya wabunge yanavyoambatana na Majibu ya “NDIYOOOO”, huwa yanaunga mkono zaidi maamuzi ya aina gani kati ya: “MAAMUZI BORA na BORA MAAMUZI.” Vinginevyo maamuzi bora chini ya shirikisho yanachangiwa sana na hali ya ushindani iliyopo baina ya nchi shirikishi, hasa kutokana na ukweli kwamba chini ya shirikisho, member states have the RIGHT OF CHOICE & EXIT; Kwa maana nyingine rahisi, nchi shirikishi wanakuwa kwenye mkao wa Kujitegemea Zaidi, hivyo kujituma zaidi, kuliko chini ya mfumo wa Unitary ambao umejaa uvivu, kutojituma, kutegeana, na mkao wa kutegemea zaidi;

Ebu tutazame kwa undani kidogo jamii za wenzetu zinatuonyesha nini; Tukianza na marekani, kutokanana mfumo wake shirikishi, hii inajenga sana hali ya Uwazi katika utendaji wa serikali zote yani serikali shirikishi (states) na serikali kuu (Federal), kwani maamuzi na matendo ya serikali yanaonekana kwa urahisi zaidi na umma kuliko chini ya Unitary government kama yetu; Kumekuwa na tafiti nyingi pia zinazoonyesha kwamba, Economic growth, Economic development, and Civilization Marekani ilichangiwa sana na MFUMO WA SERIKALI WA FEDERATION;

Tutazame mfano wa pili, ambao unatuhusu zaidi sisi; Wakati wa ukoloni, Mjerumani alitumia mfumo wa DIRECT RULE kututawala, na mfumo huu ulimgharimu sana; Alipokuja Mwingereza, mara moja akabadilisha mfumo kutoka ule wa DIRECT RULE, na kwenda kwenye INDIRECT RULE, kwani alijua kwamba Indirect System of Rule is Less costly and more Efficient – delivers more; Mwingereza alilenga kuokoa gharama; kwa maana nyngine rahisi, maamuzi ya mwingereza kubadilisha mfumo kutoka DIRECT kwenda INDIRECT yalichangiwa sana na ECONOMIC REASONS than POLITICAL REASONA, ingawa watanzania tunapenda kulitazama hili the other way round; Lakini hii ni kawaida yetu kwani wanasiasa wametuambukiza kuweka Politics iwe SUPREME to everything else, so the damage has already been done!

Tukirudi kwenye hoja ya msingi kuhusu kupungua kwa gharama za usimamizi chini ya federation – Usimamizi wa karibu wa wananchi kwa serikali is a FUNCTION ya Gharama Ndogo za Usimamizi; hii ni kwasababu, kwanza watumishi wa serikali wanakuwa ni wachache zaidi, na kama tulivyo kwisha ona, vile vile kunakuwepo miradi michache zaidi na yenye kulenga maeneo muhimu zaidi kwa wananchi; kwa maana nyingine, application ya 20-80 principle inakuwa rahisi – yani matumizi ya 20% of resources/input kupata 80% Output, tofauti na sasa ambapo seriali yetu ya JMT inatumia 80% of input/resources, lakini Output ni 20%;

Ni suala la mantiki tu hapa kwamba chini ya shirikisho ambapo Tanganyika na Zanzibar zinakuwa na serikali zake huru, kiasi cha kodi kitachotumika kitakuwa ni kidogo zaidi; Wananchi wataweza kusimamia watendaji wa serikali kwa ufanisi na urahisi zaidi when everything is SMALLER; Kumbuka, Mfumo wa sasa wa Serikali Mbili is BIG GOVERNMENT [rejea orodha ya masuala ya muungano tokea mwaka 1964 hadi sasa], wakati mfumo wa Serikali Tatu is SMALL GOVERNMENT[masuala ya muungano yanapungua, huku kila nchi ikijikita na masuala yake kwa kutumia mapato yake]; Kama hili bado ni gumu kulielewa, basi niwape pongezi wanasiasa kwa kuweza kupandikiza kiini macho hiki ambacho pengine kamwe hakitatoweka;

Sababu nyingine kwanini shirikisho ni bora zaidi kwa wananchi ni kwamba – Serikali kubwa kama hii yetu ya JMT– ambayo tuna aminishwa ni Serikali mbili, ukweli ni kwamba – serikali ya Jamhuri ya Muungano wa TANZANIA inasimamia mambo yote ya muungano na yale ya Tanzania Bara (TANGANYIKA), ambayo SIYO ya Muungano, kama Afya, Elimu n.k; Huu ni mzigo mkubwa, lakini pia ni gharama kubwa zaidi kwa walipa kodi; Serikali ya sasa ya JMT ipo more Centralized na ni kubwa sana kuliko ingekuwa chini ya mfumo wa shirikisho; Tatizo jingine linalojitokeza hapa ni kwamba, mfumo wa sasa una ‘encourage’ wasteful lobbying of different interest groups, suala ambalo Wachumi wanalijadili kama dhana ya ‘RENT SEEKING’ – kwa maana rahisi, rent seeking ni utafutaji wa benefits & priveledges za different interest groups, e.g. wawekezaji pamoja na wale wote wanaotaka kufanya biashara na Serikali; Tumekuwa tunashuhudia hili kwa miaka mingi sana tabia hii ya rent seeking; mabilioni yaliyopo Uswisi ni moja ya mifano hai;

Ni rahisi sana kwa tabia ya rent-seeking kulelewa chini ya mfumo wa serikali kubwa na centralized kama hii ya JMT kuliko chini ya serikali ndogo ambayo ipo more decentralized - shirikisho; kwa maana nyingine, ni rahisi sana kwa wananchi/UMMA kuona nini kinaendelea chini ya mfumo wa shirikisho kuliko chini ya mfumo wa sasa ambao, bila ya wabunge kuamua kumwaga siri hadharani, au watendaji serikalini kuamua kuvujisha siri za serikali, nchi yetu chini ya mfumo wa serikali mbili wa JMT, itaendelea kitafunwa mchana kweupe; Hii ni gharama kubwa kwa walipa kodi kwa maana rahisi sana – miradi mingi nchini, chini ya serikali ya mfumo wa sasa, maamuzi yake hayapo transparent, haieleweki upande gani wa muungano unachangia na unachangia kwa lipi, miradi mingi wananchi hawaijui, hawashirikishwi kimaamuzi, na tumeona kwamba wananchi wakija fahamu juu ya miradi hii, huwa hawaridhii baadhi ya miradi hiyo; ingawa inafanikishwa kupitia fedha zao; mifano hai ya miradi ya namna hii mnaijua;

Hoja nyingine ni kwamba – tukubali kwamba uwepo wa nchi kubwa (physical size) bila ya mfumo wa shirikisho is UNGOVERNABLE; Kwa mfano, tazama hali za wananchi wa vijijini nchini “TANZANIA BARA”; Serikali imekuwa mbali sana na wananchi hawa lakini ni kutokana na mfumo mbovu wa sasa wa serikali; Wapo wanasiasa watakaojenga hoja kwamba serikali imesogea zaidi kwa wananchi kupitia Serikali za Mitaa; Hoja hii inazidi kuichongea serikali kuliko kuitetea kwa maana rahisi sana: Decentralization inafanyika katika maeneo yote, lakini linapokuja suala la maamuzi ya kule chini jinsi gani fedha zitumike, this decision remains centralized; tatizo lingine ni kwamba, fedha huwa hazifiki kule kwa wakati, na mara nyingine hazifiki kabisa; Kwahiyo YES, tuna decentralization, but not in RESOURCES, and that makes a huge Difference;


Nikiwa bado katika hoja hii kwamba “uwepo wa nchi kubwa (physical size) bila ya mfumo wa shirikisho is UNGOVERNABLE”, hata Rais wa tatu wa Marekani, Thomas Jefferson, wakati wa uongozi wa nchi hiyo iliyokuwa na idadi ya majimbo chini ya nusu ya idadi ya leo, alipata kutamka kwamba – Taifa la Marekani ni kubwa sana na ni mzigo iwapo masuala mengi yataendelea kuwa chini ya serikali moja; Tukirejea kwenye hoja kuhusu mfumo wetu, Muungano wetu ulianza na masuala kumi na moja tu ya muungano, lakini leo idadi ya masuala haya imeongezeka badala ya kupungua; Hoja ya msingi hapa ni kwamba – iwapo kweli tupo serious na kujenga taifa la kidemokrasia na lenye kusimamia vyema fedha za walipa kodi, na lenye nia ya kweli ya kuulinda muungano wetu, basi - DEVOLUTION OF POWER IS INEVITABLE!!

Ningependa nimalizie kwa kusema kwamba - Viongozi wanaopinga hoja ya Tanganyika huwa wanajisahau kwamba: “GOVERNMENTS EXISTS FOR THE PEOPLE”. Kama wanakubaliana na dhana hii, basi ikifikia wakati wa UMMA wa “Tanzania Bara”, kutaka Sheria Namba 24 ya Bunge, 1967, iliyofuta Jina la Mzazi wa Tanzania - yani ‘TANGANYIKA’ na kuja na Jina Jipya la Mzazi huyo kuwa kuwa ‘TANZANIA BARA”, ikifikia hatua ya UMMA kutaka sheria hii ya bunge ibadilishwe, basi nia yao itakuwa ni nzuri tu kwamba: Wanataka serikali yao irudi ili iwe karibu zaidi nao kuliko hali ya sasa ambapo ambapo masuala ya Muungano na Masuala Yasiokuwa ya Muungano, yote yanaendeshwa na serikali hiyo hiyo ya Muungano, huku Zanzibar wakiwa na serikali yao inayosimamia mambo yasiokuwa ya muungano;

Matakwa kama haya yakijitokeza kwenye UMMA, ni wajibu wa viongozi kufuata matakwa haya, hasa iwapo wanaamini katika dhana kwamba: GOVERNMENTS EXISTS FOR THE PEOPLE.” Tukirudi kwenye dhana ya MZIGO kwa UMMA, tukiondoa kiini macho hapa, maana rahisi ya MZIGO ni “More Responsibility”, na pia “Hali ya Kujituma Zaidi”, kitu ambacho wananchi wengi wamekuwa wanafanya hivyo katika kuendesha maisha yao [kupitia kodi], lakini wamekua wakiambuliwa ‘return’ ndogo sana. Isitoshe, zipo tafiti zinazo onyesha kwamba, wananchi wapo tayari hata kulipa kodi zaidi IWAPO TU, wataona kuna manufaa katika kufanya hivyo; Ujio Wa Serikali ya Tanganyika maana yake, wananchi wa TANZANIA BARA kuwa karibu zaidi na serikali yao kama nilivyojadili, hvyo kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kupata huduma zitazoendana na malipo yao ya kodi; Kwa kutumia dhana yetu ya MZIGO, Wananchi hawa watakuwa tayari kujituma zaidi, kwani kufanya hivyo itakuwa ni kwa manufaa yao wenyewe.

Ningependa nimalizie kwa swali lifuatalo:


  • JE: Tunawezaje Kujenga Spirit ya KUJITEGEMEA iwapo hatujui Tunajitegemea katika mambo yepi kutokana na kiini macho cha muungano?



 
Mchambuzi

1. Umefanikiwa kuibua michango ya kila mtazamo.

2. Kama ni academic exercise imefanikiwa pia.

3. Maudhui na madhumuni ya thread yako yananitatiza kwa sababu sielewi unachotaka kuanikisha kwenye huu mjadala kama umekipata basi ujue baadhi yetu hususan mimi binafsi umeniacha bila cha kushika cha kusonga nacho mbele.

4. Nashauri utoe majumuisho kama update ili angalau tuende na maoni ya wengi.

5. Pamoja na yote, hujagusia kukosekana kwa hotuba ya TL kwenye Hansard, sijui ndiyo umeridhika au funika kombe.

6. Unapopewa changamoto na ambao wanakerwa na michango yako, tushirikishe nasi tuwachome zaidi maana hii fursa ni ya members na wageni kama hao wafaidike au wajitazame walivyo kama wanavyojitazama kwenye kioo.

Bado nakupongeza natumaini utaendelea na moyo wako wa kutupa hoja zenye changamoto na kujitahidi kutujibu inapowezekana na ionapostahili.
 
Nonda,

..Let me make it simple here.

..ukipitia the current list ya dola zinazotambulika duniani kule UN hutakuta majina ya Tanganyika na Zanzibar. Utakuta jina TANZANIA. kwa maana hiyo basi TANZANI ndiyo dola iliyochukua nafasi ya dola za Tanganyika na Zanzibar baada ya utiaji saini wa yale mambo 11 original ya muungano.

..There is only ONE government of the UNITED REPUBLIC OF TANZANIA. Kuwepo kwa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar hakumaanishi kwamba kuna serikali mbili za jamhuri ya muungano, au kuna amiri jeshi wakuu wawili. Jamhuri na dola ni moja tu, nayo ni Tanzania.


..Kuhusu hukumu ya mahakama ya Rufaa, shauri lililokuwepo mbele yake ni kama Zanzibar ni dola, na kama unaweza kutenda kosa la uhaini dhidi ya Zanzibar au serikali ya mapinduzi ya Zanzibar. Mahakama ya Rufaa ilikubaliana na hoja za chama cha CUF kwamba Zanzibar siyo dola, na pia huwezi kutenda kosa la uhaini dhidi ya Zanzibar.

..Mahakama haikuweza kutamka kwamba Zanzibar ni mkoa au wilaya kwasababu hilo halikuwa shauri lililokuwa mbele ya mahakama hiyo.


..Mwisho, hata ukisikiliza madai na kauli zinazotolewa na Maalim Seif na Ismail Jussa, wote kwa nyakati mbalimbali wamesema wanataka Zanzibar iwe "huru" tena na kuwa dola inayotambulika kimataifa.

Zanzibar ni nchi huru yenye jeshi huru na amiri jeshi mkuu ambaye ni rais wa Zanzibar. Rejea katiba ya Zanzibar ya Mwaka 2010 utapata majibu yote. Kuhusu hukumu ya mahakam ya rufaa, ikumbukwe kuwa hukumu na kesi hii vilitokea kabla ya mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010.

Kuhusu Jusa na Hamad, wote wasumbuliwa tu na upeo mdogo wa uelewa. Wanaongea kutokana na mazoea ya nyuma tu na huwa nadhani hawaisomi hiyo katiba yao mpya. Wakiisimamia kwa umakini, nakuambia Zanzibar inakuwa dola huru kabisa bila tatizo lolote kwani katiba yao ndivyo inavyosema.

Tatizo kubwa ni kuwa Rais wao bado ana uprimitive kwani aliwekwa na Watanzania bara hivyo hana jeuri ya kwenda kinyume na waliomuweka madarakani. Kama rais Shein leo akiamua Zanzibar itekeleze mambo yake yenyewe kama mabadiliko ya katiba yao yanavyosema, Zanzibar inakuwa huru kabisa.
 
Nguruvi3,

Kwa kawaida, kuwasili kwako huwa ndio mwanzo wa mjadala, Kwahiyo karibu sana; Naomba nijibu hoja zako moja baada ya nyingine kama ifuatavyo:
Muungano una matatizo tena makubwa, nashukuru nilianza kuliona hili wakati nilipohoji kwanini twende Zanzibar kwa Passport? Hapo ndipo nilianza kufuatilia muungano na nashukuru kuwa yote yanayoongelewa na akina Lisu niliyaona mapema sana, tena mengine hayakusemwa.
Kwanza naomba niseme kwamba nimekuwa nasoma hoja zako nyingi juu ya muungano wetu, lakini sikuwa na interest ya kujiingiza sana katika mjadala wowote wa muungano kwani nilikuwa sina uelewa sana, hasa wa kisheria juu ya suala hili; Vinginevyo kama ni suala la mtazamo uliojaa hoja za kisiasa, hakika tungekuwa tunakesha kwani hoja hizo zipo nyingi tu; vinginevyo mjadala wenye manufaa zaidi, in my humble opinion, ni uliojaa hoja za kisheria zaidi; Sasa nipo tayari kujadili suala la Muungano kwani nimefanya utafiti wa kutosha, tena utafiti huru na kwa umakini mkubwa sana; Iwapo kuna neno moja tu la mwisho ninalo weza kulitamka kabla ya kuishiwa pumzi, basi neno hilo ni "TANGANYIKA", iwapo sauti itakuwa imeniisha na nitakuwa nakoroma kukata roho, na kuwa na nafasi ya kuongezea neno lingile kimkoromo, basi neno hilo ni "IRUDI".

Nguruvi3, natambua kwamba sote tuna nia ya kuokoa nchi yetu isiingie katika machafuko yasio ya lazima, kabla hatujachelewa; Tofauti yangu na wewe katika hili ni jinsi ya kufikia kwenye jamii ya namna hiyo, huku wewe ukiegemea zaidi kwenye hoja kwamba hatuwahitaji wazanzibari kwa mtindo wao wa sasa kwani haujengi bali unabomoa muungano, huku mimi nikiwa na mtazamo kwamba, ni kweli muungano unakabiliwa na mgogoro mkubwa sana, lakini nina amini zaidi katika kurejea kwenye Mkataba wa Muungano 1964, na kuangalia ni wapi tulijikwaa; na iwapo tukikubaliana katika meza moja na ndugu zetu wazanzibari kwamba hakuna haja ya kurekebisha tena yaliyokiukwa, na badala yake tusonge mbele kwa mikataba mipya n.k, hili litapunguza sana msimamo wangu wa sasa; Kinachoendelea sasa visiwani kwa mtazamo wangu sio official, ni choko choko tu; ninachosuburia ni referendum ya wananchi wa Zanzibar juu ya hatima ya muungano; Sitaki kuwasikiliza wanasiasa wao kwani hawa watapita katika utawala na watakuja wengine; kwa maana nyingine, naunga mkono hoja yako ya awali kwa barubaru, hasa pale ulipotamka kwamba udhaifu wa mwinyi ndio ulipelekea wabunge wale 55 kufanya walichofanya na hii ilikuwa ni hatari kwa taifa letu; Ninawatazama viongozi wa Zanzibar wenye kutoa kauli zao mbalimbali juu ya muungano kwamba wana hasira na madhaifu fulani, kama vile wale G-55 walivyokuwa na hasira na utawala wa Mwinyi; Madhaifu ya sasa kwa mtazamo wangu kweli yapo, lakini iitishwe referendum ili wananchi waamue' Until then, nitaunga mkono hoja kwamba Muungano uendelee lakini Per Articles of the Union, 1964, ambapo Serikali ya Tanganyika ilitambuliwa;
Kwanza nieleze kuwa sikubaliani na dhana ya kuwa wazanzibar wanauelewa mkubwa kuliko sisi. nina sababu za kusema hivyo.
Naelewa mantiki nzima nyuma ya hoja yako hii; Maana rahisi ya hoja yangu katika hili ni kama ifuatavyo: Katika mjadala wa Muungano, najaribu sana kutanguliza sheria kuliko siasa; Kwahiyo, kwa vile Muungano uliundwa kwa mujibu wa sheria, na kuja kubomolewa kwa mujibu wa siasa, kujenga hoja za kisiasa kuujadili hakuujengi bali kuzidi kuubomoa; Sheria Mama ya Muungano ilikuwa ni Mkataba wa Muungano, 1964, na leo hii, mkataba huu unaendelea kuwa nguzo kuu ya Muungano; Kwa vile Nguzo hii ilitikiswa, hasa kwa ukiukwaji wa wazi kabisa wa masharti ya Muungano chini ya Mkataba wa 1964 – hasa kutotekelezwa kwa kipengele cha SABA cha Mkataba wa Muungano, 1964, na pia kwa vile Katiba ya sasa ya JMT (1977) imejengwa kwa mfumo wa Muungano nje ya makubaliano chini ya Mkataba wa Muungano, 1964, Mgogoro wa Muungano remains kuwa "THE ZANZIBAR QUESTION", huku taratibu ukianza pia kujenga sura ya "THE TANGANYIKA QUESTION." Nikirudi kwenye hoja yangu ya msingi katika hili, ndugu zetu wa Zanzibar wanachokidai na walichokuwa wanakidai katika kipindi chote, ni kitu halali, yani – kupata their autonomy per articles of the Union, 1964; Kwa maana nyingine, sehemu kubwa ya madai yao, kiini chake ni uchakachuaji wa Mkataba wa Muungano, 1964, kupitia Katiba ya Muda 1965, na baadae katiba ya 1977; Ndio maana nazidi kusema kwamba – madai yao ya Zanzibar huru yaende sambamba na madai yetu ya Tanganyika huru, kwani hivyo ndivyo Mkataba wa Muungano, 1964, ulivyopendekeza; Kwa mtazamo huu, wazanzibari kuwa na ufahamu juu ya tatizo hili, tena kwa miaka mingi, ndio imepelekea nije na hoja kwamba, wao ni waelewa zaidi yetu;
Pili, ninaona tunazungumzia serikali 3, mkataba n.k. Kuna maswali muhimu tunayotakiwa tuyajibu kwanza kabla ya kufikiri twende wapi:1. Kwanini watu wanadhani tunahitaji muungano wa nchi mbili.
Hili ni swali muhimu sana; Majibu yake rahisi:Kwanza – Serikali mbili hivyo ndivyo walivyozoeshwa na utawala wa CCM, kuanzia pale TANU ilipochukua hatamu za nchi kwa uchakachuaji Kupitia Katiba muda ya JMT, 1965, ambapo katiba ya TANU ilikuwa ni sehemu ya Katiba ya nchi, kinyume na Makubaliano ya Muungano, 1964; Na mkakati huu ukapigiliwa msumari wa mwisho ulioua Tanganyika pale Sheria maalum ya bunge ilipopitishwa mwaka 1967 ya kuifuta Tanganyika; Kilichofuata baadae, hasa mwaka 1977 ni TANU kufanikiwa kuwaingiza ASP line ili wajiunge na TANU ili kuzaa CCM (1977), na hapo ndipo CCM ikashika hatamu kwenye kila nyanja ya nchi; Polisi, Jeshi, utumishi wa umma, n.k. Kwahiyo, watanzania wengi wamekuwa wanaishi chini ya utamaduni huu, na wameuzoea na hawaoni kama una shida yoyote; Sababu ya pili katika majibu yangu juu ya hili ni kwamba BABA WA TAIFA alipendelea mfumo uliopo, na sidhani kama kuna haja ya kufafanau influence yake katika hili; Lakini narudia tena, mimi ni muumini mkubwa sana wa Nyerere, hasa falsafa yake, lakini nikiwa kama binadamu mwenzako, alikuwa na yeye ana mapungufu; Nia ya muungano ilikuwa safi, lakini njia ya kufikia huko ndio Tatizo mpaka leo, kwani Muungano huu ulianza na a Political Union kwa matarajio kwamba, it would trickle to Economics and Social; This can never happen;
2. Kwanini watu wanadhani tunahitaji serikali 3… au mkataba.
Angalau jibu kwa swali lako hapo juu lina uhakika zaidi hata kama hatujakuwa na referendum kuhakikisha iwapo umma unataka mfumo wa sasa uendelee au ubadilike; Sasa tukija kwenye swlai lako la pili, unaposema "WATU", mimi sina jibu mpaka referendum ije, vinginevyo nina majibu ya mtazamo wa MTU MMOJA MMOJA; Mtazamo wangu kwa mfano nadhani umeshauelewa kwani ndio nguzo kuu ya mada yangu – yani, kurudishwa kwa Tangayika per articles of the Union, 1964, pamoja na kuheshimu mambo mengine yote yaliyokubaliwa chini ya mkataba ule;
Kwanini watu wanadhani tunahitaji mkataba?
Mkataba ninao utambua mimi ni ule wa Muungano, 1964; Kwahiyo, binafsi, mkataba ninao uhitaji ni ule ule wa 1964, turejee tulipokosea ili tufanye muungano wetu uwe na uhalali wa kisheria, tofauti na sasa;
3. Kwanini watu hawazungumzii kuvunja muungano?
Again, suala la WATU litakuwa na mashiko kupitia referendum vinginevyo kwa sasa itakuwa ni maoni ya mtu mmoja mmoja au makundi madogo madogo ya watu yenye malengo tofauti towards that end; Sasa ikiwa unataka kujua mawazo yangu juu ya hili – ni kama nilivyosema hapo awali kwamba nina amini katika Muungano kwani Umoja ni Nguvu, Utengano ni Udhaifu, hasa katika mazingira ya dunia ya leo; Lakini tatizo ni kwamba, wanasiasa wanajaribu kuu ‘leapfrong' muungano huu badala ya kuacha upitie evolution process kama ilivyokuwa kwa aina nyingine za muungano duniani; Kizazi chetu cha leo kijikite zaidi kutoa uhuru kwa nchi shirikishi kwani hivyo ndivyo muungano wetu utadumu na kuwa na manufaa kwa wananchi; iwapo tutawarithisha vitukuu vyetu mfumo unaoendana na Articles of the Union, wao sasa watakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuamua whether waende for serikali mbili au moja; Vinginevyo tusiwe wabinafsi kwa kutaka ku – fast track muungano huu, just kutafuta legacy ya kuacha au kutafuta maslahi binafsi;
 
Ndamo Emmanuel amekuja na formula kwamba 1 + 1= 2; Niliona formula yake hii pia kule kwenye mjadala wa barubaru, na kimsingi, anaitumia kupinga dhana ya kuzaliwa kwa Tanganyika ndani ya muungano; Suala kwamba 1 + 1 = 2, halina ubishi kwani sote tumejifunza arithmetic tukiwa na umri mdogo sana; Lakini as you grow up, unajifunza kwamba katika arithmetic, there is also synergy
Sikubaliani na hoja ya Ndamo. Muungano unakuwa best expressed arthimetically by {A} U {B}. Muungano wa seti mbili kufanya seti moja.Yaani {Tanganyika} U {Zanzibar} = {Tanganyika, Zanzibar} na seti itayopatikana haina {Tanganyika, Zanzibar, JMT}.

Synergy means – the working together of two things to produce an effect that is greater than the SUM OF THEIR INDIVIDUAL EFFECTS; In other words, you've two or more things together to produce a result that is not obtainable independently; In this context, 1+1 MUST NOT BE 2, but GREATER THAN TWO; Kwahiyo arithmetic wise, upo sahihi kwamba 1+1 = 2 kwani unachoangalia wewe hapa ni QUANTITY, sio QUALITY, na Mzigo in terms of QUANTITY kwa kawaida ni MZITO MNO; Lakini mzigo in terms of QUALITY, always huwa UNABEBEKA KIRAHISI SANA......... Ewe Mtoto Tanzania, Kwanini Unamkana Mzazi wako Tanganyika? Jukumu La Kumwangalia na Kumuenzi Liwe La Nani?
Mkuu hizi ndiyo tunaziita siasa.
anza, chini ya mfumo wa shirikisho, ambao kimsingi ndio uliokubaliwa katika Mkataba wa Muungano, 1964, ni rahisi for supervision of the state(s) by the people na pia inaboresha maamuzi yawe ya haraka na yenye tija;na mamlaka ya kuchapisha fedha ovyo kama ilivyo sasa chini ya serikali ya JMT, au kuchota chota hela kwa visingizio vya ovyo kama ilivyotokea wakati wa EPA, au kuchukua mikopo ndani na nje kiholela holela, mfumo wa shirikisho utapunguza sana this abuse of resources
Hapa unamaanisha nini? Mamlaka haya yapo chini ya legislature, central bank au executive? Je, makosa ya EPA ni systemic, traditional, political au combination of both/some? Kwa sababu matumizi ya serikali yapo chini ya bunge, be it unitary or federal. Na matumizi mabaya ya fedha in national or subnational levels hutegemea zaidi uwepo wa police-able policies.

Tatu, mfumo wa shirikisho unazipa nchi washiriki motisha na uwanja mpana zaidi wa ushindani – kiutendaji, kiufanisi, balancing the budget n.k, kwani serikali itakayokosea katika haya itaonekama wazi; hii itapunguza sana ‘WASTES' na inasaidia uwepo wa mchanganyiko mzuri baina ya mapato kutokana na KODI na HUDUMA za kijamii zinazotolewa; Kwa mfano, nchi ya New Zealand inafuata Unitary Form of Government kama Tanzania, lakini gharama za uendeshaji wa nchi hiyo, ni kubwa kuliko taifa kubwa zaidi na jirani yake la Australia, ambalo linafuata Federal form of Government; Kutokana na hili, New Zealand wanajaribu kubadilika;
Vipi kuhusu Norway (+12), US (-10) deficit?
Mkuu bila siasa, decentralization inabring about efficiency but there are federal states that are less decentralized than Unitary states. Mfano ni China na France, hii ni kutokana na mfumo wa kiuchumi na mammbo mengine ya kisiasa.
Nne, kwa vile Federation means Decentralization, hii insaidia sana supervision ya umma juu ya serikali;
Has EU decentralized or centralized Europe? Mkuu usichanganye mambo, decentralization na Federation are parallel, so is with unitarian form of government. This depends on policy.Ukiiruhusu halmashauri ya wilaya ya ilala kutoza 5% tax kwa transactions zote, basi hata ukusanyaji wa kodi zanzibar (kwa sasa hivi) utapitwa, thats just a matter of policy.
Kwa maana nyingine rahisi, nchi shirikishi wanakuwa kwenye mkao wa Kujitegemea Zaidi, hivyo kujituma zaidi, kuliko chini ya mfumo wa Unitary ambao umejaa uvivu, kutojituma, kutegeana, na mkao wa kutegemea zaidi;
Ukosefu wako wa vielelezo unafanya hoja hii kuwa ya kisiasa zaidi.

Ebu tutazame kwa undani kidogo jamii za wenzetu zinatuonyesha nini; Tukianza na marekani, kutokanana mfumo wake shirikishi, hii inajenga sana hali ya Uwazi katika utendaji wa serikali zote yani serikali shirikishi (states) na serikali kuu (Federal), kwani maamuzi na matendo ya serikali yanaonekana kwa urahisi zaidi na umma kuliko chini ya Unitary government kama yetu; Kumekuwa na tafiti nyingi pia zinazoonyesha kwamba, Economic growth, Economic development, and Civilization Marekani ilichangiwa sana na MFUMO WA SERIKALI WA FEDERATION;
Federation ni kinyume na unavyofikiria, huku federalist ni unitarist na confederacy ndiyo federalism unayoiadvocate. Mkuu kaa chini na utafakari kidogo.Ni nguvu za FEDERAL government zilizoleta civilization to the states, not otherwise.
ja nyingine ni kwamba – tukubali kwamba uwepo wa nchi kubwa (physical size) bila ya mfumo wa shirikisho is UNGOVERNABLE; Kwa mfano, tazama hali za wananchi wa vijijini nchini "TANZANIA BARA"; Serikali imekuwa mbali sana na wananchi hawa lakini ni kutokana na mfumo mbovu wa sasa wa serikali; Wapo wanasiasa watakaojenga hoja kwamba serikali imesogea zaidi kwa wananchi kupitia Serikali za Mitaa; Hoja hii inazidi kuichongea serikali kuliko kuitetea kwa maana rahisi sana: Decentralization inafanyika katika maeneo yote, lakini linapokuja suala la maamuzi ya kule chini jinsi gani fedha zitumike, this decision remains centralized; tatizo lingine ni kwamba, fedha huwa hazifiki kule kwa wakati, na mara nyingine hazifiki kabisa; Kwahiyo YES, tuna decentralization, but not in RESOURCES, and that makes a huge Difference;
Kwanini fedha zifike kule na zisitoke kule?
: Tunawezaje Kujenga Spirit ya KUJITEGEMEA iwapo hatujui Tunajitegemea katika mambo yepi kutokana na kiini macho cha muungano?
Hatuwezi kujua, kwa sababu muungano huu bado haujaridhiwa na umma. Thats the basic point ambayo nadhani unai-circumlocute;Tatizo siyo mfumo, tatizo ni ridhaa.


 
Mkuu Mtambuzi,

Salute, mimi sina mchango kwenye hii thread so far lakini nashukuru sana kwa kuweka hii thread na washukuru sana wachangiaji wote, my question is, where are you old guards of the betterment of this country are hiding? Ni MMKJ tu sijamuona huku, jamani hi nchi in watu talented i wish hizi bongo zingekuwa ndani ya govt, we'll millions miles away in development aspects, HONGERA MCHAMBUZI
 
Kobello,

You are such a spinner; Una rangi zote za CCM, na ingawa mimi ni mwanachama mwenzako wa CCM, wewe nadhani umekubali kutumia intellectual capacity uliyonayo kutumikia the status quo; Thats not what intellectuals are meant to be, especially kwenye jamii kama yetu ambapo tuliojaliwa upeo na elimu, tuna wajibu mkubwa sana wa kuwaeleweesha wale less fortunate kwenye jamii yetu juu ya nini kinaendelea katika maisha yanayowazunguka, na wafanye nini ili maisha yawe yawe nafuu, kama sio bora zaidi;

Tukianza na hoja kuhusu arithmetics za muungano, I believe more in synergy kama nilivyobainisha; vinginevyo ni sahihi tukiwa na mgongano wa mawazo katika hili;

Pili, hoja yako kuhusu mimi kutumia siasa zaidi ya sheria kuhusu mfumo uliokubaliwa chini ya Mkataba wa Muungano, ukipata muda, rejea mkataba ule mstari kwa mstari, halafu urudi kujenga hoja yako kupingana na mimi kwamba muungano ule nia yake ilikuwa ni kitu kingine nje ya serikali tatu; Nikudokeze tu kwamba ushirikiano wa mataifa hufuata mikondo mikuu mitatu:


  • Serikali Moja:
Pale ambapo ushirikiano huu SIO WA HIARI bali wa kulazimishwa na mwenye nguvu dhidi ya taifa hafifu kama vile ilivyotokea katika uhusiano wa uingereza na Ireland ya kaskazini; Serikali inayozaliwa chini ya mfumo huu ni ile ya mfumo mmoja, na chini ya mfumo huu, nguvu zote za mamlaka zinawekwa chini ya serikali ya bwana mkubwa; Dhana hii inakwenda kinyume na Mkataba wa Muungano, 1964, na hakuna ushahidi wowote kwamba dhamira ya muungano wetu ilikuwa ni hiyo kwani hakuna msingi na ushahidi wowote wa kihistoria, kisheria na kikatiba kwamba hiyo ndio ilikuwa ni nia ya waasisi wetu wawili; Kumbuka, chini ya Mkataba wa Muungano, 1964, kuanzisha serikali moja Tanzania ni kinyume na mkataba wa kimataifa wa Tanganyika na Zanzibar ambazo zina mamlaka kamili, vinginevyo hii ni ni kutafuta kesi ambayo inaweza kupelekwa mahakama ya kimataifa;

Mkuu Kobello, je, Muungano wetu kwa Mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964 ulilenga serikali moja?


  • Serikali ya Majimbo:
Mfumo huu hutokea pale nchi zinapojileta zenyewe, kwa hiari yao, hasa nchi hizo kama zitakuwa zaidi ya mbili; iwapo zinataka kuungana, zinaweza kufanya hivyo chini ya makubaliano kwamba mamlaka halisi yabakie katika nchi moja moja; Chini ya mfumo huu serikali kuu inakuwa haina nguvu na hugaiwa tu madaraka; Kwa mfano, European Union – ambapo nchi moja moja – Uholanzi, Ufaransa, Ujerumani n.k, zina nguvu ya kufanya maamuzi ya mwisho, sio Bunge la EU au Watendajiw a EU;

Mkuu Kobello, je, Muungano wetu kwa Mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964 ulilenga Serikali ya Majimbo?


  • Mfumo wa Shirikisho:
Chini ya mfumo huu wa muungano, kuna serikali kuu na serikali za mataifa ndani ya muungano husika, ambazo zinashirikiana katika madaraka; kwa mfano:
Kwanza – Kuanzishwa kwa muungano wa kisiasa wan chi mbalimbali huku kila mmoja ikibakia na utawala na uendeshaji wa mambo yake ya ndani (yasiyo ya muungano)

Pili – Mfumo wa kisiasa ambao, nchi husika zinabakisha mamlaka karibia yote ya ndani na kubakiza tu masuala kama vile mambo ya nje, ulinzi kwa serikali kuu;

Tatu – Mfumo ambao kuna kundi la nchi ambazo zimeungana na kuna serikali moja inayokuwa na mamlaka kuhusu masuala kama Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa, Ulinzi, huku kila nchi ikibakia kuwa na nguvu ya kuamua mambo yake yenyewe;

Mkuu Kobello, je, Muungano wetu kwa Mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964 ulilenga Serikali ya Shirikisho?
Jibu langu ni ndio, na sio kwa siasa, bali kwa FACTS; Ukitazama Mkataba wa Muungano, 1964, suala lililo wazi ni kwamba jibu ni SHIRIKISHO na kwa njia ya pili yani:

"Mfumo wa kisiasa ambao, nchi husika zinabakisha mamlaka karibia yote ya ndani na kubakiza tu masuala kama vile mambo ya nje, ulinzi kwa serikali kuu."

Mkataba wa Muungano, 1964 ukiusoma vizuri, hauna lengo la kuunda serikali moja ambapo mamlaka yote hurundikwa katika serikali kuu, na wala haikulenga mfumo wa Serikali za majimbo ambapo mamlaka zinabakia kwenye serikali binafsi;
Ukipitia Mkataba wa Muungano, 1964, utaona wazi kabisa kwamba, mkataba huu ulilenga mfumo ambao serikali kuu (JMT), na serikali shirikishi (Tanganyika na Zanzibar), zitakuwa na nguvu zinazolingana – mfumo wa shirikisho wenye mgao wa madaraka wa mahakama, baraza la kutunga sheria (bunge), nafasi ya Urais baina ya serikali kuu (JMT) na serikali shirikishi (Tanganyika na Zanzibar), huku kila serikali ikiwa na nguvu kamili chini ya mamlaka yake;

Nilitamka pia maneno haya:

Wewe Mtoto Tanzania, Kwanini Unamkana Mzazi wako Tanganyika? Jukumu La Kumwangalia na Kumuenzi Liwe La Nani?

Na wewe ukanijibu kwamba –
Mkuu hizi ndiyo tunaziita siasa

Kwa wale waelewa, wameshaelewa au wanaelekea kuelewa kuhusu kiini macho, hasa pale kilipoanza kwa sheria ya ghafla ya bunge, sheria namba 24, 1967, iliyofuta Tanganyika na kuzaa Tanzania Bara; Vinginevyo mkuu Kobello:

Texas Will Always Remain to be Texas in the United States of America.

Nitazidi kuzirejea hoja zako nyingine kwa mujibu wa sheria zaidi, sio kwa mujibu wa siasa kama unavyoelekea kuegemea, sijui kama ni kwa niaba ya Chama chetu cha CCM au kukosa mwamko na uzalendo wa Tanganyika?

Vinginevyo majibu yako mengi kuhusu TANU, CCM, uhalali wa kikatiba n.k, nitakuwa najirudia tu; lets agree to disagree; Ila naomba nikuulize, kwa mtazamo wako:

IS REASONING BUILT FOR WINNING ARGUMENTS OR FINDING THE TRUTH?


Nipo hapa for the later, definitely not the former. Tushirikiane kupata ukweli, tukishaukamilisha, tukawaelimishe wananchi;
 
  • Thanks
Reactions: ral
Mchambuzi,

..kiini cha matatizo ya muungano ni wetu ni ama kuuwawa kwa serikali ya Tanganyika, au kuendelea kuwepo kwa serikali ya mapinduzi Zanzibar.

..sasa ukitaka kuokoa huu muungano unapaswa kuifufua serikali ya Tanganyika, na kuunda mfumo wa shirikisho, au kuifuta serikali ya mapinduzi Zanzibar, na kuunda Jamhuri moja.

..kwa upande wangu mimi nadhani wenzetu wa Zanzibar hawataki muungano. they have already moved on. katika mazingira hayo, hakuna haja ya kuwabembeleza wala kuwalazimisha na masuala ya muungano.

..tunachotakiwa kukifanya ni kutumia BUSARA na USTAHAMILIVU wakati tunavunja muungano wetu.
Hii ndiyo ilikuwa hoja yangu kubwa nilipouliza maswali: Kwanini tunahitaji muungano, kwanini tunafikiria muundo wa muungano na kwanini tusifikirie kuvunja.

Mkuu Mchambuzi, nashukuru kwa majibu yako. Na nisingependa kubadili muelekeo wa mjadala kutoka sheria kwenda kisiasa. Hata hivyo ni jambo gumu sana kutengenisha vitu vyote viwili kwasababu vinategemeana sana.
Kwahiyo nikitoka nje tafadhali nirudishe mahali panapostahili na au univumilie.

Tunapoondoa option ya kuvunja muungano tunajifunga katika mazingira yale yale tunayoyalaani kuwa hayakuwa na uwazi, kisheria au maridhiano. Option ya kuvunja muungano katika mada hii iwepo mezani ili tuwasikie wasioutaka pia wana hoja gani.

Pili, naomba kichwa cha habari kiangaliwe tena. Tunaposema kiini macho kwa maneno mengine ni mazingaombwe ambayo hayafai kuwepo katika jamii yetu.Kiini macho ina connotation ya valuless

Nikisoma hoja ninaona wachangiaji wanaongelea mkataba wa 1964 na hata wewe kusema ni vema tuangalie muungano kisheria ili kuuobersha. Kama ni kuangalia muungano ule ule tunaouita kiini macho basi tungeweka kichwa cha habari 'matatizo ya muungano' as opposed to kiini macho ambacho kinathadharia ni irrelevant

Wakati tunaendelea na mjadala, ningependa kusema mimi ni mmoja wa watu walioupenda muungano sio tu huu bali Pan Africanism. Najiuliza ujinga wa kuua EAC ambayo leo tungekuwa mfano na sasa kuiga EU.

Matatizo ya muungano kisheria yapo, kisiasa yapo pia lakini niliamini kuwa walioanzisha muungano walikuwa na nia njema, kama matatizo yamejitokeza ni mapungufu na tulipaswa tuyaangalie hivyo kwa wakati tulio nao.
Siku zote nimekuwa nasema matatizo yapo tena makubwa kwa pande zote.

Kwa hali iliyopo sasa hivi, naungana na Joka Kuu kusema kuwa muungano huu hauna mantiki iliyokusudiwa.
Mistrust kati ya Tanganyika na Unguja imefikia mahali panaposema 'beyond repair'.
Misingi ya kuwa na muungano na maana nzima ya muungano haipo tena.
Kwa hali hiyo kilichobaki kizuri ni Kuvunja muungano tuishi kama majirani kila mmoja akishughulika na matatizo yake.

Hata kama kutalazimishwa serikali 3 au mkataba, vyote hivyo vitarudisha katika hali tuliyo nayo.
Zanzibar haswa wameonekana kutotaka kurudi kati 'central position' hivyo kukubali chochote ni kwa ajili ya manufaa yao na si muungano na hasa ndicho wanakiangalia.

Tunafanya makosa yaliyotokea huko nyuma ya kutojiuliza swali la, je tunahitaji muungano?
Hilo ndilo lililozaa matatizo kwasababu wananchi hawakushirikishwa kwanza kujua kama wanataka muungano au la.
Na hiyo ndiyo hoja ya Wazanzibar ambayo nadhani tunaweza kuitetea kisheria.

Serikali ya JK imefanya kosa lile lile la kuaanda katiba mpya bila kuuliza kama Watu wanahitaji muungano.
Na hapa kizazi chetu kinafanya kosa lile lile la kujadili muundo wa muungano kabla hatujaiuliza, je tunahitaji muungano?
 
Mkuu Kobello,

Napenda kurudia tena kwamba mimi sio mwanasheria, lakini nimejifunza kwamba bila kutumia muda wa ziada kuwa mwelewa wa sheria, hoja zako juu ya muungano zitatawaliwa na siasa zaidi, na hautaishiwa hoja; Lakini iwapo hoja zitaegemea sheria, basi utarudia yale yale tu kimsisitizo;

Nimeona kabla sijapitiwa na mambo mengine, nijibu hoja yako ifuatayo:
Sikubaliani na wewe kuwa Articles of the Union zilikuwa ndiyo sheria mama

Bandiko namba 77 katika mjadala wetu huu ndio msingi wa hoja yako hiyo juu, lakini pia umezungumzia mengine kadhaa, lakini yoye ukilenga kuhalalisha muungano wetu chini ya mfumo wa sasa, huku ukijaribu kukitetea CCM, tangia enzi za TANU kwamba walifuata taratibu zote. Ningependa kujibu hoja zako hizikama ifuatvyo:

Kwanza, bila ya CCM itakayojirudi na kukubali kwamba ilikosea kuhusu:

  • Uendeshaji MUUNGANO; na
  • Mauaji ya Azimio la Arusha

Kifo cha CCM yenye kukana hayo hakipo mbali. Ndio maana suala la muungano linaipa CCM presha kubwa kwani ni yenyewe (enzi za tanu), ndio iliuwa Tanganyika kwa mujibu wa sheria ya bunge, sheria namba 24, ya mwaka 1967. Kwahiyo defense strategy kama hizi unazotumia ku-spin facts ni kitu ambacho lazima tukitegemee, kwani huko ndiko kupumulia kwenye mashine, na pengine kifo kitaepukika. Vinginevyo CCM is clinically dead, na nikutokana na mambo mawili hayo hapo juu (Muungano & Azimio la Arusha);

Nikirudi kwenye hoja yangu ya msingi, hakika wewe ni such a political spinner; Nitafafanua hili; Unajenga hoja nzuri sana, kwa kutumia vipengele vilivyopo lakini kwa njia ya kupotosha na pia kuaminisha wengine kwamba kinachoonekana ni BLUE, kama wao wanaona ni KIJANI, basi wana matatizo ya akili; Ningependa kujirudia tena, kwani tabia ya kujirudia rudia ovyo ni sehemu ya kuwa na tatizo la akili; Nitajaribu kutumua hoja za Kisheria zaidi Kuliko Siasa, na naomba wadau wengine wanipime kwa hilo na wawe wazi kunikosoa;

Hoja yako ya kupinga hoja yangu kwamba Mkataba wa Muungano haukuwa sheria mama, nitajirudia tena kama taahira kama ifuatavyo, kwa njia ya maswali:

Swali la Kwanza: Je, kabla ya Mkataba wa Muungano, 1964, kulikuwa na kitu gani?

Jibu ni kwamba kulikuwa na taifa la Tanganyika yenye miaka miwili na ushee ya Uhuru, Kulikuwa na Taifa la Zanzibar lenye miezi kama minne ya uhuru wa mapinduzi; Pia kulikuwa na taifa la Uganda, Kenya, n.k.

Swali la Pili: Je, kama ni hivi kwanini Tanganyika haipo?

Jibu ni kwamba, nchi huru za Tanganyika na Zanzibar ziliamua kuingia MKATABA wa KUUNGANA ili kuwa JAMHURI MOJA, Sio SERIKALI MOJA; Tutaona baadae suala hili kwa undani;

Swali la Tatu: Je, Mkataba Ulijengwa kwa Nguvu Ganui ya Kisheria?

Jibu ni kwamba, Mkataba wa Muungano, 1964, ulichukua nafasi ya Sheria Mama, kwa matarajio kwamba, Muungano wetu utapewa nguvu za kikatiba ndani ya mwaka mmoja; Ni hapa ndugu Kobello unapoanza spins zako; Nitafafanua; Unaelezea vizuri sana yaliyojiri huku aidha kwa kujua au kutojua, unaruka mambo mengine muhimu zaidi ya kusaidia kufungua kiini macho hiki cha muungano; Kwa mfano, hoja yako kwamba Katiba ya Tanganyika ilikubaliwa ndio iwe Katiba ya Muda, hakuna anayebisha hili, mpaka hapa tupo sawa; Lakini hauelezei watanzania waliopo humu kwamba, ili hilo lifanikiwe, katiba ya Tanganyika ilitakiwa ifanyiwe marekebisha kwanza, bila ya hivyo, Mkataba wa Muungano, 1964 ungeendelea kuwa nguzo pekee ya kuhalalisha muungano;

Kwa makusudi au kwa kupitiwa, hautaki kujadili yaliyomo katika Mkataba wa Muungano, 1964, hasa pale unapoweka masharti juu ya matumizi ya Katiba ya Tanganyika kuwa Katiba ya Muda ya Jamhuri Mpya ya Muungano wa Tanzania (katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja). Kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964, ibara ya tatu inasema hivi:

(iii) Katika kipindi cha mpito katiba ya Jamhuri ya Muungano itakuwa katiba ya Tanganyika iliyorekebishwa ili kuweka:
a) Chombo tofauti cha kutunga sheria na Serikali kwa ajili ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria zilizopo za Zanzibar na vitakuwa na mamlaka ya mwisho katika Zanzibar kwa mambo yote isipokuwa yale tu yaliyo chini ya bunge na Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
b) Nafasi ya makamo wawili wa Rais mmoja kati yao akiwa ni mkaazi wa Zanzibar atakuwa ndiye kiongozi wa Serikali iliyotajwa kwa ajili ya Zanzibar na atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa rais wa Jamhuri ya Muungano katika utekelezaji wa kazi za Serikali kwa upande wa Zanzibar;
c) Uwakilishi wa Zanzibar katika bunge la Jamhuri ya Muungano;
d) Mambo mengine yatayofaa au kuhitajika ili kuipa nguvu Jamhuri ya Muungano na mkataba huu.

Bila ya Katiba ya Tanganyika kufanyiwa marekebisho katika maeneo haya, ili kuupatia Muungano wetu Uhalali na Nguvu ya Kikatiba, Katiba ya Tanganyika isingekuwa na uhalali au nguvu ya kutumika kama Katiba ya muda ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na badala yake, ingebakia na nguvu yake kwa upande wa Tanganyika, kama ilivyokuwa kabla ya Muungano baina ya taifa huru la Tanganyika na Zanzibar; Kwa maana hii, basi Mkataba wa Muungano, 1964, ungebakia kuwa ndio nyaraka peke yake ya kuhalalisha muungano wetu, hivyo kuendelea kuchukua nafasi ya Sheria mama katika kipindi cha mpito;

Mbali na marekebisho haya ya Katiba ya Tanganyika ili ipate nguvu za kikatiba kuendesha Muungano wakati wa kipindi cha mpito, pia kulikuwa na sharti lingine ndani ya Mkataba wa Muungano, 1964, sharti ambalo lilikuwa ni muhimu kuliko yote, kwa maana ya kuupatia Muungano wetu sasa nguvu kamili na uhalali wa kisheria wa kudumu; Sharti hili ambalo pia unakwepa kulijadili kwa mtindo wa ku-spin issues, lipo katika kipengelea cha saba cha Mkataba wa Muungano ambacho kinasema hivi:

vii) Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kukubaliana na Makamo wa Rais ambaye ni kiongozi wa serikali ya Zanzibar
a) Atateua tume kwa ajili ya kutoa mapendekezo kwa ajili ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.
b) Ataitisha Baraza la kutunga katiba ikiwa na wawakilishi kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa likutane katika kipindi cha mwaka mmoja tokea kuanza kwa muungano kwa madhumuni ya kutafakarimapendekezo ya tume iliyotajwa juu na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Nadhani sasa tupo tayari kudadisi kwa undani zaidi kuhusu Mkataba wa Muungano, 1964, na nguvu yake ya kisheria;

Kwanza tukubaliane kwamba wakati wa makubaliano yale, ilitarajiwa kwamba kipengele cha saba cha Mkataba ule kingefanyiwa kazi kwa haraka sana ili Muungano wetu uweze kupata katiba yake ya Kudumu; Sasa nini kilitokea?

Kwanza, kilichotokea ni kwamba Katiba ya Tanganyika haikufanyiwa mabadiliko yoyote kama ilivyokusudiwa;

Pili, tume ya kukusanya maoni kuhusu katiba mpya, nayo haikuteuliwa;
Kwa hoja hizi mbili, mkataba wa Muungano, 1964, uliendelea kuwa ndio nyaraka pekee halali, kinyume cha matarajio na pia madhumuni yaliyokusudiwa;

Mazingaombwe yafuatayo yakaanza:

Moja, katika hali isiyokuwa ya kawaida, ilipofika Julai 10, 1965, Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania, likapitisha sheria iliyolenga kuhairisha INDEFINATELY, ibara ya ‘7' ya Mkataba wa Muungano, 1964 amacho kilitoa sharti hili (nirudie tena):

vii) Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kukubaliana na Makamo wa Rais ambaye ni kiongozi wa serikali ya Zanzibar
a) Atateua tume kwa ajili ya kutoa mapendekezo kwa ajili ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.
b) Ataitisha Baraza la kutunga katiba ikiwa na wawakilishi kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa likutane katika kipindi cha mwaka mmoja tokea kuanza kwa muungano kwa madhumuni ya kutafakarimapendekezo ya tume iliyotajwa juu na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Badala yake, bunge hili KINYUME NA MKATABA WA MUUNGANO, 1964, ibara ya ‘7', likapitisha Katiba ya Muda (SIO KATIBA YA KUDUMU), chini ya Sheria namba 43 ya 1965.

Msisitizo: Hapa tunaona mazingaombwe kama ifuatavyo: As of 1965:

  • Kipindi cha mpito per articles of the union, 1964, kwamba kisizidi mwaka mmoja, kina expire huku ibara ya saba ya Articles of the Union ikiwa haijatekelezwa na vile vile, ibara ya pili nayo ya kurekebisha Katiba ya Tanganyika ili iwe na uhalali wa muda kama katiba ya Jamhuri, nayo haijarekebishwa; Katika hii expiry date, Mkataba wa Muungano unaendelea kuwa the only document that can be regarded as "SHERIA MAMA", whether by accident au kwa makusudi, tutaona in the future kwenye mjadala huu;


  • Kwa vile as of 1965, ambapo nchi haina katiba yenye nguvu ya kisheria per articles of the union, kama nilivyoeleza hapo awali, ibara ya saba ya articles ambayo inaweka sharti la kuteuliwa tume huru ya katiba kutoka pande mbili za muungano, sharti hili linakuwa postponed kupitia sheria ya bunge, tena INDEFINATELY, kisha bunge hili hili ambalo halina uhalali wa kikatiba na wala halina uhalalo per articles of the union, 1964, linapitisha katiba nyingine tena (mpya) ya MUDA (sio ya kudumu), chini ya sheria namba 43, 1965; katiba hii ikaendelea kuwepo kwa miaka 12 mpaka pale akili ya kuzidi kuchakachua muungano kwa uhalali wa kisiasa ilipowadia: TANU + ASP = CCM (1)being equated as TANGANYIKA + ZANZIBAR = TANZANIA (1);

Msisitizo: Ndani ya mwaka mmoja wa muungano, tunahamia kutoka katiba YA MUDA ya Tanganyika ambayo haikurekebishwa, kwenda kwenye Katiba nyingine YA MUDA TENA, huku ibara ya ‘7', ambayo ndio nguzo kuu ya muungano, ikihairishw INDEFINATELY;


  • Bunge pia mwaka 1967, likapitisha sheria namba 24, iliyompa Rais wa JMT mamlaka ya kubadilisha jina kutoka Tanganyika, kuwa Tanzania; Kwahiyo, Tanganyika iliuwawa kwa mujibu wa bunge la JMT, ambalo hata hivyo kwa waelewa, tayari wanaona kwamba bunge hili halikuwa na uhalali wa kikatiba in terms of its existence, lakini pia kujihusisha na masuala ya ku deal na majina ya nchi shirikishi, kwani suala hili halikuwa la muungano, bali la nchi shirikishi; Suala lingine la kufanya bunge hili lisiwe halali kama bunge la JMT ni kwamba ibara ya 3 (c) haikuwa imefanyiwa kazi, nayo ni:


"(iii) Katika kipindi cha mpito katiba ya Jamhuri ya Muungano itakuwa katiba ya Tanganyika iliyorekebishwa ili kuweka:
(c) Uwakilishi wa Zanzibar katika bunge la Jamhuri ya Muungano;

Swala la mwisho ambalo ningependa kuliweka hapa ni lile la TANU, hasa jinsi gani chama hiki kilivyojipenyeza katika masuala ya Muungano, kinyume cha Mkataba wa Muungano, 1964; Kwanza ijulikane kwamba katika Mkataba ule, hakuna sehemu ambapo TANU au ASP, na hata CCM, vinatajwa; masuala ya vyama yalitakiwa yabakie katika nchi husika – Tanganyika na Zanzibar, na muungano ushughulikie masuala yale kumi na moja tu katika kile kipindi cha mpito mpaka katiba mpya itakapopatikana; Katiba mpya haikutokea, na hili nimelijadili tayari;

Kama nilivyojadili, katika Mkataba wa Muungano, 1964, TANU haipo, wala ASP; Lakini cha ajabu, katika Katiba ya Muda ya 1965, tunaona TANU ikiingia humo. Katika ibara ya tatu ya katiba ya muda, 1965, inasema hivi:


  1. (1) Kutakuwa na Chama Kimoja Cha Siasa Katika Tanzania.
(2) Mpaka hapo TANU itakapoungana na ASP, na kufanya chaa kimoja cha Siasa, Chama hicho cha Tanganyika Kitakuwa ni TANU na kwa Zanzibar Kitakuwa ni ASP;

Natumaini kipengele hiki kinampa makengeza msomaji yoyote na kufikiria nimekikosea; Hivyo ndivyo kilivyo, kwa lugha ya mtaani - FULL KIINI MACHO; Zanzibar hapa ikapigwa teke la kisigino, kwani TANU ikawa Supreme to Katiba ya 1965, na Muungano kwa ujumla; Katika majibu yangu mengine humu, niliweka sehemu ya maneno ya Pius Msekwa aliyosema kwenye kitabu chake cha Towardes Party Supremacy (1977), ambapo, aidha kwa makusudi au bahati mbaya, analiweka hili bayana;

Vinginevyo, kuanzia tarehe ambayo katiba ya Muda, 1965, ilianza kutumika, ina maana kwamba KANUNI ZA TANU na KATIBA YAKE zikawa zimefanywa kuwa sehemu za Sheria ya Jamhuri ya Muungano; Madhara yake kwa Zanzibar hapa ilikuwa nini? Kwa wale waelewa, kamwe hawawezi kuwalaumu ndugu zetu wa Zanzibar kwa kutafuta autonomy yao ndani ya muungano wetu, per articles of the Union, 1964;

Huu ni mtiririko wa baadhi tu ya matukio, na kama unavyo ona, hoja zangu zimejaa mtazamo wa Kisheria, kuliko Kisiasa kama unavyopenda kuaminisha watu, ambayo yalijeruhi muungano, badala ya kutimiza wajibu wetu wa kulinda na kutetea mkataba wa Muungano, 1964.

Nitazidi kutoa mawazo yangu KISHERIA, hasa kuhusu matukio yaliyotokea baada ya mwaka 1967 Tanganyika ilipouawa kwa mujibu wa sheria za bunge, kinyume na Mkataba wa Muungano; Nitalenga hasa kuzaliwa kwa CCM, 1977, na madhara kwa Mkataba wa Muungano, 1964; Lengo kuu itakuwa kuonyesha jinsi gani CCM ILIYOSHIKA HATAMU, ilivyozidi kukiuka Mkataba wa Muungano, 1964; Ninatarajia ntakuwa mzima na ninaishi by the time Napata muda wa kuliweka hilo humu;
 
Im here for both, the thrill of victory associoated with the dissemination of knowledge. What I mean by dissemination of knowledge is you and others knowing that there's another school of thought, appreciating it and humbly agreeing or rejecting it.
The other part is finding the truth through learning about different school of thoughts, trying as hard as possible to find their weakest point and crush'em or their strongest points and humbly accepting them (learn from them) .... I like that.

kwa kuwa mara kwa mara umeniambia niisome hiyo article, why don't we start by going through it kipengele kwa kipengele?
1. It is therefore AGREED between the Governments of the Republic of Tanganyika and of the Peoples' Republic of Zanzibar as follows: -
(i) The Republic of Tanganyika and the Peoples' Republic of Zanzibar shall be united in one Sovereign Republic.

Maongezeo;
1707 Acts of Union between Scotland and England.
Article 1


That the two Kingdoms of England and Scotland shall upon the first day of May, which shall be in the year one thousand seven hundred and seven, and forever after, be united into one Kingdom by the name of Great Britain; and that the ensigns armorial of the said United Kingdom be such as Her Majesty shall appoint, and the crosses of St George and St Andrew be conjoined in such manner as Her Majesty shall think fit, and used in all flags, banners, standards, and ensigns, both at sea and land

Kwa kutumia mifano hiyo miwili unaweza kuniambia kuwa mpaka hapo kulikuwa na nia ya kuunda shirikisho? Taratibu tutaenda kipengele hadi kipengele.
 
Mchambuzi,

..huwezi kuwa ktk muungano huku ukiendelea kuwa na autonomy.

..hata ktk mfumo wa shirikisho nchi wanachama hupoteza autonomy.

..kama tunataka autonomy basi tunapaswa kuunda jumuiya ya Tanganyika na Zanzibar, kama zilivyo jumuiya za EAC, na SADC.

Muhimu ni manufaa/faida inayopatikana na siyo "title" ya Muungano. Kama nchi moja haitaipokonya maamuzi nchi nyengine (partner). Katika kila Muungano lazima kuwe na sheria ya kujitoa katika Muungano huo.
 
Mkuu Nguruvi3,

Nashukuru tena kwa mchango wako. Naomba niingie katika hoja zako tatu kuu kama ifuatavyo:

Kwanza - kuhusu matumizi ya neno "kiini macho"; Kimsingi naelewa hoja yako lakini naomba niwe muwazi kwamba – kwanza, kwangu mimi, uelewa na pia matumizi ya dhana hii ni kwamba, kiini macho au "false appearance", ingawa inaweza kuwa na synonyms nyingine ambazo zinatoa a negative connotation kama ulivyojadili; mimi nadhani ni suala la jinsi gani neno linatumika na katika mazingira yepi; Kwa mfano neno "MJINGA", it may not sound politically correct kwa mwanasiasa kupanda jukwaani na kusema

"ndugu wananchi, naombeni kura zenu kwa sababu nyinyi ni "WAJINGA", na mkinichagua, nawahakikishieni kwamba nitaenda bungeni kupigania maslahi yenu, ili mpunguze UJINGA mlio nao;"

Ingawa UJINGA ni moja ya maadui wakuu wa Maendeleo Tanzania, kwa kauli hii, kwa kweli kura hautapata; Hoja yangu ya msingi hapa ni kwamba, ni suala tu la matumizi to determine what is and what is not politically correct;

Vinginevyo, kwangu binafsi, kama nilivyosema hapo juu, kwa miaka mingi sana mimi navyoelewa neno illusion au kiini macho ni "FALSE APPEARANCE"; Sasa nilipomsikia Lissu bungeni akijenga hoja kwamba Muungano Wetu ni Kiini macho, moja kwa moja nikapata mwamko wa kwenda kuupitia tena Muungano wetu, KISHERIA ZAIDI, kwani huyu sio mwanasiasa bali Mwanasheria, kubaini zaidi the FALSE APPEARANCE relative to Mkataba wa Muungano, 1964; Kama kauli hiyo ingekuwa ya mwanasiasa, sidhani hata ningekuwa na uelewa juu ya muungano wetu kama nilivyo leo hii; kauli ya Lissu ilinisukuma nikafanye utafiti kwa miezi mitatu kabla ya kuja humu na kutoa hoja yangu hii;

Naomba uniwie radhi iwapo neno hili kidogo linakukera, lakini nia yangu ni kuliwakilisha kama lilivyowakilishwa na Mwanasheria, huku nikijaribu sana kulijadili kisheria; Vinginevyo, neno MATATIZO ya muungano, huleta mjadala uliokuwa na mwelekea wa kisiasa zaidi; Pengine sipo sahihi sana, lakini kwa kifupi, nia yangu ni kuchukua maneno ya Mwanasheria mwenye dhamana kama Waziri Kivuli wa Muungano; Naomba ieleweke kwamba sikutunga neno hili, bali nimeli ‘lift' kutoka kwa Lissu, na kwa vile yeye ni Mwanasheria, basi anajua alikuwa ana maana gani, na iwapo utasikia nimetiwa nguvuni kama mchochezi kwa matumizi ya neno hili, ndugu yangu nguruvi3, naomba uwe mtu wa kwanza kumtafuta Lissu aje kuniokoa ‘KISHERIA';

Hoja yako ya Pili - kwamba Muungano wetu ni beyond repair, kwa kum-quote Joka Kuu; Ni kweli kuna dalili nyingi na kubwa sana kwamba tumefikia hali hiyo; Lakini kama nilivyosema awali, nadhani ili tufikie final analysis juu ya hilo, ni muhimu Referendum iitishwe haraka ili tujue moja; Vinginevyo naelewa juu ya sentiments and views hizi kupitia mtu mmoja mmoja, lakini naheshimu zaidi uamuzi wa UMMA, na kwa maana hii, referendum;

Kama ulivyojadili, "NIA" ya Mwalimu Nyerere na Karume ilikuwa ni njema kabisa at the outset, na kama tatizo lilijitokeza, basi ilikuwa on the "MEANS: Vinginevyo until nipate confirmation Watanzania wanasema nini juu ya hatima ya muungano, kwa njia ya ‘Referendum', nitaendelea kutetea muungano wetu, LAKINI Per Articles of the Union(1964), not Per Katiba ya Tanzania (1977), kwani katiba ya Tanzania (1977), kwa MTAZAMO WA KISHERIA, haina mema kwa muungano wetu; Wema uliopo mle, kama upo, basi ni KISIASA tu;

Suala la Mwisho na muhimu sana ni hoja ya kuvunja muungano; Mantiki ya hoja hii naielewa vizuri sana, na sipingani nayo bila maelezo, kwani maelezo yangu ni hayo hapo juu kwamba, ili nijiunge na Kambi hii, mimi nahitaji kwanza kuona matokeo ya Referendum juu ya suala hili; Ningependa kumalizia kwa maswali yafuatayo ambayo naomba nipate mtazamo wako tafadhali, na again, maswali haya ni kutokana na approach yangu kwa muungano huu kisheria zaidi kuliko kisiasa, ingawa nakubaliana na wewe there is a thin line….:


  • Je, Muungano wetu uliundwa kwa sheria ipi? Kwani kama sheria ipo, basi kuna mawili: aidha iwe rectified, or revoked all together, ili tupate tena Tanganyika yetu;

  • Je, tunaweza kuachana na Zanzibar bila ya kufufua Tanganyika?

  • Kwa vile Tanganyika ilivunjwa kwa mujibu wa sheria ya bunge la JMT, sheria namba 24, 1967; Je, ili kurudisha Tanganyika, tunahitaji ku rectify sheria hii? Revoke? Au kutunga nyingine bila ya haya mawili?

  • Sote tulishuhudia mwaka 1995jinsi gani hoja ya Tanganyika ilizimwa, iliposhika kasi ndani ya bunge la JMT; Hoja ya kuzimwa kwake tunazijua Kwahiyo sina haja za kuzirudia, hasa kwamba - kwamba – uamuzi ule ulitakiwa ufanyike ndani ya vikao vya CCM, sio Bungeni; Je, hii ina maana kwamba kuanzisha hoja ya Tanganyika lazima ipitie vikao vya CCM, na sio chama kingine chochote cha siasa au mchakato mwingine wowote? Kama inahitaji referendum, kwanini hili halikusemwa mwaka 1995, wakati nchi ilikuwa tayari ni ya mfumo wa vyama vingi kama ilivyo leo?
 
Muhimu ni manufaa/faida inayopatikana na siyo "title" ya Muungano. Kama nchi moja haitaipokonya maamuzi nchi nyengine (partner). Katika kila Muungano lazima kuwe na sheria ya kujitoa katika Muungano huo.

Mkataba wa Muungano, 1964, umeweka wazi provision hii ya nchi kuwa na uwezo wa kujitoa; hii ndio essence ya federation, kwani chini ya unitary system, kama utajitoa, basi ni baada ya kupiga au kupigwa mabomu kama ilivyotokea north ireland; Kobello hataki kuamini kwamba Mkataba wa 1964 uliweka provision ya kujitoa, pale anapojenga hoja kwamba, hoja yangu kwamba Mkataba ule ulilenga a federation, anaita hoja yangu kwamba sio ya kweli na ni ya kisiasa;
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom