Tujikumbushe vitabu vya zamani

Tujikumbushe vitabu vya zamani

Tukumbuke na HEKAYA ZA ABUNUWASI alivyokuwa na busara enzi Sultan Harun Rashid


Hasa ile stori ya kuuza nyumba yake ya gorofa. aliipoona kuwa jamaa amenunua floor moja ya juu na yeye alitaka kuuza nyumba nzima siku moja akamwita yule mteja wake kule juu kuwa Bwana shikilia nyumba yako ya juu maana nabomoa yangu ya chini, usije ukasema sikukuambia. jamaa ikabidi anunue nyumba nzima
 
Tukumbuke na HEKAYA ZA ABUNUWASI alivyokuwa na busara enzi Sultan Harun Rashid


Hasa ile stori ya kuuza nyumba yake ya gorofa. aliipoona kuwa jamaa amenunua floor moja ya juu na yeye alitaka kuuza nyumba nzima siku moja akamwita yule mteja wake kule juu kuwa Bwana shikilia nyumba yako ya juu maana nabomoa yangu ya chini, usije ukasema sikukuambia. jamaa ikabidi anunue nyumba nzima

Mmh, umenikumbusha mbali. Pia vilikuwepo vitabu vya: Malimwengu.
 
Umenikumbusha: Kitabu cha Alfu lela ulela au siku alfu na moja (Kita'b alf laylah wa-laylah). Pia nimekumbuka: Aladdin na taa ya ajabu, Ali Baba na wezi arobaini, Safari saba za Sinbad baharia.
 
Kipindi kile, enzi za utoto wetu tukisoma: Robinson Crusoe, Kisiwa cha Hazina (Treasure Island - by Robert Louis Stevenson), Unyonge wa Mwafrika - umo utawakuta Kaombwe na makapu ya karanga, pia kitabu kimoja jina nimesahau, lakini nakumbuka the main character in Sindbad wa Baghadad. Mzee wangu akipenda kusoma gazeti kubwa sana la Mzalendo na Africa Now. LOL, Old is Gold!

The Seven Voyages of Sinbad The Sailor.
 
Nimekumbuka mbali mkuu: John Fedha = John Silver, mzee shujaa mwenye mguu mmoja, akipigwa na upepo mkali bila kutikisika ktk merikebu kubwa: 'Hispaniola', pia kijana Jim Hawkins.

Umenikumbusha 'Long John Silver', wimbo wa John Silver: 'watu 15, ho ho ho! Juu ya kasha la mfu, ho ho ho! Na chupa ya mvinyo, ho ho ho!
 
i see,hizo zilikuwa siku nzuri sana,je wakumbuka kitabu cha ''mfalme kima ambumunda shetani mfupa mweupe '' na ''kisiwa chenye hazina''??
 
Jamani nimekumbuka Hadithi za Zamani Kibanga ampiga Mkoloni, Karudi baba mmoja.... Tola ala gizani.. Yani rahaaa! Mitoto ya sikuizi kila shule na Hadithi yake. Embu 2kumbushane enzi izoo za Mr Daudi, Baraka and Neema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom