Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,122
- 17,405
LISSU KUACHIWA AGOSTI 21? MAJAJI KUAMUWA KAMA ANA KESI YA KUJIBU AU LA SIKU YA IJUMAA
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu ameieleza Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Dar es Salaam leo Agosti 17, 2026 kuwa hana kesi ya kujibu katika shauri la uhaini linalomkabili huku akiiomba mahakama kutamka kuwa hana hatia na itamke kuwa anatakiwa kulipwa fidia.
Kesi imeahirishwa hadi Agosti 21, 2026 siku ya Ijumaa ambapo Majaji watatu wataamuwa kama Tundu Lissu ana kesi ya kujibu au la.
Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu imeahirishwa hadi Ijumaa ya Agosti 21 ambapo mahakama itaamua kama Mwenyekiti huyo wa upinzani nchini ana kesi ya kujibu au la!
Kesi hiyo Na.19605/2025 ilianza kwa upande wa Jamhuri kufunga mashahidi wake 17 kati ya 30 ambao walitoa ushahidi wao.
Baada ya kufunga mashahidi hao, upande wa mashtakiwa Tundu Lissu alitoa Submission (Majumuisho) ya ushahidi wote uliotolewa Mbele ya Mahakama huku akisema baada ya kusikiliza mashahidi wote 17 wa upande wa mashtaka,upande huo umeshindwa kabisa kuthibitisha kwamba (Prima-facaie case/Evidence )ni "ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka usipojibiwa na upande wa mteteze, Mahakama inaweza kumhukumu mtumhumiwa.
Mshitakiwa amesema kuwa prima facie evidence kimsingi ni ushahidi wa upande wa mashtaka peke yake na kama haujafikia kiwango au kujibiwa hakuna kesi.
Amesema kifungu Cha 312(1) kinasema kuwa, kama haujafikia ushahidi uliotolewa,Mahakama utasema hakuna hatia.
Akiendelea kutoa utetezi wake, Lissu amesema hicho kifungu Cha 312(1) kimefanyaiwa maamzi mengi ya nchi yetu kwa kutengeneza misingi mikubwa ya Kisheria juu ya kitu gani Mahakama inatakiwa kujibu kuhusu hakuna kesi ya kujibu(No case to answer).
Amesema msingi mkuu Wa Kisheria juu ya kwamba hakuna hoja ya kujibu iliwekewa tangu miaka 70 iliyopita na mahakama ya Rufani Afrika Mashariki.
Amesema kesi hii si ya kwanza kufanyika nchini Tanzania,bali ni kesi ya tatu,iwewemo ya Khatibu Gandi na wenzake dhidi ya Jamhuri.
Amesema katika kesi ya kwanza kati ya Gray Nkunku Matata na wenzake iliweka vigezo vitatu kuthibitisha kama kesi ni ya uhaini,akitaja vipo ukurasa wa 406.
Utiifu wa Jamhuri,Je, ulikuwa na nia ya kutenda kosa la uhaini?,hiyo nia lazima uthibitishwe kwa maandishi au kwa matendo ya wazi. 39(2d) kwa mujibu wa kifungu Cha makosa ya adhabu.
Aidha Lissu ameendelea kuisisitiza Mahakama kuturuhusu kujitetea kwasababu hana kesi ya kujibu
Hata hivyo mshitakiwa amesema bado Mahakama inaweza kutoa fidia kwa hizo siku zote 496 kutokana na kifungu Cha 367.
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu ameieleza Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Dar es Salaam leo Agosti 17, 2026 kuwa hana kesi ya kujibu katika shauri la uhaini linalomkabili huku akiiomba mahakama kutamka kuwa hana hatia na itamke kuwa anatakiwa kulipwa fidia.
Kesi imeahirishwa hadi Agosti 21, 2026 siku ya Ijumaa ambapo Majaji watatu wataamuwa kama Tundu Lissu ana kesi ya kujibu au la.
Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu imeahirishwa hadi Ijumaa ya Agosti 21 ambapo mahakama itaamua kama Mwenyekiti huyo wa upinzani nchini ana kesi ya kujibu au la!
Kesi hiyo Na.19605/2025 ilianza kwa upande wa Jamhuri kufunga mashahidi wake 17 kati ya 30 ambao walitoa ushahidi wao.
Baada ya kufunga mashahidi hao, upande wa mashtakiwa Tundu Lissu alitoa Submission (Majumuisho) ya ushahidi wote uliotolewa Mbele ya Mahakama huku akisema baada ya kusikiliza mashahidi wote 17 wa upande wa mashtaka,upande huo umeshindwa kabisa kuthibitisha kwamba (Prima-facaie case/Evidence )ni "ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka usipojibiwa na upande wa mteteze, Mahakama inaweza kumhukumu mtumhumiwa.
Mshitakiwa amesema kuwa prima facie evidence kimsingi ni ushahidi wa upande wa mashtaka peke yake na kama haujafikia kiwango au kujibiwa hakuna kesi.
Amesema kifungu Cha 312(1) kinasema kuwa, kama haujafikia ushahidi uliotolewa,Mahakama utasema hakuna hatia.
Akiendelea kutoa utetezi wake, Lissu amesema hicho kifungu Cha 312(1) kimefanyaiwa maamzi mengi ya nchi yetu kwa kutengeneza misingi mikubwa ya Kisheria juu ya kitu gani Mahakama inatakiwa kujibu kuhusu hakuna kesi ya kujibu(No case to answer).
Amesema msingi mkuu Wa Kisheria juu ya kwamba hakuna hoja ya kujibu iliwekewa tangu miaka 70 iliyopita na mahakama ya Rufani Afrika Mashariki.
Amesema kesi hii si ya kwanza kufanyika nchini Tanzania,bali ni kesi ya tatu,iwewemo ya Khatibu Gandi na wenzake dhidi ya Jamhuri.
Amesema katika kesi ya kwanza kati ya Gray Nkunku Matata na wenzake iliweka vigezo vitatu kuthibitisha kama kesi ni ya uhaini,akitaja vipo ukurasa wa 406.
Utiifu wa Jamhuri,Je, ulikuwa na nia ya kutenda kosa la uhaini?,hiyo nia lazima uthibitishwe kwa maandishi au kwa matendo ya wazi. 39(2d) kwa mujibu wa kifungu Cha makosa ya adhabu.
Aidha Lissu ameendelea kuisisitiza Mahakama kuturuhusu kujitetea kwasababu hana kesi ya kujibu
Hata hivyo mshitakiwa amesema bado Mahakama inaweza kutoa fidia kwa hizo siku zote 496 kutokana na kifungu Cha 367.