Tunalazimika sasa kuifahamu SIMBA TRUST

Tunalazimika sasa kuifahamu SIMBA TRUST

Simba Trust ni ya Kikwete na familiya yake, hiyo ndio sababu kubwa ya werema, maswi na mhongo kuwa na jeuri.
 
Kasema mnamsingizia, mnachuki, wazushi yeye hana hela kiasi hicho hahahahaaaaa

Itajulikana tuu, mbona Devi aliitwa tumbili lakini mwishowe imejulikana? Itajulikana tuu hawatakaa kimya milele
 
Ukila nyama ya mtu, hutahacha kamwe! TD alipiga pesa ya EPA kufadhili kampeni zake. Miaka michache baadae akagundua kuna "same loophole BoT" akaona apige tena!

This time ameamua kupiga 50% mwenyewe maana kwenye EPA walimzunguka akajiona mjinga. Lakini, ni mkuu gani wa kaya anayeona fahari kuiibia kaya yake simply b'cause kuna "loophole somewhere"?

Mambo mawili ni muhimu kufanyika:
1. Kutungwe sheria dhidi ya fedha zinazotunzwa BoT ili kuziba "loopholes" kama za EPA na ESCROW
2. AZAKI zioneshe kuwajali Watanzania kwa kufungua kesi ICC ili uchunguzi wa vyombo vya nje ufanyike na ikithibitika, basi TD apelekwe huko Nov. 2015.

TD amepiga sana fedha ya Watanzania!!

Labda kwa ufafanuzi kwa wana jamii,TD hapa mkuu anamaanisha Tezi Dume,asanteni.
 
Ukweli huweka haki wazi,nivizuri tukamjua mhusika wa simba trust na simba trust ilihusika vip kwenye sakata la escrow

Sakata la escrow na IPTL halijaisha na katika maazimio ya bunge jana uchunguzi utaendelea. Tusibiri huo uchunguzi utaoendelea unaohusisha vyombo vyote vya uchunguzi vya dola, labda utatujulisha.

Lakini kwa mujibu wa taarifaa iliyotolewa na PAP hiyo ni kampuni ya Habinder Singh na wana familia yake walitajwa kwenye hiyo taarifa, itafute humu humu JF ipo.
 
wachana na habari ya simba trust, nchi itayumba. inagusa mahali nyeti kabisa kwenye hii nchi na hata maazimio ya bunge yamekuwa na utata kwa sababu hiyo. pesa zilizotoka stanbic zinahusika sana. imekuwa ngumu kujua ni nani walifaidika kwa kuwa zilichukuliwa taslimu yani alitoa mtu mmoja (mwenye akaunti) na kuzigawa kwa wahusika (simba trust ni mmoja wapo). ndo maana PAC walishindwa kujua ni akina nani kwa kuwa bank statement inaonesha muamala wa mmiliki tu, wakaishia kusema marumbesa, viroba, blah blah blah! na pesa zishasepa.

Duh asante kwa ufafanuzi kumbe hapo ni mchezo tu s indicate hii ilipangwa kwa ustadi sana kwa mwananchi wa kawaida huwezi kung'amua jaja hapa inanipa picha kuwa hili sakata hata BoT anahusika maana fedha nyingi km hiyo iliyochukuliwa Stanbic bank isingewezekana pasipo kibali cha BoT kutokana taratibu za BoT kwa mabank insurance n.k kwa hiyo BoT alitoa kibali kutokana na maagizo ya bwana mkubwa amakweli jamaa kaimaliza nchi bila aibu sasa sisi km raia wajibu wetu ni nn kwa hawa wakuu wetu maana imekuwa ni jadi kila anayepewa madaraka huu ndo umuhimu wa lasimu ya Warioba maskini tz yangu
 
Kasema mnamsingizia

Unategemea angekubali kwamba anahusika?

Hata hiyo escrow si walipinga kwamba haikuwa ya uma?mbona badae walinywea?

Uchunguzi ulete majibu hapa,nani ni nani ndani ya simba trust
 
Braza wangu Zitto Kabwe njoo utusaidie hili
 
Last edited by a moderator:
Kikwete kutawala nchi hii ni laana,na laana hii ni funzo mwenyezi Mungu ametupa Watanzania ili tuweze kujitambua na kujitathimini.
Kikwete kutawala ameanza siku nyingi kutuhujumu hasa kwenye umeme,1993 mtoto IPTL alizaliwa baba akiwa Kikwete,mipango yote kwenye umeme
energy sector ya nchi hii anaijua zaidi ya mtu yeyote ndani ya nchi hii na matatizo yote ya energy sector yameletwa na huyu mtu kwa maksudi tangu. 1993.
Kwahiyo
ndugu zangu Watanzania tuwe makini na aina ya watu tunaowaingiza madarakani kwa kura zetu.,
huyu jamaa TD alijipanga muda .mrefu kuwa rais wa nchi hii, infant he had a mission to ruin this country in whatever possible
way.ni mmoja wa watu waliofurahia kifo cha mwalimu.This guy had a mission na ameitimiza kwa 90%,kila kona Watanzania wanalia umaskini umetamalaki,bei za bidhaa hazishikiki,Uchumi umezorota,thamani ya pesa inaporomoka kila kukicha;
pengo la maskini na tajiri ni kama ahera na peponi,rushwa na wizi wa mali ya umma ni sawa na kunywa maji.
Watanzania tulifanya makosa,tujisahihishe ili tusirudie makosa.2015 tuwe macho na makini na aina
mtu atakayependekezwa
na hii satanic family.
 
Kwa nini hakuenda kutibiwa tezi dume wakati alikuwa na yo na iligundulika mwaka mzima uliopita? Na kwa nini aende baada ya sakata la escrow kuanza kupamba moto? Na iweje arudi siku ya mwisho ya escrow saga? Jamaa mjanja sana.
 
Naam, nimeona akiwauzia chadema mafuso chakavu mawili kwa millioni 600.
FaizaFoxy hebu kuwa mkweli katika hili, mbona lilishatolewa maelezo ya kina kabisa? Ni documents gani zinaweza kuthibitisha haya madai yako?
 
Last edited by a moderator:
Hayo maelezo yako wapi? mimi sijayaona.

Mmh basi ni wazi hujui mengi, lakini basi hebu tusaidie kuondoa utata juu ya Simba trust na hizi tuhuma zinaelekezwa kwa familia ya rais, nafahamu umahiri wako wa kuchimba mambo hebu chimbachimba na hili
 
Back
Top Bottom