Naaam MM UMEFIKA huko tena mkuu!!!Hao ndio watanzania wakenya wanawaita watz. Mkuu tatizo sio vyama tatizo ni MFUMO mkuu!!mfumo wetu unaitaji RESTRUCTURE, tena sio ya kubabaisha.Na atakae simamia hiyo naweza kutoka humo humo CCM, au CDM haitaji chama kingine.Kwa kuwa gharama ya ujenzi wa chama kingine njia ni zile zile alizopitia CDM kukua mpka hapo alipofika kinachotekea fikra za wanachama ndio zinaboreka.
Ndio maana sie wengine vyama tulimalizana navyo tukiwa A-level,hakika kwa mfumo wa Kitanzania siasa za vyama kwa malezi yale ya chama kushika hatamu,kunageneration fulani bado ina amini kuwa Taifa bila aina fulani ya mfumo wa kikundi/kijikundi fulani ndani ya chama kuendesha mambo katika kufanya maamuzi yote yaliyo ya msingi na yasiyo ya msingi kwa niaba ya umma bila kuwashirikisha wengine/umma na hao wengine/umma kuwa wao ni kundi la kupokea tuu kutoka kwa watoaji bila kuhoji ni gharama kwa umma na kwa kikundi pia katika siku za sasa na zijazo.
Aina hiyo ya mfumo wa kijikundi/[ningetumia jina zuri ''those who run the show''] limefikisha Taifa sehemu sote tunadapt.Na kwa kuwa umma wetu kihistoria una nasaba ya USWAHILI KITABIA [Jumla ya zao la tabia za nasaba za Uafrika , Uarabu na Uhindi] , basi nasaba hiyo ya Uswahili [Uafrika, Uarabu na Uhindi] imetufanya kuishi kwa mchanganyiko unaozalisha aina fulani ya tabia za ujanja ujanja, ujuaji, uelevu, uzushi, utapeli,uongo,na mengineyo yote yasiyo na hekima na hasa wengine kujiona ndio chama na hao hao ndio wenye dhamana ya Taifa kuliko raia wengine.
Ebu angalia hii MM, mtu ambae ujana wake hapo zamani alikuwa mnyanganyi, dhurumati, mwongo akatajirika kwa njia haramu na ovu, lakini baadae akahalalisha shughuri zake kwenye umma, baadae kwenye aina fulani ya utu uzima mtu huyo huyo anatumia nasaba ya Uswahili na kujishughulisha na siasa kwenye vyama mtu huyo huyo anapewa madaraka kwenye umma. hapa hivi ni aina gani ya mfumo utaishi?.
Matokeo ya aina hiyo ya nasaba ndiyo yaliyozalisha tabia ya watanzania na hasa familia zetu kushabikia watu wezi/ wadanganyifu waliopewa dhamana za umma/mashirika/makampuni au idara na kuzitumia dhamana hizo kuyaibia na kujineemesha na kwa wale ambao wanageuka na kuwa watendaji na viongozi waadilifu wenye kujali uadilifu [integrity] au unaminifu [honesty] wanageuzwa kuwa wajinga wa ovyo ambao hawakutumia nafasi zao vyema kujitajirisha na kuinua familia zao na marafiki zao.Na kwa kuwa Future security life ya watu haiko bayana hata kama alikuwa mwema na mwaminifu hatosita kuiba na kujifaidisha kwa kulimbikiza kwa niaba yake na familia yake kwa ujumla, kwa kuwa mfumo umeecha Umma kukumbatia tabia ya kusifia vile ambavyo havistahiki kusifiwa katika ulimwengu wa wastaarabu.
MM unajua dhahiri ulimwengu wa wastaarabu ni upi?Je nasaba zetu zinakidhi sie kuadapt yale tunayoweza kusema ni ustaarabu na kujiaminisha kwayo kwa ajili ya ujenzi wa vyama ambavyo tunavipa dhamana ya kuendesha Nchi.Kumbuka wapiga kura na wanachama wa vyama hivyo ndio wale wale wasifiaji wa wale watendayo yasiyostahiki kutendwa.
Mfumo umeruhusu vitu vingi ambavyo [Nikisema mfumo namaanisha waelevu] wenye kuona mbali wamekubali kuwa na aina fulani ya kuachia vijitabia na matendo yasiyo stahiki, kuanzia level za familia mpaka Taifa, na kuvipa ruksa ya kukua na kugeuka kuwa tabia tunazoziishi.
Binafsi mimi ni kijana, lakini sipendi na sitaki kwa kwa kuzingatia kizazi [generation] ya sasa ya wanaochipukia [teenagers-someone who is between thirteen and ninteen years old ] kumiliki simu akiwa maeneo ya Shule.Swala la mtoto kumilki simu akiwa Shule sio swala la mtoto na familia yake na kisha kuamia kwa mwalimu wake kumzuia asiingie shule na simu hiyo.Kimfumo swala ilo ilipaswa kuwa ni swala la maalufuku kwa mtoto yoyote ndani ya jamhuri ya muungano wa Tanzania anayesoma kuanzia Primary school mpaka Secondary school kumiliki simu akiwa Shule. Onyo kali na adhabu kubwa itatolewa kwa muhusika wa tendo ilo, yote haya yangetendwa kwa kutumia ama sheria kubwa au sheria ndogo ndogo.Lengo kuu hapa ni Taifa kushape kizazi kwa faida ya wote kwenye aina fulani ya umri na sio swala la holelaholela tu, yani mzobe mzobe tu twende tutajua mbele kwa mbele.
Je waelevu wanaratibu future the generation kwa kuzuia kabla ya kutokea au wanaacha yaje yatokee ndio waratibu matokeo ya yasiyo ratibiwa.Nini matokeo ya kuratibu kitu ambacho hakikuratibiwa? Hivi leo aliyekuwa mwizi, jambazi, muongo, mlaghai, mnafiki, wapambe, wanaingia kwenye vyama na kupewa dhamana kesho utegemee matokeo gani, atakae tofautina nao katika mikakati au mipangilio yao ananafasi gani katika taasisi, idala au kampuni husika.
Najifunza nitaendelea kujifunza ila uwa naumia sana kwanini mfumo [system] inalea kibovu kikue na kuishi katika kizuri na daima kwa mfumo wetu kibovu kuonekana kukumbatiwa na mfumo na kuhakikisha kizuri kinakufa na kupotea kabisa.Kisha kibovu kikisha leta madhara ndio mfumo unaanza kuratibu na kutafuta kizuri kilipo na hatimae kukuta hata kizuri nacho baada ya kugundua kuwa uzuri wake hauthaminika unavunjika moyo na kukata tamaa na kuamua ama kugeuka na kufanana na kibovu au kupoteza maana ya uzuri wake.
Labda kwa hili la kunzisha vyama ushauri wangu kwako ebu twende navyo hivi hivi CDM vs CCM, kitaeleweka tu If you can defeat them join them!!Jibu lipo ila muda kwa kuwa mfumo unaenda unakumbana na changamoto!! Uliamini dogo angekosa busara na kutapika hayo aliyotapika kiasi kuwa mifumo ya pande zote mbili imepata majeraha si CDM wala si CCM wote Manche ga Nyanza.