KILA MMOJA AENDE ALIPOSOMA SHULE AKIWA NA CHOCHOTE AMTAFUTE MWALIM WAKE AMBAE ALIMTOA AKIWA HAJUI KUANDIKA WALA KUSOMA...
Mkuu IDIMI nashukuru sana mzee kwa information hizi, kwa kweli nimekumbuka mbali sana na najihisi hata machozi kunidondoka mtu wangu.
Nilikuwa dogo enzi hizo napiga soka balaa, begi kubwa mgongoni ndani madaftari kibao,Kuhusu ile Stori ya Twende Tukawinde ,nimeikumbuka majamaa wameenda kuwinda ngedere ,dingi kabeba gobore, dada yao kawaandalia Mabumunda. katika hiyo stori nakumbuka jamaa alivyokuwa akilalamika kwa machungu jinsi ngedere wanavyomaliza mazao shambani, nanukuu "Ni nani aliyekula Matango yetu?, huyu atakuwa ni Mnyonyaji".
Umenikumbusha tena kuhusu sikiri na Sadiki
ngoja niwakumbushe vizuri hapa,
Sikiri mimi masikini,
uvivu wangu nyumbani,
ukiwa huu njiani,
nakufa hapa kwa nini,
Sadiki sasa ashiba
Chakula kingi kwa baba
Nirudi tena kwa baba
Nakufa hapa kwa nini?
Halafu kuhusiana Na Bendera ya Tanzania
kulikuwa na shairi pia, nakumbuka ubeti mmoja
wakoloni walifika,huku na dharau zao
Kudharau Afrika,kutukuza nchi zao
Sasa wanaaibika, hawana tena kikao
..........................,,,,>
Nakumbuka kidoogo kuhusiana na shairi hili
Twakukaribisha Mwenge
Mgeni wetu uringe
na wenyeji tukupambe
Huku tukishangiria!
Idimi unaikumbuka ngonjera ya(mimi nimeikumbuka kwa mbaali,nadhani nitakuwa nimekosea ila najaribu kuvuta feeling)
Dada Asha sikilza
Maneno ya kupendeza
Azimio la Arusha
Lilizaliwa Arusha
Arusha unaitaja
sijui inavyokuja
Azimio la arusha
Azimio kitu gani?
.......KILA MMOJA AENDE ALIPOSOMA SHULE AKIWA NA CHOCHOTE AMTAFUTE MWALIM WAKE AMBAE ALIMTOA AKIWA HAJUI KUANDIKA WALA KUSOMA...
Dah mkulu umenikumbusha pa kunikumbusha.....Yaani we acha tu.Enzi hizo mtu akifaulu (kuchaguliwa) darasa la saba kwenda form one nyumbani inakuwa bonge la shangwe lakini si siku hizi hamna tena hiyo sherehe maana ni muda wa mzazi kujikuna kumpelekea mamilioni mama Lwakatare (St. Marys) tehe tehe !
Dah nakumbuka hicho kitabu mkuu...tulikuwa nacho pale skonga....Kuna mshkaji hivi sasa ni mkubwa katika taasisi fulani dar, ilikuwa darasa la tano kama sikosei. Somo la sayansi kilimo, si unajua tena darasa la tano yanaongezeka masomo mawili kama nakumbuka vizuri (Kilimo na Historia), Basi mimi na mshkaji tukawa tunajifanya watoto wa mjini hatutaki kusoma sayansi kilimo tunaingia mtini kipindi chake. Tuna recruit watu wengine kuandaa mechi na shule ya jirani. Basi huo ndio ulikuwa mchezo wetu kwa kipindi kadhaa, kilichoniepusha mimi kuingia kwenye black book ni kuwa madarasa mengine naatendi ila mshkaji wangu yeye akafanya across the board.Mnakumbuka "KITABU CHEUSI???????",iliaminika kabisa ukiandikwa humo wewe utakuwa na maisha mabaya kweeli baadaye. Kuna mshikaji aliandikwa tukiwa darasa la nne tulikuwa tunaogopa hata kutembea naye maana ilionekana atatuambukiza the expected misfortunes......... Kweli tumetoka mbaaaali
Stori za Juma Rose and Baraka?
Hizi stori zilikuwa zinanikosha ile mbaya, mwanzoni ngeli ilikuwa haipandi kabisaa, ila nilikuwa nikiona picha za Juma,Rose na baraka stori ilikuwa inapanda kwelikweli.ila stori ya mwisho ktk series za stori Za juma and baraka ilikuwa chapter ya mwisho wakati huo tuko darasa la saba, Juma anaaga anasema byebye, it was too emotional, from that moment i was not a kid again!
Halafu kwa Upande wa vitabu vya Kiswahili, nako ilikuwa burudani tupu.
stori kama KIBANGA AMPIGA MKOLONI, SIZITAKI MBICHI HIZI,SIKU YA GURIO KATERERO,BENDERA YA TANZANIA,ANDUNJE(mtoto mdadisi), NGANENEPA ANG'ATWA NA NYOKA,AHADI KUMI ZA MWANA TANU na nyingine nyingi zote ilikuwa burudani tupu.
Kweli wakati ule mtaala ulikuwa umetulia, kwa sasa hivi sifahamu mitaala ikoje lakini nakiri mtaala katika somo la kiswahili, ulikuwa umetulia.
Nimalizie kwa beti ninazozikumbuka(japo sizikumbuki vizuri sana) kutoka katika shairi la sizitaki mbichi hizi
Hadithi inayokuja, ni ya sungura sikia
hadithi uliyongoja leo ninakuletea
Alitoka siku moja njaa aliposikia
njaa aliposikia sungura nakuambia
Siku hiyo akaenda porini kutembelea
akayaona matunda mtini yameenea
sungura akayapenda mtini akasogea
Mtini akasogea sungura nakuambia
SIZITAKI MBICHI HIZI, sungura akagumia
naona nafanya kazi bila faida kujua
yakamtoka machozi matunda akalilia
Matunda akalilia Sungura nakuambia
Mh imenikumbusha mbali, nakumbuka hadithi ya kwanza ya kitabu cha darasa la kwanza, JUMA NA ROZA
Huyu ni Juma,
Juma ana dada,
Dada yake ni Roza,
Juma anasema,
Tia sukari Roza,
Tia maziwa,
Roza una kiu?
Kunya chai Roza.
Na pia kama sikosei kitabu cha darasa la tatu kilikuwa na hadithi ya Selina na Mariamu walienda msituni, na kuna picha wanaruka kamba, na mwisho kilikuwa kina hitimisha na hadithi ya watu walikuwa wanataka kuchagua kiongozi wao, na kulikuwa kuna picha ya wananchi na mtu mrefu kuliko wote.
Primary school kabla ya ukaguzi utasikia kiranja akisema
.......Mikono mbele, juu, kando, chini.
.......Shoto kulia shoto kulia, nyumaaaaaaaaaa geuka
......Mguu pandee, mguu sawa,legeza mwili (ukikosea, AJUWA)
......Walio mbele, nyumaaaaaaaaa geukaaaaaa
......Mstariiiiiiiiiiii nyoosha (hapo kila mwanafunzi anajificha mgongoni kwa mwenzie bila kutokeza kichwa)
Sana tu na mimi nililifikiria hilp hilo hilo la kutaja shule lakini nikaona kuna unspoken rule ya kutomention identities humu kijiweni. Na mmoja akianza tu mimi nitafuatia. Na ili kuepusha watu kuongopea, watoe na kaishu fulani hivi ambacho kinaambatanisha na kuwa mwenyeji wa mazingira hayo. Ni wazo tu!!Jamani mnanimaliza yaani nacheka mpaka mbavu zinauma kweli ya kale dhahabu, tuanze kutaja shule za msingi tuzlizosoma labda tutakuwa tunajuana humu....
Nawapongeza wote ambao mmechangia ktk hili la kumbukumbu za Primary...its very interesting...Ushauri wangu MSIWASAHAU WAALIM WETU, WAZEE WETU HAO WALITULEA na hadi sasa wengine wapo hai lkn mishahara yao MIBOVU kupindukia...bado akina MRAMBA walienda kuwakopa...wakati wao wakikaa pale BOT siku moja tu mshahara wa mwalim mwezi mzima...KILA MMOJA AENDE ALIPOSOMA SHULE AKIWA NA CHOCHOTE AMTAFUTE MWALIM WAKE AMBAE ALIMTOA AKIWA HAJUI KUANDIKA WALA KUSOMA...
Sana tu na mimi nililifikiria hilp hilo hilo la kutaja shule lakini nikaona kuna unspoken rule ya kutomention identities humu kijiweni. Na mmoja akianza tu mimi nitafuatia. Na ili kuepusha watu kuongopea, watoe na kaishu fulani hivi ambacho kinaambatanisha na kuwa mwenyeji wa mazingira hayo. Ni wazo tu!!
...Katibu tarafa LY ndio ilikuwa noma nakumbuka nilipoingia darasa la 7 nilikuwa nafuga nywele ndefu ili uonekane na wewe gangwe mwalimu mmoja kwenye ukaguzi asubuhi alikuja na mkasi akampitia kila mwenye nywele ndefu anachofanya anakuanzishia kunyoa kwa style ya msalaba katikati ya kichwa ili ukirudi kwenu ukamalizie. Si unajua enzi zile ukiwa na nywele ndefu unaweza kutengeneza matuta!!!....LY nayo ilikuwa na raha yake...LY mnalikumbuka pia neno hili.hapo ndio mmeshaingia std seven