Morani kumbe na wewe ni Ilboru? Mie nilimaliza mwaka 1989 pale Arusha Tech na akina Method Mogella. Nakumbuka miaka hiyo waliletwa watoto wa ma Diplomat na wakaja na nywele za ajabu (cut style). Ilboru wakazifunga timu zote za shule ya Secondary pale Arusha na wakaamua kujikakamua kuja kucheza na sisi. Wakachukua goli zao nzuri tu. Sisi tulikuwa na marehemu Mogella na marehemu Sonda.
Hivi huyu kijana aitwaye Killer, ni kweli alirusha mtu dirishani? Jamaa zangu waliotoka Tanga School walinipa hiyo story. Alikuwa akija watembelea pale ATC siku za weekend na hasa Ilboru walikuwa wanakuja wengi sana kuangalia VIDEO siku ya IJUMAA. Kiingilio Shillingi 5 sijui? Unawakuta akina Mhagama wamekaa mlangoni. Mlivyowatilia ngumu akina Bob Venny na Mwanza kuserebuka kwenye Graduation ya form 6, ukaanza ugomvi. Nakumbuka Ilboru wakawa hawaruhusiwi kuingia kuangalia Video. Utoto bwana??
Nilikuja siku moja hapo Ilboru. Jamaa yangu alikuwa na ndugu yake aitwaye John (Mnyamwezi wa Sikonge.) Huyu alikuwa akiimba kwaya kwa Mchungaji Mtangoo pale kanisa la Anglican. Huyu Mzee nimepata habari kawa Mzee na karudi kwao Dodoma. Pia alikuwepo Askofu Alpha na gari lake Alpha Romeo.
Kwa wale waliopo sasa, kuna kijana mmoja mtoto wa mshikaji wangu anaitwa Chagulla (Nusu Mzungu) ameshamaliza? Alikuwa akijisifu kuwa ni mchezaji mzuri sana wa mpira. Namfahamu huyu dogo tangu akiwa mdogo sanaa. Baba yake husema MAJAMBAZI YANGU. Kijana Chagulla kama umo ndani basi tuwasiliane, maana siku nyingi ati. Nakumbuka mwaka huu mwanzoni tulivyoenda kuangalia ile film ya 3D huku tumevaa miwani...🙂
Hiyo njia naikumbuka sana. Inaanzia pale Mianzini kuelekea Ilboru. Hapo unawapita akina Mama yeyo na Maharage yao, Ndizi na UGOLO.....🙂