Tukubali tu: Sisi wajinga... (I know, it hurts)

Bin Maryam, haya maneno mazito sana yaani nakubaliana na wewe 100% isipokuwa binafsi nawaogopa hata wazawa sasa hivi kwa sababu sijui mzalendo ni nani haswa ikiwa watu wenyewe ndio hawa Mafisadi...
 
unajua kuna kitu kimoja kinachonisumbua sana kuhusu hili.

a. Hivi watu wanaosoma katika vyuo vyetu vikuu hivyo vitu wanavyovisoma vinatofauti kubwa kiasi gani na vile watu wanasoma nchi nyingine? Yaani, engineer wa umeme wa Tanzania, au Engineer wa barabara anatofauti gani kiujuzi na yule wa nje? Je tukimpa nafasi ya kufanya kazi kama US au UK atafanya hayo anayoweza kufanya Tanzania (kama alivyosema Kuhani Mkuu)?

b. Ni kitu gani kinachomfanya mtumishi wa TAnzania anapowatumikia watanzania wenzake anawapa minimal quality of service lakini akija mzungu au mtu wa nje hasa nchi za magharibi anamuonesha ukarimu na huduma bora kweli. Nazungumza toka personal experience.

NIlipokuwa home mara ya mwisho about four years ago, nilikaribisha marafiki zangu toka Ujerumani na tukawa tunaenda nao kutembelea Serengeti. Through out the tour wao walikuwa wanapapatikiwa ingawa ni mimi nilikuwa nalipia gharama nyingi. Kwanini? Sitoshangaa wengine mmewahi kwenda kupata huduma na ukachukuliwa with contempt lakini mtasha na mabegibegi yake anakaribishwa na "welcome sir, how can I help you" with bis a.s smile! kwanini Watanzania wanastahili huduma ya chini au bidhaa za chini?

c. Je Mtanzania akipewa nafasi ya kuitumikia nchi yake anavutiwa kwa kiasi gani to provide the best quality service? Kuna utaratibu gani wa kuhakikisha the Standard Operating Procedures katika maeneo mbalimbali zinafuatwa to the letter?
 
Kwa watu wenye idea ya financial system utaona jinsi huyu jamaa Ndulu anavyohangaika kubadili mfumo mbovu wa usimamizi wa fedha.

Kusema kweli Tanzania haina watalaamu hata wa kufanya capital budget analysis, hakuna mwenye idea na mineral economy, accounting katika sector ya madini, hakuna lawyer mwenye idea na contract za madini.

Huyu jamaa alikuwa world bank hapo DC, bado anaisoma monetary system ya Tanzania. Also, anajitahidi kutumia njia zote za Fed kucontrol inflation. I am happy wameweza kulow T-bills na kuifanya benchmark kwenye kudetermine other interest rates.

Kumbuka zile Bank zote kutoka njee ya Tanzania hazipo pale kukopesha watu, zilikuwa pale kwa ajiri ya kununua T-bills, T-bond and T-Note kisha kuwauzia wateja wao nchini kwao. Lakini kwa sasa swala hilo litapungua sababu T-bills rate inashuka, and Inflation inapungua.

We have a long way to go, but we make a progress. Hii inatokana na mfumo mbovu uliowekwa kuanzia mzee wenu abdulrashid sijui mpaka Balali.

Visit BoT website sometime, and you will see.
 
Bin Maryam, haya maneno mazito sana yaani nakubaliana na wewe 100% isipokuwa binafsi nawaogopa hata wazawa sasa hivi kwa sababu sijui mzalendo ni nani haswa ikiwa watu wenyewe ndio hawa Mafisadi...

Neno uwazi ambalo ndugu yangu Nkapa alilianza lilikuwa na maana kubwa sana na inavyoonekana yeye mwenyewe alishindwa kulifuata.

Tunatumia rocket science pale ambapo science haiitajiki. Tuwe wa wazi. Toa tenda kwa uwazi, fanya malipo kwa uwazi na kwa wakati unaotakiwa na haitachukua muda mwingi kwa kuona wasanii wanapotea na kubaki wenye uwezo wa kuzifanya kazi.
 
.....NN, ingelitokea kuwa umekaa karibu nami halafu ukawa umetamka maneno kama hayo juu, na katika mazingira ya ajabu ajabu nami nikajikuta nimeshika baseball bat mkononi.... hakika ningeitumia.... the thick end of it could have landed on you at the highest velocity possible!!!!!!

.....NN, but why why why you tryna indoctrinate us with this self-hatin' sh...t?! dawg, you oughtta bring it to a halt....... pliiiiiiiiiz!

nuff' respect

No..no..no! I am not trying to indoctrinate anyone and it's not self hate. I'm simply calling it as I see it. Sorry if it hurts.
 
Prof Ndulu said Tanzania would only manage to retain the remitted earnings when local contractors attain competence to compete equally with foreign firms.

Hii inauma kweli! Mpaka pale mpito huu wa uhuru wa kichumi, (ambayo bado ni ya kifisadi) ukipita bado, tutaona haya(ya Prof Ndulu). Inatia haya, mbali na ujinga, inauma.

Sikubali niwe mjinga ntakubali wajinga waliwao!

Foreign firms?
 
Rev.Kishoka,
Nakubali sana kuwa wakoloni walitumia hila kutuweka chini wapate kutawala lakini sidhani kama moja wapo ni pamoja na kutufundisha Ujinga..isipokuwa walitunyima nafasi sawa ktk kila kitu cha kujiendeleza ikiwa ni pamoja na Umoja wetu.
Ujinga ni kutokuwa na Elimu na mkoloni katukuta tukiwa wajinga na katuacha wajinga... moja ya imani za kijinga ni hizo za kuutukuza Uzungu ambazo zilikuwepo hata kabla Mjarumani hajaweka mguu Afrika. Hizi imani za kulaumu Biblia ama Kuran penye tafsiri chafu ni mafundisho yetu sisi wenyewe, tumefundishana sisi kuwatukuza wazungu.
Nina imani kubwa kwamba haya mafundisho tumeyatunga sisi iwe ni sababu kubwa ya kuleta mapinduzi ya kifikra ama Unafiki wa baadhi makolokoloni wa wazungu kwa sababu dini zote hizi zilitufundisha UPENDO... na ni katika mafundisho hayo ya Upendo ndipo sisi tuliposhusha ngao zetu kuwapa mwanya wakatumia UPENDO huo huo kuboresha azma zao za kutawala..
Hawa hawana tofauti na viongozi wetu leo hii ambao wanatumia sheria, maazimio na sera za vitabu vyetu kupora mali zetu za taifa lakini hata siku moja hawawezi kufundisha kitu kutujaza ujinga...kwa sababu elimu yoyote inayotolewa mara nyingi humwamsha mjinga akili yake na akaanza kuitumia akili yake...
Ni katika mafundisho hayo hayo ya Biblia na Kuran yaliweza kuwaamsha viongozi wengi Machief wetu enzi hizo kukataa kutawaliwa. As a fact vitabu hivi vinajenga zaidi self esteem kutokubali kutawaliwa hata kama wewe ni mtumwa..Ni vitabu kama hivi vilivyoanzisha vita toka enzi za Nabi iDaud hadi kina Kinjeketile - Majimaji kina Kenyatta na Maumau na hata Ghandi wakitumia quotes za vitabu hivi..
Kwa mfano siku zote tulikuwa ktk ujinga wa kuamini viongozi wetu ni makini na hakuna somo la siasa ambalo limepokewa kuwaweka wao mbele yetu zaidi ya unyenyekevu wao kwetu. Ni katika hali hiyo waliweza kuvuta Upendo wa wananchi na kupewa nafasi ambazo wao wamezitumia kutimiza azma (ambition) zao..hawakutujaza Ujinga isipokuwa ujinga tayari tulikuwa nao kabla hawajaingia madarakani. Wanayafanya yote haya wakifahamu sisi ni Wadanganyika, wajinga kina Ndivyo tulivyo hali ktk Ujinga huo huo wao pia wamo kwa sababu walikuwa ktk kundi la wajinga na ni reflection yetu sote. Hivyo basi wajinga ni pamoja na wao wanapotumia nafasi kama hizi za Uongozi kutawala badala ya kuboresha maisha ya kizazi chao..Kesho Tanzania itabaki maskini na kizazi chake kitaendelea kuishi ktk mazingira duni..
Kama nilivyosema Ujinga ni pale mtu hajui na akafikiria kuwa anajua...Ukisha jifahamu kwamba hujui na kweli hujui kitu basi hiyo ni hatua ya kwanza ya kuondokana na Ujinga..

Mkuu Mkandara!
Kwenye hili la biblia kutumika kutukandamiza na kuhalalisha biashara ya utumwa, mchungaji yuko sahihi! Ukweli ni kwamba maandiko matakatifu yametumika sana na wale walio waovu kutetea uovu wao. Na baada ya hapo yalitumika kuhakikisha kuwa tunazidi kuwanyenyekea watawala wetu ili tuweze kupata thawabu hapo baadaye. Ili kuweza kumtendea binadamu mwenzako unyama ni lazima umtoe katika ubinadamu. Hiki ndicho kilichofanyika. inasemekana Jomo kenyatta alisema" walipokuja wazungu, walikuwa na bibli na sisi tulikuwa na ardhi. Wakatufundisha kusali tukiwa tumefumba macho. Tulipofungua macho, tukajikuta sisi ndio wenye biblia na wao wenye ardhi!" Ni vita vikuu vya kwanza na vya pili ambavyo vilituamsha watu weusi. Ni katika vita hivi, babu zetu waligundua kuwa mzungu analia na kuvuja damu kama tunavyofanya sisi. Matokeo yake ni wanamapinduzi wakina Fanon na wenzake. waarabu nao hawakusita kutumia maandishi kuhalalisha biashara hii dhalimu. Wengine wao wanaiendeleza mpaka hivi leo. Mchungaji hakukosea katika hili. Tulifundishwa kuudharau na kuukana utamaduni na utu wetu wenyewe na wale waliotuetea hizi dini! Wala sio sisi. Sisi baada ya kufumbuka macho ndio tumeanza kuyaelewa na kuyafasiri kwa mtazamo wa kimapinduzi. Mfano mzuri ni huyo Rev.Dr. Wright na jinsi anavyoandamwa.

Amandla!
 
hamuwezi kuamini lakini huo ndiyo ukweli, yafuatayo ni mambo yaliyowekwa na wakuu kuhakikisha kuwa local contractors hawawezi kufurukuta
1.0, kila tender inayotangazwa hapa nchini kuna sharti la kuwa na bid security in form of unconditional bank guarantee, yaani kama una-tender kazi ya 100m, lazima uwe na angalau cash bank 10m, ukipata kazi wANAKUDAI UNCONDITONAL BANK GUARANTEE YA 20%, NA ILI UPATE ADVANCE LAZIMA UWE NA GUARANTEE KAMA HIYO, KWA MAHESABU YA HARAKA HARAKA LAZIMA UWE NA KAMA 45M BANK. sharti hili liliwekwa na wenzetu walioko maofisini kuwabaeba wahindi kwa kuwa wao wanapata guarantee kwenye benki zao kama vile savings&finance hata kama hawana shilingi kule ndani, wachina nao wanakuja na za kwao toka chinatoka kwenye mabenki yao hata kama ni feki hakuna anayejua!
pamoja na tanroads kukakomalia kuwa badala ya hizo guarantee kampuni za ki-local zitoe kitu kinaitwa tender securing declaration, bado mashirika kama PPF, NSSF, lapf etc, yamekomalia sysytem ya bank guarantee, kazi zote za majengo ambazo ndizo zenye peasa na zinaweza kufanywa na wazalendo wahandisi waliosoma pale UDSM, au ardhi university zinafanywa na wahindi kupitia benki zao uchwara. asilimia 90% ya contrators class one wahindi waliobebwa na mfumo huu uchwara list ni kama masasi construction, bh ladwa, gk patel,nk, hawa ndo wanafanya majengo yote nchi nzima, hawana cha maana zaiidi ya kubebwa na kamfumo walikojitengenezea wenyewe

Hapo awali, bid security za national Insurance company zilikuwa zikikubalika. Mkandarasi alikuwa akipeleka hata kadi ya gari, Bima walikuwa wanampa bid security. matokeo yake ni kuwa mkandarasi akishindwa kutekeleza aliyopaswa mshitiri hakuwa na pakumkamatia! Yalipokuja mabeni binafsi na baada ya uzoefu ndipo mikataba ikabadilishwa kudai Bid security kutoka benki.sasa, mku, maana ya hii security ni kuwa kama ukishindwa kutekeleza mkataba, waliokutolea itabidi walipe kiasi hicho cha fedha,ulitegemea benki zifanye nini? Advance paymen na yenyewe ni mkopo unaotakiwa kurudishwa, mara nyingi kwa makato wakati wa utekelezaji wa mradi. Na kwenyewe ulitegemea nini? ieleweke kuwa advance si ya kukuwezesha wewe ufanye kazi, la hasha. Ikumbukwe kuwa ukishasaini mkataba unatakiwa kuigia gharama za kujenga uzio, stoo, ofisi, kuvuta maji, umeme n.k. Vyote hivi kabla haujapata hiyo advance. Mkandarasi anaandika claim,consultant anaandika certificate ambayo mshitiri ana muda wa kumlipa na si kwa mtindo wa nipe nikupe. Ndiyo maana uwezo wa mkandarasi kifedha ni muhimu. Sasa kama unatenda kazi ya milioni 100 na huna milioni kumi au 45, kweli uko serious? Kwa nini usianze na hizo ulizo na uwezo nao na kujenga kitita hadi kikafikia hizi zinazohitajika?

Kwa bahati mbaya baadhi ya makandarasi wetu walikuwa wakitumia hiyo advance kuwakatia kitu kidogo waliowapa miradi na hivyo ku'compromise' uwezo wao wa kutenda kazi. Makandarasi hawa walikuwa pia na mchezo wa front loading na mara wanapolipwa maipo ya awali walianza kudai mabadiliko(variations) maana hatua za mwisho za mradi hazikuwa na fedha za kutosha! Hao unaowalaamu wanaangalia kuwa kazi inamalizika ndiyo wanapotoa hizo asante (kama kuna haja!) Ninavyojua ni kuwa kuna makandarasi wengi tu waswahili wanaofanya kazi vizuri katika huu mfumo. Badala ya kubaki kulalamika inabidi tujitahidi tuweze kutimiza masharti tuliyowekewa. Kama hatuwezi, basi hii kazi si ya kwetu tuwaachie wenye kuweza!
 
unajua kuna kitu kimoja kinachonisumbua sana kuhusu hili.

a. Hivi watu wanaosoma katika vyuo vyetu vikuu hivyo vitu wanavyovisoma vinatofauti kubwa kiasi gani na vile watu wanasoma nchi nyingine? Yaani, engineer wa umeme wa Tanzania, au Engineer wa barabara anatofauti gani kiujuzi na yule wa nje? Je tukimpa nafasi ya kufanya kazi kama US au UK atafanya hayo anayoweza kufanya Tanzania (kama alivyosema Kuhani Mkuu)?

b. Ni kitu gani kinachomfanya mtumishi wa TAnzania anapowatumikia watanzania wenzake anawapa minimal quality of service lakini akija mzungu au mtu wa nje hasa nchi za magharibi anamuonesha ukarimu na huduma bora kweli. Nazungumza toka personal experience.

NIlipokuwa home mara ya mwisho about four years ago, nilikaribisha marafiki zangu toka Ujerumani na tukawa tunaenda nao kutembelea Serengeti. Through out the tour wao walikuwa wanapapatikiwa ingawa ni mimi nilikuwa nalipia gharama nyingi. Kwanini? Sitoshangaa wengine mmewahi kwenda kupata huduma na ukachukuliwa with contempt lakini mtasha na mabegibegi yake anakaribishwa na "welcome sir, how can I help you" with bis a.s smile! kwanini Watanzania wanastahili huduma ya chini au bidhaa za chini?

c. Je Mtanzania akipewa nafasi ya kuitumikia nchi yake anavutiwa kwa kiasi gani to provide the best quality service? Kuna utaratibu gani wa kuhakikisha the Standard Operating Procedures katika maeneo mbalimbali zinafuatwa to the letter?

a. Kuna jambo moja ambalo Morani75 na mimi tumekuwa tukilipigia sana kelele lakini naona hatueleweki. Hili ni kuwa na institutions zenye kuhakika haki inatendeka bila kisingizio chochote. Nchi zote huko ulaya na marekani, zina vyombo vinavyohakikisha kuwa kazi inafanyika katika msingi uliokubalika. Kwa hali hii wale wote wenye kutoa hizo huduma wanahakikisha wana nyenzo ikiwa pamoja na vichwa zitakazowawezesha kutimiza hayo masharti. Wahandisi, mafundi mchundo wetu wakifanya kazi huko wana'dilive' si kwa sababu tu ya mshahara mzuri bali kujua ukweli ni kuwa ukivurunda, you are OUT,hakuna kisingizio. Ukifanikisha vile vile utatuzwa. Ili kuweza kufika hapa tunahitaji kuwa na wasimamizi wenye uwezo (si wa makaratasi tu kama tunavyopenda) na wenye kujiamini na kuaminika. Ndiyo maana mimi nashangaa tunapowakazia macho wmawaziri badala ya kuwandama watendaji wakiongozwa na makatibu wakuu!

b. Hii ya minimal service ni kwa wote. Katika level ya chini mara nyingi wanamchangamkia mzungu kwa sababu mbili:
1. Historically wanajua wao ni wepesi wa kuwaonea huruma na kuwatupia makombo. Sisi waswahili tunatoa baada ya kuzungushwa.
2.Wanajua kuwa wana uwezo wa kuwachongea. Sisi waswahili mara nyingi tunasema ewala na kukimbila kulalama JF wakati wenzetu watahakikisha wanaambiwa nini kulikoni. Wanoko kama hawa ni heri kuwatimizia ili waondoe kiwingu.
3. Historia ilitufundisha kuwaogopa wazungu.

Kwenye bidhaa za chini, wanatujua tunavyopenda dezo. Ukienda Kitumbini mwenye duka anakuonyesha bidhaa aina mbili, moja anasema ni jenuini kwa hiyo bei mabaya na nyingi feki kwa hiyo bei poa! Tunakimbilia ya bei poa wakati kumbe vyote ni feki!

Ninaposema minimal service ni kwa wote ninamaanisha kuwa kkwa mwekezaji halali na makini, usumbufu ni ule ule bila kujali rangi. Hii ndiyo maana hakuna wawekezaji wa maana wanaokuja kutoka nje isipokuwa hao matapeli wenzetu! Malalmiko makubwa hata kwa hao wazungu ni sheria zisizoeleweka, ukiritimba usio na maana n.k. Yote haya yanatukumba wote, wageni na wenyeji. Nakumbuka muwekezaji aliyetaka kuanzisha kiwanda cha kuisndika matunda mkoani Tanga na jinsi alivyopata thuluba kuanzia serikali ya kijiji na kuendelea, wote wakiwa wamekaa katika mkao wa kula. Huyu mheshimiwa alipeleka kiwanda chake Msumbiji!
 
Kuna mheshimiwa alitoa mfano wa kupewa Kilimanjaro Hoteli Kempinski badala ya Mengi au Mlibya! Napenda kumfahamisha kuwa kigezo cha uzalendo kilitumika kutoa Hoteli ya Mikumi Wildlife kwa mzawa mwenzetu ambaye ndio akaipeleka kaburini. Hoteli haitamaniki. Uzalendo ulitumika kutoa hoteli ya Savoy Morogoro kwa wazawa. Hii hoteli ambayo waswahili tulikuwa tunaogopa hata kuikaribia enzi zake, iliishia kupangisha vyumba kwa wafanya biashara na si malazi. Hoteli haitamaniki. Hoteli ya Bhahari beach aipewa mlibya. Kwa kifupi, na yenyewe haitamaniki. Mengi hana uzoefu wa kuendesha hoteli na baada ya kuumwa mara kadhaa si ajabu serikali kuona heri apewe mtu mwenye track record kwenye nyanja hii ambaye tuna hakika aaweza kuifufua na kuiendesha! For the record, mimi sifurahii alichokifanya lakini inaelekea nipo katika minority. Pamoja na kupinga dhana hii ya ujinga, ni lazima tukubali udhaifu wetu pale ulipo.

Amandla!
 
Hivi ni wangapi kati yetu tunapotaka kujenga kasri zetu nyumbani tunatumia wataaalamu wazalendo? Wangapi tunaajiri kampuni za architects, quantity surveyors, structural engineers, electrical engineers wazalendo? Baada ya hapa ni wangapi tunaajiri makandarasi wazalendo? Naamini sio wengi.

Michoro tunaitoa kutoka kwenye magazeti, ku'download kwenye intanet, kutoka kwa washikaji ambao nyumba yao tumehusudu (?), kuajiri mafundi mchundo wenzangu walio kwenye hizo ofisi kwa ujira mdogo n.k. Hata kwa nyumba ya milioni 100 hatuajiri mkandarasi bali tunawaendea mafundi wazoefu! Tunatumia ndugu, rafiki na jamaa zetu kusimamia miradi yetu ambao mara nyingi wanatuliza! Sasa tunamtegemea nani awawezeshe hao makandarasi wa daraja la saba na sita ( ambako wazawa wanakobanana)kama sio sisi? Serikali haiwezi kila kitu.
 
ujing wetu hautolewi shule, ni ukosefu wa maadili, hufundishwa na wazazi. Uzalendo, uungwana, ukweli, ujasiri, yani walking the talk.
Wengi hatuna, maneno mengi jukwaani, kwenye blogu, lakini, nani wanaochukua hatua hapa wanahesabika, waliotayari kujitoa kwa Tanzania wanahesabika, kujitoa muhanga wajukuu waje kurithi ni wachache.
hii vita mimi nashauri ipiganwe kwa malengo ya muda mrefu, si tu kwa malengo ya kuona Lowasa kaondoka, kashitakiwa au Balali kafungwa.
Bora waachiwe, lakini tuweke misingi kuwa asitokee Balali mwingine wala asipate fursa tena karamagi mwingine kuingia kwenye system.
La sivyo tutakuwa tunarudi hizi issue miaka na miaka,
Kwa kifupi, 'KUZIBA MIANYA' japo msamiati tunao, lakini hatuufanyii kazi.
Tuanzie na katiba
 
kazi wanazopewa makandarasi wa kizalendo hasa za halmashauri hazina tija yeyote, rushwa ndo kikwazo kikubwa, utaoewa kazi ya kuweka kifusi km 5, kwa shilingi 35m, utatakiwa kupeleka hongo kama 10m, zinazobaki hazitoshi kazi ndo maana watu wanalipua kazi, nimekuwa kwenye hii industry as profession kwa miaka 18 sasa, usanii ni mwingi. kilichowashinda konoike kumaliza dodoma-manyoni road project ni hicho hicho, ukisikia kazi inafadhiliwa na g0vernment ya tanzania kaa chonjo. kutoka singida -to shelui kazi imemalizika vema contractor ni mchina pesa zimetoka world bank hakuna rushwa, toka singida-manyoni contractor mchina, kazi imeshindikana, pesa ni za serikali shauri ya rushwa..., toka manyoni-dodoma, contractor konoike kazi inasua sua ile mbaya, pesa za serikali ya tz shauri ya rushwa, toka makuyunu-ngorngoro, konoike hao hao wamemaliza kazi nzuri sana, pesa iantoka na kulipiwa japani rushwa hamna, jifunzeni kable hamjawalaumu makandarasi. ukifanya kazi nzuri bila kutoa rushwa unaweza hata kufutwa ukandarasi
 
kazi wanazopewa makandarasi wa kizalendo hasa za halmashauri hazina tija yeyote, rushwa ndo kikwazo kikubwa, utaoewa kazi ya kuweka kifusi km 5, kwa shilingi 35m, utatakiwa kupeleka hongo kama 10m, zinazobaki hazitoshi kazi ndo maana watu wanalipua kazi, nimekuwa kwenye hii industry as profession kwa miaka 18 sasa, usanii ni mwingi. kilichowashinda konoike kumaliza dodoma-manyoni road project ni hicho hicho, ukisikia kazi inafadhiliwa na g0vernment ya tanzania kaa chonjo. kutoka singida -to shelui kazi imemalizika vema contractor ni mchina pesa zimetoka world bank hakuna rushwa, toka singida-manyoni contractor mchina, kazi imeshindikana, pesa ni za serikali shauri ya rushwa..., toka manyoni-dodoma, contractor konoike kazi inasua sua ile mbaya, pesa za serikali ya tz shauri ya rushwa, toka makuyunu-ngorngoro, konoike hao hao wamemaliza kazi nzuri sana, pesa iantoka na kulipiwa japani rushwa hamna, jifunzeni kable hamjawalaumu makandarasi. ukifanya kazi nzuri bila kutoa rushwa unaweza hata kufutwa ukandarasi


Mkuu, Mwikimbi!
Hata sisi hii industry tunaifahamu kwa zaidi ya miaka hiyo uliyoitaja. Tatizo ni kuwa utakubalije kutoa rushwa ya milioni kumi kwa mradi wa milioni 35? Kwa nini usimchomee anayekudai hiyo rushwa? Na ukikataa kutoa ina maana atakataa kukuandalia certificate? Mara nyingi, na hii inatokana na uzoefu, makandarasi wetu wanatanguliza ahadi za kuwekana sawa mara watakapopata mradi! sasa mradi ni competitive na unatakiwa kuweka bei itakayokuwa chini ya wenzako, hiyo hela ya hongo utaitoa wapi? Wenzetu walipoona haya wakajitoa kwenye local projects, na hizo nyingine zilipopotea, wakafunga virago! Sisi tunashindwa nini? Kwani lazima tuwe makandarasi? Kwa mtazamo huu wa kutaka kazi hata kama ni ya hasara ndiyo kunakowafanya waseme kuwa tu wajinga!
 
Mkuu, Mwikimbi!
Hata sisi hii industry tunaifahamu kwa zaidi ya miaka hiyo uliyoitaja. Tatizo ni kuwa utakubalije kutoa rushwa ya milioni kumi kwa mradi wa milioni 35? Kwa nini usimchomee anayekudai hiyo rushwa? Na ukikataa kutoa ina maana atakataa kukuandalia certificate? Mara nyingi, na hii inatokana na uzoefu, makandarasi wetu wanatanguliza ahadi za kuwekana sawa mara watakapopata mradi! sasa mradi ni competitive na unatakiwa kuweka bei itakayokuwa chini ya wenzako, hiyo hela ya hongo utaitoa wapi? Wenzetu walipoona haya wakajitoa kwenye local projects, na hizo nyingine zilipopotea, wakafunga virago! Sisi tunashindwa nini? Kwani lazima tuwe makandarasi? Kwa mtazamo huu wa kutaka kazi hata kama ni ya hasara ndiyo kunakowafanya waseme kuwa tu wajinga![/FONT]

Awethu Fundi Mchundo:

Tumeshazungumza katika mada nyingi za kiufundi lakini inaonyesha kuwa matumaini (expectations) ya taifa kwa watu
waliosomea ufundi ni makubwa sana kuliko ule uwezo wenyewe.

Shule wanafunzi wanasoma taaluma. Na wanaweza kutumia taaluma hivyo kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya kila siku.

Lakini kwenye miradi inayotumia pesa na faida kutafutwa hiyo tena sio taaluma. Shughuli nzima inaanguka katika kundi
la BIZNISI (Biashara) na taaluma inayotumika inakuwa ni NATURE ya biashara yenyewe. Na kitu kinapokuwa biashara basi
components za kibiashara zinajingiza. Moja ya components hizo ni mtaji (capital).

Kwa kuwa tunazungumzia miradi basi swali lisiwe kwanini ma-injinia wanashindwa kutumia taaluma zao. Swali
liwe ni tatizo gani linalofanya ma-injinia kutofungua BIZNIS (Biashara) zenye nature ya taaluma zao zenye kuleta faida. Hapa wapo mainjinia, mafundi, madaktari na watu wa fani nyingine wanaoweza kutupa maoni ya ugumu wa kufungua BIZNIS katika fani zao na ni mazingira gani yanawakumbuka kila siku katika nchi hile ya mababu.

Tusing'ang'anie tu kuwa mtu akiwa chuo kikuu na anasoma engineering basi achimbe kisima cha maji. Kama kushimba kisima
cha maji ni mradi na wenye kutumia pesa basi ufanywe kama BIZNIS zingine.

Vilevile tusing'ang'anie zitumike kampuni za wazawa kujenga barabara hili pesa zibaki nyumbani. Hili pesa zibaki nyumbani
ni lazima mzawa afanye BIZNIS.

Tukiweka suala zima la kubaki pesa nyumbani katika context ya kufanya BIZNIS tutakuwa na picha kubwa ya kutatua
matatizo yetu.
 
Mhandisi ujenzi aliyesomea Tanzania ana uwezo saa wa kitaaluma na Mhandishi aliyesoma Marekani? Je mhasibu wa Tanzania amesomea sawasawa na yule aliyesomea Uingereza?
 
tumesha kubali kuwa sisi ni wajinga na inauma je tumefanya au tunafanya nini ili kujikwamua?

Kujikwamua kirahisi ni tuwe au kuanazisha tabia ya kupenda kazi zetu yaani mtu anakuwa proud kwa kazi anyoifanya iwe kuzoa taka au kuendesha ndege.

Pili kuwajibishwa hili nadhani ni muhimu zaidi kwa sababu itatufanya kuwa na tabia ya kupenda kazi


Fundi Mchundo said:
Hivi ni wangapi kati yetu tunapotaka kujenga kasri zetu nyumbani tunatumia wataaalamu wazalendo? Wangapi tunaajiri kampuni za architects, quantity surveyors, structural engineers, electrical engineers wazalendo? Baada ya hapa ni wangapi tunaajiri makandarasi wazalendo? Naamini sio wengi.

Wengi wanaogopa kwa saabu kwa bei zao na unajiuliza kuwa kweli nikimpa contract huyu je ata deliver? jibu ni hapana
 
Mhandisi ujenzi aliyesomea Tanzania ana uwezo saa wa kitaaluma na Mhandishi aliyesoma Marekani? Je mhasibu wa Tanzania amesomea sawasawa na yule aliyesomea Uingereza?

Kwa level ya digrii ya kwanza na entry level position (yaani wote wametoka shuleni bila kuwa na uzoefu wa kazi). Kwa wastani Mhandisi wa Tanzania atakuwa amechimba sana kuliko yule wa Marekani. Sasa swali lako hapa ni lipi?
 
Back
Top Bottom