Tumemchoka sasa Mtangazaji wa TBC1 na TBC Taifa Enock Bwigane abadilike upesi na huu ushamba!

Mleta hoja una hoja nyingine zaidi ya hiyo?.Kama alivyosema mdau mmoja mbona mwenzake Mwalimu Kashasha anachanganya kiingereza kwenye maelezo na hujamsema?Enock ni mmoja wa Watangazaji bora wa mpira wa miguu redioni (kwangu ni namba 1).Mara nyingi huyatumia kama vionjo kwenye mechi zinazohusu timu za Mbeya City na Prison na hana nia yoyote ya Ukabila.Mtangazaji Charles Hilary wakati akiwa RTD alitumia vionjo hivi kwenye mechi za Tukuyu Stars au Mecco.Unajua hapa nchini kuna lugha za makabila fulani zinavutia masikioni mwa wasikilizaji ndiyo maana hutumika kama vionjo vya matangazo ya biashara redioni mfano:Aise Meku....,nitakuarrest Mura,namgambila inafu, nshomile bwana mpaka fomu six, ndaga fijo....nk.
 
Afadhali angetagaza kisukuma lugha ambayo inajulikana na wengi japo mipango inafanyika mipango ya kuiboresha ili mda si mrefu ikawa lugha ya taifa!
 
Ni Mtangazaji Bora wa Mpira aliyesalia East Africa..
Mashabiki ya Simba baada kuona mnazidi puyanga na timu lenu mwahamishia hasira kwa watangazaji..!!

Nyivu za kike..
Mkuu nyivu ndio wingi wa wivu? Hahaaaa
 
Inaonekana mtoa mada unapenda sana ukabila, ndo maana unachukizwa na matumizi ya lugha ya Kinyakyusa lakini hukemei matumizi ya Kiingereza kutoka kwa Mwalimu Gashasha.Acha upotoshaji wa kimantiki.
 
Mma umwana ujhu nndeke aghoneghe ukutuhobhola fiijho muunda twe bha kukaajha. Kyala aje nungwe Bhwighane kukaajha taasi.
 
Ni sehemu ya burudani mkuu!
Umesahau kuna mwingine hotuba za kitaifa kabisa lazima aweke kisukuma!
"Hiiiiiii bhangosha" na rais wa bank ya dunia yupo anasikiliza siku ile pale ubungo mataa!.Sembuse huyo tena kwenye michezo
Aisee
 
Nilidhani ni Kitendo tu cha siku moja labda alikikosea lakini sasa naona kama ni Kitendo ambacho amekibariki na anakifanya sasa bila hata aibu au kujishtukia kuwa anachokifanya kiukweli ni kinyume kabisa na maadili ya Utangazaji na nashangaa kwanini Uongozi wake kupitia kwa Mwalimu wangu Kipenzi Dkt. Ayub Ryoba ambaye ndiyo Mkurugenzi Mkuu wa hivyo Vyombo bado hawajamwonya.

Ni kwamba kila anapokuwa anatangaza mipira hasa hii ya Ligi Kuu ya Tanzania bara VPL huyu Mtangazaji Enock Bwigane amekuwa na tabia ya kuudhi kama si ya kukera kabisa ya kupenda kutangaza huku akiweka maneno ya lugha yake ya Kinyakyusa kila mara kitu ambacho kiukweli nisimfiche kinatukera wengi na pengine ndiyo maana kwa udhaifu wake huu Watu wengi sasa hawasikilizi tena matangazo yao ya moja kwa moja ya mpira na badala yake sasa tumekimbilia SIKUKA fm na Radio One ambapo Watangazaji wake wanajua maadili yao.

Kila mara tu utamsikia sijui ' ndaga fijo ' akitangaza tu kidogo sijui ' kukoya ' hatujakaa sawa utasikia tena anaongea kilugha chake cha Kinyakyusa na akisema tena sijui ' ndaga fijo ' yaani ni full ' kutuboa '.

Kama vipi TBC1 na TBC Taifa hebu anzisheni haraka sana idhaa ya Lugha ya ' Kinyakyusa ' halafu mpeni Mtangazaji Enock Bwigane awe ' anatiririka ' nayo mwenyewe kila siku na Wanyakyusa wenzake ila huku TBC1 na TBC Taifa mtuachie tu akina ' Poti ' Chacha Maginga na Bingwa wa Utangazaji wa mipira kwa sasa Tanzania nzima Kamarada Jesse John.

Atakayepata ujumbe huu ' murua ' kabisa na akijua yupo karibu na huyo Mtangazaji Enock Bwigane basi amfikishie na tunamtaka abadilike haraka kama siyo upesi sana na asitake kupandikiza mbegu ya ukabila hasa katika Chombo kikubwa cha Habari ambacho ni cha Kitaifa kama hicho anachokifanyia.

Kama kawaida yangu GENTAMYCINE huwa silei ' upuuzi ' na kazi yangu siku zote ni ' kunyoosha ' tu ili Watu wakae sawa katika mstari na hatimaye twende sawa. Tanzania official language ni Kiswahili na siyo sijui Kinyakyusa au Kizanaki au Kimakuwa au Kinyarwanda.

Nawasilisha.
Sema umemchoka wewe sio kwamba tumemchoka wote,kwanza sisi wengine hata hatumjui maana Mara ya mwisho kisikiliza TBC Ni miaka kama mitano nyuma,...sa nitamjulia wapi?,....
 
Back
Top Bottom