Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Mkimchagua Magufuli, ana lengo la kubadili Katiba kuondoa ukomo wa vipindi vya kutawala

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,503
51,098
Mgombea Urais kupitia Chama cha Chadema ndugu Tundu Lissu, amewaasa Wananchi wa Bagamoyo kuwa, Magufuli ana lengo la kubadili ukomo wa vipindi vya utawala na ndiyo maana hilo Suala lilizungumzwa bungeni na Spika Ndugai.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, Ndugai asingeweza yeye binafsi kulizungumza hilo bila kufahamu kinachoendelea kwenye mipango ya Magufuli.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, wafikirie hali ngumu za maisha, ukatili na uonevu uliotokea katika kipindi hiki cha miaka mitano halafu eti Magufuli aongezewe miaka mingine.

Lissu amesema, serikali ya Chadema itakuwa ni Serikali ya Haki, Uhuru na Maendeleo. Itakuwa serikali itakayoheshimu watu tofauti na hii ya Magufuli yenye kudhalilisha watu hususan wanawake.

Lissu akasema kujenga miundo mbinu siyo hoja ya kunyima haki za watu kama vile nyongeza za mishahara zilizoko kisheria. Akasema kuwa hata mkooni alijenga reli, lakini hiyo haikuwa sababu ya kwa nini Tusimpinge, Akasema kuwa tulimpinga mkoloni kwa sababu hakuwa anatutendea haki.

Lissu akasema kuwa Nyerere alijenga reli ya TAZARA, tena ndefu zaidi lakini hakudhulumu stahiki za wafanyakazi

Kwa taarifa zaidi juu ya hoja nzito za Lissu tazama video hii

 
117195765_3213508722074131_2911542144163865371_n.jpg

ukilinganisha na kauli zake,jibu unapata. Huu ukorofi na kutisha watu huwezi kuondoka kizembezembe tu halafu nani atakulinda. Hawa kina M7 wanapenda wapumzike ila wanaogopa maisha baada ya uraisi
 
Kwanini kule chadema kila anayegombea uenyekiti anafukuzwa au kuhama au kufariki? Kwanini asianze ndani ya chama chake kuleta huo Uhuru, demokrasia na ukomo wa uongozi ndo aje atoe shutuma zisizo na ushahidi ambazo ni za kudhania tuu kwamba eti Magufuli atabadilisha katiba aongoze Kama Mbowe.

Aache kuropoka Mambo ya kubuni.
 
TOO MUCH LIES
Halafu wanalalamika kuwa vyombo vya habari hawaandiki habari zao

Jana tu walitoa press release kuwa TCAA imezuia Helukopta kuruka kwa sababu zisizoeleweka!!! Nashukuru press waka wa ignore wakijua hawako reliable taarifa zao wakaenda TCAA wenyewe wakaambiwa rubani mrusha helikopta kapita umri wa kisheria na hilo ndilo likatangazwa TV zote lile la uongo likatupiliwa Mbali

Kifupi chadema wamepoteza Truth Reliability kwenye media tofauti na enzi za Dr Slaa.Alikuwa akiongea anashusha ushahidi wa ukweli na uhakika usio na chembe ya shaka
Kiasi kuwa media hazikuhangaika ku counter check wanajua kuwa alichotamka kiko sahihi

Lisu sio presidential material anaongea vitu vya kuokoteza na kutunga kama mswahili tu wa mtaani
 
Mgombea Uraisi kupitia Chama cha Chadema ndugu Tundu Lissu, amewaasa wananchi wa Bagamoyo kuwa, Magufuli ana lengo la kubadili ukomo wa vipindi vya utawala na ndiyo maana Hilo Suala lilizungumzwa bungeni na Spika Ndugai.
Lissu watu hawataki kusikia hayo,wanataka kujua ukichaguliwa wewe utaletaje maisha bora?
Hata lissu akichaguliwa hakuna garantii kwamba hataongeza muda,atasema ccm imetawala miaka 50,acha na sisi tutawale miaka 20 hakuna uchaguzi,na kwa vile anaungwa mkono na mabeberu watamshangilia tu
 
lissu watu hawataki kusikia hayo,wanataka kujua ukichaguliwa wewe utaletaje maisha bora?
Hata lissu akichaguliwa hakuna garantii kwamba hataongeza muda,atasema ccm imetawala miaka 50,acha na sisi tutawale miaka 20 hakuna uchaguzi,na kwa vile anaungwa mkono na mabeberu watamshangilia tu

Umerogwa wewe, kwani hujui uhusiano wa udikteta na maisha mabovu?
 
Mgombea Urais kupitia Chama cha Chadema ndugu Tundu Lissu, amewaasa wananchi wa Bagamoyo kuwa, Magufuli ana lengo la kubadili ukomo wa vipindi vya utawala na ndiyo maana Hilo Suala lilizungumzwa bungeni na Spika Ndugai.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, Ndugai asingeweza yeye binafsi kulizungumza hilo bila kufahamu kinachoendelea kwenye mipango ya Magufuli.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, wafikirie hali ngumu za maisha, ukatili na uonevu uliotokea katika kipindi hiki cha miaka mitano halafu eti Magufuli aongezewe miaka mingine.

Lissu amesema, serikali ya Chadema itakuwa ni Serikali ya Haki, Uhuru na Maendeleo. Itakuwa serikali itakayoheshimu watu tofauti na hii ya Magufuli yenye kudhalilisha watu hususan wanawake.

Lissu akasema kujenga miundo mbinu siyo hoja ya kunyima haki za watu kama vile nyongeza za mishahara zilizoko kisheria. Akasema kuwa hata mkooni alijenga reli, lakini hiyo haikuwa sababu ya kwa nini Tusimpinge, Akasema kuwa tulimpinga mkoloni kwa sababu hakuwa anatutendea HAKI.

Lissu akasema kuwa Nyerere alijenga reli ya TAZARA, tena ndefu zaidi lakini hakudhulumu stahiki za wafanyakazi

Kwa taarifa zaidi juu ya hoja nzito za Lissu tazama video hii


Hii ni dalili tosha ya mfa maji. Hana sera. Badala ya kusema atawafanyia nini Watanzania anakuja na mambo ya kufikirika. Mwaga sera TL kama huna basi kaa kimya.
 
Back
Top Bottom