Tujikumbushe vitabu vya zamani

duh...hivi vitabu bwana usipime....

wakati huo kipindi cha mama na mwana kilikuwa kinasimulia hadithi zake zikirushwa na RTD, mida ya saa nane, nakumbuka hadhithi chache kama ua jekundu, binti chura, akajasembamba, kina bibi aga, na kuna kitabu kingine kilikuwa kinaitwa 'adili na nduguze' mambo ya mji wa mawe n.k.....

kweli watoto wa siku hizi hawafaidi kabisa
 
alfu lela ulela elfu mia na moja
amina anakula wali kwa sindano
man umenirudisha,bali sana
Nimevisoma vyote hivyo. Vilikuwa vinanitia hamasa sana ya kusoma.Halafu kulikuwa na vipindi vya radio kujifunza Kiingereza, 'A Thousand Miles to Tanga'. Siku hiyo mwalimu akileta radio darasani ni furaha tupu!
 
Bulucheka na kabila la wagagagigigogo!

du! mkuu enzi za kaptula ya kaki na shati jeupe, ukivaa stocking na raba mtoni unaonekana bonge la mshua!
Ni WAGAGAGIGIKOKO, na vitabu "original "vya ALFU LELA U LELA vinapatikana , vimerudufiwa na Mkuki na Nyota na kimoja ni 8000, vipo namba moja mpaka namba saba,
 
Ama kweli nyinyi ni vijana wa zamani, kukumbuka vitabu vyote hivyo vya akina Bulicheka na mkewe Lizabeti, Bibi Tarabushi na Kalume Kenge alipokataa kwenda shule!

Ni kweli nilikutana na baadhi ya vitabu vya Alfu lela u lela pale mtaa wa Samora. Nilivinunua vol 1 mpaka 3 nitatafuta vyengine.

Munakumbuka hadithi ya chura aliyekuwa akisema "my name is Shokolokobangoshei" na binti hawezi kutamka neno hilo. Sikujua kumbe lile neno ni la Kisukuma?

Ooooooooh the good old days, leo ni siasa siasa siasa hata kwa watoto wadogo jamani dunia yetu inakwenda wapi?
 
Umenena kweli. Kwa mfano mimi nilianza darasa la kwanza mwaka 1962. Mpo?
 

Mnanitoa machozi. Watoto siku hizi hawafaidi Preta. Hawafaidi. Namwomba Mungu anipe nguvu, nina mpango wa kurudisha nguvu za Adili na Nduguze, baadaye after few years nitafanya kwa vitendo. Let's pray.
 
Ni WAGAGAGIGIKOKO, na vitabu "original "vya ALFU LELA U LELA vinapatikana , vimerudufiwa na Mkuki na Nyota na kimoja ni 8000, vipo namba moja mpaka namba saba,
Hao wanatafuta hela tu, vitabu vyenyewe haswa ni kuanzia namba 1-4.
 
Bulucheka na kabila la wagagagigigogo!

du! mkuu enzi za kaptula ya kaki na shati jeupe, ukivaa stocking na raba mtoni unaonekana bonge la mshua!

mkuu ni WAGAGAGIGIKOKO halafu na mfalme wao ni HUHIHUIHUI pia yupo mzee mmoja anitwa MZEE MIRAJI.
 
Msisahau kitabu cha safari za Allan Quterman akina Msolopagazi,kibibi Gagula,wajivuni,n.k :A S 39:

Awww hichi kitabu cha umslopogaas (sp) nilikisoma kikiwa kimeshararukararuka sana yaani enzii hizoo umenikumbusha mbali nyuki dume, nakumbuka nilikuwa nanunua willy gamba series na hela za tuition, plus vitabu vyooooote vya Shafii Adam, kosa la bwana Msa..what I won't give to relish reading them again! Oh time !
 
kweli kabisa those were the days nadhani mambo yalianza kwenda downhill baada ya vitabu kama kandanda kitandani kuanza kutungwa
 
wadau... nakumbuka sana kitabu kikiitwa KISA CHA HASSAN BASRI NA MUHAMMED SIHIRI, kulikuwako VISA VYA ABDULI, hakika ni vitabu vikimpa mtu uelewa wa mambo na kutanua FIKRA.:smile-big: Je vingaliko pia?
 
Hadithi za Allan Quatermain

 
Nadhili ya Umslopogaas
 

ni siasa tu kwa kuwa ndiyo kuna short cut ya utajiri - ufisadi.
 
mkuu ni WAGAGAGIGIKOKO halafu na mfalme wao ni HUHIHUIHUI pia yupo mzee mmoja anitwa MZEE MIRAJI.

Bila kumsahau Mpiga Filimbi wa Hamelin - I think ni kama chama fulani cha siasa hapa nchini kwa sasa. Kina makelele kibao ya ahadi lakini kinawapeleka wananchi kwenye maisha magumu kila kukicha
 
Msimsahau ABUNUWAS ambaye aliazima sufuria kwa rafiki yake akarudisha na kasufuria kadogo ndani yake na kumwambia mwenyewe kuwa sufuria yake imezaa na yeye siyo mwizi hivyo anamrudishia sufuria yake na katoto kake. Alipokwenda siku nyingine kuazima sufuria hiyohiyo mwenyewe akajisemea nyumba ya Abunuwasi ina baraka, hivyo akamwazima kwa roho safii. Safari hii sufuria haikurudi hadi mwenyewe alipoifuata na Abunuwasi akamwambia kwa vile sufuria ilizaa safari imekufa, kila kizaacho lazima kife. Abunuwasi alikuwa mwamuzi mzru sana wa kesi wakati Harun Rashid
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…