PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,725
Kwa waliotazama habari jana TBC1, waziri wetu wa mambo ya nje, Berbard Membe anatuhumiwa na vyama pinzani vya nchi hiyo kwamba alifanya ziara nchini Komoro ambayo ilionyesha wazi upendeleo kwa Chama tawala cha nchi hiyo kinachoongozwa na Rais Osambi.
Inadaiwa hakutoa nafasi kwa Kambi ya upinzani ya huko kukutana naye, kitendo ambacho kimewaudhi sana wananchi hao, hasa ukizingatia nchi hiyo iko katika mgogoro wa kiuongozi, ambapo inaonyesha Osambi anataka kung'ang'ania kuendelea kutawala kwa kutumia ushawishi wa Bunge.
Ikumbukwe pia Tanzania ilishalaumiwa na kambi ya upinzani ya Malawi enzi za Ben MkaaHapa juu ya shida ya namna hii!
Sasa swali ninalijiuliza mimi, Tanzania sisi tuna nini na Komoro ya watu jamani?..Mbona tunaonyesha kuimezea mate sana nchi hii na kuitiatia vidole?...Ziara za wakuu wa nchi hizi mbili kutembeleana zimekuwa za mara kwa mara sana..!
Embu wana jamvi tuitazame hii maneno kwa undani!
Inadaiwa hakutoa nafasi kwa Kambi ya upinzani ya huko kukutana naye, kitendo ambacho kimewaudhi sana wananchi hao, hasa ukizingatia nchi hiyo iko katika mgogoro wa kiuongozi, ambapo inaonyesha Osambi anataka kung'ang'ania kuendelea kutawala kwa kutumia ushawishi wa Bunge.
Ikumbukwe pia Tanzania ilishalaumiwa na kambi ya upinzani ya Malawi enzi za Ben MkaaHapa juu ya shida ya namna hii!
Sasa swali ninalijiuliza mimi, Tanzania sisi tuna nini na Komoro ya watu jamani?..Mbona tunaonyesha kuimezea mate sana nchi hii na kuitiatia vidole?...Ziara za wakuu wa nchi hizi mbili kutembeleana zimekuwa za mara kwa mara sana..!
Embu wana jamvi tuitazame hii maneno kwa undani!