Tunajifunza nini juu ya kesi ya Prof. Assad?

Tunajifunza nini juu ya kesi ya Prof. Assad?

Kesi km hizi zinatakiwa hikumu itolewe mapema ili haki itendeke, sasa mgoni wako hayupo ndiyo unavua shati upigane ni upumbavu mtupu.Walimuogopa sana yule jamaa.
Kawaulize ccm hata kesi ya kina Mdee na wenzake hukumu itakuja kutolewa hivi hivi ni matakwa ya ccm wala siyo ya Wananchi.
 
Asad alipaswa tena kufukuzwa kabisa hakufaa. Mi naona hata uteuzi walikosea kumteua mtu ambaye ni fundamentalist ambaye anaamini ktk kile anachoamini yeye.

Ndiyo maana mfumo ndiyo ulimuondoa wala siyo Dkt Magufuli. Ukikumbuka kuna hela fulani nadhani zilikuwa za kitengo yeye Asad akaomba azikague wakamuambia hapana utaratibu siyo huo, akakomaa ila kaenda kusoma ripoti asubuhi hakukuta kitu hahaha. Hii habari alisimulia yeye mwenyewe.

Kikubwa Asad siwezi kumtetea ni moja ya wasomi majanga wasiokuwa na mchango wa taifa. Kila jambo lina mipaka yake, halafu kibaya kabisa akawa anatumika kupindisha report.
Tatizo utawala wa jiwe kila mtu alitakiwa kuimba mapambio ila Professor Assad MchaMungu wa kweli alikataa kuwa sehemu ya waimba mapambio.

Hapo ndo kosa lake sio vinginevyo.
 
Katiba inatoa freedom of expression sasa ni wapi Professor Assad alivunja katiba?
Wapi nilipoandika Assad kavunja katiba. Umesoma ukaelewa ujumla wa comment ama umechagua vipengele/majina maalum kufikia tamati ya kuwa nimesema Assad kakosea?

Inasikitisha kuwa Assad alionewa lakini inasikitisha zaidi kuwa watu walishindwa kuhoji chochote kipindi cha Magufuli. Nina yakini kama Magufuli angekuwa hai leo hii, achilia mbali hukumu hata hiyo kesi isingesikilizwa.

Kama taifa tuna kubwa la kujifunza juu ya mustakabali wa maisha yetu. Ikiwa mahakama ambayo ni muhimili unaojitegemea unashindwa simamia haki kwa kuogopwa mtu mmoja, tujiulize wangapi walihukumiwa/waliwajibishwa pasi kuwa na hatia.

Kuna kina Assad wengi wataendelea kuwepo kupitia tawala zote zijazo endapo katiba haitobadilishwa. Mamlaka ya raisi yamekuwa makubwa mno kiasi cha kujisahau nae ni binadamu.
rejea comment yangu ya juu niliyo i quote hapo labda utaelewa point yangu.
 
Mungu alitusaidia kuondoa mungu mtu,wakaja wana wa adamu, ghafla nao wamekuwa miungu
 
Magufuli was a dictator right? Reasons?
Utasikia aliwakandamiza upinzani.. okey vipi sahivi upinzani bado wamekandamizwa au kuna ishu wanasikilizia?

Kwahiyo kama wapinzani sasa hivi hawapati haki, ndio utetezi kuwa Magufuli alikuwa mzuri ama?
 
Mimi nilichojifunza ni kuwa mahakama zetu zinasubiri.rais afe ndio ziseme amekosea au alikosea. Mahakama zinatoa hukumu kwa wafu na Sio walio hai. Kesi za walio Hai zinafunikwa hadi wafe ndio hukumu itoke. Kiufupi mahakama hazina weledi kwenye kutoa hukumu dhidi ya wenye mamlaka.
 
Mimi nilichojifunza ni kuwa mahakama zetu zinasubiri.rais afe ndio ziseme amekosea au alikosea. Mahakama zinatoa hukumu kwa wafu na Sio walio hai. Kesi za walio Hai zinafunikwa hadi wafe ndio hukumu itoke. Kiufupi mahakama hazina weledi kwenye kutoa hukumu dhidi ya wenye mamlaka.
Ungesema hivi;
Mahakama ziwe zinaharakisha kutoa maamuzi kwa kesi ambazo ni za kikatiba, ambazo masuala yake yana husu ukiukwaji wa katiba.

hata hivyo Mahakama zinajitahidi sana kutenda haki kwa uhuru, mifano ipo mingi sana.

Jambo la msingi tunapaswa tuwe tuna heshimu maamuzi ya mahakama, haswa wanasiasa na wafuasi wao wanapaswa wajenge tabia ya kuheshimu maamuzi ya mahakama yawe mazuri au mabaya kwa upande wao ndio kazi ya Mahakama.
 
Huwezi kwenda Marekani kulisema bunge letu eti ni dhaifu alafu wewe ukajibatiza eti ni muhimili na bado Magufuli akakuangalia tu.
Natumai umejifunza kitu katika Maisha, hakuna mmiliki wa nchi au dunia ,ni Mungu pekee ndio mwenye mamlaka,tenda wema uishi kwa furaha na amani
 
Na amekufa kweli kwa ushamba wake lakini Assad yupo anatamba mtaani na wakati wowote ule anaweza kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hawakuwa wakishindana kwamba nani atatangulia kufa na nani atabaki? Kushindwa kwa Assad ni pale alipoachia ofisi.
 
Tatizo utawala wa jiwe kila mtu alitakiwa kuimba mapambio ila Professor Assad MchaMungu wa kweli alikataa kuwa sehemu ya waimba mapambio.

Hapo ndo kosa lake sio vinginevyo.
Hao wawili hawakuwa wakipatana toka Jiwe akiwa bado waziri hana hata dalili ya kuja kugombea urais, na wote walikutana ni viburi na watu wa visasi.
 
Hawakuwa wakishindana kwamba nani atatangulia kufa na nani atabaki? Kushindwa kwa Assad ni pale alipoachia ofisi.
Heri tu kwa wale wenye akili mpaka leo makanisani tunashangilia kuwa tumemkanyaga shetani na watu wanacheza lakini uovu bado upo tu,tarehe 9/12/2022 itakuwa sikukuu ya Uhuru na Jamhuri na husherekewa kila mwaka lakini mkoloni CCM yupo,hata sisi tunashangilia kufa kwa dhalimu Magufuri ingawa kifo kipo palepale,alijiona hawezi kufa amekufa na watu wanafurahia matunda ya uhuru wao yeye analiwa na mchwa na haitatokea tena Tanzania kuweka mtu kama Magufuri kila mtu amejifunza,ccm wenyewe wamejifunza.
 
Asad alipaswa tena kufukuzwa kabisa hakufaa. Mi naona hata uteuzi walikosea kumteua mtu ambaye ni fundamentalist ambaye anaamini ktk kile anachoamini yeye.

Ndiyo maana mfumo ndiyo ulimuondoa wala siyo Dkt Magufuli. Ukikumbuka kuna hela fulani nadhani zilikuwa za kitengo yeye Asad akaomba azikague wakamuambia hapana utaratibu siyo huo, akakomaa ila kaenda kusoma ripoti asubuhi hakukuta kitu hahaha. Hii habari alisimulia yeye mwenyewe.

Kikubwa Asad siwezi kumtetea ni moja ya wasomi majanga wasiokuwa na mchango wa taifa. Kila jambo lina mipaka yake, halafu kibaya kabisa akawa anatumika kupindisha report.
Wow!!!
 
Magufuli hakumfukuza kazi Asaad. Alichofanya ni kutokumpa mkataba wa pili pale mkataba wa kwanza ulipoisha. Na sheria ya National Audit Act ilimruhusu Magufuli kufanya hayo. Na hiyo sheria ilitungwa na kupitishwa kabla Magufuli hajawa Rais wa JMT. Walichosema High Court ni kwamba hiyo sheria inapingana na Katiba. Hapo Magufuli kosa lake ni lipi? Hiyo sheria hakuitunga yeye mbona?
Kws hiyo Zitto alikwenda mahskamani kwa ajiri ya nini?
 
Na amekufa kweli kwa ushamba wake lakini Assad yupo anatamba mtaani na wakati wowote ule anaweza kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hujui kitu wewe. Unaongea kwa mihemko.
Nimecheka, eti atachaguliwa kuwa Rais 😀😀😀😀😀
 
Magufuli tabia zako ulizoishi hapa duniani sasa unazalilika sana kila ulichofanya kibaya kimetinduliwa wakiwemo vibwengo wako mapunda na clock bad.
Unazalilika =unadhalilika
 
Sometimes kiongozi anavunja katiba Kwa Benefits za watu wengi so hakuna shida

Sidhan kama magu alimtoa bila kosa, lazima kulikuwa na makosa

And possibly yangegharimu uongozi wake and sio kila kitu cha kutolea maelezo Kwa wanainchi
Mbona uwezo wako wa kuchambua mambo ni mdogo namna hii!!!
 
Asad alipaswa tena kufukuzwa kabisa hakufaa. Mi naona hata uteuzi walikosea kumteua mtu ambaye ni fundamentalist ambaye anaamini ktk kile anachoamini yeye.

Ndiyo maana mfumo ndiyo ulimuondoa wala siyo Dkt Magufuli. Ukikumbuka kuna hela fulani nadhani zilikuwa za kitengo yeye Asad akaomba azikague wakamuambia hapana utaratibu siyo huo, akakomaa ila kaenda kusoma ripoti asubuhi hakukuta kitu hahaha. Hii habari alisimulia yeye mwenyewe.

Kikubwa Asad siwezi kumtetea ni moja ya wasomi majanga wasiokuwa na mchango wa taifa. Kila jambo lina mipaka yake, halafu kibaya kabisa akawa anatumika kupindisha report.
Wewe sio mjinga Bali ni
 
What if 1.5 zilinunua vifaa vya jeshi?

Kwani ni lazima yy ambiwe? But magu sio mjinga amtoe Kwa kuhoji 1.5 lazima kuna kitu na sio muhimu Sisi kujua, as long as mambo yameenda vizuri
Vifaa vya jeshi ni siri?
Unafikiri kule uliponunua watatunza siri?
Kwa hiyo ukitaka kuiba hela ni kusema zilinunua vifaa vya jeshi...
Nchi ina watu wa ovyo sana hii..
 
Back
Top Bottom