Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,210
- 12,710
Zamani kuna historia kuwa Mobutu alipoona uchumi unaenda hovyo akaajili mbobezi kutoka Ulaya kuwa gavana wa benki kuu.
Jamaa akaja na mipango mizuri sana ya kuokoa uchumi. lakini alikuta vikwazo kibao, Mobutu alikuwa anaifanya benki kuu kama kibubu chake.
Wakashindwana jamaa akasepa. Mkapa baada ya kuona uzembe wa kuendesha mambo serikalini akaleta mtaalamu wa kuendesha hospitali kutoka Ulaya aendeshe hospitali ya Muhimbili. Nasikia jamaa alifanya kazi yake kwa weledi sana. alijenga uzio wa hospitali.
Na kuweka mipaka ya wahadhiri wa chuo na wafanyakazi wa hospitali. kabla ya hapo wahadhiri walikuwa na cheo wakisimamia kitengo hospitali huku wanavitengo vingine chuoni.
Pengine mashirika yetu mengi yanababaika kwa sababu maadminstrator hawana weledi wa kufanya hizo kazi. kuwa na elimu tu haitoshi, inaonekana ubobezi unahitajika kuendesha mashirika kwa ufanisi.
sasa badala ya kubinafsisha mashirika yetu kwanini tusitafute wabobezi wayaendeshe, Ulaya kumejaa watu waliopiga kazi hizi miaka na miaka, wanaweza kutusaidia.
Jamaa akaja na mipango mizuri sana ya kuokoa uchumi. lakini alikuta vikwazo kibao, Mobutu alikuwa anaifanya benki kuu kama kibubu chake.
Wakashindwana jamaa akasepa. Mkapa baada ya kuona uzembe wa kuendesha mambo serikalini akaleta mtaalamu wa kuendesha hospitali kutoka Ulaya aendeshe hospitali ya Muhimbili. Nasikia jamaa alifanya kazi yake kwa weledi sana. alijenga uzio wa hospitali.
Na kuweka mipaka ya wahadhiri wa chuo na wafanyakazi wa hospitali. kabla ya hapo wahadhiri walikuwa na cheo wakisimamia kitengo hospitali huku wanavitengo vingine chuoni.
Pengine mashirika yetu mengi yanababaika kwa sababu maadminstrator hawana weledi wa kufanya hizo kazi. kuwa na elimu tu haitoshi, inaonekana ubobezi unahitajika kuendesha mashirika kwa ufanisi.
sasa badala ya kubinafsisha mashirika yetu kwanini tusitafute wabobezi wayaendeshe, Ulaya kumejaa watu waliopiga kazi hizi miaka na miaka, wanaweza kutusaidia.