Baada ya kukubaliana namna ya kuondoa kesi na ili isionekane kuwa serikali alimbambikia kesi "atapewa" kesi ya kujibu kisha muda mfupi baada ya kuanza utetezi ndipo DPP ataleta ile "taarifa". (Rejea kesi ya FEM) Hii itawapa faraja kubwa wahafidhina kuwa pamoja na serikali kutoendelea na kesi mhaini alikutwa na kesi ya kujibu.
It doesn't work that way...
Scenario ya kesi hii Iko hivi:
Juma.Pumba .Maharage(JPM) amemshitaki mahakamani
Makoye Membe Ng'wigulu kwa kosa la
kumuibia baiskeli yake..
Mlalamikaji au mshitaki ata lay down kesi yake mbele ya mahakama na mwisho wa siku ataitoa hiyo baiskeli iliyoibiwa na kukamatwa kama ushahidi kuthibitisha maelezo yake..
Katika kuu - scrutinize huo ushahidi baadaye inagundulika receipt ya kielelezo hicho (baiskeli)kilicholetwa mahakamani kama ushahidi ina jina la
Gigwa Pondamali Maige..
Kwa sbb hiyo tu, mtuhumiwa anapinga kupokelewa kwa kielelezo hicho kama ushahidi wa upande wa mashitaka. Mahakama inakubaliana na upande wa utetezi na kielelezo hicho kinakataliwa kuingizwa.
SWALI: Unafikiri Mahakama mwisho wa siku itaamua nini?
Obvious uamuzi utakuwa ni huu:
Upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha kosa la mtuhumiwa kwa ushahidi ulio wazi. Kwa hiyo mahakama haijamwona mshitakiwa na kosa lolote. Mshitakiwa huna kosa, wewe ni mtu huru..!
Ndivyo ilivyo katika Shauri hili la uhaini kati ya Jamhuri vs Tundu Lissu kwa sbb:
1. Ushahidi mkuu (video clip ya JamboTV iwe upo kwenye flash disk au CD) ambayo ndiyo yenye maneno hayo yanaoitwa "uhaini" haipo mahakamani kwa kuwa ilikosa vigezo vya kisheria kuingia kama kielelezo cha ushahidi dhidi ya mtuhumiwa..!
Mtuhumiwa ajitetee kutokea wapi? Utetezi uwe ktk sababu hiyo ili akubali au akanushe???
2. Mashahidi wote 16 ukimwacha PW17 walidai kuhamasika kufanya uasi tokana na maneno ya mtuhumiwa. Lakini swali linabaki kuwa, hayo maneno yako wapi ili mahakama nayo iyasikie na iyapime kisheria ili Ione km yana elements za uhaini?
Jibu ni kuwa hayapo. Na kama hayapo mahakama itatumia ushahidi gani wa vielelezo vilivyobeba kosa (la kutamka maneno ya uhaini) ili kuiwezesha mahakama kujua iwapo mtuhumiwa hayo yanayodaiwa ni kosa la uhaini kweli ni kosa kwa kipimo cha sheria ya uhaini Ili ajitetee au ni blahblah tu za wahuni na hayawani wa CCM?
3. Upande wa mashitaka unamtegemea PW17 pekee aliyesema yeye alikuwepo siku mtuhumiwa akisema maneno na aliyarekodi. Lakini naye hajakitenda mahakamani kielelezo hicho, wanacho wao mpaka leo walipofunga ushahidi wao.
Sasa mahakama izingatie ushahidi upi ili imwone mtuhumiwa kuwa ana kesi ya kujibu?
Na hata ikisema mtuhumiwa ajitetee kwa kuwa ana kesi ya kujibu. Swali utetezi wake usimame ktk msingi upi ulio mbele ya mahakama?
Tundu Lissu aliuliza swali simple tu, kuwa, nijitetee kwa kipi hasa??
Sikiliza ndugu: HATA SAA MBOVU KUNA WAKATI HUONESHA MUDA SAHIHI KAMA SAA ILIYONZIMA!
Majaji hawa hawawezi ku - ruin reputation yao kwa kufanya maamuzi ya kijinga huku wakijuwa kwa uwazi kabisa kuwa wanadanganya..!