Tunahitaji chama kipya?

Tunahitaji chama kipya?

Ni aibu sana inapofikia watu waambiwa kuwa hata waskae na wazee wao nyumba moja kisa utofauti wa vyama huku wao wakifanya biashara na hao maadui zao pia, kuna mengi ninayashangaa lakini jibu ni kuwa waadilifu wa kweli bado haujafika wakati wao, ni suala la muda tu
 
MM Mimi nimekuwa big believer wa Chama kipya tangu awali. Tukumbuke vyama hivi vya upinzani vimeanza miaka ya 90s waanzilishi wa vyama hivi walikuwa na malengo yao binafsi wengi ni recycled from CCM. Either tunataka au hatutaki ulipo anzia pana nafasi kubwa sana kutengeneza unapokwenda Since majority of "wapinzani" wanatoka CCM basi ideology Zao zimejengeka Kwa misingi ya KiCCM. Tazama katiba zao basi utaona CCM ndani yake, tazama mipango ya ungozi wao basi utaona CCM ndani yao.

Sikubaliani kabisa na wanao sema Watanzania ndio tatizo, Hapana taifa hili ni Changa na wenye upeo wa kuona hili taifa linatakiwa lifike wapi ni wachache na tuliowapa dhamana wote ni wezi. Iwe CCM au CHADEMA ni hao hao. Wametengeneza misingi ya kulindana na wanzilishi bado wapo. Angalia ANC ilikuwa butu Kwa miaka 30 baada ya waanzilishi Kufa ndipo ilipoanzishwa youth league ambayo ili fanya mapinduzi makubwa ya kifikra.

Kuna haja ya kuanzisha chama kipya ambacho kitaanzishwa na kundi la watu at least 100 wenye uwezo na uweleo mbali mbali ambao watatengeneza katiba ambayo si ya kumuweka mtu bali katiba itakayo saidia kuleta maendeleo ambayo Watanzania wenzangu wamengoja tangu na kabla ya kuwa Tanzania.

Nchi hii inataji mapinduzi ya kifikra na yeyote ambae alishakuwa CCM hata Kwa weekend moja kama mwanachama basi amepoteza uwezo wa kufikiri. Ni muda muafaka kuachana na siasa mchwara na kuanzisha movement.

mkuu ni vigumu kwetu watanzania kukwepa lawama,sisi ndio tatizo kuu la nchi hii.CCM,CHADEMA,CUF n.k ni vyama vilivyoanzishwa na watz na si wageni.Watanzania hawa unaosema ni wachache ambao ni mafisadi wanawakilisha taswira halisi ya taifa letu.Tuachane na ngazi ya uongozi,tuje huku chini kwetu kwa wananchi wa kawaida maofisini,biashara,nyumbani,vyuoni,mashuleni,kwenye muziki n.k hebu tupia jicho la makini uniambie ni watz wangapi unawaona wanaqualify quality za kimaadili tunazozitaka ili kuwa na jamii inayozalisha viongozi bora?ingawa kuna watu hawakubaliani na hili lakini binafsi hupenda kutoa mfano wa Nyerere,ni kiongozi aliyejitahidi kimaadili yeye binafsi lakini aliangushwa na watu waliomzunguuka.Kilichomkuta Nyerere kinamkuta kila mtu msafi hapa nchini.Waliowahi kuwa viongozi katika nchi hii wanaelewa,iwe umeneja,ukurugenzi,ukocha,udiwani n.k wanaijua picha halisi ya watz.Ukipewa uongozi mahali ukajaribu "kunyoosha mapito" cha moto unakiona toka kwa seniors wako na hata juniors!narudia tena,waliowahi kuwa ktk nafasi za uongozi hata umeneja tu,wanawaelewa watz!Tunalalamika kwa vile hatujapata sisi ule mkate.Tunaendekeza ufisadi kwa vile hatujayaona vizuri madhara ya kukandamizana na kunyimana haki.Ndio maana nasema,acha CCM iendelee,ndio mwalimu pekee wa kuwafundisha watz uchungu wa uovu ili wachague wema.Hebu pitia post ya Kiranga hapo juu,ameeleza vema sana.Jamii ya kifisadi haiwezi kuzalisha waadilifu na jamii yenye maadili haiwezi kukubali kuongozwa na mafisadi miaka yote hii na nchi iko shwaari!
 
Last edited by a moderator:
hatuhitaji chama kipya, tunahitaji watu wapya katika vyama
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!
Hapa tulikofikia hatuwezi kwenda kwa mwendo huo wa kuwekana ndani na kunyongana kwa kuwa wote ndio sisi sisi. Mimi ni masikini lakini mjomba wangu fisadi ndiye ananilipia kodi ya nyumba. Mimi ni fisadi lakini nategemewa na ukoo mzima bila kujali natoa wapi pesa. Mimi ni masikini lakini nafoji vyeti mwanangu aingie jeshi au chuo. Sasa wote tumo ndani na tunaishiriki zambi hii nani atapona likiinuliwa panga? mimi naona hatuwezi kufunga au kunyonga asilimia arobaini ya raia ambao ni uozo katika nchi hii. Kinachofaa hapa tuingie katika kipindi cha mpito cha suluhu. Tutengeneze maadili mapya turudishe azimio la Arusha kisha tuanze moja na kusema yaliyopita yamepita na aliyepata kapata na aliyekosa kakosa tuanze upya. Mambo ya kuangalia nyuma na kulipa visasi hatutaenda mbele bali tutaingia kwenye mauaji ya halaiki
 
Mwanakijiji,
Tuna tatizo ambalo ni kubwa zaidi ya haya tunayoyaona.
1. Uanzishwaji wa vyama vyetu ulisukumwa na nguvu sawa na Uanzishwaji wa NGO nyingi nchini kwetu.
Na ukiangalia hizi NGO idadi yake ikilinganishwa na kazi wanazofanya - utaona uwiano ni mdogo sana.

2. lengo la waanzilishi kuanzisha hivi vyama linatofautiana na lengo la wanachama kwa kiasi kikubwa.

3. Mategemeo ya waanzilishi ni tofauti sana na mategemeo ya wanachama au washabiki

4. Malengo ya kisiasa (viongozi)wanayagundua kadri wanavyosonga mbele.

5. Viongozi wa kisiasa wana ajira kwenye vyama vyao na sio wito wa kutumikia wananchi
 
Kule Australia kulifanyika mashindano ya mbio za mbwa. Katika ya mashindano sungura akakatiza kwenye njia za mbio na mbwa wote wakasahau mashindano na wakaanza kumfukuza sungura.

Now: Kwenye uanzishaji wa vyama vya siasa Tanzania kuna nia nzuri tu kama vile mashindano ya mbio za mbwa. Lakini kuna kitu kinaitwa ruzuku ya serikali kwa vyama vya upinzani (sungura).

Nini sungura...hata angepita paka wangeahirisha...mumbwa ni mumbwa tu muzee...........
 
Mwanakijiji bila Shaka umeadhirika sana na propaganda zinazoendelea Ndani ya CDM na kutokana na alichokisema Zitto Jana kuhusu mwenyekiti Mbowe Nadhani kimepelekea uondoe Imani juu ya chama hiki na hili ni kosa Kubwa.

Nije kwenye Maada, hatuhitaji chama Kipya kwa sasa vilivyopo vinatutosha na kwakweli tunatakiwa kupunguza Idadi ya vyama na Kuwa navyo vichache vyenye nguvu. Watanzania ni wale wale ukifikiria kuanzisha chama Kipya niambie utaanzisha na Watu gani Kama sio Hawa Hawa watanzania? Tunahitaji ku change minds za watz ili waelekee Palipo na ukombozi wa kifikra kwa kutumia vyama hivi hivi na Watu Hawa Hawa cha msingi tuwe na kiongozi ambae anafanya anachokisema Siku zote, kinda Nyerere waliweza wakuwadanganya wanaongoza Kizazi chao cha Wakati ule na hata sasa inawezekana.
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!

Kwa hali ilivyo mzee MM, CCM bado inahitajika kwa muda mrefu ujao!
 
Mzee Mwanakijiji, kwa vyama tulivyonavyo havina tatizo kabisa tena kimsingi hata ccm haina tatizo .Ukizisoma sera za vyama,Malengo na Katiba zao ni safi kabisa.Tatizo kubwa watu ambao ni wachafu kabisa wengi wamekuwa wajanjawajanja na kujipenyeza kwenye vyama kwa sura ya Utakatifu kumbe ni watakavitu.

Hawa watu wachafu wameziba milango na watu wasafi na wastaarabu wanajaribu kuingia lakini kila wakifika mlangoni wanaogopa kuchafuliwa na hawa wajanja wajanja kwani ni wachafu sana na wameziba mlango na madirisha hata pasiwepo pa kupita bila kugusana nao. Ukijitoa Muhanga kwamba liwalo na liwe naingia kupitia mlangoni au dirishani Ukifika ndani kwa sababu ya kukuru kakara za mlangoni hapa ni na maanisha (rushwa,makundi,ukabila,udini nk) vinakuwa vimenata kwenye mavazi yao kwahiyo hata kama una roho safi kwa macho unaonekana mavazi yako kuwa machafu kabisa kwani wakati wa msuguano walikuchafua.Lakini tofauti ya "wajanjawajanja" ambao ni wachafu wa roho na mavazi hawa "wastaarabu" wanakuwa wamechafuka mavazi tu na siyo roho hivyo wanapopata fursa hudhihirisha utu,upendo na uzalendo wao kwa wananchi,Vyama vyao na Taifa.

Kuna watu ambao wamo kwenye vyama hivi ambao wakipewa nafasi wanaweza kurejesha matumaini ya wananchi ,huo uchafu tunao uona katika mavazi yao au kuoneshwa kwao(Kupitia vyombo vya habari) ni wa nguo zao tu lakini siyo katika dhamira zao kwani waliamua kulazimisha kuingia malngoni ili waweze kulikomboa Taifa na kujikuta wakipakwa uchafu na wajanjawajanja.

Kwa maoni yangu kinacho hitajika siyo utitiri wa vyama bali ubora na uimara wa vyama.Hizi changamoto zinazojitokeza ni lazima zitokee kwani vyama vinaongozwa na watu na kila mtu anatabia zake.
 
Siyo kweli kwamba vyama vilivyopo haviwezi kuleta mabadiliko kwa watanzania ninaamini tatizo lililopo kwenye vyama ni dogo sana na tatizo lenyewe ni ubinafisi wa watu wachache sana ambao ukiwasikiliza wanapo ongea unaweza kuwaamini kwamba kweli wanauchungu na watanzania wakati hawana lolote ni ubinafusi tu umewajaa mioyoni mwao
 
Chadema kila mtu akitaka kugombea ndio mizengwe inaanza ila vinajiita vyama vya demokrasia ukweli ni uzushi tu kwa kweli sasa tumejua hakuna chama siasa Tanzania kuna magenge ya watu na mali zao!! lazima kuwa na fikra huru sasa ukifanya ndani ya chadema jua utafukuzwa
 
Tatizo letu kubwa ni "Chumia tumbo" Matukio yanayoendelea huku JF utaona kila mmoja anataka kupata madara ili afaidi yeye na familia yake, malengo amabyo walijipangia/walipanga kama Chama yanaachwa pembeni. Tukiweza kubadili umimi na tuakaangalia Utaifa, basi tunaweza kufika. Vinginevyo tutakuwa na utitiri wa vyama bila mafanikio yeyote
 
Kule Australia kulifanyika mashindano ya mbio za mbwa. Katika ya mashindano sungura akakatiza kwenye njia za mbio na mbwa wote wakasahau mashindano na wakaanza kumfukuza sungura.

Now: Kwenye uanzishaji wa vyama vya siasa Tanzania kuna nia nzuri tu kama vile mashindano ya mbio za mbwa. Lakini kuna kitu kinaitwa ruzuku ya serikali kwa vyama vya upinzani (sungura).
Point nzuri. Naomba pia nitoke out of point, huyo jamaa kwenye profile picture ni wewe unamsaidia shemeji ama?..Kama ni wewe, Hongera.
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!

Unaweza ukalaumu watu wengine lakini kwa maoni yangu wewe ni mmoja wa watu mlio na maoni yanayoyumbisha mitazamo ya watanzania wenye vijihela vya kununua magazeti na kuingia kwenye mitandao.Naamini tofauti sana na unavyoamini.CHADEMA bado inaweza kuchukua utawala nchi hii.Umafia wa ccm na wasomi wap.umba.avu wanaoua vyama tumekwisha wastukia na watashughulikiwa tuu.Hatuhitaji malaika kuja kutuongoza bali mtu mwingine yoyote ambaye hatafungwa na mfumo uliopo wa ccm.Msije mkaanza kurubuni watanzania waendelee na zimwi likujualo.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!

Watanzania wengi na hasa wanasiasa wanajua kuwa ukianzisha chama basi hiyo inakuwa ni mali yako kwa namna yoyote ile. Hawapo tayari kupokea mawazo mapya au upinzani. Mwanachama yeyote anayeibua mawazo mapya huonekana kuwa ni msaliti au anatumiwa. Nikiviangalia vyama vya siasa vilivyopo, wakati mwingine huishia kuhitimisha kwamba ni bora tuendelee na ZIMWI HILIHILI LITUJUALO linaloitwa kwa jina maarufu CHICHIEM.
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!
Mimi binafsi nafikiri ss vyama tulivyonavyo vinatosha. Tuviimarishe hivi hivi na tusonge mbele.

Tunachopaswa kufanya ni kuruhusu mawazo na fikira huru kupenya kwenye bongo zetu na kufikiri kwa bidii huku tukiwa na picha kubwa vichwani mwetu juu ya Tanzania tunayoitaka na si vyama utitiri! Kusoma si kutoka mrango mmoja wa darasa na kuingia mwingine bali kuelimika na kujitambua. Hili la kujitambua kwa kweli Watanzania tulio wengi limetupita kushoto vilivyo ndo maana kila mara huwa najiuliza kuwa huwenda tumerogwa na aliyeturoga kesha fariki!! Hainiingii akili kuona wasomi wetu na hata wasio wasomi kujifanya wafalme ktk vyama wanavyo viongoza na wakati wakihanikiza kila kukicha CCM itoke madarakani kwa njia ya demokrasia.

Hii ni sawa na nyani kutoona kundule na utakuwa ni ujanja wa Mbuni kufunika kichwa mchangani ili mwindani asimwone ilihali mwili ute uko nje! Ni aibu kwa vyetu kutopanua demokrasia ili wananchi waweze kuona tofauti kati ya chama kilicho choka na chama kipya na chenye vijana wenye damu changa. Napenda kutoa ushauri ambao ni somo la karibuni kutoka Uganda kwa Kiiza Beseje aliachia chama kwa watu wengine ili waendeleze harakati na si kung'ang'ania tu bila kuonyesha mbinu mbadala za kushindana na chama twawala. Look guys Beseje leo hii hata akisimama jukwaani akawambia wananchi kuchagua chama chake tayari maneno yake na vitendo vyake vina mashiko. Tuje hapa kwetu tuchukulie mfano chama cha CUF. Hivi Mh. Lipumba kuna nn kingine nikiazima maneno ya marehemu bibi yangu alipenda kusema kwa kilugha (Tona ende ubisile heh). Maana yake huna jingine uliloficha. Kwa maana kwamba kama ni kwenye vita huna mbinu mpya ambayo kwayo hiyo ukiitumia basi mgomvi au adui yako ndo utakuwa mwisho wake.

Niambieni waJF kwamba kwa kuendelea kugombea kwa Mh.Lipumba kunaisadia CUF au ndo kunaendelea kuizika CUF? Je, leo hii ikitokea (simwombei) Mh. Lipumba amefariki ghafla ni nani amemwandaa kuwa mrithi wake asiye kuwa na shaka kushika nafasi hiyo na si peke yake na wanachama wote wakubaliane naye kwa kwa fulani aah hatuna shaka chama chetu kitaendele kuwa salama ni nani waJf niambieni!. Jibu ni hakuna the same na vyama vingine Bussines as usual kutahamaki 2015 CCM imerudi madarakani!!!!!!!!!!!!!!! Tutamsaka paka wa kuvisha kengere huyo! Tutaenda Sumbawanga kumtafuta mchawi tutaambiwa yuko Kigoma huko tutaenda hatutampata mchawi wetu na kumbe mchawi tunaye kwenye miguu yetu aibuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!

Mwisho napenda nisistize tena kuwa tuna muda wa kujisahihisha na kuerkebisha makosa yetu. Kuliondoa dude linalo itwa CCM si kazi ya kufanyia mzaha.

Ukicheka na CCM utavuna
1. Kung'olewa meno bila ganzi.
2. Watoto wako kusoma kwenye vituo vya kukulia watoto wao waviita shule.
3. Tembo kuisha Serengeti Na mbuga zote.
4. Kuuziwa sembe-(madawa ya kulevya) kwa maroli kama Azam anavyofanya.
5. Kama ww ni msanii kama Ray C basi Rais atakutibu ukiathirika.
6. Ukiiba uombe usikamatwe, ikishtukiwa tu unaambiwa urudishe kwa raha zako n.k.

Napita tu jamani mm mwenyewe mgeni nahurmia kucha na meno yangu!!!!! Magamba OYEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE.
 
Back
Top Bottom