Tukubali tu: Sisi wajinga... (I know, it hurts)

ehe mambo magumu. kweli watanzania tu wajinga lakini nyie mnaosoma ulaya miaka nenda rudi bila kuhitimu ndio wajinga zaidi kwani hamna kitu mnachangia hapa zaidi ya kuleta usanii kwenye mambo mazito. Malizeni digirii zenu mrudi nyumbani kama kweli mnataka kuleta mabadiliko maana hii forum wengi wenu ni wazamiaji mko ulaya hata hamjui kinachoendelea bongo. Wengine mko miaka nane hata digrii ya kwanza hamjapata sijui mnategemeaje kuleta mabadiliko hapa bongo. Tunachoka na porojo zenu rudini nyumbani wana wapotevu nyie.

Kama kuna thread niliyoposti ambayo inakukuna then meza wembe stupid!

Niko tayari kupambana na panya kama nyie

Hapa hatishiwi mtu wala intimidation!

Sasa mbona unakurupuka kwa chuki zote hizi we unafikiri ni wote wanasomeshwa na mafisadi ama serikali!?

Kwi kwi kwi...Karibu JF were we fight MAFISADI!

Una akili nzuri!?

Tafuta pengine pa kuanzia maana hata Chenge mwenyewe kagonga mwamba!
 
Bin Maryam kaongea vizuri kuhusu mfumo wa elimu na mfumo wa kiuchumi kuenda bega kwa bega, utajifunza computer science all you want with your textbooks, lakini kama huna computer ya kufanyia projects/prcatice utatoka hapo mtupu hata ki script kiddie cha high school kitakutoa nishai.

Sasa sisi tulikuwa tunafundishia mibuku mambo ya engineering kama ungwini vile, kisa hatuna mfumo wa uchumi unaoruhusu ma practical ya maproject makubwa ya kutosha kumfanya mhandisi akomae.Ndiyo maana huku west kila miezi fulani fulani ikifuika unakuta maofisini interns kibao wanajaa, tena hata hawalipwi hela nzuri, ni experience tu ya kufanya kazi.

Sasa nyumbani tunakosa uchumi na culture inayoweza ku absorb interns.Hili hata Nyerere alishalisema, kwamba how can a poor afford not to make use of its student while the richest nations are doing that? Jibu ni kwamba basically hatumthamini mtoto/mwanafunzi, tunaona hajui na atatuharibia kazi tu. Yeye mwenyewe (Nyerere) alikuwa ndiyo architect wa hiyo system halafu akajifanya kushangaa alivyong'atuka.
Swadakta yeye ndio alileta siasa katika mashule na kupoteza ile hadhi ya academicians...akawaleta ma head master waliopigwa msasa Kivukoni...jamani tumetoka mbali eeh

Hivi kuna mtu anakumbuka picha ya JKN ilyokuwa ikiwekwa mashuleni akionyesha kidole imenitoka caption yake tafadhali mtu kama anakumbuka hebu iwekeni hapa
 
WE ulitaka na sisi tufungue matawi ya CCM kama tujifisadi twengine tudogo tudogo tulivyoamua kufanya!? Si ni heri wale wanaopambana na life kuliko kuwaibia wananchi!
STUPID!
Your Darn wrong!

Eti kwetu!
Kwenu wapi fisadi we!

Huna pa kwenda!
 
Naomba mnapoangalia suala hili msiliangalie kwenye mwanga wa uhandisi tu, bali katika fani nyingine tofauti pia; ualimu, uuguzi, polisi, afisa wa kodi n.k

I'm trying to find a rational explanation ya kutoweza kwetu kusimamia mambo yetu kwa mafanikio sisi wenyewe lakini tukishirikiana na wazungu we excel..

Je malipo kwamba tukiwalipa sana ndio watakuwa waadilifu na makini zaidi (hawatataka kutukamua zaidi); je kuna sense ya uduni mbele ya kiongozi mzungu?

Kwenye kikao kimoja nilichowahi kuhudhuria wazo lilitolewa na mtu wa kijijini jinsi ya kupitisha mfereji wa maji kwa kilimo cha umwagiliaji na akatumia model ya mzee mmoja hivi na kusema tukifanya hivi na kupitisha kwenye shamba la fulani basi ile terrain ni nzuri sana. Waendesha semina toka Dar wakamtolea nje kwamba isingeliwezekana, ni ya gharama, na wakashangazwa anafikiri vipi hilo kuwezekana kwenye kijiji cha Dongobesh huko Mbulu.

Baada ya mjadala kidogo Mswede fulani aliyekuwa anashiriki semina hiyo hiyo akaamua kutoa mchango na kuelezea haja ya kufanya alichosema mzee Akonaay, guess what? It was the best idea ever!!!

Mzee wa watu hadi leo ameshindwa kuelewa na jamaa wakampa credit mzungu kwa mawazo yake "endelevu". Leo hii ukienda maeneo hayo utaona mfereji wa maji ukipita na kukata kijiji cha Dongobesh...
 
Mwanakijiji,
Mkuu jibu lako ni NJAA, hakuna kitu zaidi ya Umaskini wa hali na mali yaani sisi kila siku ni misiba mitupu..Maisha yetu kila siku ni Tsunami hivyo mkuu sii rahisi kuona wasomi wetu wakifikiria kwanza Taifa ikiwa hata familia yenyewe ilimpeleka shule ili aje kuwa mwokozi kifedha na sio swala la kupata elimu...

Ebu fikiria masinia mawili ya Biriani yameshushwa katika meza mbili moja ya wale waliokwisha fanikiwa na jingine kwa kina Yakhe walalahoi.. nambie vita ya pale sinia la pili sidhani kama kuna haja ya kutumia elimu kusukuma matonge haraka upate shibe kabla sinia halija isha..Phd yako utaiweka kwenda sambamba na wale wasiokuwa na elimu.
Kuna mshikaji wangu mmoja aliwahi kunambia, ati unajua kwa nini sisi Waswahili tunapenda kula kwa mikono yetu?... akasema ni kwa sababu ya ujazo wa tonge kwa sababu maisha yetu siku zote ni mashindano toka kula hadi kulala..Kwa mtaji huo tumefikia kuzoea kula hivyo hata kama chakula kipo cha kutosha bado mtu akafukanya kwa mkono pamoja na kwamba ujazo wa sahani ni ule ule hata kama akila kwa kijiko, kiasi cha chakula atakacho kula ni kile kile...
Mimi nilicheka sana na kumuuliza Je, wale wanaokula na vijiko hali wana njaa sii nao wanajaribu kuiga mzungu hali rohoni mwao tamaa ya kula kwa mkono na kushindana bado ipo?..Unajua ni fun fulani kula sinia moja kisha mkashindana.. Akasema - Haswaaa, ndio tatizo la watu tunaoishi Ulaya, hatutumii vijiko kwa sababu tunaelewa ujazo wa chakula isipokuwa tunatumia vijiko ili nasi tuonekane civilized... hii inatokana na elimu chafu tuliyopewa kiasi kwamba hata kula yetu inatakiwa ifanane na ile ya mzungu hata kama hatufahamu kwa nini wao hutumia kisu, uma na vijiko kula chakula ambacho ungeweza kumaliza haraka ukitumia mkono...
Hivyo fanya mahesabu mkuu, mwisho wa yote haya utakuta kitu kinaitwa ULIMBUKENI....
 
Kama kuna thread niliyoposti ambayo inakukuna then meza wembe stupid!

Niko tayari kupambana na panya kama nyie

Hapa hatishiwi mtu wala intimidation!

Sasa mbona unakurupuka kwa chuki zote hizi we unafikiri ni wote wanasomeshwa na mafisadi ama serikali!?

Kwi kwi kwi...Karibu JF were we fight MAFISADI!

Una akili nzuri!?

Tafuta pengine pa kuanzia maana hata Chenge mwenyewe kagonga mwamba!



kweli nimeamini nyie ni wazamiaji tu sasa mbona unabwata ndugu yangu we rudi tu ili upambane na hao mafisadi huko ulaya husaiidii kitu kama una uchungu na nchi yaako rudi umalize mambo acha kuosha masufuria na kutandika vitanda na kulea vizee vya kizungu
 
WE ulitaka na sisi tufungue matawi ya CCM kama tujifisadi twengine tudogo tudogo tulivyoamua kufanya!? Si ni heri wale wanaopambana na life kuliko kuwaibia wananchi!
STUPID!
Your Darn wrong!

Eti kwetu!
Kwenu wapi fisadi we!

Huna pa kwenda!


unajua ni leo yu tulikuwa tumekaa mtu akawa anaelezee juu ya hii forum ndio mtu mmoja akatuambia kuwa ni wazamiaji walishindwa maisha na mimi nilitaka tu kuthibitisha na wewe umenithibitishia. kwa kwa tehe tehe
 
kweli nimeamini nyie ni wazamiaji tu sasa mbona unabwata ndugu yangu we rudi tu ili upambane na hao mafisadi huko ulaya husaiidii kitu kama una uchungu na nchi yaako rudi umalize mambo acha kuosha masufuria na kutandika vitanda na kulea vizee vya kizungu

Tukutane kampeni 2010 nyapara we! NA KAMA WEWE NI MMOJA WAPO THEN SUBIRI KUWA MTOTO WA WATU WHEN TIME COMES!

Eti kuosha masufuria! Kwi kwi kwi!

Soma hii!

Matukio ya ufisadi, ubadhirifu wa mali yamewaamsha Watanzania

2008-05-12 08:59:11
Na Dunstan Bahai


``...Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni, na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri. Tumekuwa yatima waliofiwa na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.

Tunakunywa maji yetu kwa fedha, kuni zetu twauziwa.

Watufuatao wako juu ya shingo zetu, tumechoka tusipate raha yoyote Baba zetu walitenda dhambi hata hawako, na sisi tumeyachukuwa maovu yao. Watumwa wanatutawala, hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.

``Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu, kwa sababu ya upanga wa nyikani. Ngozi zetu ni nyeusi kama tanuu, kwa sababu ya hali ya njaa ituteketezayo Wakuu hutungikwa kwa mikono yao, nyuso za wazee hazipewi heshima.

``... Wazee wameacha kwenda langoni, na vijana kwenda ngomani. Furaha ya mioyo yetu imekoma, michezo yetu imegeuka maombolezo.

``Mbona watusahau siku zote, na kutuacha muda huu mwingi. We Bwana, utugeuze kwako nasi tutageuka, zifanye mpya siku zetu kama siku za kale. Isipokuwa wewe umetukataa kabisa, nawe una hasira nyingi sana juu yetu,`` hayo ni baadhi maneno ya Bibilia yanayopatikana kwenye kitabu cha Maombolezo sura ya 5:1-22.

Nimelazimika kunukuu sehemu hiyo ya Biblia kama kitabu kitakatifu, kuonyesha maonyo yaliyotolewa wakati wa zamani na dhuluma iliyopo sasa duniani, hasa katika nchi maskini na zile zinazoendelea, dhuluma zinazofanywa na baadhi ya watawala wake.

Katika kipindi cha takribani miaka miwili na miezi minne hivi, Watanzania na Walimwengu kwa ujumla, wameshuhudia viongozi wa juu wa serikali ya awamu ya nne wanavyoachia nyadhifa zao.

Hatua hiyo ya viongozi kuachia nyadhifa zao haimaanishi wamehusika na tuhuma zinazoenezwa juu yao, bali ni ishara ya heshima na uwajibikaji.

Hatuwezi kuwahukumu viongozi hao kuwa `walivaa ngozi ya kondoo`, huku wakijijua ni `mbwa mwitu` bali walionyesha mfano mzuri wa kuwajibika ingawa wapo wengi wa aina hiyo wanaotakiwa kufuata nyayo zao.

Kuwajibika si dhambi, wala kuwajibika si aibu bali kama kiongozi, anazidi kujijengea heshima.

Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu, anatanabaisha kwamba baada ya Tanzania kupata Uhuru, uongozi wa wakati huo ulikuwa ukitegemea Rais zaidi.

Hata hivyo, alikiri kuwa viongozi wa wakati huo walikuwa na maadili makubwa ikilinganishwa na wa sasa.

Alisema mtu mbadhirifu au aliyepatikana na rushwa, alikuwa hana nafasi wala sifa ya kuendelea kuwa kiongozi, kwani Rais, wakati huo hayati Mwalimu Julius Nyerere, hakusita kumchukulia hatua kali ikiwa ni pamoja na kumfukuza kazi moja kwa moja.

``Wakati huo ilikuwa amri moja tu kwa kiongozi asiye na maadili. Zamani kiongozi akiitwa Ikulu anatetemeka, anajua akirudi hana kazi, ni kiama kwake, lakini sasa hivi mambo tofauti.`` alisema.

Alisema kipindi cha awamu ya kwanza, kulikuwa na matukio mengi ya viongozi kujiuzulu, kufukuzwa na kustaafishwa kazi.

Miongoni mwa tukio la kujiuzulu kwa kuwajibika ni la aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, kutokana na makosa yaliyotokea katika wizara yake.

Katika serikali ya sasa viongozi wengine walioachia ngazi zao kwa uwajibikaji mapema mwaka huu ni aliyekuwa Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Nazir Karamagi, aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha na hivi karibuni aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge.

Hata hivyo, aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Daud Balali, alifukuzwa kazi ingawa ni baada ya kumuandikia Rais kuwa ameamua kujiuzulu.

Uwajibikaji ni sehemu ya uadilifu, nidhamu na kujijengea heshima ndani ya familia ya anayewajibika, lakini zaidi nje ya familia yake na nje ya mipaka ya nchi, kwani kiongozi anaonyesha kujutia kilichotokea akiwa kiongozi katika eneo lake, lakini kujiuzulu kwa shinikizo la umma, hilo halimletei heshima kiongozi.

Kwa mujibu wa Profesa Baregu, kumekuwa na matukio mengi ya ubadhirifu, hali ambayo imewaudhi wananchi hadi kufikia umma huo kuchukia kudanganywa huku mali zao wakishuhudia zikiporwa.

Profesa Baregu alisema shinikizo la nguvu ya umma limechangia kuibuka kwa mambo mengi maovu.

Pia alivipongeza vyama vya upinzani hasa ushirika wa vyama vinne vya CHADEMA, CUF, TLP na NCCR-Mageuzi.

Alisema vyama hivyo kwa kushirikiana na umma wa Watanzania, waliweza kufanikiwa kuufikisha ujumbe, kilio chao cha kuporwa mali zao, na matokeo yalijidhihirisha na kwa upande mwingine serikali imeonyesha nia ya kushughulikia malalamiko hayo.

Hatua iliyofikiwa na serikali ya kuanika uozo uliojitokeza, ni hatua muhimu sana na ya kuungwa mkono na wananchi wengi, hicho ndicho kilichokuwa kikisubiriwa na umma wa Watanzania.

Aidha, hatua hiyo itairejesha heshima na imani ya Watanzania kwa uongozi wa Taifa na mihimili yote ya nchi.
Naye Askofu Mkuu Msaidizi wa Kanisa Katholiki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Methedius Kilaini, ameonyesha kukerwa na watu wanaohusika na ufisadi.

``Mimi simjui fisadi, lakini ninachukia sana hali hiyo. lakini nimeridhika jinsi suala hili lilivyoibuliwa, kwani haya mambo yalikuwepo tangu enzi za mababu, lakini, nani awe wa kwanza kumfunga paka kengele,`` alisema.

Aliwashauri Wabunge, kutokana na ujasiri wao kuliibua suala hili na kulizungumzia kwa kina, waendeleze jitihada hizo hadi mafisadi watakapojulikana na kufikishwa mahakamani, kwani huko wananchi watakapowajua na kupata haki yao.

Askofu Kilaini alikuwa akimaanisha, huwezi kumnyooshea mtu kidole kuwa ni fisadi, kwani wengi wanaamini viongozi wote waliojiuzulu ni mafisadi, la hasha, hao walifanya hivyo kama sehemu ya uwajibikaji, kwani tuhuma hizo zimeibuka wakati wao wakiwa ni viongozi wa maeneo yanayotuhumiwa.

Kwa maana hiyo, uchunguzi unaofanywa na serikali katika maeneo hayo wananchi wanaamini utawaibua mafisadi, pengine ni wale waliojiuzulu kwa heshima au wengine.

Inawezekana kabisa, Rais Kikwete ana dhamira ya kweli ya kuwaondolea umaskini na kero zote zinazowakabili wananchi, lakini wapo wanaokwenda kinyume na dhamira hiyo.

Hata hivyo kuna dalili yawezekana Rais Kikwete ameonyesha kukerwa na ufisadi pamoja na rushwa, ndiyo maana alishindwa kulitolea maamuzi suala hilo na badala yake ameviachia vyombo vya dola kulishughulikia, na Watanzania wanasubiri kwa hamu sana matokeo ya uchunguzi huo.

Kumekuwa na maoni mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na wananchi na viongozi wa dini, juu ya nini kifanyike kwa wale wote watakaobainika kuhusika na kupora mali za Watanzania.

Pia yapo maoni yaliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, kuchunguza tuhuma za Richmond.

Baadhi ya maoni ya wananchi na viongozi wa dini ni serikali kuwachukulia hatua haraka wale wote wanaodhani ni mafisadi ikiwa ni pamoja na kufilisi mali zao.

Maoni hayo ni ya haraka sana, tunaamini hakuna mtu anayemfahamu fisadi, cha msingi ni wananchi kuwa na subira, kusubiri uchunguzi unaoendelea wa vyombo vya dola.

Cha msingi ni vyombo hivyo kufanyakazi yake kwa umakini na ukweli na uwazi ili Watanzania waendelee kujenga heshima kwa serikali yao ya awamu ya nne na hata Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ili suala hili lisiendelee kuwa mjadala, tena mjadala wa kutoaminiani, dhamana ya ukweli wa mambo yenyewe iko mikononi mwa vyombo vilivyoteuliwa na serikali katika kuchunguza masuala hayo.

Vyombo hivyo visipofanyakazi yake kwa makini na ukweli, viongozi waliojiuzulu nyadhifa zao hawatakwepa hasira za wananchi, na maisha yao yatakuwa juu ya mikono ya Watanzania.

Watanzania kama kawaida yao ni wapole, hivyo upole wao usichukuliwe kama ni mazuzu.

Tanzania ni yetu, hakuna mgeni atakayetutengenezea amani na utulivu, kwani suala hili likichukuliwa kwa jazba, urithi wa amani yetu utabakia kama historia, Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
  • SOURCE: Nipashe
 
Heee tumeingiliwa!
Kama hatusaidii kitu mkuu, wewe unafuata nini hapa!.. site zote hizo duniani imekuwaje hata ufike hapa..
Kisha neno Wazamiaji ndugu yangu lina maana nzito sana, tafadhali fanya heshima kidogo!
 
kweli nimeamini nyie ni wazamiaji tu sasa mbona unabwata ndugu yangu we rudi tu ili upambane na hao mafisadi huko ulaya husaiidii kitu kama una uchungu na nchi yaako rudi umalize mambo acha kuosha masufuria na kutandika vitanda na kulea vizee vya kizungu


sasa ndio hayo tumeongelea sana humu kuhusu kazi yaani kuheshimu kazi....wewe unaona mtu anye lea wazee hafanyi kazi au yule anayefagia barabara sio mfanyakazi

Hili ta tizo la wtu kudhrau kazi na kuka kijiweni kupiga gumzo ndio narudisha maendelaeo nyuma....Kwetu huyo anosha sufuria au kutandika kitanda ni mchapa kazi ambye anlipa tax na kuendeleza nchi we unadharau jamni si ndio huu ujinga
 
unajua ni leo yu tulikuwa tumekaa mtu akawa anaelezee juu ya hii forum ndio mtu mmoja akatuambia kuwa ni wazamiaji walishindwa maisha na mimi nilitaka tu kuthibitisha na wewe umenithibitishia. kwa kwa tehe tehe

Kama wewe umerudi kwa jina la tofauti then umekutana na watu smart hapa ndugu yangu!

Na nimeshakwambia kama huamini subiri 2010!

Mwisho wenu umefika!
 
sasa ndio hayo tumeongelea sana humu kuhusu kazi yaani kuheshimu kazi....wewe unaona mtu anye lea wazee hafanyi kazi au yule anayefagia barabara sio mfanyakazi

Hili ta tizo la wtu kudhrau kazi na kuka kijiweni kupiga gumzo ndio narudisha maendelaeo nyuma....Kwetu huyo anosha sufuria au kutandika kitanda ni mchapa kazi ambye anlipa tax na kuendeleza nchi we unadharau jamni si ndio huu ujinga

Mi nakwambia Chenge huyu karudi!

Si ndiye hu huyu MATIKSA?
 
WE ulitaka na sisi tufungue matawi ya CCM kama tujifisadi twengine tudogo tudogo tulivyoamua kufanya!? Si ni heri wale wanaopambana na life kuliko kuwaibia wananchi!
STUPID!
Your Darn wrong!

Eti kwetu!
Kwenu wapi fisadi we!

Huna pa kwenda!


How can u fight mafisadi ukiwa mtoni? rudi rudi acha hasira za pweza. Kuosha masufuria sio profession maliza kusoma ili uje kwa pamoja tupambane na mafisadi lakini kwa sasa huna jipya siendi popote niko nyumbani hata kama ni maskini lakini sijakimbia matatizo ya nyumbani kama wewe., Kukimbia matatizo sio suluhisho la kudumu
 
How can u fight mafisadi ukiwa mtoni? rudi rudi acha hasira za pweza. Kuosha masufuria sio profession maliza kusoma ili uje kwa pamoja tupambane na mafisadi lakini kwa sasa huna jipya siendi popote niko nyumbani hata kama ni maskini lakini sijakimbia matatizo ya nyumbani kama wewe., Kukimbia matatizo sio suluhisho la kudumu

Na wewe lini umeacha ile kazi yako ya ........
 
Kama wewe umerudi kwa jina la tofauti then umekutana na watu smart hapa ndugu yangu!

Na nimeshakwambia kama huamini subiri 2010!

Mwisho wenu umefika!

Mimi sisubiri 2010 kama wewe na wala sina haja kwani sina sababu ila mnaniudhi mnapotuita wajinga wakati nyie mmekimbia nchi huyo fisadi chenge na wengine wala hawanitishii amani anawatisha nyie mlioko ulaya sisi wabongo tutapambana naye hapa kwa karibu, je wewe utafanya nini kupambana nae ndio swali, naona mafindofindo yanakupata unaaza kukosa mwelekeo
 
unajua ni leo yu tulikuwa tumekaa mtu akawa anaelezee juu ya hii forum ndio mtu mmoja akatuambia kuwa ni wazamiaji walishindwa maisha na mimi nilitaka tu kuthibitisha na wewe umenithibitishia. kwa kwa tehe tehe

Kwa hiyo unataka kusema hii forum ni ya wazamiaji walioshindwa maisha?
 
Mimi sisubiri 2010 kama wewe na wala sina haja kwani sina sababu ila mnaniudhi mnapotuita wajinga wakati nyie mmekimbia nchi huyo fisadi chenge na wengine wala hawanitishii amani anawatisha nyie mlioko ulaya sisi wabongo tutapambana naye hapa kwa karibu, je wewe utafanya nini kupambana nae ndio swali, naona mafindofindo yanakupata unaaza kukosa mwelekeo

Kwani tangu lini umetoka ulaya? Na je ulitoka au ulifukuzwa? Sema story yako yote ya kilichokupata "ulaya"
 
How can u fight mafisadi ukiwa mtoni? rudi rudi acha hasira za pweza. Kuosha masufuria sio profession maliza kusoma ili uje kwa pamoja tupambane na mafisadi lakini kwa sasa huna jipya siendi popote niko nyumbani hata kama ni maskini lakini sijakimbia matatizo ya nyumbani kama wewe., Kukimbia matatizo sio suluhisho la kudumu

Mbona ghafla umesahau kuwa kashafa zote zili EPa ,Buzwagi yaani zote alizotoa Dr Slaa Bungeni na akasema amezitoa kwenye mtandao.
Umejiuliza ilikuwaje?

Nimeshaona jamaa wengi wametoka soma nje na mashahada wamekuja hapa na kufisadiwa kishenzi kubali mwenzangu ni aidha hujapata nafasi hiyo ukaenda huko nje na wewe labda una kawivu kidigo
 
Back
Top Bottom