Tunajifunza nini juu ya kesi ya Prof. Assad?

Tunajifunza nini juu ya kesi ya Prof. Assad?

Baada ya Mahakama kuu kutoa Hukumu yake na kubaini kuwa Prof. Asad aliondolewa katika nafasi yake ya CAG kimakosa, kwamba katiba ilivunjwa, Viongozi katika maeneo mbalimbali ya Serikali mnajifunza nini?!

Kuna mambo mengi sana ya kujifunza katika sakata la Prof. Asad kuondolewa katika nafasi Ya CAG;

Kwanza baada ya Hukumu ya Mahakama Kuu kutamka kuwa katiba ilivunjwa kumuondoa CAG Asad, nilivuta picha ya siku Prof. Asad alipokabidhi Ofisi na kubeba kilicho chake kweye gari yake ndogo na kisha kuondoka!!
Picha ya siku ile ilinihuzunisha sana na ilionesha kuwa kulikuwa na uonevu na udhalilishaji mkubwa.

Jambo la kujifunza;
1. Viongozi mliopewa dhamana katika maeneo mbalimbali ya taasisi za Serikali acheni kuwaonea walio chini yenu kwani malipo ni hapahapa duniani, lazima utadhalilika.

2. Tuache uonevu na unyanyasaji kwa walio chini yetu.

3. Cheo ulicho nacho leo ni dhamana tu huwezi kuzikwa nacho, watendee mema walio chini yako.

4. Tuheshimu katiba na sheria za nchi.

Ushauri;

Prof. Asad arudishwe kwenye nafasi yake au apewe nafasi ya juu zaidi, ikiwezekana awe hata Gavana wa BOT.
Assad hakumuonea mtu, kilichomponza Ni kusema ukweli na kufukunyua madhambi ya gvt
 
Unajua maana ya kiapo cha SITO TOA SIRI?

sasa Kwa mfano mtu anataka kuhatarisha usalama wa taifa zima unataka bado awepo Tu just because akitolewa katiba inavunjwa?

Kuna mambo mengi zaidi viongozi wanafanya Kwa ajili ya manufaa ya wanainchi
usalama wa taifa kwa kuhoji zailpo trilion 1.5 ? kwani Asad alifanya nini zaidi?
 
Asad alipaswa tena kufukuzwa kabisa hakufaa. Mi naona hata uteuzi walikosea kumteua mtu ambaye ni fundamentalist ambaye anaamini ktk kile anachoamini yeye. Ndiyo maana mfumo ndiyo ulimuondoa wala siyo Dkt Magufuli. Ukikumbuka kuna hela fulani nadhani zilikuwa za kitengo yeye Asad akaomba azikague wakamuambia hapana utaratibu siyo huo, akakomaa ila kaenda kusoma ripoti asubuhi hakukuta kitu hahaha. Hii habari alisimulia yeye mwenyewe. Kikubwa Asad siwezi kumtetea ni moja ya wasomi majanga wasiokuwa na mchango wa taifa. Kila jambo lina mipaka yake, halafu kibaya kabisa akawa anatumika kupindisha report.
Mahojiano yake kule New York niliyasikia vizuri tu. Na ndicho kilichowakera wanaojiona wenye nchi. "IKIWA SISI (CAG) TUMEONYESHA UBADHIRIFU SERIKALINI NA HATUA HAZIKUCHULIWA BASI UTAKUWA NI UDHAIFUWA BUNGE" Kwani sisi kazi yetu ni kuionyesha bunge, na bunge ndiyo inaichukulia hatua serikali kikatiba. Sasa hapa kosa la Asad lilikuwa wapi ?!

Na kama ni hizo fedha za kitengo ndiyo ilikuwa ni tatizo. Ujue ndiyo kichaka cha ubadhirifu. Kutumia kodi za wananchi bila kulitolea maelezo ni ufisadi ule ule. Kitengo lazima kiwe adilifu ili kutoa mfano. Siyo kichaka cha kufichia matumizi mabaya serikalini.
 
Baada ya Mahakama kuu kutoa Hukumu yake na kubaini kuwa Prof. Asad aliondolewa katika nafasi yake ya CAG kimakosa, kwamba katiba ilivunjwa, Viongozi katika maeneo mbalimbali ya Serikali mnajifunza nini?!

Kuna mambo mengi sana ya kujifunza katika sakata la Prof. Asad kuondolewa katika nafasi Ya CAG;

Kwanza baada ya Hukumu ya Mahakama Kuu kutamka kuwa katiba ilivunjwa kumuondoa CAG Asad, nilivuta picha ya siku Prof. Asad alipokabidhi Ofisi na kubeba kilicho chake kweye gari yake ndogo na kisha kuondoka!!
Picha ya siku ile ilinihuzunisha sana na ilionesha kuwa kulikuwa na uonevu na udhalilishaji mkubwa.

Jambo la kujifunza;
1. Viongozi mliopewa dhamana katika maeneo mbalimbali ya taasisi za Serikali acheni kuwaonea walio chini yenu kwani malipo ni hapahapa duniani, lazima utadhalilika.

2. Tuache uonevu na unyanyasaji kwa walio chini yetu.

3. Cheo ulicho nacho leo ni dhamana tu huwezi kuzikwa nacho, watendee mema walio chini yako.

4. Tuheshimu katiba na sheria za nchi.

Ushauri;

Prof. Asad arudishwe kwenye nafasi yake au apewe nafasi ya juu zaidi, ikiwezekana awe hata Gavana wa BOT.
Hivi unahisi kama asingekuwa allah kuingilia kati haki ya assad ingepatikana leo??
 
What if 1.5 zilinunua vifaa vya jeshi?

Kwani ni lazima yy ambiwe? But magu sio mjinga amtoe Kwa kuhoji 1.5 lazima kuna kitu na sio muhimu Sisi kujua, as long as mambo yameenda vizuri
Kosa lako ni kuamini watu badala ya katiba. Watu ni viumbe hai huja na kupita . Kama zilivyo tawala nazo huja na kupita. Lakini katiba ipo kwa masilahi ya taifa siku zote za uhai wa taifa husika.

Mfano leo yuko wapi Maghufuli, lakini Tanzania ipo na katiba ipo. So mapenzi yasikupofushe ukaiacha kweli.
 
Sometimes kiongozi anavunja katiba Kwa Benefits za watu wengi so hakuna shida

Sidhan kama magu alimtoa bila kosa, lazima kulikuwa na makosa

And possibly yangegharimu uongozi wake and sio kila kitu cha kutolea maelezo Kwa wanainchi
Hao wawili walikuwa chui na paka, Assad alianza kumponda Magu toka Magu hajawa rais mara ghafla Magu kawa mkuu wa nchi.
 
Hukumu imetoka 2022.

Rejea nilichoandika mbali ya kuhoji nimesema kusikilizwa na kutolewa hukumu. Toka January 2020 hukumu imekuja kutolewa 2022. Inamaanisha ilichimbiwa chini ya uvungu.

Dhamira sio kumkandamiza Magufuli hapa hivyo hifadhi utetezi wako. Magufuli alikuwa muhanga (nasema muhanga sababu ya kupewa nguvu kubwa na katiba kupelekea makosa aliyofanya) wa madaraka makubwa kiasi cha kutia dosari dhamira yake njema ya uzalendo.
Endapo kungekuwa na katiba stahiki ambayo ingeweza kum control Magufuli kwa hakika angefanya makubwa zaidi pasikuwa na kasoro.

Nguvu nyingi humpa hata aliye muungwana kiburi.

Point sio Magufuli bali nguvu kubwa aliyopewa yeye, waliomtangulia na waliopo sasa na katiba iliyopo.
Kwa hiyo unaamini sasa umuhimu wa kuwa na Katiba mpya? Mwalimu Nyerere aliliona siku nyingi hili kuwa katiba hii inampa Rais umungu mtu.
 
Magufuli alikuwa na uchungu kweli na maendeleo ya hii nchi. Shida ni pale alipoamini kuwa ni yeye pekee alikuwa anajua kila kitu. Ule ulikuwa ni ubinafsi.
Magufuli hakumfukuza kazi Asaad. Alichofanya ni kutokumpa mkataba wa pili pale mkataba wa kwanza ulipoisha. Na sheria ya National Audit Act ilimruhusu Magufuli kufanya hayo. Na hiyo sheria ilitungwa na kupitishwa kabla Magufuli hajawa Rais wa JMT. Walichosema High Court ni kwamba hiyo sheria inapingana na Katiba. Hapo Magufuli kosa lake ni lipi? Hiyo sheria hakuitunga yeye mbona?
 
Magufuli hakumfukuza kazi Asaad. Alichofanya ni kutokumpa mkataba wa pili pale mkataba wa kwanza ulipoisha. Na sheria ya National Audit Act ilimruhusu Magufuli kufanya hayo. Na hiyo sheria ilitungwa na kupitishwa kabla Magufuli hajawa Rais wa JMT. Walichosema High Court ni kwamba hiyo sheria inapingana na Katiba. Hapo Magufuli kosa lake ni lipi? Hiyo sheria hakuitunga yeye mbona?

Hawa si wazee wa uchawa? Hawawez kujua hayo mambo
 
Asad alipaswa tena kufukuzwa kabisa hakufaa. Mi naona hata uteuzi walikosea kumteua mtu ambaye ni fundamentalist ambaye anaamini ktk kile anachoamini yeye. Ndiyo maana mfumo ndiyo ulimuondoa wala siyo Dkt Magufuli. Ukikumbuka kuna hela fulani nadhani zilikuwa za kitengo yeye Asad akaomba azikague wakamuambia hapana utaratibu siyo huo, akakomaa ila kaenda kusoma ripoti asubuhi hakukuta kitu hahaha. Hii habari alisimulia yeye mwenyewe. Kikubwa Asad siwezi kumtetea ni moja ya wasomi majanga wasiokuwa na mchango wa taifa. Kila jambo lina mipaka yake, halafu kibaya kabisa akawa anatumika kupindisha report.
Assad anaamini yeye yupo sahihi kuliko wengine wote, alijiona yeye ni kama boss wa nchi nzima kwa hiyo nafasi ya kuwa CAG, na kama nae angekuwa rais pengine angekuwa ni majanga zaidi na mwisho Assad nae ni mtu wa visasi.
 
Jitu kwa kukosa maarifa linamtetea Magufuli, tuonyeshe basi kivipi hakuvunja katiba- hawezi. Eti oooh mzalendo, wapi pameandikwa ukiwa mzalendo ruksa kuvunja katiba
Kwani katiba ni msaafu?? Kwamba hata angemtukana rais basi aangaliwe tu sababu kuna katiba?

Nafasi yake ilikuwa finyu kuliko nafasi ya urais ya mwenzie. Akitaka achukue fomu 2025 kama rahisi.

Huyu alianza kutofautiana na Magufuli pale ofisi yake ilipopunguziwa bajeti.Akaanza kusema atashindwa kuwapeleka vijana wako nje kusoma na kuchukua mafunzo. Hapo tayari kila ofisi ilipunguziwa bajeti ya safari, warsha, posho na vikao. Wakati ye anaona kisima mwenzie alikuwa anaona bwawa.

Kuongezea juzi mama kasema mtu akimpinga hatoshirikiana nae, na hata sheria za nje zikimbana yeye atatumia kanuni zake kuwabana. Ndivyo ilivyo.
 
Magufuli tabia zako ulizoishi hapa duniani sasa unazalilika sana kila ulichofanya kibaya kimetinduliwa wakiwemo vibwengo wako mapunda na clock bad.
Kuzuia mikutano ya kisiasa kwa wapinzani mbona Samia kaona ni jambo zuri kutoka kwa Magu.
 
Sometimes kiongozi anavunja katiba Kwa Benefits za watu wengi so hakuna shida

Sidhan kama magu alimtoa bila kosa, lazima kulikuwa na makosa

And possibly yangegharimu uongozi wake and sio kila kitu cha kutolea maelezo Kwa wanainchi
Hii kali kidogo kumeza
 
Back
Top Bottom