Gracious
JF-Expert Member
- Jul 12, 2011
- 1,890
- 1,082
Slaa yuko wapi? Pole mzee wa watu, sasa nenda kalee hicho kitoto chako.
Mtu makini yule,sio mropokaji kama nyie CCM.Ukimsikia anaongea ujue kua kuna jambo,na haongei pumba
Slaa yuko wapi? Pole mzee wa watu, sasa nenda kalee hicho kitoto chako.
yani unanikumbusha zamaaani,unachomaanisha ni sawa na ''kufungwa tumefungwa lakini chenga twawala''.CCM ni chama makini hili limeoneka na lazma litafanyiwa kazi.
Tatizo lenu CDM mlivyo majuhah hii rate ya ushindi mlio upata licha ya kua mmeshindwa imewalevya,hivi siku 2kiwapa nchi sitampagaw a!
Hii siyo sababu, mnashangilia kuchaguliwa na wananchi wa vijijini, wasio na upeo wowote wa kufikiria, wanao gawiwa pande za kanga na sukari, pilau etc, ambao haohao utawasikia hatan leo ukisikiliza kwenye media wakilalama na kuomba serikali iwasaidie shida hata za majumbani kwao, hawana hata haki ya kupiga kura ! Kuwaiga ati hawa wezi wa kura wasio na haya kujenga ofisi wilayani ni upuuzi, ukweli uko palepale, katiba mpya itaainisha level za watu kupiga kura wale wa vijijini hawawezi kuwa wanatuamulia, mind you, mbunge akishateuliwa anafanya makosa kujiona ati ni wa CCM tu, bali ni mwakilishi wa wananchi wote wa jimbo husika! Pili, wananchi waliojitokeza kwenda kupiga kura ni wachache mno, chini ya nusu ya 50% ya waliojiandikisha, mnajivunia nini hapa, kuwatisha wananchi ati CDM ikiongoza kutakuwa na vurugu? oneni haya nawatahadhalisha, na mkae mkijua kwamba mnatakiwa kujifunza sasa, kwamba mwaka 2015 muwe radhi kukubali matokeo mtakaposhindwa! Kuwa muungwana na mkweli, tume ya uchaguzi italkapo kuwa huru kutoka kwa yeyote, ndipo uchaguzi utakuwa wa haki! waangalizi wa kimataifa wa uchaguzi wa 2010 walieleza wasiwasi wao kuhusu idadi ya wapiga kura, ivi huna aibu kujivunia kuchaguliwa na robo ya wananchi? uchaguzi huu ungerudiwa kuwapambanisha wawili hawa CDM ingeshinda pamoja na utaratibu mbovu! sasa utaratibu utakapokuwa mzuri ninyi mtakaa wap! pamoja na maguvu yooote mliyotumia tofauti ya asilimia ya ushindi ni ndogo mno!Hongera yenu ccm, cdm mjipange na muandikishe wanachama vijijin na jengen ofice kwenye wilaya na kata. Maandamano yanayohusisha mashabiki siyo kura. Mkijua idadi ya wanachama wenu ndo kura zenyewe.
Unamaana ipi unaposema 'makini?' hivi ni hilohilo neno la kwenye kamusi! Sidhani kama unalielewa, kitu kimoja tu kitakacho kupa mwanga ktk umakini huo, niambie CCM mara ya mwisho kuhakiki mahesabu yenu ilikuwa lini? je pesa mlizowanunulia ndizi na mihogo waswekeni wa Igunga mnaweza kuzi-account?yani unanikumbusha zamaaani,unachomaanisha ni sawa na ''kufungwa tumefungwa lakini chenga twawala''.CCM ni chama makini hili limeoneka na lazma litafanyiwa kazi.
Tatizo lenu CDM mlivyo majuhah hii rate ya ushindi mlio upata licha ya kua mmeshindwa imewalevya,hivi siku 2kiwapa nchi sitampagaw a!
Magwanda huwa hawana sababu za maana, wao wanasusa tu, ngoja uone watavyosusa.
Nawapa pole sana Magwanda kwa kujeruhiwa kisiasa Igunga. Igunga ilikuwa ni turufu ya 2015. Majeraha yaliyowakumba Igunga si madogo yasipelekee kifo chenu, yatafutieni tiba za haraka haraka. Niwajuavyo magwanda wataanza kutafuta machawi kwani katika chaguzi zilizopita tuliona walivyokuja na kusema Zitto ni msaliti anaongea na Rostam Aziz na Jack, hata vielelezo vya sms vikaletwa, sasa safari hii sijui mchawi ni nani, kwani walijisifu sana humu wamedhibiti kila mahali na ushindi ni wao. Napenda kuwajulisha kuwa mchawi wao ni ufinyu wao wa maarifa na wamekuwa wakiongelea watu badala ya mambo muhimu. Hata Igunga ilikuwa ni hivyo hivyo, niliwasikiliza hotuba za Slaa na Mbowe, nikadhani ni wachungaji wanaohubiri Jangwani, walibadili hata sauti zao na kuzifanya za kixhungaji walipohuburi, sijui ni nani aliwadanganya kuwa ukitumia sauti za kichungaji utawapata wengi, well, wamewapata wengi lakini haikuwa good enough.
Ulikuwa wapi weye?CDM kwa CCM hana tofauti na mtoto mdogo tena uliemlea mwenyewe tabia zake lazma uzifaham.Sisi tumewazoea haya vp kelele zenu zimeishia wapi?Vipi CCM wameingiza tena kontena la vipodoz?
Ushindi ni strategy sio kulalama!
Na mkishatupatia tu.Mzee Ben wa kwanza The Hague.Wezi wote tunawafilisi warudishe hela za watanzania.Ninaisubiri 2015 kwa hamu sana