Tume ya mabadiliko ya katiba

Tume ya mabadiliko ya katiba

Nakubaliana na wewe sana tu labda pengine sisi tujiulize kama tume hii ni huru ama laa, uwezo wa kila mmoja wao kiutendaji. Maana wajumbe wa tume hii asilimia 90 ni wana CCM na katiba tunayoitaka sii ya kukilinda chama kimoja, siasa ya Ujamaa na kujitegemea au utawala wake tena, bali kulinda muungano ktk Utaifa wetu.

Pili, swala la wajumbe wa Zanzibar na bara pengine lingezungumziwa uwezo wa watu hawa 17 toka bara kuweza kuifanya kazi kwa ufanisi sawa na Zanzibar ikiwa wajumbe wa Zanzibar wana asimilia ndogo ya kukusanya mawazo yao tofauti na bara ambako wananchi ni wengi sana kupita kiasi. Hivyo kinachotazamwa ni kuwawezesha hawa wajumbe waifanye kazi yao kwa ufanisi maana namba za population hazifanani.. Hayo tu ndio hoja yangu kubwa kuhusiana na tume hii..

Mkuu kwenye hoja yako ya kwanza sina wasi wasi sana na idadi ya wana CCM maana baadhi yao na hasa Mwnyekiti Warioba ni majeruhi wa siasa za Makundi na hasa mtandao wa JK uliomuundia zengwe Salim asiwe Rais wetu nadhani nao wamepata rungu la kumalizia hasira zao siyo kwa kufanya upendeleo bali kwa kutenda haki, sina wasi wasi sana na hili.

Hoja yako ya pili nadhani Kamati ya Chadema inayofanya uchambuzi wake ndiyo itakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuliongelea hili nina uhakika wanalifahamu vyema na hata Tundu Lisu alishawahi kuliongea hili Bungeni akaonekana kama adui wa Wanzanzibar.
 
Mkuu wangu naona sasa umenichoka!.. Nachozungumza mimi ni mtazamo wangu na kuwepo kwangu CDM ni kutokana na dhlma inayofanywa na chama CCM kwa Watanzania. Nimeeleza wazi wapi sikubaliani na CCM ktk maswala ya Dini, sasa bora miye niliyeko Chadema nabeba mabegi ya Mapadre yenye ujumbe wa kufuta Udini kuliko wewe unayetumikia CCM hali wakiumiza Waislaam, sawa na Nyapala linaloshika bakora au askari wa Kaburu dhidi ya watu wako mwenyewe.

Mkuu mabegi ya mapdre yenye ujumbe wa kubeba udini; umemsikia MUASISI aliyeandaa misingi ya chama anasemaje? Allah ana namna nyingi za kuwaibisha wanafiki; wasio na masikio wala macho ndio watashindwa kuelewa??

Wewe chadema hiyo ndio misingi yake ukristo kwanza; uchaga na waislam wabeba mabegi kama nyerinyeri na kawawa..sasa kama umeamua; chadema ilivyo na chuki na waislamu hata kula nao inaweza kuwa makruhu
 
Mkuu Bob,
Nakubaliana na wewe kuwa tunatakiwa kupiga vita dalili zote za udini na ukabila ingawa naweza kutofautiana nawe juu ya kulinda muungano kwani muungano kwa mfumo tulionao mimi natamani uvunjike hata leo.

Kwa upande mwingine, ninasikitika sana kwamba kauli tunayolalamikia imetolewa na mzee ninayemheshimu, mzee Mtei. Kwanye andiko lake, mzee Mtei kaandika, rightly, kwamba madhehebu ya dini yana inflluence isiyoweza kupuuzwa kwenye jamii . Kwa mtazamo wangu, kama maoni yake yangelenga ile tume kupata uwakilishi toka BAKWATA, CCT, PCT nk sioni kama ingeleta mkanganyiko huu ulioletwa kwa kuangalia tu idadi ya wajumbe waislam na madhehebu mengine.

Tumepiga sana kelele baada ya Mkapa kutoa kauli zisizostahili kwenye kampeni za ubunge huko Arumeru. Kwangu mimi, heshima ya mzee Mtei kwenye jamii si ya chini sana kuliko Mkapa, mzee Mwinyi nk. Mimi naweza kuandika kile ninachojisikia kuandika, lakini hawa ni watu wanaopaswa kupima kauli zao kabla ya kuzitoa. Katika hili mzee Mtei kachemsha big time.

Mkuu nakuunga mkono kakika kuonyesha kutokubaliana na andiko la muasisi wenu, ila nakupinga kabisa kuweka uwakilishi wa viongozi wa dini na taasisi zao.
Hawa watu wafuatwe kwa ushauri tu pale panapohitajika lakini wasiwe engine wataharibu mchakato mzima.
Tumewashuhudia hasa katika uchaguzi wa 2010 wanaingilia sana siasa na wameharibu demokrasia ya kweli kwa kujiingiza katika siasa.
 
Licha ya kwamba J.K. kajitahidi kuwa na vigogo kweli kweli, na Katiba ya sasa imezingatiwa ktk kuandaa m'badala wake, muundo wa hii Tume umedhihirisha kwamba demokrasia ya kweli ni ndoto kwa Watanzania wa leo. Kama tunanuia kwa dhati kuwa na Demokrasis ya kweli, itabidi Watanzania wanaoamini kwamba hilo ni muhimu, waendelee na juhudi za kuandaa hata Mabadiliko kwa Katiba Mpya ijayo.

Kwa mfano ni jambo la kichekesho kwamba Tanzania Bara ambayo ina Watu takriban 42 milioni iwakilishe na wajumbe sawa na Tanzania Zanzibar ambayo ina watu wasiozidi 1.5 milioni. Mfano wa pili ni kwamba, licha ya kwamba Tanzania siyo nchi inayozingatia dini katika maamuzi yake ya kisiasa, ni lazima tukubali kuwa madhehebu ya dini yana influence katika mchakato na hatimaye maamuzi. Nikihesabu Waislamu katika hii Tume kwa kuzingatia majina naona zaidi ya theluthi mbili ni Wao. Wengine ni Wakristo au watu wasiokuwa na dini yoyote.

Hata kama ni lazima tujali Muungano wa Jamhuri yetu, hatuwezi kupuuza ukweli kuwa sasa kuna matatizo ya umilikaji wa raslimali maliasili (e.g. gas), na kuna wananchi wamediriki hata kwenda Umoja wa Mataifa kudai Zanzibar ijiondoe.

Haya ni mambo mazito na nimeona ni vema niyataje sasa, siyo tu yajadiliwe na Tume, bali ikiwa ni lazima, basi mjadala uendelee hata baada ya Tume kutoa taarifa na Bunge Maalum kupitisha Katiba Mpya.

Nafikiri wengi hatujakuelewa,kama inawezekana jitokeze tena utoe ufafanuzi kwa ufasaha zaidi ili wachangiaji tuweze kuchangia vizuri.Ninahisi una maana kubwa zaidi ya jinsi tunavyofikiri na hii pengine ni kutokana na kuwa umeitumikia hii serikali yetu na hatimaye upinzani.Huenda wengi hatufahamu historia vizuri.

Hatahivyo ningependa kukuuliza;
Kwa kuzingatia sheria ya mabadiliko ya katiba ya 2011 na kurekebishwa 2012,je kuna kifungu chochote rais amekiuka katika kuteaua hao wajumbe tume?Kama ndiyo ni ipi?Kama siyo kuna,kuna haja gani ya kuanza kupingana na sheria tuliopitisha juzi hata miezi 2 haijaisha?
Ni vigumu sana kuhoji usawa wa wajumbe kwa misingi ya dini kama haikutamkwa kwenye sheria ya mabadiliko ya katiba.
 
Mkuu kwenye hoja yako ya kwanza sina wasi wasi sana na idadi ya wana CCM maana baadhi yao na hasa Mwnyekiti Warioba ni majeruhi wa siasa za Makundi na hasa mtandao wa JK uliomuundia zengwe Salim asiwe Rais wetu nadhani nao wamepata rungu la kumalizia hasira zao siyo kwa kufanya upendeleo bali kwa kutenda haki, sina wasi wasi sana na hili.

Hoja yako ya pili nadhani Kamati ya Chadema inayofanya uchambuzi wake ndiyo itakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuliongelea hili nina uhakika wanalifahamu vyema na hata Tundu Lisu alishawahi kuliongea hili Bungeni akaonekana kama adui wa Wanzanzibar.
Hoja yangu ya kwanza pengine hukunielewa. Swala sio ugonvi ndani ya CCM yenyewe maana katiba ni ya Taifa ambayo itatupa dira ya kitaifa. Warioba na Salim bado ni wanaCCM na wataitetea CCM ile ya mwalimu ambayo bado itakilinda chama kimoja, siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na kadhalika haya yote ni itikadi ya chama chao..Je kweli wako huru kukubali hata yanayopingana na muundo wa chama hiki CCM?

Swali langu ni (mfano) Je, kina Warioba wataweza kukubaliana na mawazo ya chama CCM kurudisha mali zote za wananchi ambazo zilichukuliwa kiholela na chama hiki?, Kuondoa cheo cha waziri mkuu badala yake rais ndiye awe mwakilishi wa serikali hadi bungeni. Wabunge lazima wawe wakazi wa sehemu wanazogombea na kadhalika, maana haya ni mawazo yetu ambayo sii lazima yachukuliwe..

Je watakubaliana na dira za Kibepari, nini nafasi ya WAKULIMA na WAFANYAKAZI dhidi ya ubepari na utandawazi..Maana ikumbukwe tu kwamba kule bungeni CCM inatupiga bao kwa kuwa na wajumbe wengi sidhani kama kamati itakayo undwa itakuwa na Upinzani sawa na chama tawala..Kuna hatari ya kupewa katiba ya CCM iliyorekebishwa badala ya katiba ya Kitaifa.
 
Licha ya kwamba J.K. kajitahidi kuwa na vigogo kweli kweli, na Katiba ya sasa imezingatiwa ktk kuandaa m'badala wake, muundo wa hii Tume umedhihirisha kwamba demokrasia ya kweli ni ndoto kwa Watanzania wa leo. Kama tunanuia kwa dhati kuwa na Demokrasis ya kweli, itabidi Watanzania wanaoamini kwamba hilo ni muhimu, waendelee na juhudi za kuandaa hata Mabadiliko kwa Katiba Mpya ijayo.

Kwa mfano ni jambo la kichekesho kwamba Tanzania Bara ambayo ina Watu takriban 42 milioni iwakilishe na wajumbe sawa na Tanzania Zanzibar ambayo ina watu wasiozidi 1.5 milioni. Mfano wa pili ni kwamba, licha ya kwamba Tanzania siyo nchi inayozingatia dini katika maamuzi yake ya kisiasa, ni lazima tukubali kuwa madhehebu ya dini yana influence katika mchakato na hatimaye maamuzi. Nikihesabu Waislamu katika hii Tume kwa kuzingatia majina naona zaidi ya theluthi mbili ni Wao. Wengine ni Wakristo au watu wasiokuwa na dini yoyote.

Hata kama ni lazima tujali Muungano wa Jamhuri yetu, hatuwezi kupuuza ukweli kuwa sasa kuna matatizo ya umilikaji wa raslimali maliasili (e.g. gas), na kuna wananchi wamediriki hata kwenda Umoja wa Mataifa kudai Zanzibar ijiondoe.

Haya ni mambo mazito na nimeona ni vema niyataje sasa, siyo tu yajadiliwe na Tume, bali ikiwa ni lazima, basi mjadala uendelee hata baada ya Tume kutoa taarifa na Bunge Maalum kupitisha Katiba Mpya.
Imenibidi nisome tena bandiko la Mzee Mtei lakini sioni uongo wake uko wapi, labda nikiri watu tunatofautiana uelewa...kwa sababu kazungumzia mambo mawili makubwa..

1. Idadi ya waislamu kwenye tume ni kubwa....isn't true?
2. Zanzibar ina watu wachache kulinga na tanzania bara....isn't true?

So, tatizo liko wapi?
 
Hoja yangu ya kwanza pengine hukunielewa. Swala sio ugonvi ndani ya CCM yenyewe maana katiba ni ya Taifa ambayo itatupa dira ya kitaifa. Warioba na Salim bado ni wanaCCM na wataitetea CCM ile ya mwalimu ambayo bado itakilinda chama kimoja, siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na kadhalika haya yote ni itikadi ya chama kimoja.
Swali langu ni Je, Warioba ataweza kukubaliana na mawazo ya chama CCM kurudisha mali zote za wananchi ambazo zilichukuliwa kiholela na chama hiki?. Je watakubaliana na dira za Kibepari, nini nafasi ya WAKULIMA na WAFANYAKAZI dhidi ya ubepari na utandawazi..Maana ikumbukwe tu kwamba kule bungeni CCM inatupiga bao kwa kuwa na wajumbe wengi sidhani kama kamati itakayo undwa itakuwa na Upinzani sawa na chama tawala..Kuna hatari ya kupewa katiba ya CCM iliyorekebishwa badala ya katiba ya Kitaifa.

Tunatakiwa kujiuliza power za wajumbe kwenye kuandaa katiba..je nini nafasi ya mjumbe mojamoja na wao kama wajumbe wana nafasi na uwezo kiasi gani kuathiri maoni ya wananchi?

Ukiangalia mtu kama Warioba- ni pro-nyerere na mjamaa conservative kwelikweli; Salim pro-nyerere lakini mwanadiplomasia (mwepesi kukubali mawazo mapya); A. Ramadhani experts sijajua misimamo yake ya kisiasa...

Kama wajumbe wana nafasi na uwezo wa kuweka na kutoa maoni ya wananchi (bila kuathiri namna wanavyotaka mambo yawe) tutapata katiba nzuri..

Lakini kwa aina ya kina warioba; i am very disapointed.
 
Imenibidi nisome tena bandiko la Mzee Mtei lakini sioni uongo wake uko wapi, labda nikiri watu tunatofautiana uelewa...kwa sababu kazungumzia mambo mawili makubwa..

1. Idadi ya waislamu kwenye tume ni kubwa....isn't true?
2. Zanzibar ina watu wachache kulinga na tanzania bara....isn't true?

So, tatizo iko wapi?
Tatizo sio Uongo bali what is right or wrong.. tunasema amekosea hatusemi amesema uongo. Hatugombanii fito kujenga Tanzania kwa makundi ya udini wala Ubara na Uzanzibar bali nani mwenye uwezo wa kujenga..mifano yake haina maana kabisa..
 
Imenibidi nisome tena bandiko la Mzee Mtei lakini sioni uongo wake uko wapi, labda nikiri watu tunatofautiana uelewa...kwa sababu kazungumzia mambo mawili makubwa..

1. Idadi ya waislamu kwenye tume ni kubwa....isn't true?
2. Zanzibar ina watu wachache kulinga na tanzania bara....isn't true?

So, tatizo iko wapi?

So ulitaka idadi wakristo iwe kubwa kwe tume au siyo? kwanini?

Umesoma sheria ya uundaje wa tume? wajumbe wa zanzibar ulitaka wawe wangapi kwa mujibu ya sheria?
 
Imenibidi nisome tena bandiko la Mzee Mtei lakini sioni uongo wake uko wapi, labda nikiri watu tunatofautiana uelewa...kwa sababu kazungumzia mambo mawili makubwa..

1. Idadi ya waislamu kwenye tume ni kubwa....isn't true?
2. Zanzibar ina watu wachache kulinga na tanzania bara....isn't true?

So, tatizo iko wapi?

Changia hapo juu post ya Mkandara kuhusu wajumbe wa ccm kuwa wengi naomba usiturudishe nyuma kwenye masuala ya dini.
 
Imenibidi nisome tena bandiko la Mzee Mtei lakini sioni uongo wake uko wapi, labda nikiri watu tunatofautiana uelewa...kwa sababu kazungumzia mambo mawili makubwa..

1. Idadi ya waislamu kwenye tume ni kubwa....isn't true?
2. Zanzibar ina watu wachache kulinga na tanzania bara....isn't true?

So, tatizo liko wapi?

1. Idadi ya wajumbe wa Tanganyika waislamu 4 vs. 11 wakristo; kwanini Tanganyika inawapendelea wakristo (hapo ndiko kuna tatizo kubwa sana

2. Idadi ya wajumbe wa Zanzibar 15 vs 15 wa Tanganyika kwa mujibu wa sheria; sidhani kama wazanzibar wanawakilisha waislam wa Tanganyika katika tume bali Zanzibar yao...
 
Tunatakiwa kujiuliza power za wajumbe kwenye kuandaa katiba..je nini nafasi ya mjumbe mojamoja na wao kama wajumbe wana nafasi na uwezo kiasi gani kuathiri maoni ya wananchi?

Ukiangalia mtu kama Warioba- ni pro-nyerere na mjamaa conservative kwelikweli; Salim pro-nyerere lakini mwanadiplomasia (mwepesi kukubali mawazo mapya); A. Ramadhani experts sijajua misimamo yake ya kisiasa...

Kama wajumbe wana nafasi na uwezo wa kuweka na kutoa maoni ya wananchi (bila kuathiri namna wanavyotaka mambo yawe) tutapata katiba nzuri..

Lakini kwa aina ya kina warioba; i am very disapointed.
Usiwe disapointed ikiwa tuna mawazo tofauti hasa ktk maswala ya Kitaifa. Kuwa pro Nyerere haina maana unapingana na jamii yote bali unaleta hoja ambayo haikutazamwa. halafu tunapigishana kelele bure tu hii tume kazi yake ni kuratibu mawazo na maoni ya wananchi. Ukisema wewe sitaki Ujamaa wa Nyerere unamfuata mtu wako unayeamini atalifikisha.

Nadhani tunaogopa bure tu sasa hivi lakini hawa wajumbe wa tume hii sii watoto wadogo wala vimeo, ila ni watu waliokwisha pitia siasa za kila aina tena nadhani wao wanayajua mengi mabovu kikatiba kuliko hata sisi. Wasiwasi yangu bado ipo kwa UCCM wenu ambao unakosa wafuasi hivo katiba inaweza jengwa kuhakikisha wanabakia madarakani mwaka 2015.
 
Usiwe disapointed ikiwa tuna mawazo tofauti hasa ktk maswala ya Kitaifa. Kuwa pro Nyerere haina maana unapingana na jamii yote bali unaleta hoja ambayo haikutazamwa. halafu tunapigishana kelele bure tu hii tume kazi yake ni kuratibu mawazo na maoni ya wananchi. Ukisema wewe sitaki Ujamaa wa Nyerere unamfuata mtu wako unayeamini atalifikisha.

Nadhani tunaogopa bure tu sasa hivi lakini hawa wajumbe wa tume hii sii watoto wadogo wala vimeo, ila ni watu waliokwisha pitia siasa za kila aina tena nadhani wao wanayajua mengi mabovu kikatiba kuliko hata sisi. Wasiwasi yangu bado ipo kwa UCCM wenu ambao unakosa wafuasi hivo katiba inaweza jengwa kuhakikisha wanabakia madarakani mwaka 2015.

Huu ni ukweli lakini ni uwezo (wa chair) kwenye hili;

Pili kwanini Mtei amekuwa na wasiwasi wa kidini?
 
Huu ni ukweli lakini ni uwezo (wa chair) kwenye hili;

Pili kwanini Mtei amekuwa na wasiwasi wa kidini?
Chairman ana uwezo gani?..
Kuhusu Mtei hata JK ameteleza mangapi mkuu wangu wakimtuhumu hata Salim kwa Uarabu wake, kina Mkapa na yaleyale anayoyafanya yeye..tuwakosoe inapowezekana na sii kufanya unazi..Sijakusikia hata siku moja ukimkosoa JK zaidi ya kutafuta sababu wakati unajua fika mkuu kachemsha.
 
1. Idadi ya wajumbe wa Tanganyika waislamu 4 vs. 11 wakristo; kwanini Tanganyika inawapendelea wakristo (hapo ndiko kuna tatizo kubwa sana

2. Idadi ya wajumbe wa Zanzibar 15 vs 15 wa Tanganyika kwa mujibu wa sheria; sidhani kama wazanzibar wanawakilisha waislam wa Tanganyika katika tume bali Zanzibar yao...
Angalau wewe umejaribu kulielewa swali lakini hata hivyo hujajibu, nauliza uongo wa Mtei ni upi, bado nitaendelea kumwona yuko sahihi kabisa maana kasema ukweli ambao ni mchungu. Huo ni msimamo wangu.
 
Hivi nani mwenye kujua kama aliyetuma hii thread ni Edwin Mtei original ?:focus:
 
Namkumbuka Jussa alivyoshambuliwa alivyotoa kauli zake kuhusu matokeo ya uzini...hapa honestly naona Mzee wetu amecheza kama alivyocheza Baloteli jana...Hii kauli ni hatua kadhaa nyuma kuelekekea kwenye ushindi 2015.
 
Angalau wewe umejaribu kulielewa swali lakini hata hivyo hujajibu, nauliza uongo wa Mtei ni upi, bado nitaendelea kumwona yuko sahihi kabisa maana kasema ukweli ambao ni mchungu. Huo ni msimamo wangu.
Sawa, na uongozi wa Chadema kuna waislaam wangapi? mbona sisi hatuoni ubaya japokuwa ni ukweli. Again swala ni right or wrong sio ukweli. Nikisema wewe Mchagga kuna uongo? au sii right mimi kuyaandika hapa.
 
Back
Top Bottom