Tujifunze Kutoka Libya

Tujifunze Kutoka Libya

Huyo Ana miaka 65 na yupo UN miaka 30 sasa sijui yeye na wewe nani mjinga .

Ningekupa na jina lake ukamjua ndo ungejua kuwa nani mjinga
Kufanya kazi UN ndio kipimo cha kutokuwa mjinga? what if namzidi kipato? Anyway mimi nipo zaidi kwenye hiyo kauli uliyosema alikwambia acha tuishambulie kauli zaidi
 
Kuitoa CCM sio jambo jepesi Kama unavyofikiria .

Nadhani ile 29/10 umejionea mwenyewe .

Lazima uwe na mikakati na haya maneno yenu mnayokuwa mnaandika kufarijiana.


Ile 29/10 inakupa picha kamili kuwa kelele , maandamano n.k bado ni njia dhaifu na duni.

Sisi tutatumia mazungumzo na nyie tumieni maandamano.
Mtatumia mazungumzo au risasi!? Acha upotoshaji .
 
Bora wao walikuwa wanafaidi keki ya taifa ,tunaweza kuwalaumu ila kwa TZ hakuna kitu ,watu wanatekwa kila kukicha ,keki ya taifa wanakula kina Abdul ,kizhiga na wahuni wachache waliowazunguka.

Huduma za jamii ni Zero ,Majengo makubwa hakuna madaktari wala dawa ,shule kubwa lakini hakuna walimu ,wanajenga majengo maana wanajua kuna UPIGAJI kwenye miradi.

TZ hapa wanaharakati ,wapinzani ,watoa ushauri wanaishi kama wapo vitani na mafichoni.
kwa sasa maji hakuna Dar es saalam
 
Wazungu hawapo kumsaidia Mwafrika wao ni opportunity seeker

Mimi nina Shanganzi yangu kaajiriwa UN kituo cha Kazi SUDAN.

Wakati Ana re new contract yake Aliwahi kutuambia kuwa wale wasudani wakigombana wao wanapata hela


Anasema kwa sasa kipato kimeshuka kwakuwa hawagombani

Kwahiyo USA n.k huenda kuiba Mafuta kule

Kwahiyo ukisikia VITA zinakuwa zinadhaminiwa na hao Mabeberu na ndo UN na ndo huiba Mafuta , madini n.k

kwahiyo ninapokuwa nawaona hawa Chadema wanawasifu wazungu najua kabisa washalipwa

ni vile sisi hatuna Mali nyingi Kama Mafuta Ila tungekuwa nazo tungewapa wazungu na Kama tungewanyima basi wangeingiza nchi yetu katika machafuko

Utajiri wa USA ukiufatilia Unatokana na wizi
Utajiei wa akina samia na jamaa zake JK umetokana na nini!?
 
Tuchukulie kwamba upo sahihi kwa maelezo yako

Je, kuondoa mfumo huu kandamizi ni kupitia maandamano ya fujo na vurugu?
Tumejaribu kupiga kura wameiba zote,vipi kina mdude, mzee kibao waliouliwa na kina lisu waliokamatwa na kupewa uhaini kwa kuongea tuu,na maandamano na mikutano ya kisiasa si haki ya kikatiba, acha kujitoa ufahamu na kutetea wahuni hao, utekaji na mauaji sio poa
 
Hizo habar potofu ndio propaganda kubwa zIlizo fanywa dhidi ya Utawala wa Gaddafi

Gaddafi alisema sitamjengea mama yangu nyumba mpaka wananchi wangu wapate makazi,je hilo linasemwa?

Wanandoa kupewa nyumba na pesa ya kuanzia maisha je inasemwa?

Nchi haikuwa na deni hata shilingi,je inasemwa?

Gaddafi kaacha nchi ina reserve ya kitu kama dola million 300,je inasemwa?
Pure propaganda, hata kama ni kweli ni mali za Libya sio Gaddafi, they can afford ni very rich state kutokana na oil
 

View attachment 3515158

My people,​


15 - February -2011

Benghazi, Libya

Ghasia zilianza rasmi baada ya Utawala wa Muammar Gaddafi kumkamata mwanasheria anayejulikana kwa jina la Fathi Terbil ambaye alikuwa mtetezi wa haki za binadamu

Baada ya wananchi kujua hilo tukio walikasirishwa sana,na hapo ndipo Maandamano rasmi yalianza viunga vyote vya Libya

Baadae Serikali ilitumia nguvu kubwa kwa kuwapiga risasi waandamanaji,baadae wandamanaji nao wakapora silaha na kuunda vikundi wa uasi dhidi ya Serikali

Kutoka maandamano ikaja kuwa vita ya wenyewe kwa wenyewe, nchi yote ikachafuka hatimaye NATO ikaingilia kati na kufunga anga na kuanza kuwapiga au kuwashambulia askari au wanajeshi wa jeshi la libya,mwisho wa siku Utawala wa Gaddafi ukaanguka

Kilichofuatia baadae nchi haikutawalika tena,uasi ukawa mwingi na machafuko ikawa sehemu ya maisha ya kila siku ya Libya

Watu ambao walikuwa hawajui kulipa bill za maji au umeme,watu ambao walikuwa wanaingiziwa gawio kwenye account zao kutoka kwenye uchumi wa mafuta,leo hii hawana amani,wengi wanakufa baharini huko katika jitihada za kueleka Ulaya.

Wananchi jua kwamba nasi ikifikia hatua hiyo ya machafuko,wazungu wataingilia kati ,si kwakuwa wanatupenda ila kwa ajili ya Kuja kuvuna rasilimali za Tanzania

Ndio maana baadhi yetu tunapoamua kuwa mabalozi wa amani tunajua nini maana ya kukosa amani,tunajua si ushujaa kuwa wakimbizi

Kwahiyo tujue kwamba AMANI NI TUNU YETU BASI TUILINDE KWA WIVU MKUBWA

Tunashukuru na kufurahi kuona kwamba kuna members wengi wanatuunga mkono kwenye hii kampeni itakayodumu hadi 31 Dec 2025

Tanzania ni yetu basi tudumishe amani ya nchi yetu

Ni hayo tu!
Toa haki, watu hawaanzishagi vurugu tu bila sababu, sema sababu huwa zinapuuziwa na viongozi wakizani kwamba hawawezi kufikiwa. Kiburi na jeuri za viongozi kote duniani madhara yake ni huwa hivyo.
 
Ukifuatilia vizur historia ya Libya chini ya Colonel Muammar Gaddafi, nchi ilikuwa inaweka maslahi ya walibya mbele

Na makapuni ya nje hayakuruhusiwa kuchimba mafuta na hata yalichimba basi yalikuwa kwa maslahi ya Libya zaidi,mwa maana Serikalli ilikuwa makini kuhakikisha Libya inanufaika na uchumi wake

Kama unavyojua,mabwana wakubwa hiki hawakulipenda hivvyo wakaanzisha fitina kupitìa wazawa ili Utawala wa Gaddafi uonekane una matatizo,ili mwisho wa siku wapate uhalali wa regime change

Haya ndio yanayotokea sasa hapa Tanzania, inasemekana baadhi ya wanaharakati wanafadhiliwa na makampuni ya nje kama Ford

Cha kujiuliza ni wangapi wapo nyuma ya Ford??

Je, dhumuni lao ni nini hasa?

Watanzania tutulize vichwa vyetu na kutafakari kwa kina sana,tusiingie kwenye anga za adui yetu

..serikali ya Tanzania haijabinya maslahi ya mabeberu wawe nchi za magharibi, ulaya mashariki, China, na hata nchi za kiarabu.

..mradi wa LNG wamewekeza makampuni ya Marekani, na Ulaya.

..mradi wa Uranium wamewekeza kampuni ya Kirusi.

..mradi mkubwa wa chuma na makaa ya mawe wamewekeza Wachina.

..bandarini wapo Waarabu, Wahindi, na Wafaransa.

..mbuga za Wanyama na hewa ya ukas wamewekeza Waarabu.

..madai kwamba Mabeberu wanataka kuleta machafuko ili wazifikie rasilimali zetu ni UONGO. Ccm ina mashirikiano mazuri na mabeberu katika kufisadi mali za Watanzania.

..kuhusu kufadhiliwa na Ford Foundation hakuna tatizo lolote. Kama wanaharakati wana mahitaji ya fedha au utaalamu hakuna ubaya ikiwa watasaidiwa na nchi wafadhili, na mashirika ya kimataifa. Hata Ccm inapokea misaada toka nje ya nchi.
 
Sio kweli,only in shit hole countries like Tanzania sio kwa wanaojielewa

Habari unasoma na kuona ktk TV ni zilichojuwa

Wewe hauwezi kuelewa mambo ya USA

Ila ujue Rushwa zipo Sana , upigaji n.k

Nitakutumia kitabu cha Jay Z kinaitwa Decoded

You will see a lot of Motherfuckers Hapo USA
 
HIyo wote umeileta ili kuhalalisha uhalifu wa unaowatetea!?
Pia kuwa mwanasiasa sio jambo jepesi , kwahiyo usitishwe na mafanikio walionayo

Kwakuwa ktk siasa kuna kuuliwa pia , kupewa sumu , kupigwa risasi n.k

Ndo maana ukiwa hauwezi siasa usilalamike aliyeichagua hiyo Kazi

Swala la kuiba umeliongea wewe Ila wao wanayonya Kama ambavyo wewe boss anavyokunyonya anakulipa ujira mdogo lakini Kazi unafanya kubwa that's game.


Kulalamika mitandaoni haisadii kitu .
 
Wanasiasa wote sio Tz tu duniani hutajirika kupitia siasa
HIyo wote umeileta ili kuhalalisha uhalifu wa unaowatetea
Pia kuwa mwanasiasa sio jambo jepesi , kwahiyo usitishwe na mafanikio walionayo

Kwakuwa ktk siasa kuna kuuliwa pia , kupewa sumu , kupigwa risasi n.k

Ndo maana ukiwa hauwezi siasa usilalamike aliyeichagua hiyo Kazi

Swala la kuiba umeliongea wewe Ila wao wanayonya Kama ambavyo wewe boss anavyokunyonya anakulipa ujira mdogo lakini Kazi unafanya kubwa that's game.


Kulalamika mitandaoni haisadii kitu .
Kukaa kimya pia kunasaidia nini!?
 
Bwana Kalamu,

Hilo liko wazi juu ya mtazamo wako kwangu mimi,binafsi halinipishida

Sisi hapa tunapigania amani ambayo kama wananchi tunaweza kuendelea na maisha yetu ya kila siku,tukalima,tukafanya biashara,tukasoma,na kushiriki katika shughuli mbali mbali za uchumi

Hayo mambo ya haki nyingine nyingi ni mambo mtambuka,ni process,sasa wakati inatafutwa namna ya kukaa mezani na kutatua changamoto ambazo nyingine ni za kikatiba,basi mwananchi huyu wa kawaida aendelee na maisha ya kila siku
Tatizo lenu; watu wenye nia hasa ya upotoshaji ni kuwa mnapoandika ni kama mmezima akili za kufikiri kuwa watakaosoma maandishi yenu na wao wanazo akili za kuchambua na kuelewa mnacholenga nyinyi.

Uliwahi kuona wapi amani inayotokana na kuvuruga utulivu wa nchi kwa kuwanyima wananchi haki?

Hiyo amani ya kugawiwa kwa mitutu ya bunduki ni amani hiyo?

Wewe siyo mtu wa kwanza aliyekuja na hadaa za aina hii; huu ni msimamo toka BAKWATA na pengine mafunzo yenu ndivyo yanavyo elekeza; hili sijui.

Tanzania kama taifa, hatuwezi kufuata maelekezo ya imani ambayo yanahimiza kunyima watu haki zao za msingi kama kuchagua viongozi wanaowataka wao.

Umemuuliza Samia Suluhu Hassan kwa nini kakataa kila aina ya njia za kutafuta uelewano kwa mazungumzo, unayoyahimiza wewe ili pawepo na uchaguzi huru?Hayo mazungumzo unayoyataka wewe ili taifa liwe na amani ni mazungumzo ya namna gani hayo; anayolazimisha Samia kwa mitutu ya bunduki?
 
Halafu wanakuja watanzania wasio jitambua maskini ya mungu wanaongea upuuzi mtup

Siwezi kusema chochote kuhusiana na comment yako kwamba sasa hivi hakuna CCM, maana hizo ni tuhuma tu,sasa huwezi kupoteza muda kuzungumzia porojo

Je hiyo mikakati ndio maandamano ambayo kila kukicha mnayapangia tarehe mpya?
Mtu kama wewe utaanzia wapi kujuwa kuwa CCM ni jina tu linalotumiwa na waovu akina Samia, Kikwete kutimiza malengo ya upande huo unaokuleta hapa na kejeli tele!

Unajitangaza "uzalendo", upi hasa; wa kugawanya waTanzania katika makundi na kuwatawala kwa nguvu na vitisho?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom