Mzee ES,
Kyoma,
Kitu ambacho umekielezea kama "mechi" kwa kweli kilikuwa ni mjadala mzito ulikuwa ukiendelea kuhusu mustakabali wa kiuchumi wa tanzania. mwalimu, ambaye umemtaja kama mwamuzi, alikuwa akipokea ushauri unaokinzana toka kwa sokoine na msuya kuhusu hatua za kuchukua kukabiliana na matatizo ya uchumi ya wakati ule. inaelekea mwalimu alimwamini zaidi sokoine, na kumtema msuya. kumbuka kwamba msuya ndiye aliyepewa jukumu la kusimamia industrial master plan ya tanzania baada ya kuvunjika East African Community. mwalimu aliheshimu sana ushauri wa msuya katika masuala ya fedha,uchumi,na mipango, isipokuwa ule wa kukubaliana na masharti ya IMF na WB. mwalimu alipoondoka madarakani naweza kusema ndiyo ilikuwa mwisho wa "mechi" uliyoitaja. tanzania ilifuata masharti ya IMF na WB, na kuachana na sera za Mwalimu na Sokoine. .
Mzee ES,
Kyoma,
Kwa maoni yangu Mwalimu alisuasua mno katika majadiliano yake na IMF na WB. Wakati akisuasua uchumi uliendelea kuharibika, na kufikia mahali nchi zote wafadhili zikatususa. Naamini tungekubali ushauri wa kurekebisha uchumi mapema yasingetufika haya yanayoendelea leo hii Tanzania.
Kafara,
Sokoine alisoma wakati akipata "matibabu" huko YUGOSLAVIA. Vilevile aliporudi Tanzania na hata alipokuwa Waziri Mkuu alikuwa akisomea masters chuo kikuu cha DSM.
Sidhani kama kipindi alichoacha Uwaziri Mkuu na kwenda "kutibiwa" kinatosha kupata shahada ya kwanza. Nadhani UDSM walimruhusu kuchukua masters degree kwa kuzingatia uzoefu wake ktk uongozi na siasa.
Mzee ES,
Hawa viongozi ni watu kama mimi na wewe. Huyo Sokoine mtu wa watu wanawe wamesoma ngambo pia. Sokoine mtu wa watu alipougua alikwenda YUGOSLAVIA kutibiwa. Kama Sokoine, na Kawawa, walikwenda Yugoslavia, na Uchina kwa matibabu, nini kinachowazuia viongozi wa sasa hivi kutibiwa nje?
Tukiendelea kuwabeba viongozi wenye "nia nzuri" lakini kazi mbaya basi Taifa letu halitaendelea. Watanzania tunapaswa ku-raise standards za kupima utendaji kazi wa viongozi wetu. So far Tanzanians have set the standards so low.
Hapo juu nimependa ulivyoanisha ripoti mbali mbali za hayo mashirika majangili na jinsi yanavyoathiri Dhamira ya Nchi MASIKINI Kujikwamua Kiuchumi.Kazi Nzuri!Kuhusu swala la vitisho lifanyie uchunguzi Lakini Usitishike ni watu wanataka kukunyamazisha tu .Wapuuze hawakuwezi!Waheshimiwa,
Hapa nilipo inakaribia saa kumi na mbili asubuhi. Kuna mtu amenipigia simu na kuacha ujumbe kuwa jumbe zangu ninazoandika Jambo Forums zitanitia matatizoni. Sijuhi ni nani, na amepata wapi namba yangu, na amejuaje utambulisho wangu. Ngoja kwanza niwasiliane na provider wangu wa simu ili nijue hiyo simu imetoka wapi, kwa sababu haionyeshi namba kwenye call Id, pia, hata nikiwa nasikiliza ujumbe, namba haitajwi. Mtu mwenyewe anaongea Kiingereza lakini sio lafudhi ya kitanzania.
ujumbe wenyewe sio mzuri, una vitisho.