Tumeripoti polisi na Mhe. Sugu

Tumeripoti polisi na Mhe. Sugu

Akiahirisha bunge jioni hii Ndugai ameonesha kuwa kwa kitendo alichofanya Sugu hakina kinga na kqa sababu hiyo sheria itachukua mkondo wake. Alishangiliwa sana na wapambe wake. Mary Nagu amemsifia sana kwakuendesha bunge kishujaa na kwa ufanisi mkubwa.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
hiyo sheria haitafanya kazi, labda sio tundu lissu kama wakili...
 
Naare Isimbaa??

Hivyo hivyo nseroo tutashinda
 
Tumekupata kamanda...ila tu muwe waangalifu na vitu vyenye ncha kali hapo kituoni
 
Baada ya Mwenyekiti na KUB Mbowe kusikia kuwa Sugu anatafutwa na polisi, jioni hii tumeamua kuripoti makao makuu ya polisi mkoa wa Dodoma ili kuondoa sintofahamu iliyokuwepo.

Tumeripoti na Mhe. Mbowe, Lissu, Sugu, Mnyika na Mimi mwenyewe.

Kwa hatua ya sasa Sugu anaandika maelezo kwa RCO akisaidiwa na wakili Tundu Lissu.

Tutawajulisha kitakachojiri

Huo ndo uzuri wa kujua sheria. Angelikuwa mtu mwingine angaenza kukukimbia. Tuko pamoja.
 
Tunatambua Juhudi zenu. Mnayo dhamira ya kweli, mnayo dhamira ya Dhati na Mna Uchungu sana na Ukombozi wa Taifa hili kutoka mikononi na mifukoni mwa Wasio waadilifu. Mungu anajua. Hata kama Mtapigwa, hata kama mtadhalilishwa kwa kiasi gani sisi hatutawasaliti. Tunajisikia vibaya sana tunapoona mnadhalilishwa, mnanyimwa haki Bungeni na Kukaripiwa kama watoto wadogo. Lakini tunatambua kwamba haya yote yatapita. Ipo siku na si mbali, hawa wanaowatendea haya watapiga magoti mbele zenu. Msikate tamaa kwa haya yanayotokea, maana kila jambo jema na mafanikio makubwa hupatikana kwa jasho jingi sana au hata wakati mwingine kwa maumivu makali sana. Sisi tuko pamoja nanyi katika kila hatua. Kumbukeni YESU alidhalilishwa, akapigwa mijaledi, akatemewa mate, wakamdhihaki, lakini mwishowe akawa mshindi na sasa kila goti hupigwa mbele zake. Hata Mtume S.A.W naye bila shaka alipitia mazingira magumu ili watu waweze kumweelewa, wapo walio mpinga lakini leo wanaheshimu harakati zake. Mhe. Joseph Mbilinyi alidhalilishwa sana na polisi wa Bungeni, Mhe. Mbowe alidhalilishwa sana kwa kauli za Ndugai. Kwa ujumla wabunge wote wa upinzani walidhalilishwa sana. Wabunge wa CCM walionekana kufurahi sana. Nataka niwambie, Wabunge wa CCM achaneni na akili za kufikiri na kuishia ndani ya ukumbi wa Bunge. Hao mnaowadharau leo kesho wanaweza kuwa viongozi wenu. Tatizo lenu hamjitambui. Hawa mnaowaona wabaya wanapigania haki yenu, watoto wenu na wajukuu wenu. Jitambueni, acheni ushaabiki wa kijinga. Fikirieni mstakabali wa Taifa hili kwa ajili ya watoto wenu. Mungu ibariki Tanzania. Mungu wasaidie Wabunge wa CCM wawe na ufahamu, kwani wamepoteza fahamu, busara na hekima kwa sababu ya kulewa na madaraka.
 
Wajinga wanadanganyana. Ni uhuni mkubwa kuvunja vifaa vya bunge na ni uhuni mkubwa kwa mbunge kupiga askari
Lakini askari kumpiga mbunge bungeni ni haki akili zingine hata ndungai afadhari!
 
Tatizo watanzania tumekosa kujitambua, na siku zote penye haki ya kufanya changes katika nchi yatubidi tuungane pamoja, kazi waifanyayo vyama vya siasa kuibadili nchi ni kubwa mno, hebu tuwape sapoti na si kuwatukana matusi tu, huu ni muda wa kuondoa mfumo wa chama kimoja!

Ninakuunga mkono. Kwa kuongezea ni kwamba HAKI HAIOMBWI bali HUPIGANIWA. Ukombozi wa pili wa Tanganyika na Zanzibar utaanza na mabadiliko ya katiba yanayofanyika kwa dhati, na sio kwa chati. Wakati wenye welewa mdogo wanaliona tukio la sintofahamu ya juzi bungeni kama tukio la aibu, wenye welewa wa kutosha tunaliona kama HATUA MUHIMU sana katika safari ya kupigania HAKI. HATUA ya kwanza ilikuwa ni Novemba 2010 Wabunge wapambanaji chini uongozi wa Kamanda Mbowe waliposusia hotuba ya Mhe JK. Wenye welewa mdogo (tulivyolelewa kisiasa) walibaki midomo wazi bila kuamini walichokuwa wakikiona lakini matokeo yake ilikuwa ni Mhe JK kuridhia (japo kwa chati) haja ya kuanza mchakato wa Katiba mpya, na wote tukatoka ndani ya viboksi na kuanza kushangilia uamuzi huo. Kwa vile ndugu magambaz hili halikutoka moyoni mwao wameamua kuchakachua mchakato. Wapambanaji chini ya uongozi wa kamanda yule yule, Mhe Mbowe, waliligundua na wameendelea kuligundua na hivyo hiki kilichotokea juzi ni ujumbe tosha (sio aibu) kwa umma wa Watanzania kama ilivyokuwa siku ile waliposusia hotuba ya Mheshimiwa sana. Tuwaunge mkono na hatimaye haki itapatikana kama si leo basi ni 2015.
 
Sugu pamoja,
haki haitafutwi kwa mzaha wala utani.
Pambana sisi wananchi tunayaona maovu yote yanayofanywa na kiti dhaifu cha speaker ndani ya bunge.
Hakuna kurudi nyuma.
Swali la kujiuliza, kama wewe mti mbichi unawaka moto iweje sisi miti mikavu.

Kataeni manyanyaso kwani hiyo ndo ponapona yetu kwa siku za usoni.
 
>Mtu mzima na midevu yako unashabikia ushenzi wa ccm...
 
Baada ya Mwenyekiti na KUB Mbowe kusikia kuwa Sugu anatafutwa na polisi, jioni hii tumeamua kuripoti makao makuu ya polisi mkoa wa Dodoma ili kuondoa sintofahamu iliyokuwepo.

Tumeripoti na Mhe. Mbowe, Lissu, Sugu, Mnyika na Mimi mwenyewe.

Kwa hatua ya sasa Sugu anaandika maelezo kwa RCO akisaidiwa na wakili Tundu Lissu.

Tutawajulisha kitakachojiri
Kuna watu wajinga wajingz wakisema Sugu analindwa na Uhuru na Haki ya Bunge, wajitokeze kumsaidia huyu baunsa akiwa mikononi mwa Polisi
 
Haki kucheleweshwa ni kitu cha kawaida ole wao wanaokalia haki za wengine siku wakipokonywa itakua kulia na kusaga meno
 
Back
Top Bottom