Tulia Ackson Mwansasu, PhD, ananikumbusha mbali sana

Tulia Ackson Mwansasu, PhD, ananikumbusha mbali sana

Hizi stori ulikua unasimuliwa na walezu wako ili usinzie unazileta huku, ujue huku unaongea na watu wazima.

huku kudekadeka mlikozoea enzi hizo saiv haipo, kama mmezoea michuzi ya nyama sasa mle ugali mkavu

Ni kweli tutawachagua CCM maana wanatutetea sana,ukiangalia michango yao ni mizuri mno,wametaka serikali iongeze kodi kwenye Diesel na Petrol kwa maana item hiyo kodi zetu ndizo zinalipia,walikataa katakata kukatwa kodi kwa maana siye wadanganyika tuendelee kulipa kodi wao marufuku maana ni waheshimiwa sana.

Wameomba kujengwa kiwanja cha mpira sababu Rais alipiga push up hapo eti sababu Lowassa alishindwa kufanya hivyo,ni sahihi kabisa hata mie nawapongeza,wameomba tubomoe yule askari pale ili tuiweke sanamu ya Diomnd,ningependa waziri wa michezo afanye hivyo haraka jiji lipate kubadilika.Wametaka bangi ihalalishwe maana wao wanakosa biashara,namshangaa waziri wa biashara na sheria hadi leo bado hawajaiondoa kwenye orodha ya items zilizopigwa vita.

Hongera sana😕😕
 
Ukawa wameanza kuchanganyikiwa,wameanza kufunika midomo kwa toilet paper,kiki imebuma wataingia wamevaa chupi kichwani
Kadiri wanavyojifanya hamnazo,ndivyo wanavyozidi kupuuzwa

Waweza kudhani hivyo lakini sivyo udhanivyo.Watanzania wa jana si wa leo.Kuna siku utakuja kujua na ukasema kwanini ulichelewa.
 
Kuna wakati mabadiliko huja hata kama hamtaki, Mungu humuongoza amtakaye...... The story reminds USA na Europe nations wanavyowapiga MAGAIDI ndio magaidi wanapata nguvu kila kukicha

Kwa hiyo ukawa ni magaidi?
 
Wanabodi salamu!

Zamani sana kulikuwa na hadithi mashuhuri sana iliyo mhusu mama wa kambo na mtoto yatima.Mama yule kimsingi hakumpenda kijana yule, alikaa nae kwasababu tu ni mtoto wa mme wake. kwakuwa familia ilikuwa inajiweza mara nyingi chakula chao kilikuwa na nyama kama kitoweo. basi mama yule minofu yote aliwagawia watoto wake na yule yatima akapewa mchuzi na kipande kidogo cha nyama.
Siku wakipika makande aliwajazia watoto wake makande na yule mtoto kuambulia mchuzi na maharage kwa mbali sana.

Siku zilisonga, miaka ikasogea lakini kilicho mshangaza yule mama ni kwamba yule mtoto yatima ndio alipendeza na kuwa mwenye afya kuliko watoto wake. Kila akijiuliza alikuwa hapati jibu. Basi kwa jinsi yule kijana alivyo kua na kupendeza,binti mfalme alivutiwa nae na akatamani aolewe nae. Mfalme akafanya mipango yule kijana akamuoa binti mfalme.

Siku moja yule mama akasema nashangaa watoto wangu nawapa nyama tele lakini yule yatima nampa mchuzi tu lakini ndio anae nawiri! Basi mme wake akamwambia, kwenye mchuzi ndio kuna kila kirutubishi, ndio maana mtoto ambae hukumpenda kwa kumpa mchuzi ulimjenga kiafya badala ya kumkomoa.

Kiukweli Wanasiasa wa upinzani kule bungeni wananyanyaswa sana lakini ndio wanao jengwa kisiasa! Dr tulia mwenyewe anadhani anabomoa upinzani lakini kumbe ndio anaujenga na kuuimarisha zaidi na zaidi.Mpaka tunafika 2020 ,kuna watu watawachagua UKAWA kwa kuwaonea huruma tu kwasababu wameteswa miaka mingi.Kuna watu watawachagua UKAWA kwa kuchukizwa na ukatili na roho isiyo na chembe ya huruma ya spika.Kwahakika UKAWA wanatafutiwa ufalme badala ya kifo.
Haruma kwa UKAWA! wapi...over our dead bodies!!!
 
PhD za hapa naanza kuzitilia mashaka kuna baadhi ya vyuo sawa ivyo vingine ni hela yako tuu...maana hapa rushwa imetawala kila nyanja mpaka katika Elimu...
 
kwa akili yako unafikili vitendo anavyofanyiwa Tulia na Ukawa ungekuwa wew ungevumilia au ungefurahi, Achen ushabik mchwala. Sasahv Ukawa wana mnyanyapaa yule Mama waziwaz hadi imefikia hatua wamekataa chakula cha wazir mkuu et kisa Tulia Akson yupo

Tulia anatakiwa kuwa NS wa wabunge wote,na anatakiwa kuzifanya sheria zifanye kazi kwa pande zote.HAtakiwi kuwabagua.Anachofanya Tulia hakistahili kupongezwa na mtu mwenye akili timamu.Ajirudi ajue kwamba Bunge si serikali ,Bunge ni taasisi inayojitegemea ya kuishauri na kuisimamia serikali na si kinyume.Bunge letu leo halina sauti,meno wala uhuru.Madaraka ya Bunge yako chini ya RAIS ni ajabu,hata wakati wa JKN haijawahi kuwa hivyo.
 
Haruma kwa UKAWA! wapi...over our dead bodies!!!

Tunaoelewa Upinzani tutawapa kura nyingi tena kwa kishindo.Tupeni Tume Huru na jeshi la polisi liwe huru muone
 
Kama PhD ndiyo inayomfanya Tulia kuwa kama alivyo, basi ni neema nchi kutokuwa na PhD holder hata mmoja.
 
Haruma kwa UKAWA! wapi...over our dead bodies!!!
wait and see!! huweze kuwaonea vijana 7800 na kuwafukuza bila huruma halafu utegemee watakupenda.Bunge zima limekosa ladha tulio izoea kwasababu vichwa vyenye akili havipo Bungeni. sasa 2020 wabunge wa upinzani lazima wafike 200 ndio ccm wajute kuwatambua upinzani.
 
Kuna wakati mabadiliko huja hata kama hamtaki, Mungu humuongoza amtakaye...... The story reminds USA na Europe nations wanavyowapiga MAGAIDI ndio magaidi wanapata nguvu kila kukicha
lakini magaidi ni magaidi tu ndio maana hawawezi kushika dola. ona taliban ona al khaeda ona boko haram. hawako sawa kwenye itikadi na malengo yao. ndio kama ukawa. wapinzani wasiokua na lengo sahihi ndio maana waliweza kula matapishi yao.
 
Hizi stori ulikua unasimuliwa na walezu wako ili usinzie unazileta huku, ujue huku unaongea na watu wazima.

huku kudekadeka mlikozoea enzi hizo saiv haipo, kama mmezoea michuzi ya nyama sasa mle ugali mkavu
Mtatetea uovu hadi lini, hata Malaika wako mlinzi anakusuta ndani yako, ukweli utabaki kuwa u kweli
 
Mkiweza kumtoa mbowe pale juu ndo mje na story zenu za mslopogazi.
 
Unajua sipendi kabisa kujadili watu na maisha yao, na wala huwa sipendi kuwekeza kwenye matukio. Nimeumbwa kupenda kujadili hoja, ambazo kwangu naona kama ndizo kuzaa na kupelekea matukio mbali mbali, tabia na maisha ya watu na mambo mbali mbali tunayoyaona.

Lakini kwa siku za hivi karibuni nimekuwa natamani sana kujua maisha ya huyu binti yangu Tulia kwa ujumla. Ninatamani kujua mazingira aliyokulia hadi yakamfanya awe jinsi alivyo. Pia ninatamani kujifunza kujua kama ana watoto na kama Mungu angeniweka nione maisha ya hao watoto wake katika Tanzania anayoijenga. Lakini zaidi nataman nikae naye meza moja katika mazingira yasiyo rasmi ili nimwelewe ni binadamu wa aina gani.

Yote tisa, kumi Tuombe Mungu. Anaweza.
Essentially motherly love hana, na kikubwa kilicho mfikisha pale ni kwanza kufahamiana na kidogo elimu aliyo nayo ya vyeti imemfanya wanao mbeba kuhalalisha kumbeba kwake! Mambo mengi hatangulizi hekima mbele na kwamba kwa umri wake alitakiwa aendelee kujifunza zaidi kuijua siasa na wanasiasa, lakini impact ya matendo yake kwake yeye binafsi siku za usoni na pengine hata kwa watoto wake.
 
kwa akili yako unafikili vitendo anavyofanyiwa Tulia na Ukawa ungekuwa wew ungevumilia au ungefurahi, Achen ushabik mchwala. Sasahv Ukawa wana mnyanyapaa yule Mama waziwaz hadi imefikia hatua wamekataa chakula cha wazir mkuu et kisa Tulia Akson yupo
Wewe hiyo unaingalia upande mmoja, kiukweli wasio furahishwa na matendo ya Tulia ni wengi. Juzi nilikuwa Hospitali moja Dar nikawaona Manesi wanamjadili huyu mtu, wote walikuwa na negative altitude towards her,mmoja alienda mbali akasema hana upendo kabisa wa kimama!
 
lakini magaidi ni magaidi tu ndio maana hawawezi kushika dola. ona taliban ona al khaeda ona boko haram. hawako sawa kwenye itikadi na malengo yao. ndio kama ukawa. wapinzani wasiokua na lengo sahihi ndio maana waliweza kula matapishi yao.
Kutoka wabunge wanne mwaka 1995 hadi wabunge 130 mwaka 2015 unadhani mchezo? je, ikifika 2020 watakuwa wangapi? kufikia 2025 wapinzani watakuwa wamenyakua Nchi.Historia haidanganyi, mpaka sasa vyama vilivyo dai uhuru barani Afrika vilivyo madarakani ni vitano tu, navyo muda umekaribia vitashindwa na new generation itashika hatamu.
 
lakini magaidi ni magaidi tu ndio maana hawawezi kushika dola. ona taliban ona al khaeda ona boko haram. hawako sawa kwenye itikadi na malengo yao. ndio kama ukawa. wapinzani wasiokua na lengo sahihi ndio maana waliweza kula matapishi yao.
We TAFUTA maarifa kwingine usiwe kipofu, je mzoga wa simba hautoi asali? Nchi zilizodharau watu wake leo zinajuta kwa kuzalisha hayo makundi uliyoyataja, mie naogopa kuyataja yasije kwetu MUNGU a tuepushe.
 
Kumjadili Dr Tuli ni kumpa umaarufu wa bure.
Ni kweli kuwa ni kama tunampa mtu umaarufu asio stahili, lakini watu tunaonesha kukerwa na tabia ambazo siyo za kawaida mwanamke kuwa nazo.wanawake naturally ni wapole, wanyenyekevu, wapenda haki na ukweli lakini inaoneka hivi vyote hana!
 
Ulijuaje kama malaika wake anamsuta na wewe ni malaika ama? watu wengine wehu kweli
Kama wewe mwenyewe ulichoandika nafsi yako inakusuta, hujui ni kwa nini nimemjibu. Dhamira yako ni <>+_-
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom