Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,305
- 33,924
Hiki kiwewe cha CCM dhidi ya Tundu Lisu kinatokana na nini hasa? Aliposema kwamba anagombea Urais wa TLS timu nzima ya CCM kuanzia Mwenyekiti wao wa taifa ikawehuka. Wengine tukajiuliza kwani TLS imeanza wakati Lissu anatangaza kugombea huo Urais wa TLS?
Wakati wa kupitisha Mswada wa Sheria ya Habari tulishuhudia bunge likiendeshwa hadi usiku sana huku wabunge wa CCM kama vile walikuwa wamejifunga kibwebwe dhidi ya Lissu. Hadi wengine tukapata hofu kwamba labda huenda Lissu anamiliki chombo cha habari ambacho sheria husika ikipitishwa basi serikali itafaidika kwa kukifuta chombo hicho.
Wakati wa uchaguzi wa mwaka 2010 inasemwa kwamba Jakaya Kikwete alipata kusema ni heri watu wa Jimbo la Lissu wasimchague yeye kuwa Rais lakini pia wasimchague na Lissu kuwa Mbunge. Hapa tena tukasema inakuwaje mtu anayetaka kuwa Rais anaona ni bora mgombea wa chama chake ashinde ubunge lakini yeye pia asipewe kura na hao hao anaoomba wamchague mgombea wake ubunge!? Kisa Lissu!
Kwa nini Jeshi zima la CCM huamia kwenye mapambano na Lissu kwenye kila jambo analolisimamia? Wakati Lissu anawatetea watu wa Bhulyankulu dhidi ya wachimbaji wawekezaji, CCM nzima ilikuwa kinyume chake. Leo wanadai anaogopa kesi wakati hajawahi kukosa kuhudhuria hata zile kesi wanazomzushia kila uchao.
CCM kwa nini inapagawa kwenye mambo mengi sana anayoyafanya Lissu?
Wakati wa kupitisha Mswada wa Sheria ya Habari tulishuhudia bunge likiendeshwa hadi usiku sana huku wabunge wa CCM kama vile walikuwa wamejifunga kibwebwe dhidi ya Lissu. Hadi wengine tukapata hofu kwamba labda huenda Lissu anamiliki chombo cha habari ambacho sheria husika ikipitishwa basi serikali itafaidika kwa kukifuta chombo hicho.
Wakati wa uchaguzi wa mwaka 2010 inasemwa kwamba Jakaya Kikwete alipata kusema ni heri watu wa Jimbo la Lissu wasimchague yeye kuwa Rais lakini pia wasimchague na Lissu kuwa Mbunge. Hapa tena tukasema inakuwaje mtu anayetaka kuwa Rais anaona ni bora mgombea wa chama chake ashinde ubunge lakini yeye pia asipewe kura na hao hao anaoomba wamchague mgombea wake ubunge!? Kisa Lissu!
Kwa nini Jeshi zima la CCM huamia kwenye mapambano na Lissu kwenye kila jambo analolisimamia? Wakati Lissu anawatetea watu wa Bhulyankulu dhidi ya wachimbaji wawekezaji, CCM nzima ilikuwa kinyume chake. Leo wanadai anaogopa kesi wakati hajawahi kukosa kuhudhuria hata zile kesi wanazomzushia kila uchao.
CCM kwa nini inapagawa kwenye mambo mengi sana anayoyafanya Lissu?