Tunamuonea Rais Kikwete?

Humjui Kikwete.

Laiti ungemjuwa usingeleta pumba ulizozileta.

Ni hotuba ipi aliyonung'umika kama utakavyo iwe?

Hotuba za Kikwete zote, ni fundisho kwa watu kama wewe wanaolalamika na kunung'unika kila siku lakini mnachonung'unika hakijulikani.

Hotuba aliyoongea na wazee kuhusu madaktari, licha ya kuwaelewesha kilichojiri, alitamba sana na hata kukejeli. Na mpaka leo tumeona madaktari ni kimya na wala hutowasikia tena wakilalamika. Huyo ndio JK.

Hotuba ya juzi umeona alivyowanyamazisha kwa kukurupuka na kudakia hoja kwa mafanikio ya jitihada zake.

Kikwete, hakupewa "favor" kuupata Urais kama ilivyokuwa kwa wote wa kabla yake. Kikwete alijuwa kabisa kuwa anataka awe Rais na alijipanga hivyo kwa miaka mingi sana na akaupata licha ya kuletewa mizengwe na Nyerere katika uhai wake.

Nakuona una haha kutafuta la kusema kuhusu Kikwete lakini ukweli ni kwamba hamumuwezi kabisa, kila afanyacho hufanya kwa maslahi ya wananchi na si ya kwake binafsi. Leo hii kikwete angekuwa na madudu japo asilimia 1 tu ya madudu ya Mkapa sijui kama angebaki kwenye Urais, maana mlivyomsakama si kidogo, lakini hamna zaidi ya kuzuwa tu na kutafuta kisichopo, mtatafuta sana lakini bure tu.

Humjui Kikwete, unamsikia tu na unamkisia, he is way too far ahead from your way of thinking. Wewe bado una fikra za kizamani sana, za wakati wa dhiki za chai kukorogwa kwa lawalawa badala ya sukari.

Mnajionea nafsi zenu wenyewe na ndio mpaka zinawafanya mnakuja kubwabwaja hapa hapa, ati "tunamuonea Kikwete", una ubavu upi wewe wa kumuonea Kikwete?

Humjui Kikwete1
Post yako ni too emotional hadi umeshindwa kutuambia Kikwete amefanya nini hata kimoja ashukuriwe, zaidi ya kusema alijipanga kuwa rais. Je, alijipanga kuwakejeri madaktari? alijipanga kuwanyamazisha wabunge? hebu tuambie alijipanga nini kuwa rais, kuinua uchumi?, maisha bora? au kupunguza mfumuko wa bei, alijipanga nini.
 
Mwanakijiji huyu mkuu wetu anataka asifiwe hata vile ambavyo ni wajibu wake mfano
1 kuruhusu report ya CAG ijadiliwe bungeni nayo hii ni kazi?
2. Kuzunguka nchi kibao na kutumia zaidi ya bilioni 600 na hizo safari zikaliingizia taifa milioni 200 nalo hili la kusifiwa?
3. kufunguliwa mashtaka ya kuzuga kwa Mramba na Yona hapa nako panahitaji sifa?
Nafikiri enzi zake za utoto alikuwa anadeka sana
 
Huyu mheshimiwa Rais kinachomtesa hadi sasa ni ule mtandao wake aliouweka mwaka 2005 wa kumuingiza Ikulu.Mtandao wao hawakujipanga iwapo wakiingia madarakani wawafanyie nini watanzania wao walijipanga kuingia Ikulu tu na kupeana madaraka wakasahau wananchi wawafanyie nini.Mambo yamebadilika Ikulu imekuwa chungu anatamani hata afanye SUB lakini haiwezekani.Wao kwa wao CCM hawapendani na kila siku wanasemana vibaya si kwa ngazi ya shina,kijiji,kata,tarafa,wilaya,mkoa hadi Taifa.Ni kweli Bwana Mwanakijiji JK analalamika hashukuriwi kwa kuwa hajawatendea wananchi kile walichohitaji kwani dhiki imetamalaki katika jamii ya watanzania na hatuwezi kumsifia kwa vile hajafanya mambo yaliyotarajiwa kulingana na imani waliyokuwa wameijenga kwake.
 
maisha ya mtanzania wa kawaida sasa hivi ni magumu na ya shida zaidi kuliko enzi za mwinyi na mkapa.. hiyo ni facts sio kwamba tunamsingizia.. Watakaomkumbuka Rais ni hao mawaziri wake ambao wananunua au kujenga nyumba za dola laki 7 lakini any tom dick and harry sidhani kama they would shed a tear if the president resigned today
 
Ukitaka kujua kwamba JK ni Rais wa namna gani, angalia alivyoshiriki msiba wa Kanumba.

Kwamba ameahirisha safari ili ashiriki. Pili katoa ubani milioni 10, tatu kawakumbusha wasanii kwamba ahadi yao anaikumbuka na hajaisahau anasubiri uongozi wa wasanii wafanyie kazi mambo fulani then wampelekee "ripoti".

Misiba mingapi inatokea na hatusikii akiahirisha safari ili ashiriki na badala yake anatuma wawakilishi? Je, kulikuwa na haja ya kusema hayo? Kulikuwa na haja ya kutangaza "ubani" ametoa kiasi gani na kukumbushia ahadi zake? Why asubiri kwenye msiba? Was that a right place ya kukumbushia hilo?

Hilo la kutoshukuriwa, anajitakia mwenyewe na mojawapo ya vitu vinavyomponza ni hilo hapo juu.

Binadamu bwana! hivi mnataka Kikwete afanye lipi? nimeamini kweli hamna shukrani hata kidogo ! hii anaonesha kumjali mtu ambae baadae ni wazi angeitangaza TAnzania, hivi hamjui kuwa Kanumba alikuwa anakuwa kwa kasi kubwa sana! ni mtu mmoja mashuhuri hapa Tanzania, na hii kuonesha ukaribu wake na watu wake leo ANASEMWA ! kweli usilolijua ni usiku wa kiza !
 
Sasa hapa umesema nini?
Naona umesisitiza MMKJ hamuwezi Kikwete....
MMKJ amesema anataka kumuweza Kikwete? kwenye nini?

Aina yako ya uandishi imekuweka Uchi kabisa hapa!! wale wale wa mitaa ya gerezani!
Humjui Kikwete.

Laiti ungemjuwa usingeleta pumba ulizozileta.

Ni hotuba ipi aliyonung'umika kama utakavyo iwe?

Hotuba za Kikwete zote, ni fundisho kwa watu kama wewe wanaolalamika na kunung'unika kila siku lakini mnachonung'unika hakijulikani.

Hotuba aliyoongea na wazee kuhusu madaktari, licha ya kuwaelewesha kilichojiri, alitamba sana na hata kukejeli. Na mpaka leo tumeona madaktari ni kimya na wala hutowasikia tena wakilalamika. Huyo ndio JK.

Hotuba ya juzi umeona alivyowanyamazisha kwa kukurupuka na kudakia hoja kwa mafanikio ya jitihada zake.

Kikwete, hakupewa "favor" kuupata Urais kama ilivyokuwa kwa wote wa kabla yake. Kikwete alijuwa kabisa kuwa anataka awe Rais na alijipanga hivyo kwa miaka mingi sana na akaupata licha ya kuletewa mizengwe na Nyerere katika uhai wake.

Nakuona una haha kutafuta la kusema kuhusu Kikwete lakini ukweli ni kwamba hamumuwezi kabisa, kila afanyacho hufanya kwa maslahi ya wananchi na si ya kwake binafsi. Leo hii kikwete angekuwa na madudu japo asilimia 1 tu ya madudu ya Mkapa sijui kama angebaki kwenye Urais, maana mlivyomsakama si kidogo, lakini hamna zaidi ya kuzuwa tu na kutafuta kisichopo, mtatafuta sana lakini bure tu.

Humjui Kikwete, unamsikia tu na unamkisia, he is way too far ahead from your way of thinking. Wewe bado una fikra za kizamani sana, za wakati wa dhiki za chai kukorogwa kwa lawalawa badala ya sukari.

Mnajionea nafsi zenu wenyewe na ndio mpaka zinawafanya mnakuja kubwabwaja hapa hapa, ati "tunamuonea Kikwete", una ubavu upi wewe wa kumuonea Kikwete?

Humjui Kikwete1
 
Tumemchagua kuonyesha ukaribu sisi?
Wewe unakula ukaribu?
Ukaribu unaleta ajira?
Ukaribu unashusha bei za bidhaa??
Ukaribu unaondoa sky rocketing inflation?

Pathetic!!..............Nataka kutapika kabisa nikiona upuuzi kama huu!!
Binadamu bwana! hivi mnataka Kikwete afanye lipi? nimeamini kweli hamna shukrani hata kidogo ! hii anaonesha kumjali mtu ambae baadae ni wazi angeitangaza TAnzania, hivi hamjui kuwa Kanumba alikuwa anakuwa kwa kasi kubwa sana! ni mtu mmoja mashuhuri hapa Tanzania, na hii kuonesha ukaribu wake na watu wake leo ANASEMWA ! kweli usilolijua ni usiku wa kiza !
 
maisha ya mtanzania wa kawaida sasa hivi ni magumu na ya shida zaidi kuliko enzi za mwinyi na mkapa.. hiyo ni facts sio kwamba tunamsingizia.. Watakaomkumbuka Rais ni hao mawaziri wake ambao wananunua au kujenga nyumba za dola laki 7 lakini any tom dick and harry sidhani kama they would shed a tear if the president resigned today

HApo sikubaliani na wewe
 
no wonder unadiriki kusema kikwete ni rais bora kuliko wote maana matatizo yaliyotokea kwa viongozi wa awamu zilizopita unaona ni matatizo lakini matatizo yanayotokea kwenye awamu ya kikwete unaona ni window of opportunity...!

Matatizo yaliyotokea awamu zilizopita uliyajuwa wewe? au unayasikia katika awamu hii tu?

Matatizo unayoyaona awamu hii ni matatizo yaliyokuwepo toka zamani sana lakini hakuna aliyediriki kuyaweka wazi kabla yake yakafikia mpaka kujadiliwa bungeni na watanzania wote kuyaona "live". Au ulikuwa unaziona ripoti za CAG zikijadiliwa bungeni kabla ya utawala wa Kikwete?
 
Post yako ni too emotional hadi umeshindwa kutuambia Kikwete amefanya nini hata kimoja ashukuriwe, zaidi ya kusema alijipanga kuwa rais. Je, alijipanga kuwakejeri madaktari? alijipanga kuwanyamazisha wabunge? hebu tuambie alijipanga nini kuwa rais, kuinua uchumi?, maisha bora? au kupunguza mfumuko wa bei, alijipanga nini.

Kikwete hana haja ya kushukuriwa na wewe wala mwingine yeyote. Ni lini alisema anataka wewe umshukuru au wengine wamshukuru? Kikwete ni Muislaam na Waislaam hushukuru Mungu, hawamshukuru binaadam mwenzao. Hata mimi siwezi mshukuru Kikwete, ntaemshukuru ni Mwenyeezi Mungu pekee. Kuwa makini kidogo ujuwe wengine hatushukuru binaadam wenzetu, kuwaenzi binaadam wenzetu huwa tunamsifu Mwenyeezi Mungu kwa kuwapa uwezo.

Kwa Kikwete tunamshukuru sana Mwenyeezi Mungu kwa kumpa uwezo mwema kwa yote ayafanyayo, ni kwa uwezo wa Mwenyeezi Mungu na tunamuomba Mwenyeezi Mungu amzidishie kila la kheri na mafanikio mema, azidi kumpa uwezo wa kuongoza vyema na kufichuwa udhalimu wa wauwa Albino (nilisoma kuna wachungaji walishikwa), waleta madawa ya kulevya (nilisoma kuna wachungaji walishikwa). Na sasa tutawajuwa karibuni ni nani wenye kufanya madudu sitoshangaa nikikumbana na majina mengine ya wachungaji.
 
Kumbe mpo wengi msio na shukrani na msiotambua mambo bwelele ambayo Kikwete kawafanyia. Jamani karudisha 'chenji ya rada' hamshukuru?

Mzee Mwanakijiji

Nitakuuwa mtu wa mwisho kumshukuruu Kiwete katika Tanzania yetu hii. Tanzania iliyojaa uoza Kiuongozi, inanuka Rushwa kila kona na imekosa UTAWALA WA SHERIA japo hata kiduchu!Mfumuko wa bei sasa haukamatiki. Badala ya sera zake za MAISHA BORA kwa Mtanzania imekuwa ni MAISHA BOMU kwa kila Mtanzania.Mishahara ya Wafanyakazi hataki kuongeza. Ameambiwa apunguza basi KODI kwenye mishahara nalo hataki. Lakini yuko tayari kusamehe WAWEKEZAJI UCHWARA NA MAFISADI KODI KIASI CHA 1.03 TRILIONI IN TSHS! Sasa huyu ni Rais gani hata astahili shukrani??? To hell.

Kiwete hastahili shukrani yoyote. Kiwete ame=prove kwa he is most weak president ever in this country. Hii maneno ya kulalamika na kutaka huruma na shukrani kutoka kwa Watanzania ni KUTAKA KUJIKOSHA ILI AONEKANA KUWA YEYE HANA MATATIZO.

Watu wanaweza kudanganyika kuwa Kiwete amedhamiria kuwapa Watanzania Katiba Mpya. Inaonekana kama kweli lakini siyo. Hii hoja ya Katiba mpya iliibuliwa na CHADEMA na ndipo baada ya Kiwete kpima upepo na kusoma alama za nyakati akaamua KUDANDIA HOJA YA CHADEMA.

Hata hili la juzi ambalo kwenye Mei Mosi kalizungumzia kwa jazba na hisia NI UNAFIKI TU. Bado CHADEMA kupitia Mbunge wake mahiri Zitto Kabwe ndiyo aliibua hoja ya KUPIGA KRA YA KUTOKWA NA IMANI NA PM. Hii ndiyo imepelekea hata report ya CAG ikaonekana kuwa na zito.Je,kabla ya hapo CAG alikuwa hatoi report?? Kwanini zilikuwa zinafungiwa kwenye makabati tu???Swali langu kwa RAIS KIWETE NI KUWA YEYE KWA SASA YUKO AWAMU YA PILI:2005-2010 na sasa yuko ya pili 2011-2015 JE, SWALA LA CAG LIMEANZA KUJITOKEZA KIKAO CHA BUNGE CHA MWAKA HUU TU?? YEYE NA WABUNGE WAKE WA CCM WALIKUWA WAPI MIAKA YOTE ILIYOPITA?

Kiwete aache nafiki bana. Asitake kuzidi kutuchefua Watanzania hapa. Tunasubiri ataje hilo Baraza lake la Mawaziri majuha ambao tuna hakika watakuwa ni walewale kwa msemo wa ''OLD WINE IN A NEW BOTTLE ALWAYS WITH THE SAME SMELL SAME TASTE''. Mzee MM mark my words, CHANGE YA RADA, I TELL YOU ITAISHIA KWENYE MIKONO YA MAFISADI. Tunasikia ETI imepelekwa kwenye UBORESHAJI WA ELIMU. Thubutu!! HIYO CHANGE ITANUNUA VITABU HEWA, ITAJENGA MADARASA HEWA AU CHINI YA VIWANGO,ITATUMIKA KULIPA WALIMU HEWA NA POSHO ZA VIONGOZI WA IDARA ZA ELIMU KITAIFA NA KIMIKOA.

Kwa hapa Watanzania wasitegemee mabadiliko yoyote ya KIUWAJIBIKAJI NA KIUTENDAJI WA KAZI WA SIKU HADI SIKU KATIKA SERIKALI YA CCM maana MFUMO ni uleule,SERA ni zile zile,CCM ni ileile na WATU ni walewale. Changes are IMPOSSIBLE!
 
JK is good sema watanzania hata uwalambe ****** hawawezi shukuru, kila kitu kipo wazi unataka ripoti unapata, sema watanzania mnataka JK huyohuyo awakamate watu na kuwasongesha mahakamani, hawezi fanya kila kitu pekeyake ndio maana kuna taasisi zimeundwa kama hazifanyi kazi zao vizuri hatuwezi msingizia JK. hata zitto alisema wacheni msingizia JK kila kitu, the president is good na hatutapata presida kama JK. wait and see hope JF remains living tutakumbushana hapa.
 
Mh JK karuhusu nchi iendeshwe na wafanya biashara kwa hili hawezi kudhibiti mfumuko wa bei, mie nashangaa tunalamika mfumuko wa bei wkt tuna mamlaka kibao kikwete kwishney
 
Nna uhakika kila ukilitafakari hilo unakosa ubishi. Yes. Nna uhakika na nilichokiandika.

I dont think so....

Natafakari yupi bora.... aliyepewa feva (Mwinyi na Mkapa), aliyepambana kiume (JKN) au aliyeiba kura 2010????

Nawaza mambo kwa kina, na bado majibu sina
uwezo wa Mungu ungekuwepo, angeamua ingwezekana

INGEKUA VIPI, INGEKUA VIPI, INGEKUA VIPI???

kama wezi wa ukweli tungewafunga kikweli........... ingekua vipi???
 
JK is good sema watanzania hata uwalambe ****** hawawezi shukuru, kila kitu kipo wazi unataka ripoti unapata, sema watanzania mnataka JK huyohuyo awakamate watu na kuwasongesha mahakamani, hawezi fanya kila kitu pekeyake ndio maana kuna taasisi zimeundwa kama hazifanyi kazi zao vizuri hatuwezi msingizia JK. hata zitto alisema wacheni msingizia JK kila kitu, the president is good na hatutapata presida kama JK. wait and see hope JF remains living tutakumbushana hapa.
ushukuru kwa lipi??
 
JK is good sema watanzania hata uwalambe ****** hawawezi shukuru, kila kitu kipo wazi unataka ripoti unapata, sema watanzania mnataka JK huyohuyo awakamate watu na kuwasongesha mahakamani, hawezi fanya kila kitu pekeyake ndio maana kuna taasisi zimeundwa kama hazifanyi kazi zao vizuri hatuwezi msingizia JK. hata zitto alisema wacheni msingizia JK kila kitu, the president is good na hatutapata presida kama JK. wait and see hope JF remains living tutakumbushana hapa.

Wewe The Infamous,

Inaonekana wewe J Kiwete huwa anakulamba ****** ndiyo UNAMSIFIA. Kiongozi mzuri ni YULE ANAYEWEKA MFUMO WA KIUTENDAJI NA UWAJIBIKAJI na akaweza KUFUATILIA KWA KARIBU. Je, wewe ni mgeni katika nchi hii? Je,hujawahi kusikia madudu ya PCCB(TAKUKURU),TBS,POLISI,MAHAKAMA,HALMASHAURI NA MASHIRIKA KAMA ATCL,TRL n.k.??Je,Kiwete anakwaga wapi wakti mambo yakizidi kuharibika katika sehemu hizo mhimu???

Mbona ENZI ZA MWALIMU NYERERE(RIP) NA EDWARD MORINGE SOKOINE(RIP) kulikuwa na usimamizi na ufuatiliaji wa karibu kiasi kwamba ILIKUWA NI VIGUM SANA KUKUTA UFISADI KAMA TUNAOSHUDUA KWA SASA??Kiwete na PM wake wanashindwa nini???Jibu liko wazi: HAWANA KIPAJI CHA UONGOZI NA HAWAFAI KUONGOZA HATA KIJIJI.
 
Ni hapo ninaposhindwa kumuelewa Rais Kikwete na dhamira yake halisi ya kuingia Ikulu. Tulishuhudia mtandao wake ukiundwa tangu mwaka 1995 baada kukosa kuteuliwa pale Dodoma. Kujiandaa karibu miaka 10 kuingia Ikulu sio kipindi cha mchezo na kubeza, Wengi walimpigia kura baada ya kushawishika na jitihada zake za kuomba kuenda Ikulu wakitegemea mambo makubwa sana. Kama analalamika hacha ile kwake kwani anajua kabisa kutokana na kulelewa na Chama tawala tangu enzi za Mwalimu, Mzee Mwinyi mpaka Mkapa kuwa wapi palikuwa pabovu na nini cha kurekebisha. Jamani miaka 10 ya maandalizi ni mingi na ukiongeza 7 ya kukaa madarakani inatosha kabisa kurebisha na kufanya mambo makubwa. Tuache usanii na uswahili maana hali ya wananchi inatisha.
Kama umemsikia Mh. Filikunjombe jana asubuhi ITV utapata uchungu. Alieleza kuwa wananchi Ludewa wananunua sukari na mchele sh 3500 kwa kilo wakati debe la mahindi ni sh. 600/=.(mia sita). Eti kuliko kununua sukari ni bora wanywe bia ya 2500/=. Wakulima wa Korosho Mtwara na Lindi wanalia na stakabadhi ghalani kwa muda. Rais Kikwete hakuna kulalamika hacha ile kwako na CCM ikikufia mikononi wenye chama chao hawatakuacha!! Watakumenya tu!!!!!!!
 
Kikwete hana haja ya kushukuriwa na wewe wala mwingine yeyote. Ni lini alisema anataka wewe umshukuru au wengine wamshukuru? Kikwete ni Muislaam na Waislaam hushukuru Mungu, hawamshukuru binaadam mwenzao. Hata mimi siwezi mshukuru Kikwete, ntaemshukuru ni Mwenyeezi Mungu pekee. Kuwa makini kidogo ujuwe wengine hatushukuru binaadam wenzetu, kuwaenzi binaadam wenzetu huwa tunamsifu Mwenyeezi Mungu kwa kuwapa uwezo.

Kwa Kikwete tunamshukuru sana Mwenyeezi Mungu kwa kumpa uwezo mwema kwa yote ayafanyayo, ni kwa uwezo wa Mwenyeezi Mungu na tunamuomba Mwenyeezi Mungu amzidishie kila la kheri na mafanikio mema, azidi kumpa uwezo wa kuongoza vyema na kufichuwa udhalimu wa wauwa Albino (nilisoma kuna wachungaji walishikwa), waleta madawa ya kulevya (nilisoma kuna wachungaji walishikwa). Na sasa tutawajuwa karibuni ni nani wenye kufanya madudu sitoshangaa nikikumbana na majina mengine ya wachungaji.
Umerudia kelele zile zile za mitaani kum-praise bila kutuambia amefanya nini, ningekuona wa maana kama ungesema kafanya nini..
Kuinua uchumi....
Kupunguza mfumko wa bei....
Kuboresha afya, (hospitali, zahanati nk)...
Kuboresha elimu, T/P ratio, enrlolment ratio nk....
Kuongeza ajira, kiwanda gani kimejengwa au hata kuanza msingi....nk nk.

Huna data zozote za kumtetea zaidi ya kupiga kelele (appreciation noise), huna tofauti na akinamama wa mitaani wanaosema tulimchagua Kikwete kwa sura yake.
 
Kumbe mpo wengi msio na shukrani na msiotambua mambo bwelele ambayo Kikwete kawafanyia. Jamani karudisha 'chenji ya rada' hamshukuru?
Mzee Mwanakijiji, ni kweli wapo wengi wasio na shukrani kwa JK, watu ambao hawana hata chembe ya appreciation!. Wao wanaweka reference ya mabaya tuu!. This is not fair!.

Ila pia tupo wengi akina sisi wenye shukrani ambao tunashukuru kwa yote mazuri na mabaya!. Pamoja na mabaya yake, pamoja na udhaifu wake as a weak president, pamoja na kuwa kutokuwa na msimamo thabiti na kushindwa kufanya maamuzi magumu, bado tuna appreciate kwa mazuri machache aliyolifanyia taifa hili na ndio maana mpaka tumemuanzishia thread ya "Miongoni mwa Mazuri ya JK..." na mode akaona ni busara kupiga sticky ile thread.

Na nilipopandisha thread ya "Mabaya ya JK..." mode hawakuipiga sticky bali waliiacha ipotelee as result watu wanaendelea kuichafua ile thread ya " Mazuri ya JK kwa kuijaza mabaya!".

Niliwahi sema Watanzania ni watu wa kulalamika sana na jf ni cross section ya Watanzania hawa hawa kazi kulalamika tuu!. Malalamiko yakizidi yanageuka nagging! na kuzaa negativity ambayo ikizidi inaweza hata kugeuka ugonjwa!.

Nilitoa wito tupunguze kulalamika, tupunguze maneno meengi!. Tuondoke kwenye maneno maneno, twende kwenye matendo!. Tufanye maneno yawe mafupi na vitendo viwe virefu. Lets be positive kuhusu huyu mtu!, Hivyo ndivyo alivyo and he can't be the other way round!.

Nilisema huko nyuma na leo nasema tena na kesho na kesho kutwa nitaendelea kusema. Kikwete ndiye rais wetu tuliomchagua wenyewe kwa kura zetu!. Haijalishi ulipiga kura au hukupiga, haijalishi hukumpigia au ulimpigia as long as yeye sasa ni rais, anastahili heshima yake kama rais!.

JK ndiye rais wa Dr. Slaa, JK ndiye rais wa wanachadema wote!. Jk ndiye rais wa Lipumba, yeye ndiye rais wa wana CUF wote!. Infact yeye ndiye rais wa Wanzanzibari na Watanzania wote no matter wako wapi be it Tandahimba au New York!. Kwa hilo tuu, tumkubali tumkatae ndiye tunaye and that is a fact!.

Ingelikuwa tumemchagua bila kumfahamu vyema, kumlalamikia ingekuwa haki yetu and that would have justify kulalamika kwa sababu hatukujua!. Lakini wakati tunamchagua tulimjua fika inside out what he is, his capabilities and weaknesses na bado tulimchagua!. Hivyo kuendelea kumlalamikia sasa sasa sio kumtendea haki!. Wajameni tumtendee haki rais wetu!.

Wahenga wanasema "Choose your love and love your choice" JK tulimchagua wenyenye na tutake tusitake ni lazima tumpende no matter what! kama ilivyo boga, penda na maua yake!. Tumpende rais wetu na madhaifu yake!.

Sisi tusio na upande wowote tunapata wakati mgumu sana kusimama kwenye hard facts kwa sababu wengi wetu humu wameshachagua upande na wanafuata the American style " You are either with us, or against us". No standing on the fence!.

Binafsi naendelea kushikilia msimamo wangu kutofungamana na chama chochote, Chadema niliwaambia "hawajajipanga", "CCM imechokwa mpaka basi!" na "CUF inaelekea mkao wa kifo" Pamoja na misimamo hiyo nilitoa wito kwa Wana JF tuwe na shukrani katika madogo ili tuweze kupatiwa makubwa!.

Tumshukuru JK yote aliyolitendea taifa hili!. Mnaweza kukuta hata huu utendaji wake ni zawadi kitoka kwa Mungu ili Watanzania tuupate ukombozi wa kweli wa pili baada ya ule wa kutupatia uhuru!.

I Love Tanzania,

Mungu ibariki Tanzania!.

Pasco.
 
Wewe The Infamous,

Inaonekana wewe J Kiwete huwa anakulamba ****** ndiyo UNAMSIFIA. Kiongozi mzuri ni YULE ANAYEWEKA MFUMO WA KIUTENDAJI NA UWAJIBIKAJI na akaweza KUFUATILIA KWA KARIBU. Je, wewe ni mgeni katika nchi hii? Je,hujawahi kusikia madudu ya PCCB(TAKUKURU),TBS,POLISI,MAHAKAMA,HALMASHAURI NA MASHIRIKA KAMA ATCL,TRL n.k.??Je,Kiwete anakwaga wapi wakti mambo yakizidi kuharibika katika sehemu hizo mhimu???

Mbona ENZI ZA MWALIMU NYERERE(RIP) NA EDWARD MORINGE SOKOINE(RIP) kulikuwa na usimamizi na ufuatiliaji wa karibu kiasi kwamba ILIKUWA NI VIGUM SANA KUKUTA UFISADI KAMA TUNAOSHUDUA KWA SASA??Kiwete na PM wake wanashindwa nini???Jibu liko wazi: HAWANA KIPAJI CHA UONGOZI NA HAWAFAI KUONGOZA HATA KIJIJI.

ngosha makoye sikubali kwamba JK hakuna mazuri aliyofanya, hebu cheki kipindi cha BENJAMINI uhuru wa habari ulikuwa vipi, CAG reports zilisomwa wapi, wangapi waliofikishwa mahakamani sampo za akina liyumba, sikatai mwalimu na moringe walifanya yao mazuri ila Jk pia karuhusu mambo mengi raia wayafahamu, hizo taasisisi ulizozitaja hapo juu je ni JK pekeyake ndio mwenye mamlaka ya kuamuru ziwajibishwe, ngosha makoye kila mtu anamabaya yake lkn pia anamazuri. sio ushabiki tu wa kisiasa.
 
Back
Top Bottom