Tuliowahi kupata madem katika mazingira magumu bila kutarajia

monotheist

JF-Expert Member
Apr 30, 2017
720
943
TUKIO LA 1:
Nakumbuka ilikua 2017 baada ya kumaliza form 6 nikaamua kwenda kumjulia hali dada yangu wa mbagara wakati narudi kuelekea home magomeni nikaona nipitie zakheim nikale matunda huwa pamechangamka sana pale

Pale mbagala zakheim kuna daladala zinazoenda mbagala kuu na kijichi aisee nilikuja kustaajabu baada ya kuona pisi kali matata inaingia kwenye gari niliacha kula matunda na mimi nikazama kwenye gari bila kujua gari inaelekea wapi nikafanikiwa kukaa nae siti moja nikaanzisha stori akawa ananipa ushirikiano akanambia anashuka kituo X na mimi nikamjibu nashuka hapo hapo kituo X wakati hata kijichi sijawahi kufika

Mimi nilikaa siti ya mwanzo yeye alikaa siti ya dirishani halafu konda alikua hatangazi vituo nikaona hapa nitaumbuka nikajifanya nimelala baada ya kufika kituo X pisi ikaniamsha tumeshafika baada ya kushuka alinambia anakaa mtaa unaofuata na mimi nikamwambia nakaa kuleee kwa chini (nilionyesha mabondeni huko) tulibadilishana namba na akajakua manzi yangu japokua kwa sasa tumepotezana

TUKIO LA 2:
Ilikua mwaka jana baada ya kumaliza mishe zangu posta nikajisogeza hadi maeneo ya mnazi mmoja kutafuta gari ya kuelekea home baada ya kufika mtaa wa kongo nikiwa kwenye daladala ikaingia pisi moja kali hivi mwembamba kiasi mrefu wa wastani amevaa suruali ya jeans baada ya kuingia ikanipita ikaenda kukaa siti ya mbele karibu na driver nilianza kujilaumu kwa nini nisingekaa siti ya mbele ili niwe karibu nae

Muda wote macho kwake ili asije kuniacha wakati wa kushuka nilipitiliza hadi kituo cha nyumbani kwa ajili yake nilidhamiria kwamba anaposhuka yeye na mimi nashuka hapohapo alipokuja kushuka na mimi nikashuka na nikafanikiwa kumsimamisha na kuanza kupiga nae stori chache nilipomuomba namba akanijibu siwezi kukupa namba barabarani fuatana na mimi hadi ofisini kwangu niliogopa ila nikavaa ujasiri hadi kwenye ofisi yake.

Huyu nipo nae hadi sasa tumetimiza mwaka mmoja kwenye mahusiano ni mdada ambaye amefanya nijue thamani ya mwanamke yupo romantic mno
 
Watu wamechezesha false 9 kwenye uzi wa riki boy magoli kibao that that day wewe unashangilia kupewa no

Levels 😁😁
 
TUKIO LA 1:
Nakumbuka ilikua 2017 baada ya kumaliza form 6 nikaamua kwenda kumjulia hali dada yangu wa mbagara wakati narudi kuelekea home magomeni nikaona nipitie zakheim nikale matunda huwa pamechangamka sana pale

Pale mbagala zakheim kuna daladala zinazoenda mbagala kuu na kijichi aisee nilikuja kustaajabu baada ya kuona pisi kali matata inaingia kwenye gari niliacha kula matunda na mimi nikazama kwenye gari bila kujua gari inaelekea wapi nikafanikiwa kukaa nae siti moja nikaanzisha stori akawa ananipa ushirikiano akanambia anashuka kituo X na mimi nikamjibu nashuka hapo hapo kituo X wakati hata kijichi sijawahi kufika

Mimi nilikaa siti ya mwanzo yeye alikaa siti ya dirishani halafu konda alikua hatangazi vituo nikaona hapa nitaumbuka nikajifanya nimelala baada ya kufika kituo X pisi ikaniamsha tumeshafika baada ya kushuka alinambia anakaa mtaa unaofuata na mimi nikamwambia nakaa kuleee kwa chini (nilionyesha mabondeni huko) tulibadilishana namba na akajakua manzi yangu japokua kwa sasa tumepotezana

TUKIO LA 2:
Ilikua mwaka jana baada ya kumaliza mishe zangu posta nikajisogeza hadi maeneo ya mnazi mmoja kutafuta gari ya kuelekea home baada ya kufika mtaa wa kongo nikiwa kwenye daladala ikaingia pisi moja kali hivi mwembamba kiasi mrefu wa wastani amevaa suruali ya jeans baada ya kuingia ikanipita ikaenda kukaa siti ya mbele karibu na driver nilianza kujilaumu kwa nini nisingekaa siti ya mbele ili niwe karibu nae

Muda wote macho kwake ili asije kuniacha wakati wa kushuka nilipitiliza hadi kituo cha nyumbani kwa ajili yake nilidhamiria kwamba anaposhuka yeye na mimi nashuka hapohapo alipokuja kushuka na mimi nikashuka na nikafanikiwa kumsimamisha na kuanza kupiga nae stori chache nilipomuomba namba akanijibu siwezi kukupa namba barabarani fuatana na mimi hadi ofisini kwangu niliogopa ila nikavaa ujasiri hadi kwenye ofisi yake.

Huyu nipo nae hadi sasa tumetimiza mwaka mmoja kwenye mahusiano ni mdada ambaye amefanya nijue thamani ya mwanamke yupo romantic mno
Dogo unajidai kibolodinda wakati unachukua namba mazingira sio magumu.
 
Back
Top Bottom