Tunamuonea Rais Kikwete?

He has failed to kick the ball to the net...he himself is the 1st problem...he is very unbelievable with what he promises...ataahidije kupunguza mfumuko wa bei wakati ameshindwa kutimiza ahadi zake za uchaguzi? Is that practical? Ameahidi mishahara kupanda wakati serikali yake inaishi kwa vimikopo vya barclays na wengine? Ameshindwa kuchukua wajibu wake kama aliyeteua na kudai anasupport bunge? Is he really serious? Anaogopa kila mtu! Hana priorities! Amekuwa situational leader...kazi kuchekacheka tu na kutafuta misiba iliko. Ameamua kuplay uswahili wakati taifa linaangamia. Kweli watz tulijiwekea mzigo...na haki ya nani hatuna rais...subiri baraza atakaloteua, utachoka na roho yako!

Kwa wale mnaosubiri hilo Baraza la mawaziri linalokuja nakuombeni muanze kunywa Aspirin msije pata Heart attack bure
 
Wahenga wanasema "Choose your love and love your choice" JK tulimchagua wenyenye na tutake tusitake ni lazima tumpende no matter what! kama ilivyo boga, penda na maua yake!. Tumpende rais wetu na madhaifu yake!.
Pasco

Unataka kutuambia kwa vile tulimchagua kwa mapenzi yetu basi kusiseme hata kama tunaona anatuibia hatekelezi wajibu wake, NO a BIG NO. Hata mke wako uliyemchagua kuishi naye maisha yote huwezi kumpa uhuru wa kufanya atakavyo sembuse huyu wa mkataba wa miaka 10.

Rais hatakiwi kupendwa anatakiwa kuheshimiwa, na ataheshimika tu kwa kutovunja waliyokubaliana kwenye mkataba, kumbuka terms za mkataba wetu ni siku alipotuahidi, Give me your votes I will pay back this and this likiwemo la maisha bora. Yes of course wako watu kama wewe no matter what wrong is doing mtaendelea ku-appreciate hayo mabaya kwa interest zenu siwalaumu. Lakini kwa mtu aliye serious na uchungu na nchi yake na maisha ya baadae ya watoto wote wa taifa hili lazima atasema na kuchukia madhaifu ya rais wake. Wewe endelea kuyapenda madhaifu ya rais wako.
 
Tumshukuru JK yote aliyolitendea taifa hili!. Mnaweza kukuta hata huu utendaji wake ni zawadi kitoka kwa Mungu ili Watanzania tuupate ukombozi wa kweli wa pili baada ya ule wa kutupatia uhuru!.

I Love Tanzania,

Mungu ibariki Tanzania!.

Pasco.

Nahici umeteleza.. So nitaendelea kukupa kaheshima japo mh.. Wanikumbusha yule aliesema JK ni chaguo la Mungu..
 
Inabidi ianze kampeni ya kumpamba Rais wetu kwa maua na sifa; picha zake zibandikwe kila nyumba, magazeti yote yaanze kutangaza habari zake ili asijisikie mnyonge sana na kuwa hapendwi...
 
Pengine kama kuna kitu ambacho bwana mkubwa Kikwete tutamkumbuka na kwa kweli kimetufikisha hapa pa kusema pasi na woga ni kukuza uhuru wa kujieleza...pamoja na kejeli zake pale awali kama vile kelele za mbu hazimzuii mwenye nyumba kupata usingizi, kwa kweli nafuu ipo kinyume na ilivyokuwa wakati wa Mr ANBEM co-founder(mh Mkapa ukipenda muite Mr Kiwira), Mzee Ruksa au Mwalimu.

Walau sasa tunaongea kwa uhuru mkubwa tu...kwa hili pongezi Rais wangu, mheshimiwa, Dk, Luteni Kanali Mstaafu J.M. Kikwete.

Nawasilisha.
Hakika hapo ndio mimi binafsi nakili kuwa kasababisha watanzania wengi kufunguka na kuweza kutambua matatizo ya mfumo wao wa kitaifa,mkoa,wilaya,kata mpaka kijiji!!!
 
Inabidi ianze kampeni ya kumpamba Rais wetu kwa maua na sifa; picha zake zibandikwe kila nyumba, magazeti yote yaanze kutangaza habari zake ili asijisikie mnyonge sana na kuwa hapendwi...

TBC wameshaanza. Huwa wanaweka kanda kuonyesha anakotembelea na hotuba anazotoa. Mwisho wanasema ni kwa hisani ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu. Ni kama vile wanamtangaza zaidi na yale anayofanya kila siku. What a waste!
 
Kumbe mpo wengi msio na shukrani na msiotambua mambo bwelele ambayo Kikwete kawafanyia. Jamani karudisha 'chenji ya rada' hamshukuru?

Mzee, chenji ya rada hajairudisha yeye. Waingereza wenyewe ndio waliochunguza then wakasema. Huyu jamaa kairukia tu juu kwa juu lakini wazungu wale ndo waliianzisha hiyo ishu tena kabla hata che Nkapa hajatoka magogoni..
 
Labda tujiulize swali la ugomvi zaidi - ni uongozi gani ambao Kikwete anapatia taifa kiasi kwamba anafanya mambo mengi mazuri lakini analaumiwa zaidi? Yaani, anafanya mambo ambayo anaamini ni makubwa lakini mbele ya wananchi yanaonekana kama 'hakunaga'?

Yawezekana, we are missing to recognize the genius in our midst? are we that blinded by whatever to the extent that we can not appreciate the work of superb and beloved leader? Ni matatizo ya sisi wananchi kutomtambua yeye au ni tatizo la yeye kutotambulika?

Red color: That's million dollar questions!

Ok watu wake wanatuambia jamaa huwa anajituma, anafanya kazi kwa bidii sana nk nk lakini ikiwa hatuoni matunda then kuna uwezekano huu:

1. Anafanya (kazi zake binafsi) kwa bidii sana lakini ni kwa faida yake mwenyewe (+familia, maswahiba zake)
2. Huwa anadhaniwa kufanya kazi kwa bidii kumbe anazuga - pseudonym
 
Mwanakijiji watanzania huwa tunasema chema chajiuza kibaya chajitembeza. Kama unakumbuka mwanzo ilkifika wakati hata kikwete mwenyewe aliona aibu. Kila gazeti lilikuwa linamsifia, wengine wakasema ametumwa na Mungu, wengine wakatoa sifa nyingi sana. Ni yeye aliyekuwa wa kwanza kukataa sifa, na alitoa mfano kutoka jimboni kwake Ukerewe wakati constituent mmoja aliyempa lift alipomwambia kuwa watu wanakupenda sana, akamuuliza wananipenda vipi wakati hawana maji, barabara mbaya etc etc?

Mwanakijiji angalia mwenyewe yanayotokea katika nchi yetu sasa. Kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiuslama kila kitu ovyo, hakuna kinachokwenda inavyotakiwa. Ni lipi unaweza kumsifu Kikwete and his administration? We are not blinded at all, and we do not need a college diploma to see the mess we are in. Nadhani washauri wake wako smart kutumia weaknesses zake kusmahuri kusafiri na kupata per diem nyingi sana.

Bongolander!
Nakubaliana nawe maisha ndivyo yalivyo. na watanzania (na waafrica kwa ujumla) hatuna tabia ya kujifunza kutokana na makosa! Mfano Dr. Slaa sasa hivi watu wengi wanamuona kama the future candidate for the top office, badala ya kukaa na kujifunza namna ya kuja kuongoza nchi kwa ufanisi au abuni model ya serikali itakayofuta mapungufu yaliyopo, bado anang'ang'ania maandamano ya kila siku na falsafa ya people's power ambayo haitumiki na nchi yoyote humu duniani zaidi ya Libya ya sasa! Akiingia magogoni atakua na jipya lipi? anaweza kuumbuka zaidi ya JK! Dr Slaa akumbuke ku-manage expectations za watanzania after CCM itakuwa sii kazi ya kitoto!
 
Hotuba zake tatu za hivi karibuni zimejaa manung'uniko na malalamiko ya mtu ambaye haeleweki, hapendwi, hasifiwi au ambaye hashukuriwi. Hotuba yake kwa wazee wa CCM wa Dar-es-Salaam baada ya mgogoro wa madaktari na hotuba yake ya Mei Mosi mbele ya wafanyakazi kule Tanga zinatuonesha hisia za mtu ambaye wananchi wake inaonekana hawamshukuru vya kutosha.

Katika hotuba zote tatu Rais amejaribu kutuonesha ni jinsi gani amejitahidi kufanya mambo kadha wa kadha ambayo kwa kweli watu wangemshukuru kuwa ameyafanya lakini inaonekana hashukuriwi. Ni hotuba ambazo zimejaa "tenda wema nenda zako" nyingi. Madaktari hawamshukuru, wafanyakazi hawamshukuru, wapinzani hawamshukuru, na hata wana CCM wenzake yawezekana hawamshukuru. Lakini pia kwenye hotuba ile ya mambo ya nishati ambapo alisifia serikali yake kufanya mengi katika kuzalisha umeme nchini kuliko serikali zilizomtangulia nayo pia ilijaa kutokuwa appreciated.

Ndio sababu najiuliza ni kweli yawezekana Rais Kikwete anaona Watanzania hawamshukuru vya kutosha na kuappreciate vitu alivyovifanya? Ni kweli Kikwete amefanya makubwa sana ambayo anapaswa kushukuriwa kwayo? Ni kweli kwamba Watanzania wanambebesha lawama kwa kumuonea tu japo "amejitahidi" sana kufikia malengo mbalimbali kulinganisha na viongozi wengine waliomtangulia?

Kama ni kweli amefanya yote ambayo anadai amefanya ni kitu gani basi kinawafanya Watanzania wasiyaona mambo hayo na kumpatia pongezi zaidi kiasi kwamba badala ya kuongeza kura zake mwaka 2010 alizipunguzwa kwa asilimia 20 hivi? Kwamba pamoja na yote mazuri anajikuta anashinikizwa kuvunja baraza, utawala wake ukilaumiwa sana na wananchi wakiwa na kiu zaidi ya mabadiliko na uongozi. Tumeona juzi hata baadhi ya viongozi wa chama chake wakimuambia waziwazi kuwa "awe mkali kidogo".

Labda tujiulize swali la ugomvi zaidi - ni uongozi gani ambao Kikwete anapatia taifa kiasi kwamba anafanya mambo mengi mazuri lakini analaumiwa zaidi? Yaani, anafanya mambo ambayo anaamini ni makubwa lakini mbele ya wananchi yanaonekana kama 'hakunaga'?

Yawezekana, we are missing to recognize the genius in our midst? are we that blinded by whatever to the extent that we can not appreciate the work of superb and beloved leader? Ni matatizo ya sisi wananchi kutomtambua yeye au ni tatizo la yeye kutotambulika?

Kaka

Swala kubwa linabaki kuwa WATANZANIA wengi wanapitia kipindi cha kuathirika kisaikolojia, watanzania hawa wameonewa, wametukanwa, hawajasikilizwa na hii inapelekea wananchi wengi kuwa na vidonda vya moyoni 'gubu' au grudge kwa sababu wamenyanyaswa, wameibiwa, wametapeliwa, wamegawanywa, wamedhalilishwa na hata matumaini ya maisha yao ya baadae yamesitishwa!

Ikifikia watanzania hawa waka 'tibiwa' yaani pale ambapo wezi wote wa taifa hiili watakapofungwa na kufilisiwa mali zao, pale ambapo ufisadi utakuwa historia....REBIRTH of real government will occur! government of the people for the people! wananchi watarudisha imani kwa viongozi wao

MKJJ utagundua ugonjwa hapo juu hausababishi matatizo kwa kikwete tu.....viongozi wengi nchi hii hawaaminiwi...yaani wanakuwa kama vile 'walewale' mbaya zaidi cancer hii imeingia mpaka nyumba za ibada!

Hata chadema ikishika nchi leo, swala la kwanza ni kudeal na hawa wezi wote...LA wasipofanya hivi....uchungu huu hautafutika kamwe!!!ambapo tutarudi kule kule

symtpoms za ugonjwa huu ni pamoja na watu kutojitokeza kupiga kura...na kuwa wabinafsi zaidi
 
Jk ni mzee wa mipasho or malkia wa mipasho, sio kosa lake ni kosa la eneo analotoka ama kutokea ama kukulia ama hulka ya watu wa pwani kote ndivyo walivyo, mfano watu wa mombasa zanzibar lindi mtwara malindi pemba bagamoyo somalia nk. Wao siku zote wanajifanya wajuwaji kumbe hawajui chochote washabiki wa zuri sana lakini sio wachezaji wa zuqi,yuko uwanjani anacheza mpira timu yake imefungwa nae pia kashindwa kufunga goli la wazi kabisa, anaanza kulalamika ooo nataka mnishukuru nimekoa magoli mengi sana tulikuwa turudi na kikapu cha magoli! Upntezf point 3 za bure na za wazi kabisa uje utuambie umeokoa magoli mengi sana? Tunachotaka ni ushindi sio uokoaji wa magoli. Pwani pwaa!!!! Hakuna kitu humo.tunahitaji ushindi na sio kutaka shukrani zisizostahiki.

mkuu....hiyo ni stereotyping, haijengi..inabomoa.

nadhani kila mtu awe judged kwa matendo yake na si asili yake....matendo yetu ni chaguo letu lakini asili zetu si chaguo letu(au mkuu ulipata nafasi ya kuchagua asili uliyo nayo, if YES hongera, binafsi sikupata).

i hope unaelewa namaanisha nini!!!!


 
Back
Top Bottom