Tumemchoka sasa Mtangazaji wa TBC1 na TBC Taifa Enock Bwigane abadilike upesi na huu ushamba!

Nilidhani ni Kitendo tu cha siku moja labda alikikosea lakini sasa naona kama ni Kitendo ambacho amekibariki na anakifanya sasa bila hata aibu au kujishtukia kuwa anachokifanya kiukweli ni kinyume kabisa na maadili ya Utangazaji na nashangaa kwanini Uongozi wake kupitia kwa Mwalimu wangu Kipenzi Dkt. Ayub Ryoba ambaye ndiyo Mkurugenzi Mkuu wa hivyo Vyombo bado hawajamwonya.

Ni kwamba kila anapokuwa anatangaza mipira hasa hii ya Ligi Kuu ya Tanzania bara VPL huyu Mtangazaji Enock Bwigane amekuwa na tabia ya kuudhi kama si ya kukera kabisa ya kupenda kutangaza huku akiweka maneno ya lugha yake ya Kinyakyusa kila mara kitu ambacho kiukweli nisimfiche kinatukera wengi na pengine ndiyo maana kwa udhaifu wake huu Watu wengi sasa hawasikilizi tena matangazo yao ya moja kwa moja ya mpira na badala yake sasa tumekimbilia SIKUKA fm na Radio One ambapo Watangazaji wake wanajua maadili yao.

Kila mara tu utamsikia sijui ' ndaga fijo ' akitangaza tu kidogo sijui ' kukoya ' hatujakaa sawa utasikia tena anaongea kilugha chake cha Kinyakyusa na akisema tena sijui ' ndaga fijo ' yaani ni full ' kutuboa '.

Kama vipi TBC1 na TBC Taifa hebu anzisheni haraka sana idhaa ya Lugha ya ' Kinyakyusa ' halafu mpeni Mtangazaji Enock Bwigane awe ' anatiririka ' nayo mwenyewe kila siku na Wanyakyusa wenzake ila huku TBC1 na TBC Taifa mtuachie tu akina ' Poti ' Chacha Maginga na Bingwa wa Utangazaji wa mipira kwa sasa Tanzania nzima Kamarada Jesse John.

Atakayepata ujumbe huu ' murua ' kabisa na akijua yupo karibu na huyo Mtangazaji Enock Bwigane basi amfikishie na tunamtaka abadilike haraka kama siyo upesi sana na asitake kupandikiza mbegu ya ukabila hasa katika Chombo kikubwa cha Habari ambacho ni cha Kitaifa kama hicho anachokifanyia.

Kama kawaida yangu GENTAMYCINE huwa silei ' upuuzi ' na kazi yangu siku zote ni ' kunyoosha ' tu ili Watu wakae sawa katika mstari na hatimaye twende sawa. Tanzania official language ni Kiswahili na siyo sijui Kinyakyusa au Kizanaki au Kimakuwa au Kinyarwanda.

Nawasilisha.
sema umemchoka so tumemchoka we na nani sasa,mi namkubali sana na sema bwigane piga kazi usiskilize Maneno ya mitandao...
 
Binadamu mwenzio unawaita Mimtu! Hii chuki unaitoa wapi?
Mie hapa nilipo matangazo ya mpira nasikiliza TBC .Vituo vingine havioni umuhimu na coverage yao sio kubwa.
kweli mkuu kwenye matangazo ya mpira tbc taifa haikwepeki
 
Enock Bwigane piga kazi.!!! Jana umenitangazia tulipompiga mwarabu.mikia fc wamepagawa.

hakuna redio inayotangaza mpira vzr zaidi ya TBC.mnyobge mnyongeni haki yake mpeni.
 
Mleta Uzi analo la moyoni. Bwigane hunogesha sana matangazo ya mpira. Huchanganganya lugha tofauti. Kireno, (Obrigado, )kiarabu (wahed) Kinyakyusa (ndaga) kihaya (maweeee) kisukuma (ng'wadila) kikurya (mura mangana) kiingereza.
 
Nilidhani ni Kitendo tu cha siku moja labda alikikosea lakini sasa naona kama ni Kitendo ambacho amekibariki na anakifanya sasa bila hata aibu au kujishtukia kuwa anachokifanya kiukweli ni kinyume kabisa na maadili ya Utangazaji na nashangaa kwanini Uongozi wake kupitia kwa Mwalimu wangu Kipenzi Dkt. Ayub Ryoba ambaye ndiyo Mkurugenzi Mkuu wa hivyo Vyombo bado hawajamwonya.

Ni kwamba kila anapokuwa anatangaza mipira hasa hii ya Ligi Kuu ya Tanzania bara VPL huyu Mtangazaji Enock Bwigane amekuwa na tabia ya kuudhi kama si ya kukera kabisa ya kupenda kutangaza huku akiweka maneno ya lugha yake ya Kinyakyusa kila mara kitu ambacho kiukweli nisimfiche kinatukera wengi na pengine ndiyo maana kwa udhaifu wake huu Watu wengi sasa hawasikilizi tena matangazo yao ya moja kwa moja ya mpira na badala yake sasa tumekimbilia SIKUKA fm na Radio One ambapo Watangazaji wake wanajua maadili yao.

Kila mara tu utamsikia sijui ' ndaga fijo ' akitangaza tu kidogo sijui ' kukoya ' hatujakaa sawa utasikia tena anaongea kilugha chake cha Kinyakyusa na akisema tena sijui ' ndaga fijo ' yaani ni full ' kutuboa '.

Kama vipi TBC1 na TBC Taifa hebu anzisheni haraka sana idhaa ya Lugha ya ' Kinyakyusa ' halafu mpeni Mtangazaji Enock Bwigane awe ' anatiririka ' nayo mwenyewe kila siku na Wanyakyusa wenzake ila huku TBC1 na TBC Taifa mtuachie tu akina ' Poti ' Chacha Maginga na Bingwa wa Utangazaji wa mipira kwa sasa Tanzania nzima Kamarada Jesse John.

Atakayepata ujumbe huu ' murua ' kabisa na akijua yupo karibu na huyo Mtangazaji Enock Bwigane basi amfikishie na tunamtaka abadilike haraka kama siyo upesi sana na asitake kupandikiza mbegu ya ukabila hasa katika Chombo kikubwa cha Habari ambacho ni cha Kitaifa kama hicho anachokifanyia.

Kama kawaida yangu GENTAMYCINE huwa silei ' upuuzi ' na kazi yangu siku zote ni ' kunyoosha ' tu ili Watu wakae sawa katika mstari na hatimaye twende sawa. Tanzania official language ni Kiswahili na siyo sijui Kinyakyusa au Kizanaki au Kimakuwa au Kinyarwanda.

Nawasilisha.
Pole ndugu yangu... Hakika umeumia sana..

Karaha kama hizo na nyinginezo nami nilishakutana nazo..

Ila kwangu nimezipatia ufumbuzi wa kudumu kwa kutoangalia TBC TV wala TBC RADIOS...

Sio rahisi kubadilika kwa vyombo hivyo... KAMA HUTAKI KUUMIZA ROHO YAKO, KAA NAVYO MBALI..
 
Kamarada maana yake nini??

Inamaanisha ' mwenza ' katika Kazi zenu zinazofanana au za Tasnia moja na mara nyingine hutumika kama Marafiki hasa mnaoshibana kwa ukaribu wenu. Na ni Kireno hicho ambacho kimetoka katika neno la Kiingereza la ' Comrade '.
 
Back
Top Bottom