Tujionee kwanza haya maajabu ya Kikokotoo kwa Watumishi wa Umma

Halafu TUCTA wasivyo hata na chembe ya aibu wanasema Wafanyakazi eti mameridhia uwepo wa hicho kikokotoo! Na wakati wastaafu wengi wanalalamikia huo wizi na uonevu wa wazi kabisa.
TUCTA ni mithili ya BAKWATA tu, wote matawi ya CCM.

Hii nchi inahitaji divine intervention. Manung'uniko ya nafsi kwa wananchi yamekuwa mengi mno kiasi kwamba bila ya rehma ya Mungu kunaweza tokea tafrani kubwa kuwahi kutokea na majambazi wahusika hawatoamini.
 
Unaambiwa Mtumishi wa uuma wa ngazi ya chini aliyefanya kazi serikalini kwa zaidi ya miaka 30. Anapostaafu analipwa 33% tu ya mafao yake.

Yaani kama mtumishi hiyo wa umma alistahili kupata milioni 100 kama mafao (kumbuka hii ni pesa yake halali aliyokatwa kupitia mshahara wake kwa miaka yote hiyo 30+), basi atapatiwa kiasi cha shilingi milioni 33 tu. Na kiasi kinachobakia analipwa kila mwisho wa mwezi kwa muda wa miaka 12! Ikitokea mstaafu akafariki wakati wowote ule baada tu ya kustaafu, na hicho kiasi nacho kinakomea hapo hapo (Wizi wa mchana huu )
Halafu kichekesho zaidi ni kwamba hiki kikokotoo ni kwa baadhi tu ya Watumishi wa umma! Mfano walimu, Manesi, Maafisa ugani, nk.

Ukija kwa Vigogo wa ngazi za juu, mfano Wabunge; eti wenyewe hawahusiki na hiki kikokotoo! (Ona ubaguzi na upendeleo wa wazi huu ) Ingawa na wenyewe eti ni watumishi wa umma!! Yaani wenyewe kila baada ya miaka 5 ya Ubunge wao, wanapatiwa mafao yao yote yanayokadiriwa kuwa kiasi cha shilingi milioni 250 za Kitanzania!

Ukija kwa vigogo wengine wa juu zaidi; mfano Rais, Makamu, Waziri Mkuu, Spika, na sasa wake wa hao vigogo; ikitokea wamestaafu! Wanapewa mafao yao yote! Na kila mwezi wanalipwa mshahara wa 80% kama ule wa Kigogo aliyeko madarakani kwa wakati huo kwa maisha yake yote! (Ubaguzi mwingine huu )

Swali la kujiuliza!! Kwa nini serikali mnawafanyia wafanyakazi wenu uonevu na wizi wa mchana kiasi hiki?

Mkiulizwa, mnatoa sababu za kipuuzi tu; eti wafanyakazi wakipewa hela zao zote kwa mkupuo wanaishia kuzitapanya na kutapeliwa, na mwisho wa siku wanakuwa masikini!! Sasa hao wafanyakazi wastaafu wakizitapanya hizo hela zao, nyinyi mnapata athari gani? Je, waliwaomba muwatunzie kupitia hicho kikokotoo chenu cha wizi?

Na kama mnaona ni muhimu kufanya hivyo, kwa nini msifanye mpaka kwa Wabunge? Je, ni kwa mini msitoe uhuru kwa Wastaafu kuchagua kama wanataka kupewa 33% pekee, au mafao yao yote?

Binafsi nimeandika haya malalamiko baada ya kushuhudia wastaafu fulani hivi niliopanda nao daladala sehemu fulani, wakilalamika kwa uchungu baada ya kulipwa mafao kiduchu kwa mfumo wenu huu kandamizi wa 33%.

Ushauri wangu kwa serikali; rejesheni mara moja kikokotoo cha zamani. Acheni kuwadhulumu wastaafu pesa zao.

Akifa wategemez si wapo, watalipwa hiyo pension
 
Wewe idiot huna elimu ya kikokotoo, ni mbumbu na lijinga. Kikokotoo ni kizuri sana. Imagine anayelipwa mil 1,300,000 kwa mwezi anakuja kupokea 46 mil kama lumpsum, na bado kila mwezi atapata kama 500k, hivi huyu mtu akiamua kuiwekeza hiyo 46m kwenye duka au mifugo si atatengeneza kama laki tano zingine ukijumlisha anapata kama mil moja, compare na wakati wa ajira ana pungukiwa hela kidogo tu. Na hapo anakuwa na uhakika na cashflow yake.

Unawekezaa 46M at your 60s;

You don’t sound smart
 
Dah hizi akili za wapi. Hamjui hata kikotoo na ni kwa sababu sio watumishi wa uma. Kwa akili yako hapo unfkr zamani kabla ya kikotoo kipya walikua wakilipwa 100%

Unajua zamani walikua wakilipwa % ngapi?
 
Serikali walifanya hivyo kwa sababu wanajua maisha ya wafanyakazi wao , baada ya kustahafu ni wachache wanaotoboa miaka 12 baada ya hapo wanabaki na pesa

Eti "akipewa hela zote atatapeliwa au kuzitumbua hadi ziishe" kwani hao wabunge na wezi wengine wenyewe hawawezi kutapeliwa au kuzitumbua na warudi kua maskini yani mtu anajikaza miaka zaidi ya 20 kupambana kufanya kazi mnajidai kumtunzia pesa zake alafu anakuja kusalitiwa na kutapeliwa na serikali yake mwenyewe serikali inacho wafanyia hawa wazee ndio maana wanakufa mapema mpeni mtu pesa yake akimaliza na kua maskini ni yeye ametaka hana wakumlaumu

Decision haikuwa inclusive and participatory

Bad
 
Formula

[1/580]×N×APE×12.5×33%

Where:
1/580 = accrual factor
APE = The best three years avarage salary
12.5 =Avarage life expectancy after retirement
33% = pension lumpsum at retirement
N = Number of months contributed

Hii ni copy na paste . Chakata data ili lower level waweze kuelewa
 
Mnacholalamikia ni kitu gani?

Waopanga kikokotoo ni Wanasiasa Wabunge. Anayesaini iwe sheria ni Mwanasiasa Rais.
Wanaopata 80% hadi kufa wao na watoto wao ni viongozi wa Siasa.

Ni ninyi wale wale mkiambiwa kushirikia siasa , hamtaki kwa kauli ' mambo ya siasa hayanihusu''
Mkiambiwa muandamane ili tutengeneze mifumo yenye haki mnasema ninyi si Wapinzani.

Mkiambiwa mtumie 'voting block' kama Walimu, Wauguzi n.k. ili kuwafanya Wanasiasa wawasikilize, hamtaki kufanya hivyo badala yake mnatumia 'voting block zenu kama Chama cha Walimu' kumchukulia Form mwanasiasa.

Mtazungumzia kikokotoo na kitawazingua hadi siku mtakapo baini ni ninyi WAAJIRI wa hao Wanasiasa na kwamba siasa inaamua maisha yako ya kilas siku utake usitake.

Kukaa pembeni na siasa ni kusikilizia maumivu taratibu. Kusubiri Wapinzani wafanye ni kuahirisha maumivu.

Wenye hatma ya kikokotoo ni ninyi wenyewe mkiamua na mkitaka!

Tulieni sindano iingie.

JokaKuu Tindo Pascal Mayalla

Unampeleka babu tale bungeni akawe policy maker

Mtasubiri

Most of the policy makers ni Academic failures . Wakati wa kikokoto decision haikuwa inclusive kwa lower level . Hakuna feasibility study iliyofanyika kuonesha je ni kweli wastaafu wanataka iwe ivo

Kama kungekuwa na inclusivity. IBet kikokoto kingekataliwq

Ila
Yule JPM ipo shida alikuwa nayo kwa head
 
Au wangetoa option kwenye hicho kikokotoo. Yaani kama kuna wastaafu wanataka kupewa hela zao zote baada ya kustaafu, basi wangepewa. Na kama kuna wale wanaotaka kupewa kwa mfumo huu mfumo wao mpya, na wenyewe wangepewa.

Yawe makubaliano,sio kulazimishana.
 
May be these are some of the issues walizomuondolea JPM.There is a lot of money at stake here,na naamini JPM angekuwepo asingekubali upuuzi huu.R.I.P. JPM.
 
Akifa wategemez si wapo, watalipwa hiyo pension
Hakuna kitu kama hicho. Sheria inasema mstaafu akifa, na mafao yake yanakomea hapo.

Wategemezi wanatakiwa kumuombea mstaafu wao aishi kwa muda wa muaka 12 baada ya kustaafu. Na hiyo miaka 12 nayo ikipita, na mafao nayo yanakata.
 
Unaambiwa Mtumishi wa uuma wa ngazi ya chini aliyefanya kazi serikalini kwa zaidi ya miaka 30. Anapostaafu analipwa 33% tu ya mafao yake.

Yaani kama mtumishi hiyo wa umma alistahili kupata milioni 100 kama mafao (kumbuka hii ni pesa yake halali aliyokatwa kupitia mshahara wake kwa miaka yote hiyo 30+), basi atapatiwa kiasi cha shilingi milioni 33 tu. Na kiasi kinachobakia analipwa kila mwisho wa mwezi kwa muda wa miaka 12! Ikitokea mstaafu akafariki wakati wowote ule baada tu ya kustaafu, na hicho kiasi nacho kinakomea hapo hapo (Wizi wa mchana huu 🤭)
Halafu kichekesho zaidi ni kwamba hiki kikokotoo ni kwa baadhi tu ya Watumishi wa umma! Mfano walimu, Manesi, Maafisa ugani, nk.

Ukija kwa Vigogo wa ngazi za juu, mfano Wabunge; eti wenyewe hawahusiki na hiki kikokotoo! (Ona ubaguzi na upendeleo wa wazi huu 🤭) Ingawa na wenyewe eti ni watumishi wa umma!! Yaani wenyewe kila baada ya miaka 5 ya Ubunge wao, wanapatiwa mafao yao yote yanayokadiriwa kuwa kiasi cha shilingi milioni 250 za Kitanzania!

Ukija kwa vigogo wengine wa juu zaidi; mfano Rais, Makamu, Waziri Mkuu, Spika, na sasa wake wa hao vigogo; ikitokea wamestaafu! Wanapewa mafao yao yote! Na kila mwezi wanalipwa mshahara wa 80% kama ule wa Kigogo aliyeko madarakani kwa wakati huo kwa maisha yake yote! (Ubaguzi mwingine huu 🤭)

Swali la kujiuliza!! Kwa nini serikali mnawafanyia wafanyakazi wenu uonevu na wizi wa mchana kiasi hiki?

Mkiulizwa, mnatoa sababu za kipuuzi tu; eti wafanyakazi wakipewa hela zao zote kwa mkupuo wanaishia kuzitapanya na kutapeliwa, na mwisho wa siku wanakuwa masikini!! Sasa hao wafanyakazi wastaafu wakizitapanya hizo hela zao, nyinyi mnapata athari gani? Je, waliwaomba muwatunzie kupitia hicho kikokotoo chenu cha wizi?

Na kama mnaona ni muhimu kufanya hivyo, kwa nini msifanye mpaka kwa Wabunge? Je, ni kwa mini msitoe uhuru kwa Wastaafu kuchagua kama wanataka kupewa 33% pekee, au mafao yao yote?

Binafsi nimeandika haya malalamiko baada ya kushuhudia wastaafu fulani hivi niliopanda nao daladala sehemu fulani, wakilalamika kwa uchungu baada ya kulipwa mafao kiduchu kwa mfumo wenu huu kandamizi wa 33%.

Ushauri wangu kwa serikali; rejesheni mara moja kikokotoo cha zamani. Acheni kuwadhulumu wastaafu pesa zao.
Kikokotoo ni janga na kimepoteza morali ya kazi..!
 
Acha uongo, mfano ma prof vyuoni walipata mpaka mil 30 tu. Kwa ufupi kila mfuko ulikuwa na fomula yake, ila kwa sasa inatoa fursa sawa. Nimemtukana kwa sababu ni mjinga anapotosha watu. Kikokotoo cha sasa kinamuwezesha mstaafu kuishi bila wasiwasi kwa sababu monthly pension ni kubwa na mstaafu akiiwekeza vizuri lumpsum kwenye miradi mbali mbali inamlipa vizuri hata kama ikitokea lumpsum imeisha anaweza kuishi vizuri. Mleta maada aacha uzuzu
chawa huna akili.acha wenye akili wajadili.kwa akili zako ndogo unaona milion 46 ni nyingi,aliyekwambia ela yakustafia niyakwenda kunzishia biashara ni nani.bure kabisa wewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaambiwa Mtumishi wa uuma wa ngazi ya chini aliyefanya kazi serikalini kwa zaidi ya miaka 30. Anapostaafu analipwa 33% tu ya mafao yake.

Yaani kama mtumishi hiyo wa umma alistahili kupata milioni 100 kama mafao (kumbuka hii ni pesa yake halali aliyokatwa kupitia mshahara wake kwa miaka yote hiyo 30+), basi atapatiwa kiasi cha shilingi milioni 33 tu. Na kiasi kinachobakia analipwa kila mwisho wa mwezi kwa muda wa miaka 12! Ikitokea mstaafu akafariki wakati wowote ule baada tu ya kustaafu, na hicho kiasi nacho kinakomea hapo hapo (Wizi wa mchana huu )
Halafu kichekesho zaidi ni kwamba hiki kikokotoo ni kwa baadhi tu ya Watumishi wa umma! Mfano walimu, Manesi, Maafisa ugani, nk.

Ukija kwa Vigogo wa ngazi za juu, mfano Wabunge; eti wenyewe hawahusiki na hiki kikokotoo! (Ona ubaguzi na upendeleo wa wazi huu ) Ingawa na wenyewe eti ni watumishi wa umma!! Yaani wenyewe kila baada ya miaka 5 ya Ubunge wao, wanapatiwa mafao yao yote yanayokadiriwa kuwa kiasi cha shilingi milioni 250 za Kitanzania!

Ukija kwa vigogo wengine wa juu zaidi; mfano Rais, Makamu, Waziri Mkuu, Spika, na sasa wake wa hao vigogo; ikitokea wamestaafu! Wanapewa mafao yao yote! Na kila mwezi wanalipwa mshahara wa 80% kama ule wa Kigogo aliyeko madarakani kwa wakati huo kwa maisha yake yote! (Ubaguzi mwingine huu )

Swali la kujiuliza!! Kwa nini serikali mnawafanyia wafanyakazi wenu uonevu na wizi wa mchana kiasi hiki?

Mkiulizwa, mnatoa sababu za kipuuzi tu; eti wafanyakazi wakipewa hela zao zote kwa mkupuo wanaishia kuzitapanya na kutapeliwa, na mwisho wa siku wanakuwa masikini!! Sasa hao wafanyakazi wastaafu wakizitapanya hizo hela zao, nyinyi mnapata athari gani? Je, waliwaomba muwatunzie kupitia hicho kikokotoo chenu cha wizi?

Na kama mnaona ni muhimu kufanya hivyo, kwa nini msifanye mpaka kwa Wabunge? Je, ni kwa mini msitoe uhuru kwa Wastaafu kuchagua kama wanataka kupewa 33% pekee, au mafao yao yote?

Binafsi nimeandika haya malalamiko baada ya kushuhudia wastaafu fulani hivi niliopanda nao daladala sehemu fulani, wakilalamika kwa uchungu baada ya kulipwa mafao kiduchu kwa mfumo wenu huu kandamizi wa 33%.

Ushauri wangu kwa serikali; rejesheni mara moja kikokotoo cha zamani. Acheni kuwadhulumu wastaafu pesa zao.
In the name of

Tunamtunzia pesa zake!!!!

Unafiki MKUBWA!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom