Tume ya mabadiliko ya katiba

Tume ya mabadiliko ya katiba

Mkuu wangu lazima utazame na kupima vitu kwanza kabla ya kukubaliana na mawazo ya mzee Mtei. Hili ni Taifa linalopiga vita Ukabila, Udini, na kuvunja Muungano wetu sasa wewe nambie ktk mawazo yake hayo yeye alitaka iwe vipi?..Mbona Chadema hatuna uuwiano sawa na hayo anayoyadai? Je, ukweli huo unaukubali na mnafanya nini kuuondoa maana nakuona siku zote unampiga vita Zitto na watu wanasema kwa sababu yeye ni Muislaam, Je nao wanasema kweli kama unavyouona hapa?
Mkuu Bob,
Nakubaliana na wewe kuwa tunatakiwa kupiga vita dalili zote za udini na ukabila ingawa naweza kutofautiana nawe juu ya kulinda muungano kwani muungano kwa mfumo tulionao mimi natamani uvunjike hata leo.

Kwa upande mwingine, ninasikitika sana kwamba kauli tunayolalamikia imetolewa na mzee ninayemheshimu, mzee Mtei. Kwanye andiko lake, mzee Mtei kaandika, rightly, kwamba madhehebu ya dini yana inflluence isiyoweza kupuuzwa kwenye jamii . Kwa mtazamo wangu, kama maoni yake yangelenga ile tume kupata uwakilishi toka BAKWATA, CCT, PCT nk sioni kama ingeleta mkanganyiko huu ulioletwa kwa kuangalia tu idadi ya wajumbe waislam na madhehebu mengine.

Tumepiga sana kelele baada ya Mkapa kutoa kauli zisizostahili kwenye kampeni za ubunge huko Arumeru. Kwangu mimi, heshima ya mzee Mtei kwenye jamii si ya chini sana kuliko Mkapa, mzee Mwinyi nk. Mimi naweza kuandika kile ninachojisikia kuandika, lakini hawa ni watu wanaopaswa kupima kauli zao kabla ya kuzitoa. Katika hili mzee Mtei kachemsha big time.
 
Naona una lengo lako nafikiri endelea kujadili nitakusoma, good bye.
Sina lengo lolote zaidi ya kukuelewa nini msimamo wako kifikra maana alichosema Mtei hakina tofauti na madai ya kina Ritz...Unajua mkuu wangu nimeambiwa siku nyingi sana kwamba watu wa kaskazini wana Ukabila na Udini kwa asili..Wachagga hawapendani ndani ya makabila yao wenyewe wanabaguana lakini ni wamoja wasiopenda makabila mengine na ndio maana Nyerere alimtema Chief Marealle tulipokuwa tunagombea Uhuru, yeye alitaka kujua nafasi ya Wachagga na uhuru wa Wachagga na sii Tanganyika.. Hii inatisha sana kuendeleza fikra zile wakati kama huu. Tunataka kuijenga Tanzania moja na katiba haiwezi kuendekeza fikra za Ukabila Udini na rangi za wahusika.. Nisome vizuri mkuu wangu nisome ufahamu malengo ya katiba mpya...
 
Mtei, ebu tujibu na hili kwa nini hakuna uwiano kwenye wabunge wa viti maalam wa Chadema...

Kuna wabunge 25 Wakiristu 19 na Waislama 6.

Mlitumia vigezo gani kuwapata?
 
Sina lengo lolote zaidi ya kukuelewa nini msimamo wako kifikra maana alichosema Mtei hakina tofauti na madai ya kina Ritz...Unajua mkuu wangu nimeambiwa siku nyingi sana kwamba watu wa kaskazini wana Ukabila na Udini kwa asili..Wachagga hawapendani ndani ya makabila yao wenyewe wanabaguana lakini ni wamoja wasiopenda makabila mengine na ndio maana Nyerere alimtema Chief Marealle tulipokuwa tunagombea Uhuru, yeye alitaka kujua nafasi ya Wachagga na uhuru wa Wachagga na sii Tanganyika.. Hii inatisha sana kuendeleza fikra zile wakati kama huu.
Is this Necessary mkuu? kwamba Wahaya wote wanauza miili yao!!.....wazaramo na mafiga matatu!!.......All born Muslim is terrorist?
Nadhani tusiende huko hapa hoja ni kumkemea Mzee Mtei na siyo otherwise, Mtei kosa alilolifanya ndilo wewe unarudia kulifanya in the same thread.
 
Nadhani badala ya kupoteza energy zako hapa ni bora ungempigia simu athibitishe kwamba ni yeye ndiyo ameandika haya au ID yake imekuwa Hacked?
Mkuu Matola kama kila anayeleta thread utampigia simu kuhakikisha kama ni yeye basi itabidi utafute secretary wa kupokea simu. Kinachotakiwa humu ni kujadili whether ni cha ukweli au uongo, kizuri au kibaya, kinasaidia au hakisaidii, mwisho unachuja mwenyewe chuya na mchele. Hata hii hoja ya Mtei si ya kuiacha ndio maana watu wanaichambua, mwisho kila mtu atapata atakachojifunza.
 
Mtei, ebu tujibu na hili kwa nini hakuna uwiano kwenye wabunge wa viti maalam wa Chadema...

Kuna wabunge 25 Wakiristu 19 na Waislama 6.

Mlitumia vigezo gani kuwapata?
Mtumie Private Msg Kitila Mkumbo, hapa tunakemea jambo lolote la kutugawa kwahiyo na wewe usiturudishe nyuma, kama hii ndiyo level ya ufahamu wako basi nenda kwenye vijiwe vya kahawa.
Nilidhani kama ungekuwa muelewa ungejifunza kitu kwamba watu wengi wanaoisupport Chadema siyo misukule wanakemea jambo lolote litakalofanywa na kiongozi wao bila kujali cheo chake siyo kama misukule ya CCM ambayo haijui hata kuhoji.
 
Mkuu Bob,
Nakubaliana na wewe kuwa tunatakiwa kupiga vita dalili zote za udini na ukabila ingawa naweza kutofautiana nawe juu ya kulinda muungano kwani muungano kwa mfumo tulionao mimi natamani uvunjike hata leo.

Kwa upande mwingine, ninasikitika sana kwamba kauli tunayolalamikia imetolewa na mzee ninayemheshimu, mzee Mtei. Kwanye andiko lake, mzee Mtei kaandika, rightly, kwamba madhehebu ya dini yana inflluence isiyoweza kupuuzwa kwenye jamii . Kwa mtazamo wangu, kama maoni yake yangelenga ile tume kupata uwakilishi toka BAKWATA, CCT, PCT nk sioni kama ingeleta mkanganyiko huu ulioletwa kwa kuangalia tu idadi ya wajumbe waislam na madhehebu mengine.

Tumepiga sana kelele baada ya Mkapa kutoa kauli zisizostahili kwenye kampeni za ubunge huko Arumeru. Kwangu mimi, heshima ya mzee Mtei kwenye jamii si ya chini sana kuliko Mkapa, mzee Mwinyi nk. Mimi naweza kuandika kile ninachojisikia kuandika, lakini hawa ni watu wanaopaswa kupima kauli zao kabla ya kuzitoa. Katika hili mzee Mtei kachemsha big time.
Mkuu hata hapo bado sikubaliani naye kwa sababu influence ya dini ktk jamii ni ya mtu mmoja mmoja. Naweza kuwa Musilaam/Mkristu lakini sifuati dini na kama watasema Pombe iharamishwe wakati mimi sipendi watakuwa hawaja niwakilisha mimi bali matakwa ya dini zao..Na mawazo haya yanapatikana ktk kukusanywa na sio muundo wa tume. Bakwata sijui CCT, PCT hawana nafasi ktk tume hii maana ndio kuuendekeza Udini.. Fikiria likija swala la kuvunja muafaka wa MoU huku kuna Askofu Kilaini na Sheikh Ponda kweli kikao kitakalika?..Tume inatakiwa kukusanya mawazo tu ya wananchi halafu yanapelekwa kwa kamati ya katiba ya Bunge ambayo ndiyo itafanya kupitia mapendekezo hayo kabla ya kuyawakilisha bungeni. Kuna sehemu nyingi sana zinapitiwa kabla ya katiba haijafikia maamuzi ya mwisho na kukubaliwa na wananchi, hii tume ni mwanzo tu.

Nitakukumbusha kitu kimoja. Mkoloni aliweza kututenga kwa kuwashirikisha viongozi wa dini na makabila (machief) wakatutawala tukichukiana..Na Nyerere aliweka kuvunja Ukabila na Udini kwa kutowashirikisha viongozi wa dini na Machief ktk Utawala wake na ndipo tukaweza kuungana na kuwa Taifa moja lisilo na ukabila wala Udini. Mchagga utamkuta mkuu wa wilaya Ukerewe na Mzanzibar waziri bara. Muhimu ni uwezo wa mhusika ktk kuleta mabadiliko nchini na kwa maslahi ya WATANZANIA...
 
Is this Necessary mkuu? kwamba Wahaya wote wanauza miili yao!!.....wazaramo na mafiga matatu!!.......All born Muslim is terrorist?
Nadhani tusiende huko hapa hoja ni kumkemea Mzee Mtei na siyo otherwise, Mtei kosa alilolifanya ndilo wewe unarudia kulifanya in the same thread.
Haikuwa muhimu lakini inaudhi sana hawa watu maana wanapenda kuzungumza vitu ati ni ukweli wakati sisi tukitoa mifano inayouma kwao wanakuja juu. Nimefanya makusudi kabisa nipate kumsikia Feedback atajisikia aje japokuwa ulikuwa ukweli..Nia na lengo ya Utaifa wetu ni kuvunja ukabila na Udini sasa tunapo waendekeza watu kama hawa wanapata mianya ya kutuvuruga.
 
Huyu ndio Mtei muasisi wa Chadema? Basi kazi ipo kumbe ni mdini?

kaka kama muasisi wa chadema ana mtizamo huo juu ya Udini je unafikiri chadema ina msimamo gani? kila siku wazalendo wanasema cdm siyo chama cha kuwaunganisha watanzania. Mzee kisha filisika kimawazo nakushauri ujikalie kimya ili uzeeke kwa heshima. Una chuki kubwa sana na uislam na waislam ndio maana umepata msimamo huo. Je kama nasisi waislam wa bara ambao sisi ndio wengi tukisema kwenye hiyo list ya bara waislam ndio tuwe wengi ungesemaje?
 
Haikuwa muhimu lakini inaudhi sana hawa watu maana wanapenda kuzungumza vitu ati ni ukweli wakati sisi tukitoa mifano inayouma kwao wanakuja juu. Nimefanya makusudi kabisa nipate kumsikia Feedback atajisikia aje japokuwa ulikuwa ukweli..Nia na lengo ya Utaifa wetu ni kuvunja ukabila na Udini sasa tunapo waendekeza watu kama hawa wanapata mianya ya kutuvuruga.
Ni kweli inaudhi na ndiyo maana mimi sikubaliani na Hizi hoja za Mtei hata kama kulikuwa na mantiki ndani yake basi hakupaswa kuzitoa yeye, maana kama amejamba shuzi ametuachia sisi tupulize Air freshener yeye anakunywa mbege shambani kwake na wajukuu zake!!
Nadhani Mbowe anapaswa na ndiye uwezo wa kumueleza huyu Mzee kwamba hapaswi kutoa kauli hizi hata kama anazo hoja za Msingi ni heri azifoward kwa Mtikila ndiyo mtu ambaye huwa hashangazi kwa kauli tata.
 
Mtumie Private Msg Kitila Mkumbo, hapa tunakemea jambo lolote la kutugawa kwahiyo na wewe usiturudishe nyuma, kama hii ndiyo level ya ufahamu wako basi nenda kwenye vijiwe vya kahawa.
Nilidhani kama ungekuwa muelewa ungejifunza kitu kwamba watu wengi wanaoisupport Chadema siyo misukule wanakemea jambo lolote litakalofanywa na kiongozi wao bila kujali cheo chake siyo kama misukule ya CCM ambayo haijui hata kuhoji.

Kitila Mkumbo ndio nani? Kwanza sina utaratibu wa kuandika PM.

Naona unajipa kazi za mods eti nisiwarudishe nyuma nisiwarudishe nyuma wewe na nani?

JF ni huru kama unaona unarudishwa nyuma unaweza kwenda kwenye thread ingine.

Wewe upo hapa JF kupangia watu vitu vya kuandika kauzu kweli.
 
Ni kweli inaudhi na ndiyo maana mimi sikubaliani na Hizi hoja za Mtei hata kama kulikuwa na mantiki ndani yake basi hakupaswa kuzitoa yeye, maana kama amejamba shuzi ametuachia sisi tupulize Air freshener yeye anakunywa mbege shambani kwake na wajukuu zake!!
Nadhani Mbowe anapaswa na ndiye uwezo wa kumueleza huyu Mzee kwamba hapaswi kutoa kauli hizi hata kama anazo hoja za Msingi ni heri azifoward kwa Mtikila ndiyo mtu ambaye huwa hashangazi kwa kauli tata.

Afadhali ya mtikila kuliko wanafiki kama Mtei na nyie ambao mnajua kabisa chadema ajenda yake ni kulinda wakristo; halafu mnawadanganya wananci eti wakombozi WTF!

Misingi ya chadema ameasisi Mtei (je misingi imebadilika lini?)..sasa mnyika (rubber stamp mlamba viatu vyeo 7 mtu moja) atatueleza nini sisi wenye akili zetu phwe!
 
Ni kweli inaudhi na ndiyo maana mimi sikubaliani na Hizi hoja za Mtei hata kama kulikuwa na mantiki ndani yake basi hakupaswa kuzitoa yeye, maana kama amejamba shuzi ametuachia sisi tupulize Air freshener yeye anakunywa mbege shambani kwake na wajukuu zake!!
Nadhani Mbowe anapaswa na ndiye uwezo wa kumueleza huyu Mzee kwamba hapaswi kutoa kauli hizi hata kama anazo hoja za Msingi ni heri azifoward kwa Mtikila ndiyo mtu ambaye huwa hashangazi kwa kauli tata.
Nakubaliana na wewe sana tu labda pengine sisi tujiulize kama tume hii ni huru ama laa, uwezo wa kila mmoja wao kiutendaji. Maana wajumbe wa tume hii asilimia 90 ni wana CCM na katiba tunayoitaka sii ya kukilinda chama kimoja, siasa ya Ujamaa na kujitegemea au utawala wake tena, bali kulinda muungano ktk Utaifa wetu.

Pili, swala la wajumbe wa Zanzibar na bara pengine lingezungumziwa uwezo wa watu hawa 17 toka bara kuweza kuifanya kazi kwa ufanisi sawa na Zanzibar ikiwa wajumbe wa Zanzibar wana asimilia ndogo ya kukusanya mawazo yao tofauti na bara ambako wananchi ni wengi sana kupita kiasi. Hivyo kinachotazamwa ni kuwawezesha hawa wajumbe waifanye kazi yao kwa ufanisi maana namba za population hazifanani.. Hayo tu ndio hoja yangu kubwa kuhusiana na tume hii..
 
kaka kama muasisi wa chadema ana mtizamo huo juu ya Udini je unafikiri chadema ina msimamo gani? kila siku wazalendo wanasema cdm siyo chama cha kuwaunganisha watanzania. Mzee kisha filisika kimawazo nakushauri ujikalie kimya ili uzeeke kwa heshima. Una chuki kubwa sana na uislam na waislam ndio maana umepata msimamo huo. Je kama nasisi waislam wa bara ambao sisi ndio wengi tukisema kwenye hiyo list ya bara waislam ndio tuwe wengi ungesemaje?

Nyie waislam wajinga ambao hamuwezi kutumia vichwa na akili vizuri ndio mkiambiwa chadema haina udini; au taifa hili hakuna udini mnakubali; lakini wakristo walianza udini zamani sana tangu enzi st. nyerinyeri huku wakiwadanganya waislamu..

Choice is yours, either uwe kama kina mkandara (wabeba mabegi ya mapadre) au usimame mwenyewe katika ukweli; nchi hii kuna udini tena mkubwa sana..chadema inaongoz katika siasa na misingi ya kidini
 
Kitila Mkumbo ndio nani? Kwanza sina utaratibu wa kuandika PM.

Naona unajipa kazi za mods eti nisiwarudishe nyuma nisiwarudishe nyuma wewe na nani?

JF ni huru kama unaona unarudishwa nyuma unaweze kwenda kwenye thread ingine.

Wewe hupo JF kupangia watu vitu vya kuandika kauzu kweli.

Kama humjui Kitila Mkumbo ndiyo nani ni kwa nini uko interested kujuwa Wabunge wa viti maalum walipatikane CHADEMA?
Naona umekosa hoja sasa unaleta viroja upo hapa JF kudandia dandia vitu tu wakati upstairs empty!!.....kwa akili zako ulidhani watu wenye akili timamu kama sisi tupo hapa kupromote udini ambao thread hii ndio ilikuwa weakeast point yenu, mmeshindwa kabla hata hamjaaza.

Kama unapenda siasa jifunze CHADEMA watu wanasifu panapostahili kusifu na tunakosowa pale panapostahili kukosowa na ndio maana watu wote makini tunasema Mzee Mtei ameteleza. niambiye nyinyi CCM mna uwezo huo kama mmeshindwa hata kumkeme Lusinde kwa Matusi yake?
 
Licha ya kwamba J.K. kajitahidi kuwa na vigogo kweli kweli, na Katiba ya sasa imezingatiwa ktk kuandaa m'badala wake, muundo wa hii Tume umedhihirisha kwamba demokrasia ya kweli ni ndoto kwa Watanzania wa leo. Kama tunanuia kwa dhati kuwa na Demokrasis ya kweli, itabidi Watanzania wanaoamini kwamba hilo ni muhimu, waendelee na juhudi za kuandaa hata Mabadiliko kwa Katiba Mpya ijayo.

Kwa mfano ni jambo la kichekesho kwamba Tanzania Bara ambayo ina Watu takriban 42 milioni iwakilishe na wajumbe sawa na Tanzania Zanzibar ambayo ina watu wasiozidi 1.5 milioni. Mfano wa pili ni kwamba, licha ya kwamba Tanzania siyo nchi inayozingatia dini katika maamuzi yake ya kisiasa, ni lazima tukubali kuwa madhehebu ya dini yana influence katika mchakato na hatimaye maamuzi. Nikihesabu Waislamu katika hii Tume kwa kuzingatia majina naona zaidi ya theluthi mbili ni Wao. Wengine ni Wakristo au watu wasiokuwa na dini yoyote.

Hata kama ni lazima tujali Muungano wa Jamhuri yetu, hatuwezi kupuuza ukweli kuwa sasa kuna matatizo ya umilikaji wa raslimali maliasili (e.g. gas), na kuna wananchi wamediriki hata kwenda Umoja wa Mataifa kudai Zanzibar ijiondoe.

Haya ni mambo mazito na nimeona ni vema niyataje sasa, siyo tu yajadiliwe na Tume, bali ikiwa ni lazima, basi mjadala uendelee hata baada ya Tume kutoa taarifa na Bunge Maalum kupitisha Katiba Mpya.

.... I don't want to believe this!!!
 
Nyie waislam wajinga ambao hamuwezi kutumia vichwa na akili vizuri ndio mkiambiwa chadema haina udini; au taifa hili hakuna udini mnakubali; lakini wakristo walianza udini zamani sana tangu enzi st. nyerinyeri huku wakiwadanganya waislamu..

Choice is yours, either uwe kama kina mkandara (wabeba mabegi ya mapadre) au usimame mwenyewe katika ukweli; nchi hii kuna udini tena mkubwa sana..chadema inaongoz katika siasa na misingi ya kidini
Mkuu wangu naona sasa umenichoka!.. Nachozungumza mimi ni mtazamo wangu na kuwepo kwangu CDM ni kutokana na dhlma inayofanywa na chama CCM kwa Watanzania. Nimeeleza wazi wapi sikubaliani na CCM ktk maswala ya Dini, sasa bora miye niliyeko Chadema nabeba mabegi ya Mapadre yenye ujumbe wa kufuta Udini kuliko wewe unayetumikia CCM hali wakiumiza Waislaam, sawa na Nyapala linaloshika bakora au askari wa Kaburu dhidi ya watu wako mwenyewe.
 
... Udini kwenye Tume ya Katiba...??

... I am very disappointed la hili jambo!!!

... Bora CHADEMA kama CHAMA wamejitokeza mara moja na kukanusha ... !!!
 
Kama humjui Kitila Mkumbo ndiyo nani ni kwa nini uko interested kujuwa Wabunge wa viti maalum walipatikane CHADEMA?
Naona umekosa hoja sasa unaleta viroja upo hapa JF kudandia dandia vitu tu wakati upstairs empty!!.....kwa akili zako ulidhani watu wenye akili timamu kama sisi tupo hapa kupromote udini ambao thread hii ndio ilikuwa weakeast point yenu, mmeshindwa kabla hata hamjaaza.

Kama unapenda siasa jifunze CHADEMA watu wanasifu panapostahili kusifu na tunakosowa pale panapostahili kukosowa na ndio maana watu wote makini tunasema Mzee Mtei ameteleza. niambiye nyinyi CCM mna uwezo huo kama mmeshindwa hata kumkeme Lusinde kwa Matusi yake?

Jifunze kwanza kuandika unaandika kama dogo wa Kindergarten...
 
Back
Top Bottom