Tunaokumbuka ' Differential Equations na Integral ' tukutane hapa..

Tunaokumbuka ' Differential Equations na Integral ' tukutane hapa..

Mi niliisoma mpaka f6.. sikuona ugumu wake! Najua huko mbele iko advanced sana... alafu kuna mtu anakuja hapa anauliza eti inakusaidia nini kwenye maisha yako [emoji3][emoji3]
Ni kutokujua tu. Hayo mavitu mbele ya safari huko hutumika kwenye kuderive formula mbalimbali. Kwa mfano zege hilo ulijualo,kuna kitu kinaitwa stress block( zege fc na nondo fy)! Hizo hapo hutumika kwenye design ya nguzo,beams,Slabs,deck za madaraja,Minara ya Simu,Minara ya Tanesco nk. Bila kujua centroid,neutral axis ya umbo,maana yake maghorofa yatadondoka kwani ukikosea Centroid,unatengeneza Eccentricity,ambayo hutengeneza Moment. Mfano wa hiyo eccentricity ni kama vile umebeba ndoo ya maji kichwani,badala ya kuiweka katikati ya kichwa,ukaweka pembeni,kwa vyovyote utapata maumivu makali. Sasa kwenye design ya majengo,mitambo nk,kuna jinsi ya kufanya hesabu kuepuka hiyo 'e', na kama haiepukiki,unafanya option ya kupambana nayo. Kwa kweli licha ya usumbufu,masomo hayo yana ladha yake,ila ujipinde hasa
 
Integration, huku differential equation, pale complex numbers, kule kuna cordinate geometry. Like Physics, kufaulu hayo masomo kunategemea zaidi huruma ya mtunga mtihani kuliko uwezo wa mfanya mtihani.

Sanasana physics, mtungaji akiamua asitoke mtu, hatoki mtu kweli. Ukute swali la Magnetism limevimba sijui unaambiwa toroid imefanyajefanyaje, thubutuuuuu. Hata usolve hilo swali ukiwa uchi huchomoki.
 
Hiyo ni kweli tupu. Na kwa bahati mbaya,ukiwa DIT kwa mfano,matumizi ya hesabu hizo unakutana nayo hapo hapo. Kwa mfano,kwenye masomo ya Strength of Materials,kwenye First and Second Moment of Inertia nk,bila kujua hizo dx or dy ili kupata xtreme fibre points kama zile Modulus,Y and X Bar(Centroid and centroidal axis perpendicular distances) perpendicular to X or Y Axis,ndugu yangu lazima ubebeshwe virago kwa Supplementary na discontinuation.

Kwa mfano,unaambiwa locate centre of mass au Centroid ya maumbo yafuatayo
1. Triangle
2. Rectangle& Square
3. Cycle
4. Composite figure
Na maumbo hayo unapewa vipimo vyake ni kwa mfano Upana 'w' na urefu 'l', pembetatu unapewa kitako 'b' na kimo 'h', hakuna namba wala nini. Hapo anakuambia locate hiyo Centroid about X- Axis na Y- Axis. Hakika kama hujui Intergral,lazima utoe macho.
Kwa mfano majibu kwa pembe tatu ni h/3, 2h/3 na b/3 na 2b/3 kutegemea swali limetaka nini. Lakini kwanza lazima ukate umbo lako katoka infinite small portion dx au dy ikiwa na limit 0-h au limit 0-b. Nimeanza kusahau,kwa sababu ni muda mrefu.

Laplace, Green theorem, Fourier series, Partial differentiation.
 
Back
Top Bottom