Tunahitaji chama kipya?

Tunahitaji chama kipya?

Kwa mwendo tunaoushuhudia siki, majuma na miezi michache iliyopita taifa linahitaji chama kipya ambacho kitakuwa kwa ajili ya wananchi, sio hivi vilivyopo ambavyo ni vyama vya viongozi, wananchi wanachukuliwa kama misukule tu!
 
Kwa mwendo tunaoushuhudia siki, majuma na miezi michache iliyopita taifa linahitaji chama kipya ambacho kitakuwa kwa ajili ya wananchi, sio hivi vilivyopo ambavyo ni vyama vya viongozi, wananchi wanachukuliwa kama misukule tu!
Mkuu mbons vyams vipya viko vingi?Kuna CCJ,CCK,Kuna Chama cha dovuta,TTP maendeleo etc wewe Tu na roho yako
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!


Uchaguzi wa 2015 ni vigumu opposition kushinda. Mtu anayeweza kushinda ni independent candidate hawa kwenye vyama wengi ndio wale wale tu.
 
Mwanangu mwanakijiji, hatuhitaji chama kingine, nadhani CDM ni mbadala tosha wa CCM. Watu watapanda na kushuka, watakufa na kuzaliwa, lakini kwa kuwa nchi yetu ni hiii hii, mifumo itabadilika. CCM ikianguka, CDM itachukua uongozi, lakini mabadiliko ya kweli yatachukua muda. Nadhani maendeleo tunayoyawaza (economic development) yatawakuta wajukuu zetu wakiwa na umri kama wetu leo.

Tatizo langu halipo katika hayo mambo madogo-madogo, bali katika 'moral development' hapa vizazi vyetu vijavyo kumi, vinanitia wasiwasi. Maana 'you can't have economic development without affirmative moral ground'

Pole mwanangu mwanakijiji kwa kuona kipenzi chako ZZK akipita katika mtikisiko utakao myumbisha na kumdunisha kisiasa. Pole sana. Ila uwe na imani na amani, maana CDM na TZ zitaumu hata bila ZZK





Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!
 
je wakija wenye hela zao na kuwanunua wakati mko kwenye mkakati wa kuchukua nchi? manaake thats what is happening with CDM, it also happened to NCCR! dont be a worst Thomas!

Pevuka and kama you have doubt, you need doubt your doubt! hela ni hatari kwa asiyejitambua na mwenye tamaa like your frends!

Me I know Kitila, nadhani by the time nagraduate alikuwa fresher! the trust that i had for him! nimeamini ''amelaaniwa amfanyaye mwanadamu kuwa tumaini lake'',
 
MM,vyama vipya kwa watu wapi?,kama vyama vipya kwa watu wapya tena wazalendo inawezekana,lakini kama vyama vipya kwa watu hao hao haiwezekani ni sawa na kulia na kucheka,zote ni kelele tu!
 
mi naona tunahitaji chama kipya kwani vyama vilivyopo mpaka mda huu vimetofautiana majina tuu lakini vyote vinatabia zinazofanana
 
mi naona tunahitaji chama kipya kwani vyama vilivyopo mpaka mda huu vimetofautiana majina tuu lakini vyote vinatabia zinazofanana

Mkuu chama kipya watu wale wale na sera zile zile si bora tuendelee tu na hivi tulivyokuwa navyo.
 
Sasa naanza kuamini maneno yako babu hivi vyama hakuna jipya zaidi ya madarka na sasa tuona haya ya CHADEMA tayari kansa imeingia hawawezi kupona itawatafuna wote wewe ngoja
 
Tatizo ni vyama yaliyotokea uchaguzi wa CUF kwa Professor Saffari kukashifiwa au Chadema Zitto Kabwe kuzuiliwa nani anaweza kuviamini vyama hivi kienyeji tu?TLP uchaguzi wao walitaka kugombea wakavuliwa uanachama.

Kibanda alikuwa mkali kama Mbogo sababu kubwa ni mkate wa Tajiri yake kuhatarishwa.uchaguzi wa vijana umeahirishwa hadi miezi sita ijayo sababu Mgombea wa kaskazini alikosa nafasi.

nani Mwenye akili timamu anaweza kujiunga huko Chadema kwenye mazingira kama haya? Zitto ana miaka 16 ndani ya Chadema haaminiwi.jee Mkandara anaweza kuaminiwa?

Hivi karibuni imeletwa Taarifa kuwa Maaskofu wako nyuma ya DR.Slaa /Chadema ambaye alikuwa katibu mkuu wao kwa miongo kadhaa nani atajiunga kwenye chama ambacho hakina maaamuzi ya kikatiba zaidi ya vizee vinne tu?

ndiyo akili yako yote imeishia hapo?
 
unajua I'm getting to that point kwa kweli... tuwaache watawale.. hadi tuchoke

Huu mwaka nadhani tutaachana njia panda..... Dalili ya kuwa watu wazima lol!

Kama Musa angewasikiliza wana wa Israel walipoifikia bahari ya Sham huku nyuma Pharaoh na majeshi yake wakiwakaribia pembeni kukiwa na milima basi sidhani kama tungekuwa na tumaini ss wa leo!

Report zenu ni mbaya kwetu ashukuriwe Mungu kwakutupatia mioyo thabiti ya Kaleb na Haruni..... Pamoja na ukubwa ya miili yao watageuka chakula chetu!

Hakati tamaa mtu hapa na siyo wakati mwingine 2015 tumo ndani ya nyumba!
 
Kuunda chama kipya haitasaidia kitu.Hakuna chama ambacho kitakuja na jipya zaidi ya CHADEMA,CUF,NCCR na TLP.Tatizo si hao.Tanzania kuna matatizo mawili,CCM na watanzania wenyewe.Vyama vya upinzani vinavurugwa na nguvu ya CCM na huu mtego wa CCM unafanikiwa kwa sababu wapinzani hawana sapoti ya kutosha ya wananchi.Kwa mfano CHADEMA haina sura ya kitanzania kwa sababu watz si werevu,si wapambanaji,si jasiri wa maamuzi magumu.CCM ina sura ya kitanzania,watu waoga,wenye kupenda rushwa,sifa za kijinga,wabinafsi,wasio wazalendo,wanaothamini wageni kuliko damu yao.Ndio maana spidi ya upinzani ni ndogo sana huku CCM ikifanikisha fujo zake.Kwa hiyo ukitaka kuiokoa nchi hii ni lazima uanze na wenye nchi,wafanane na wanamabadiliko,hapo upinzani utafanikiwa.Mtaunda chama kipya lakini kitavurugwa na mkono mrefu wa Lumumba,labda uniambie vyama viundwe vingi vikiwa na command center moja ili kuipoteza maboya lumumba na kuipa wakati mgumu kibajeti kuhandle hiyo vita kubwa.Lakini hili linahitaji discipline ambayo nahisi bado hatuna.Nadhani watz watafunzwa na CCM yenyewe,wanyonywe na kunyanyasika hadi wakumbuke kujitetea na kusimamia haki zao.Acha tu CCM iendelee kutawala ili ijikaange kwa mafuta yake.Miaka 10 mbele akisimama mtu kusema neno la mabadiliko,mtamshangilia huku machozi yakiwatoka na hao ndio wapiga kura watakaoleta mabadiliko(wapiga kura wenye machozi baada ya kusulubiwa sana na watawala wakorofi).
 
Tatizo sio vyama vilivyopo, tatizo ni understanding ya Watanzania ambao wizi,ufisadi na madhia mengine ya namna Watanznia kummpa jina jipya la mtafutaji au mchalikaji. Dhana hii ya kukosa elimu yauzalendo na kujua kuwa huy hana msamiati wakumwita ila ni mwizi na muhujumi huchumi, hatutafika popote pale.kingine ni umasikini uliokithiri miongoni mwa Watanzania hasa waishio vijijini kunafanya watu wanunulike kirahisi. Kwa hili la pili ndilo chanzo cha matatizo yote.
 
Chama ninachokifiria hakitafanana na chama chochote ambacho kipo sasa hivi; kimuundo, kiitikadi, kimwelekeo na kimfumo. Kitakuwa ni chama ambacho kinarudisha nguvu ya kutawala kwa wananchi wenyewe. Chama ambacho kitakuwa radical in its ideology, liberal in its pursuit of economic prosperity, and conservative in its application of the rule of law and justice. It will be an attempt to bring immediate and recognizable change in our society.

It will stand on certain principles that were the foundations of the building of our Republic. It will not be a mere creation of an idealist but a true manifestation of the reality of our ambition we have as a people. Believe me... change is coming.

CCJ :smiling:
 
Vyama karibu vyote vikiwa vipya vinakuwa na nafasi ya kuwapa matumaini watu kwamba vitaleta mabadiliko makubwa, hapa Tanzania historia imeonesha vyote vimeshindwa kutimiza matumaini haya.

Kabla ya kuanzisha chama kipya na kurudi kwenye mzunguko huu huu (I call this the "vicious cycle of disappointment") kwa mara nyingine, labda inabidi tujiulize kwa nini vyama vyote vimeshindwa kuleta mabadiliko tunayotaka?

Tatizo liko wapi?

Tuna tatizo katika vyama ama lipo katika kina zaidi kuzidi vyama? Tuna matatizo yaliyojikita katika utamaduni wetu? Taasisi zetu za elimu? Taasisi zetu za kiserikali na zisizo za kiserikali? Malezi? Lishe?

Tukianzisha chama kipya, kitaepukaje matatizo yaliyovikabili vyama vya awali ambavyo vilikuwa tegemeo la watu? Kitaepukaje ubinafsi mbaya, migogoro ya kijinga, ubabaishaji, uongo, uzandiki, undumilakuwili na vingine vilivyosababisha maanguko katika vyama ambavyo vilionekana kimbilio hapo awali?

Kwa maana kama tuna matatizo yaliyozidi ngazi ya vyama, kuanzisha chama kipya maana yake ni kujaribu kutatua tatizo bila ya kupita ngazi ya tatizo, kujaribu ku uninstall operating system ukiwa ndani ya hiyo operating system au kujaribu kung'oa msingi wa nyumba ukiwa ndani ya nyumba.

Albert Einstein alisema ukichaa ni kujaribu kitu kile kile na kutegemea matokeo tofauti.

Nahofia kwamba kuanzisha chama kingine cha siasa kunaweza kuwa ni kurudia kitu kile kile, na kutegemea matokeo tofauti.

Tunahitaji vyama vingine, lakini tunahitaji mabadiliko makubwa kuzidi ngazi ya vyama kwa mtazamo wangu.

Otherwise, tutaanzisha chama kipya na kutumaini tu kwamba over time tutafanya self correction, even in a trial and error style, na hatimaye siku moja tutapatia. This could be a very long process indeed with no systemic checks to guarantee a convergence towards our goals.
 
MM Mimi nimekuwa big believer wa Chama kipya tangu awali. Tukumbuke vyama hivi vya upinzani vimeanza miaka ya 90s waanzilishi wa vyama hivi walikuwa na malengo yao binafsi wengi ni recycled from CCM. Either tunataka au hatutaki ulipo anzia pana nafasi kubwa sana kutengeneza unapokwenda Since majority of "wapinzani" wanatoka CCM basi ideology Zao zimejengeka Kwa misingi ya KiCCM. Tazama katiba zao basi utaona CCM ndani yake, tazama mipango ya ungozi wao basi utaona CCM ndani yao.

Sikubaliani kabisa na wanao sema Watanzania ndio tatizo, Hapana taifa hili ni Changa na wenye upeo wa kuona hili taifa linatakiwa lifike wapi ni wachache na tuliowapa dhamana wote ni wezi. Iwe CCM au CHADEMA ni hao hao. Wametengeneza misingi ya kulindana na wanzilishi bado wapo. Angalia ANC ilikuwa butu Kwa miaka 30 baada ya waanzilishi Kufa ndipo ilipoanzishwa youth league ambayo ili fanya mapinduzi makubwa ya kifikra.

Kuna haja ya kuanzisha chama kipya ambacho kitaanzishwa na kundi la watu at least 100 wenye uwezo na uweleo mbali mbali ambao watatengeneza katiba ambayo si ya kumuweka mtu bali katiba itakayo saidia kuleta maendeleo ambayo Watanzania wenzangu wamengoja tangu na kabla ya kuwa Tanzania.

Nchi hii inataji mapinduzi ya kifikra na yeyote ambae alishakuwa CCM hata Kwa weekend moja kama mwanachama basi amepoteza uwezo wa kufikiri. Ni muda muafaka kuachana na siasa mchwara na kuanzisha movement.
 
Back
Top Bottom