JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Prof. Charles Kihampa, akizungumza na Waandishi wa Habari, Dar es Salaam, leo Oktoba 13, 2023 kuhusu kufunguliwa kwa dirisha la Awamu ya Nne ya dirisha la Udahili kwa programu ambazo bado zina nafasi kwa mwaka wa masomo 2023/2024.
Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imefungua awamu ya nne ya udahili kwa wanafunzi wa shahada ya kwanza na wanafunzi wametakiwa kutumia fursa hiyo vyema kwani hiyo ni nafasi ya mwisho kabisa waliyoitoa.
Hayo yamebainishwa na Katibu Mtendaji wa TCU, Charles Kihampa wakati akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam.